kwanini redio za kiswahil za njei zote zipo kenya?

engmtolera

JF-Expert Member
Oct 21, 2010
5,150
1,437
karibia redio zote zinazo tangaza kwa lugha ya kiswahili zipo kenya,hii inamaanisha nini juu ya hii lugha yetu ya kiswahili?
sasa hata wachina wanaredio yao ya kiswahili ipo kenya,je lugha hii ya kiswahili mwanzo wake ni wapi?
Redio hii ina taarifa, habari, burudani za muziki, vipindi vya salamu na vipindi vingine vingi. Redio hii hurusha matangazo kwa saa nne kwa siku, asubuhi, kisha mchana sita hadi saba na mbili hadi nne usiku (wakati wa habari na salam huu).

hata watangazaji wake ni kutoka Kenya ambao hata kiswahili chenyewe hawajui,kunatatizo gani ktk nchi yetu?

Tovuti ya Radio China Kimataifa inapatikana katika anwani hii china radio international
 
Hapa kwetu HATUELEWEKI, HATUTABIRIKI, HATUTAFSIRIKI. Tuongeacho sicho TUMAANISHACHO. Mizengwe imetuzungu, we are corrupted everywhere. Nilifatilia kwa kina kisa cha radio China kwenda Kenya, MIZENGWE ilisheheni.
 
Hapa kwetu HATUELEWEKI, HATUTABIRIKI, HATUTAFSIRIKI. Tuongeacho sicho TUMAANISHACHO. Mizengwe imetuzungu, we are corrupted everywhere. Nilifatilia kwa kina kisa cha radio China kwenda Kenya, MIZENGWE ilisheheni.

duuuuuuu,kweli mwana usimacho TUONGEACHO SICHO TUMAANISHACHO,kwani nasikia baada ya uchaguzi Serikali ikaanza kuwavalia njuga Radio RAF-Kiswahili na BBC -Kiswahili kuwa wana eneza uchochezi hapo bongo,tumekuwa ni watu wa kujihami sana na wenzetu wanatumia hizo opportunity kupeleka kenya Radio za Kiswahili ambazo zinawapa kazi wananchi wa kenya ktk kutangaza kiswahili

Pia hata hapa china nimeona Hongkong Mwingereza ndio anaye fundisha kiswahili ktk chuo kikuu furani,sasa sielewi tatizo lipo wapi kwa sisi wabongo na nchi yetu kwa ujumla?
 
kwani kiswahili ni cha bongo pekee yake?

lakini ebu angalia ufasaha wa kiswahili ktk east Africa,na vipi kuhusu baadhi vyuo kuwatumia waingereza kufundisha kiswahili,unadhani kuwa labda sisi hatuna uwezo wa kufundisha ama hatuaminiwi kwa hili,hebu sikiliza kiswahili cha huyu mtangazaji china radio international
 
Kule miundombinu imekamilika, halafu historia yetu miaka ile ya kutopenda tamaduni za magharibi iliwazuia wengi kuweka vituo vyao hapa.
 
Kwa sub saharan africa Kenya ndio hub ya mashirika mengi pmoja na south afrka. Kama ilivyo London kwa Euro.
Hii ni kutokana na miundombinu, ubora wa sera za kibiashara na upatikanaji wa qualified staffs.
 
Kwa sub saharan africa Kenya ndio hub ya mashirika mengi pmoja na south afrka. Kama ilivyo London kwa Euro.
Hii ni kutokana na miundombinu, ubora wa sera za kibiashara na upatikanaji wa qualified staffs.

kwahiyo mkuu unamaanisha Tanzania hatuna QUALIFIED STAFFS ktk maswala ya kiswahili hususani ktk swala la utangazaji?
 
Sisi sijui tumelaaniwa? Hata kiswahili tunaonekana hatujui? Ndo maana hata tanzanite ambayo jina lake ni kama la nchi yetu wazungu wanajua inachimbwa kenya.
Nimechunguza sana kuhusu nchi hii nimegundua hatuna mafanikio kwenye nyanja yoyote ukiondoa ukiondoa "big brother africa"
 
Hapa Bongo ilikuwa Idhaa ya Kiswahili ya Uingereza (BBC) iwe na makao yake makuu hapa ktk ukanda wa EA lakini serikali ikaktaa kwa kile kilichoelezwa kwamba ingemulikwa sana na uozo wake kuwekwa hadharani.
 
Hapa Bongo ilikuwa Idhaa ya Kiswahili ya Uingereza (BBC) iwe na makao yake makuu hapa ktk ukanda wa EA lakini serikali ikaktaa kwa kile kilichoelezwa kwamba ingemulikwa sana na uozo wake kuwekwa hadharani.
Kwa mtindo huu tutaendelea kuwa nyuma hadi lini?
 
DAR: kwikwi katika upatikanaji wa wataalamu, umeme wa wasiwasi, miundo-mbinu hohehahe, mkongo wa internet umechelewa, bureaucracy, lack of political will kuwa-attract hawa watu, welfare (housing, entertainment, etc.) bado

NBI: hub ya E & C Africa since English rule, direct flights to most Euro-region, Asia, na N America kupitia KQ, tukubali tukatae hawa watu wametupiga bao kwenye nyanja nyingi tu. They ruthless capitalists who will do aything to get what they want in their place (pride).
 
Kujua kuongea kiswahili siyo qualification
hata hao wachache waliosomea utangazaji kwa lugha ya kiswahili nao matupu

ila sukubaliani nawe kwani kiswahili nikisikiacho Redio Kiswahili China hata msukuma na rafudhi yake ama masai kina afadhari bana
 
Back
Top Bottom