NG'OMBE
JF-Expert Member
- Mar 26, 2011
- 362
- 80
Wanajf habari, poleni na shughuli za harakati za maisha. Mimi nauliza ni kwa nini serikali ya JK inaendelea kuwalipa pesa wawazili wa AFYA na naibu wake? Watu hawa wanafanya kazi gani, maana MADAKTARI walimwambia JK bila kumficha kuwa hawatashirikiana nao kwa kazi yoyote ile, na wao ndiyo viongozi wa wizara wanaongoza nani basi?. Mimi ninapata shida sana, sielewi ni nini hasa wanachokifanya hapo wizarani? Kama JK hajapata mbadala wao angeacha wazi basi nafasi hizo hapo angeeleweka kwa watanzania lakilni kwa sasa haeleweki na hataeleweka kwa watanzania yeye na chama chake. Mwisho wa siku wataanza kusema tutafanya tasimini ili tujue tumeshindwaje kwenye uchaguzi. Haya yote watu wanayaona na wanakusanya hasila tu iko siku watafanya jambo ambalo ccm hawataamini kitakachotokea.
MY TAKE: Naomba watanzania wote wapenda haki walisemee suala hilo na hatua zichukuliwe ili kuondoa hali hii.
MY TAKE: Naomba watanzania wote wapenda haki walisemee suala hilo na hatua zichukuliwe ili kuondoa hali hii.