Nkamu
JF-Expert Member
- Dec 14, 2007
- 223
- 84
Mimi ni mhandisi wa ujenzi (Civil Engineer), ambaye nimekuwa katika fani hii kwa miaka ipatayo kumi hivi. Katika kipindi chote hiki, sijaona kampuni ya kitanzania iliyoweza kupata mafanikio na kukua kiasi cha kuweza kushindana na makampuni yanayotoka nje ya nchi.
Nimekuwa nikifikiria sana njia ya kuweza kuzisaidia kampuni hizi ili ziweze kukua lakini sijaweza kupata kitu kilicho halisi ambacho kinaweza kuwa sababu ya kushindwa kufanikiwa na jinsi gani ya kuweza kuepuka changamoto hizo na hatimaye mafanikio.
Nimeona ni vema kuleta hapa jambo hili ili tuweze kufikiria kwa makini na kupendekeza ni njia gani tunaweza kufanikiwa kama taifa katika kuwasaidia wakandarasi wetu waweze kukua.
Nawakaribisha kwa michango yenu yenye tija, karibuni!
Nimekuwa nikifikiria sana njia ya kuweza kuzisaidia kampuni hizi ili ziweze kukua lakini sijaweza kupata kitu kilicho halisi ambacho kinaweza kuwa sababu ya kushindwa kufanikiwa na jinsi gani ya kuweza kuepuka changamoto hizo na hatimaye mafanikio.
Nimeona ni vema kuleta hapa jambo hili ili tuweze kufikiria kwa makini na kupendekeza ni njia gani tunaweza kufanikiwa kama taifa katika kuwasaidia wakandarasi wetu waweze kukua.
Nawakaribisha kwa michango yenu yenye tija, karibuni!