kwanini wakenya wanauchumi mzuri kuliko sisi watanzania?

Status
Not open for further replies.

Red Giant

JF-Expert Member
Mar 9, 2012
15,658
20,886
zamani nilikuwa siioni kenya kama reference country lakini siku hizi nabadili mtazamo, kwa mfano
1.kenya ina ardhi ndogo lakini wana viwanda zaidi ya saba vya sukari nakulima zaidi ya hekta laki moja wakati tanzania viwanda vinne na na havifikishi hata hekta elfu hamsini
2.kenya kwenye umeme wana geothermal, wana wind farm wakati sisi tuna hydro power potential ya kutosha na hatafanyi chochote achilia mbali geothermal and wind power
3.wanatuzidi GDP wakati tunawazidi ardhi, natural resources na watu
kuna mifano mingi tu, watz wengi tunalalamikia viongozi lakini najiuliza
kwani wakenya wanapewa mitaji na viongozi wao?, kwani viongozi watanzania wana kataza mtu kuwekeza kwenye umeme au kilimo kikubwa? au watanzania hatuna entrepreneurial skills? au hatuna mitaji?
hebu tujadili hili na wakenya mtusaidie.
 
Hata mimi kama mtanzania mzalendo sielewi kamwe mbona kenya iko juu juu zaidi nakubalikiwa zaidi kuliko sisi
 
Sababu kuu tatu za umaskini wetu

1. CCM


2. CCM


3. CCM
lakini hiyo CCM sisi ndio tunaiweka madarakani je uoni sisi ndio tatizo. kama vile mind zetu hazipendi mabadiliko! huoni kama sisi ni waoga na uoga huo unakuja hata kuazisha miradi.
 
sisi wenyewe ni tatizo, mwl. aliliona hili akaanza kujenga viwanda hivyo vya sukari nk, leo hii niambieni kuna kiwanda gani kipya cha serikali kilichojengwa zaidii ya ahadi za maziwa na asali ambayo mpaka sasa ng'ombe amegoma kutoa. TATIZO KUBWA NI UZALENDO KWA TAIFA UMEKUFA
 
siasa za siasa mpaka vyuoni watu wanajiandaa kuwa wanasiasa matokeo yake hajui nini kinatakiwa kufanywa kuinua uchumi wetu,1.baada ya uhuru tuliangaika kukomboa waafrika wenzetu.
2.tupo kiposho zaid kuliko kikazi
3.UDSM walijiona chuo bora na tuliamin hivyo kumbe ni siasa tupu na uchwara sipati picha kama vyuo vidogo visingefanya juhudi binafsi kijiimarisha ili viwe acredited unversity sijui tungekuwa wapi?
 
sisi wenyewe ni tatizo, mwl. aliliona hili akaanza kujenga viwanda hivyo vya sukari nk, leo hii niambieni kuna kiwanda gani kipya cha serikali kilichojengwa zaidii ya ahadi za maziwa na asali ambayo mpaka sasa ng'ombe amegoma kutoa. TATIZO KUBWA NI UZALENDO KWA TAIFA UMEKUFA
mkuu nakubaliana na wewe kwa kiasi fulani, lakini hebu tuseme watanzania wameishiwa uzalendo na kuwa wabinafsi nafikiri tungekuwa tunaona watanzania wakimiliki ardhi kubwa na kulima kibiashara au wakianzisha viwanda ili wajimlimbikizie mali badala yake wanaenda kuiba! hivi hakuna tatizo kwenye mind zetu kweli? tunaridhika na tuhela twa wizi! sijaona mabilionea duniani walioupata kwa wizi/rushwa
 
sisi wenyewe ni tatizo, mwl. aliliona hili akaanza kujenga viwanda hivyo vya sukari nk, leo hii niambieni kuna kiwanda gani kipya cha serikali kilichojengwa zaidii ya ahadi za maziwa na asali ambayo mpaka sasa ng'ombe amegoma kutoa. TATIZO KUBWA NI UZALENDO KWA TAIFA UMEKUFA

Uzalend gani unaoongelea?
Siamini kama wakenya ni wazelendo sana wa nchi yao kupita sisi, siamini wanigeria kama ni wazalendo wa nchi yao sana kupita watanzania. Wakati wa mwalimu tulikuwa wazelendo sana lakini umasikini ulishamili, wakati wa mwalimu tulikuwa na rais makini/asiyejilipizia mali/asiye na makuu baada ya kustafu akaenda kushika jembe la mkono lakini bado umasikini ulishamili.

Kuna kitabu hapa huwa nakiangalia kila siku kinauliza hivi kwanini Tanzania iliyokuwa na just leader(mwalimu) ilikuwa inadidimia kwa umasikini wakati Malysia yenye corrupt leader inaendelea?
Same is true kwa Kenya na Tanzania. Kenya ina corruption nyingi sana kuzidi Tanzania, Nigeria ina corruption kubwa sana lakini wanatuzidi tatizo ni nini?

KWa pretext nyepesi tunasema ni ccm, lakini kwa argument yangu hapo juu ina nullify argument hiyo, ni kweli ccm ni tatizo lakini tatizo la msingi sio ccm. Tatizo lamisngi naona liko miongoni mwa watanzania.
 
KWa pretext nyepesi tunasema ni ccm, lakini kwa argument yangu hapo juu ina nullify argument hiyo, ni kweli ccm ni tatizo lakini tatizo la msingi sio ccm. Tatizo lamisngi naona liko miongoni mwa watanzania.[/QUOTE]
mkuu umenena vema CCM kweli ni tatizo ambao nao ni watz, tatizo kubwa lipo miongoni mwetu watanzania swali ni kwamba nini tumepungukiwa ambacho wakenya wanacho?, uongozi bora! inamaaana toka mwinyi,mkapa hadi jmk hakuna mzuri?, au planning commission yetu mbovu? wakenya mtusaidie huko mmewezaje?
 
sisi wenyewe ni tatizo, mwl. aliliona hili akaanza kujenga viwanda hivyo vya sukari nk, leo hii niambieni kuna kiwanda gani kipya cha serikali kilichojengwa zaidii ya ahadi za maziwa na asali ambayo mpaka sasa ng'ombe amegoma kutoa. TATIZO KUBWA NI UZALENDO KWA TAIFA UMEKUFA

We subiri tu maziwa wenzio NGOMBE washa chinja na wankula nayama sasa, Utakuta NGOZI na PEMBE.
 
We ndo uko Namtumbo?
Una idea yoyote kuhusu economic redistribution na kanuni zake?
nafikiri watanzania wengi tuko kama huyu kazi kusema kanuni na madesa ya shuleni lakini vitendo zero, inamaana uliposema nihamie kenya ulikuwa unamaanisha kanuni za ikonomiki ridistribyusheni.
 
KWa pretext nyepesi tunasema ni ccm, lakini kwa argument yangu hapo juu ina nullify argument hiyo, ni kweli ccm ni tatizo lakini tatizo la msingi sio ccm. Tatizo lamisngi naona liko miongoni mwa watanzania.
mkuu umenena vema CCM kweli ni tatizo ambao nao ni watz, tatizo kubwa lipo miongoni mwetu watanzania swali ni kwamba nini tumepungukiwa ambacho wakenya wanacho?, uongozi bora! inamaaana toka mwinyi,mkapa hadi jmk hakuna mzuri?, au planning commission yetu mbovu? wakenya mtusaidie huko mmewezaje?[/QUOTE]

Mkuu,
Tatizo sio uongozi, tena naweza kusema ktk nchi za afrika Tanzania ni moja ya nchi iliyowahi kupata viongozi waadilifu kabisa,
Na ndio maana siamini sana kama tukibadirisha uongozi tutakuwa na maendeleo. Mwalimu yani Nyerere amekuwa kiongozi miaka karibu 25, na nikiongozi mie naweza kusema ni namba moja kwa uadilifu duniani. Nitajie mwingine duniani rais aliyestaafu akarudi kushika jembe bila ya bodigadi?

Hata tukibadirisha uongozi vipi, lakini bado siamini kama tutakuja kupata mwingine kwa wakati huu kama mwalimu. Na kama ndivyo mbona tuko/tulikuwa masikini?

Naamini tatizo sio uongozi/chama tatizo ni sisi, kama sisi tungekuwa wema basi by default tutakuwa na viongozi wema pia
 
We subiri tu maziwa wenzio NGOMBE washa chinja na wankula nayama sasa, Utakuta NGOZI na PEMBE.
Kibanga kwa kweli umenisababishia usumbufu mkubwa sn, kwa7bu sikuwa nampango wa kucheka ktk huu mjadala, ila ww umenifanya nicheke, ASANTE KWA HILO.

Turudi kwenye hoja: Kuna ukweli WaTZ ni wavivu lkn vilevile uzalendo hakuna, chunguza WABONGO wakipata pesa wanawekeza wapi. Sio ktk mitradi ambayo itawafanya kufikiri sn, kinachofafadhaisha zaidi hata hao wanaokwapua kiujanjajanja hawawekezi ktk mambo ya maana kama vile viwanda,ufugaji, kilimo cha umwagiliaji, sana sana tunachoona sasa ni hotel na nyumba za kulala wageni,vilabu vya pombe. Huwezi kuinua uchumi wa nchi kwa kuwekeza ktk maeneo hayo kwani hayo maeneo ya ulaji sio uzalishaji. MUDA Umefika kwa WABONGO KUWA WEZI WA TECHNOLOGY kutoka mataifa mengine, kuangalia kwa umakini uzalishaji wa umeme hii pamoja na kupunguza bei ili bidhaa zetu zishindane ktk soko la ndani na nje

Pia ni muhimu kuhamasisha uzalishaji ktk kilimo bila unafiki in z sense that mkulima akizalisha akipata soko zuri Burundi , asiwekewe ukuta wa kumzuia kuuza bishaa yake huko. Serikali ni lazima ikaidi baadhi ya maagizo yua watu wa Britons wanaosisitiza kuwa serikali isifanye biashara. Ktk usafirishaji serikali ni lazima iplay role yake ktk usafiri wa reli maana huu ndio uti wa mgongo kufikisha bidhaa sokoni kwa bei nafuu, Tunaendelea na mnakasha wetu, ASANTE SN KIBANGA KWA KUNIFANYA NICHEKE< RIIL ZIS IS JF
 
Uzalend gani unaoongelea?
Siamini kama wakenya ni wazelendo sana wa nchi yao kupita sisi, siamini wanigeria kama ni wazalendo wa nchi yao sana kupita watanzania. Wakati wa mwalimu tulikuwa wazelendo sana lakini umasikini ulishamili, wakati wa mwalimu tulikuwa na rais makini/asiyejilipizia mali/asiye na makuu baada ya kustafu akaenda kushika jembe la mkono lakini bado umasikini ulishamili.

Kuna kitabu hapa huwa nakiangalia kila siku kinauliza hivi kwanini Tanzania iliyokuwa na just leader(mwalimu) ilikuwa inadidimia kwa umasikini wakati Malysia yenye corrupt leader inaendelea?
Same is true kwa Kenya na Tanzania. Kenya ina corruption nyingi sana kuzidi Tanzania, Nigeria ina corruption kubwa sana lakini wanatuzidi tatizo ni nini?

KWa pretext nyepesi tunasema ni ccm, lakini kwa argument yangu hapo juu ina nullify argument hiyo, ni kweli ccm ni tatizo lakini tatizo la msingi sio ccm. Tatizo lamisngi naona liko miongoni mwa watanzania.
OOOOOOOOOOOOOOhhhhhhhh:A S-fire1:!!!!!!!!!! unaongela tiger, hao hawakuwa walarushwa, kilele za rushwa ilikuwa ni propaganda ya Western and some Asian countries, wale jamaa sera ya bomba sana, hapa BONGO Idd Simba alijaribu kuileta apigwa vita sn ila ni sera iliyonufaisha sna nchi za Mashariki ya Mbali nayo ni sera ya uzawa, hapa mzawa anapewa kipaumbele lkn hapa Bongo kama ulivyosoma kwenye post zingine serikali yetu ipo tayari kumnyiima mzawa mradi hata kama anauwezo na kumpa mgeni, mpaka sasakuna maeneo nchi hii ukifika utastaajabu kuona mgeni kamilikishwa ardhi wakatimbongo anawekewa urasimu kuanzia asb mpaka jioni kupata hiyo ardhi in short tuna pia wivu wa kijinga

Heri mgeni apate kuliko mmatumbi mwenzangu haya ni mawazo ya ajabu kabisa. Back to Tgers hawa jamaa
mean biz at work angalia Chinese, Korea nk, huko ukileta za kuleta wanakutafuna nyama, hiyo sera inatakiwa ije BONGO kutafunana nyama yaani kutokuwa na huruma kwa wezi, walau kwa miaka mitano adabu itarudi. WATUMISHI NI LAZIMA WAISHI KWA JASHO LAO NA SITAHILI ZAO SIO KWA USANII KAMA ILIVYO SASA
 
wanasema serikali isifanye biashara watanzania tunakubali, hivi BP ni shirika la binafsi ? hivi huko kenya serikali haimiliki viwanda/biashara? tujuzane.
mwakaboko umeongea kitu ya msingi mtu amebahatika hela anafungua hoteli, bar,gest na uzembe mwingine vitu vya kujifikirisha na kuleta hela nyingi anaona uvivu, tungekuwa tuna jishughulisha tusingekuwa tunalia bei ya sukari, tunashindwa hata na mauritus!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom