Kwanini tanzania tuna viongozi wasiojua wanachokifanya?

Nicazius

Senior Member
Feb 6, 2008
143
17
Hivi karibuni kumeibuka kundi kubwa sana la viongozi wa serikali wasiojua nini wanafanya na wala hawana upeo na nini kifanyike kuleta maendeleo badala yake wamekuwa ni watu wa kulalamika kila kukicha bila kujenga hoja.

Mfano: Mbunge mmoja ametoa comment hii kwenye facebook:

Nanukuu

"Hivi ni kweli CHADEMA hawajui sababu za ukweli za mfumuko wa bei Tanzania? Kwa nini wameamua kuzunguka nchi nzima wakitafuta umaarufu wa bei chee kwa ku-take advantage ya uchumi mbovu wa kidunia? Napata wasiwasi kama watu hawa hawajui sababu na miongoni mwao kuna wabunge 'makini! ' Au wamekumbwa na upofu wa kutafuta umaarufu kwa gharama yoyote ile?"

Mwisho wa kunukuu.

Hivi mtu kama huyu, tena mbuge aliyesoma anaweza kulisaidia vipi jimbo lake kuleta maendeleo ikiwa kama upeo wake wa kufikiria na kiasi hiki, na kama wabunge wasomi ndiyo wapo hivi Je wale ambao hawajasoma kabisa watakuwa vipi na ndiyo wanatuwakirisha katika chombo muhimu kama bunge, nashindwa kuelewa nabaki nachanganyikiwa kabisa.

Ndugu zangu JF hebu nisaidieni kumsaidia Mhe. wetu ili aweze kubadirika na kuwasaidia wananchi wake.
 
Kuna wengine wamesema Rais apigwe mawe, na huyo unamuonaje??
 
ndugu..usiogope kuweka link,kama yy (MB) kaimwaga facebuk nadhani tuwekee hapa tumwendee hukohuko....habari za kiintelegensia zinaonesha kwamba Wabunge/viongozi wasio na hoja wala mashiko wengi hukimbilia facebuk...tunataka tuwaendee hukohuko kuwapa-sure!! so tuwekee link plzeee!!tumjue ni nani huyo,usiogope!!
 
Kuna wengine wamesema Rais apigwe mawe, na huyo unamuonaje??

Omr: hiyo habari nimeisoma hapa JF na mpaka sasa hakuna source ya ukweli, Pls nipe link au source inayoonyesha kama Mhe. amesema kauli hiyo... Kama ni ukweli Mhe amesema hakika hayupo sawa hata kidogo na tunahitaji kumweleza kama Watanzania, lakini siwezi kutoa any comment mpaka nipate source ya uhakika, naamini javini tupo wengi ukweli utajulikana.

Bila kutoka nje ya mada, wewe unasemaje kuhusu huyu Mhe kutoa kauli kama hii, tena msomi kuliko mamillioni ya Watanzania... unategemea lolote kutoka kwake kwa kauli kama hizi...
 
ndugu..usiogope kuweka link,kama yy (MB) kaimwaga facebuk nadhani tuwekee hapa tumwendee hukohuko....habari za kiintelegensia zinaonesha kwamba Wabunge/viongozi wasio na hoja wala mashiko wengi hukimbilia facebuk...tunataka tuwaendee hukohuko kuwapa-sure!! so tuwekee link plzeee!!tumjue ni nani huyo,usiogope!!

Sizinga: Sina haja ya kuogopa, kwani sina ugovi naye, ila huu ni ukweli na lazima usemwe. Huyu hapo chini:

Dokta Hamisi Kigwangalla
 
Sizinga: Sina haja ya kuogopa, kwani sina ugovi naye, ila huu ni ukweli na lazima usemwe. Huyu hapo chini:

Dokta Hamisi Kigwangalla
Hamisi anafahamika ni mbunge aliyeingia bungeni kwa mchakakto wa kuomba mkataba wa mgodi jimboni kwake kwa mbwembwe kubwa,na alionekana kuwa na hoja yenye nguvu na ni mwelewa kwa kile akifanyacho
Lakini ktk hili la uchumi nadhani nae amelichukulia kisiasa zaidi kwa kuingia ktk kukemea CDM kutafuta umaarufu,lakini kwa upande wangu ninge mweleza Mh Hamisi kuwa umefika wakati sasa wa Wabunge wasomi kama wao kuwa washauri wazuri wa Mwenyekiti wa chama ili kuweza kufanikisha nchi na serikali yake kuondoka ktk dhahama ya kulaumiwa na wapiga kura wake
Kwa mfano kwa sasa bei za mafuta machafu USA ZIMESHUKA KWA 10%,Na hata bei ya mazo kama kakao na mengine pia yameshuka kwa kasi ile ya ajabu,na imefikia wakati sasa viongozi wa nchi husika wanajiuluza kwa nini hili limetokea na pia wanajiuliza watumie njia ipi kutatua

Tatizo tulilo nalo TZ hatuna hata njia mbadala ya kupambana na huo mfumuko wa bei kwa kuwa watawala wengi wapo ktk biashara na wanafurahia mfumuko wa bei kwani ndio unao wapa utajiliu

Angalia kenya serikali iliamua kupunguza hata bei za mafuta ya taa na nyingine angalau hilo linawapa moyo wapigakura kuwa kuna kazi inafanyika na kwa watawala wetu
Lakini kwa upande wetu hatuna majibu yaliyo sahihi na hata wawakilishi wetu nao wapo ktk kulalamika kana kwamba hawaweza na hawana njia mbadala ya hata kupunguza tatizo

Nilitegemea Mh Hamisi angekuja na hoja ya nini kifanyike ktk kuondokana ama hata kulipunguza hili tatizo tulilonalo,lakini nae na Usomi wake amekuwa mpiga ngoma na mwimbaji amesahahu hata kazi tuliyo mtuma ya kutuwakilisha juu ya kushauri nini kifanyike

Mh mbunge angalia Mbunge wa kagera juzi alikuwa ktk wakati mgumu jimboni kwake si kwa kuwa wapiga kura wanachuki nae la hasha ni kutokana na Kauli zake awali sasa sinamla yeye mwenyewe,ubabaishaji,na longolongo nyingi kuliko vitendo,hivyo vyote vinasababisha wapiga kura wakutolee uvivu na kukueleza kinaga ubaga

Nakuasa Mh jitahidi kuwa na majibu mazuri pindi ukutanapo na wapigakura wako juu ya swala hili la ugumu wa maisha kwani wapiga kura wasasa wanatambuwa mbichi na mbivu,ukileta longolongo na kujifanya kuwa ni mshabiki wa uchumi na sio mtatuwaji wa matatizo ya kiuchumi jiandae kukupambana na nguvu ya maswali ya umma yasiyo vumilika mbele ya macho yako

Mungu ibariki TZ
 
Hivi karibuni kumeibuka kundi kubwa sana la viongozi wa serikali wasiojua nini wanafanya na wala hawana upeo na nini kifanyike kuleta maendeleo badala yake wamekuwa ni watu wa kulalamika kila kukicha bila kujenga hoja.

Mfano: Mbunge mmoja ametoa comment hii kwenye facebook:

Nanukuu

"Hivi ni kweli CHADEMA hawajui sababu za ukweli za mfumuko wa bei Tanzania? Kwa nini wameamua kuzunguka nchi nzima wakitafuta umaarufu wa bei chee kwa ku-take advantage ya uchumi mbovu wa kidunia? Napata wasiwasi kama watu hawa hawajui sababu na miongoni mwao kuna wabunge 'makini! ' Au wamekumbwa na upofu wa kutafuta umaarufu kwa gharama yoyote ile?"

Mwisho wa kunukuu.

Hivi mtu kama huyu, tena mbuge aliyesoma anaweza kulisaidia vipi jimbo lake kuleta maendeleo ikiwa kama upeo wake wa kufikiria na kiasi hiki, na kama wabunge wasomi ndiyo wapo hivi Je wale ambao hawajasoma kabisa watakuwa vipi na ndiyo wanatuwakirisha katika chombo muhimu kama bunge, nashindwa kuelewa nabaki nachanganyikiwa kabisa.

Ndugu zangu JF hebu nisaidieni kumsaidia Mhe. wetu ili aweze kubadirika na kuwasaidia wananchi wake.

Siyo kila anayeitwa kiongozi ni kiongozi. Wengi ni watawala. Mtawala hahitaji kujua matatizo ya watu anaowatawala bali anachotakiwa kujua ni mbinu za kuwatiisha.
 
Back
Top Bottom