Taasisi za Dini zinapinga kuondolewa kwa msamaha wa kodi kwao wakati Shule zao na vyuo vikuu vyao vinatoza gharama kubwa.Je ni haki kuwaondolea msamaha wa kodi kama hawapunguzi gharama za huduma zao? Nawasilisha.
Mi nadhani ungefanya kautafiti kadogo kuona kama kuna uwiano wowote katika suala la gharama vs huduma, then ndio tuanze kujadili... Ni mtazamo wangu tu.
Ningependa sana kumpeleka Mtoto wangu lakini naogopa kwa kipato changu na ada zao zilivyo juu ataishia njiani.Hapa mkuu Magehema ndipo wengi wanapokosea wakati wanafanya comparison!
Ada zinazolipishwa na shule za dini....to me ni ndogo kabisa ukilinganisha na huduma wanazotoa huko! Mimi binafsi nimesoma huko.....bt huduma zinazotolewa acha kabisa! Kwa kifupi...mwanafunzi kuanzia form 1 to 6 anahakikishiwa kuwa na vitabu vyote vya kiada kwenye droo yake, vipindi vyote vinafundishwa, wanahakikisha wapo walimu kwa kila somo, wanafuatilia maendeleo ya mwanafunzi akiwa home au shule, wanatoa mazoezi ya kutosha....ndio maana shule hizi zinafaulisha sana!
So to me ada yao bado ni ndogo sana ukilinganisha na huduma.....!
Mmaroroi kama unamtoto jaribu kumpeleka huko....atavuna kilicho bora!
bila hivyo hawawezi kujiendesha. pia hawajalazimisha mtu kwenda kusoma pale, ni yule mwenye hela tu. they are not making any profit out of it i tell you. wengi wanapiga vita taasisi za dini, kwasababu tu ya wivu na ufahamu mdogo. hapa ndipo utaona ufahamu wa watz walio wengi ulivyo, hasa katika sakata hili lililopelekwa bungeni.
Nadhani point ni kwamba, kama ada ya sekondari ya shirika la kidini (eg. Loyola) ni sawa na ada ya shule binafsi (eg. Mzizima), ni kwanini shule ya kidini isilipe kodi ambayo shule binafsi inalipa? Sidhani kama kuna tofauti ya huduma inayotolewa Loyola na Mzizima.
Ningependa sana kumpeleka Mtoto wangu lakini naogopa kwa kipato changu na ada zao zilivyo juu ataishia njiani.
Hivi ni kodi gani ambayo hizi shule za dini hazilipi? Naomba kuelimishwa.
Nimesoma post zote hapo juu sijaona proper analysis. Unaposema ada kubwa, je, umelinganisha na huduma? Kama hujalinganisha basi bado hujasema chochote. Halafu sijaona mtu aliyetoa takwimu ya hizo ada. Kwa mfano huko St. Marian, St. Margareth, n.k. ada ni shilingi ngapi? Na katika Shule hizo walimu wapo wa kutosha? Vifaa vya kufundishia vipo? Walimu wako committed kiasi gani? Ufaulu wa wanafunzi ukoje? Wanafunzi kimaadili wanafundishwa vizuri? Tafadhali leteni takwimu, otherwise tutakuwa tunajadili kwa hisia hisia tu na tutakuwa kama Mheshimiwa Mkulo alivyokurupuka kufuta misamaha ya kodi lakini baadaye alipoelimishwa akairudisha!
Nadhani point ni kwamba, kama ada ya sekondari ya shirika la kidini (eg. Loyola) ni sawa na ada ya shule binafsi (eg. Mzizima), ni kwanini shule ya kidini isilipe kodi ambayo shule binafsi inalipa? Sidhani kama kuna tofauti ya huduma inayotolewa Loyola na Mzizima.