Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Sikutaka kulileta hili lakini inaonekana sina ujanja. Katika kikao kilichopita wabunge wetu wengi walionekana kukerwa zaidi na ripoti za CAG na zile za kamati kuhusiana na mambo mbalimbali. Wizara kadhaa zilinyoshewa kidole na hatimaye mawaziri wake wakaondolewa. Hata hivyo, binafsi naamini hakuna kashfa yenye madhara ya moja kwa moja na ya kudumu kama iliyoko kwenye elimu.
KUanzia elimu ya msingi na sekondari kuna changamoto ambazo kwa kweli ni dhambi kwa watoto wetu. Cha kuudhi zaidi inaonekana wabunge wetu wamekubali hali ilivyo na sijasikia wengi wakitaka waziri wa elimu Bw. Shukuru Kawambwa awajibike pia kama walivyowajibishwa wale wa sekta ya afya. Ni kwanini? Ni kweli hawajaona uovu uliopo kwenye sekta hiyo? ni kweli wabunge wetu hawajaona hali ilivyo kwenye shula za kata na mamia ya shule za msingi vijijini na mijini?
Hivi, inakuwaje Ngeleja anawajibishwa lakini Kawambwa anaachwa? Ni kweli sekta ya nishati ina umuhimu mkubwa kuliko elimu? Ni kweli madhara ya kukosa umeme wa kudumu kwa asilimia 14 ya wananchi wetu ni makubwa zaidi kuliko kukosa elimu bora na mazingira bora kwa asilimia zaidi ya tisini ya watoto wetu? Ni kweli kwamba wabunge wetu hawajasoma ripoti mbalimbali za elimu ambazo zimetolewa na CAG taasisi nyingine.
Kwanini, hata upinzani hauonekani kukerwa na kushindwa kwa sera ya elimu ya serikali ya chama cha mapinduzi na badala yake na wao wako kimya kutaka watu wawajibike? Hivi ni mpaka walimu na wanafunzi nao wagome ndio tutajua kweli kuwa tatizo letu ni kubwa kuliko tunavyodhania?
KUanzia elimu ya msingi na sekondari kuna changamoto ambazo kwa kweli ni dhambi kwa watoto wetu. Cha kuudhi zaidi inaonekana wabunge wetu wamekubali hali ilivyo na sijasikia wengi wakitaka waziri wa elimu Bw. Shukuru Kawambwa awajibike pia kama walivyowajibishwa wale wa sekta ya afya. Ni kwanini? Ni kweli hawajaona uovu uliopo kwenye sekta hiyo? ni kweli wabunge wetu hawajaona hali ilivyo kwenye shula za kata na mamia ya shule za msingi vijijini na mijini?
Hivi, inakuwaje Ngeleja anawajibishwa lakini Kawambwa anaachwa? Ni kweli sekta ya nishati ina umuhimu mkubwa kuliko elimu? Ni kweli madhara ya kukosa umeme wa kudumu kwa asilimia 14 ya wananchi wetu ni makubwa zaidi kuliko kukosa elimu bora na mazingira bora kwa asilimia zaidi ya tisini ya watoto wetu? Ni kweli kwamba wabunge wetu hawajasoma ripoti mbalimbali za elimu ambazo zimetolewa na CAG taasisi nyingine.
Kwanini, hata upinzani hauonekani kukerwa na kushindwa kwa sera ya elimu ya serikali ya chama cha mapinduzi na badala yake na wao wako kimya kutaka watu wawajibike? Hivi ni mpaka walimu na wanafunzi nao wagome ndio tutajua kweli kuwa tatizo letu ni kubwa kuliko tunavyodhania?