Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Mwaka 1994 mauaji ya kimbari yametoka Rwanda na maelfu ya Wakimbiza walikuwa wamevuka kuja magharibi mwa nchi yetu. Uchaguzi Mkuu wa kwanza wa Rais na Wabunge ndani ya mfumo wa vyama vingi ukafanyika Oktoba 29, 1995. Wakati ule Nyerere alishiriki kumpigia debe Mkapa karibu sehemu mbalimbali nchini ili achaguliwe.
Nakumbuka kampeni ile vizuri zaidi kwani nilikuwepo mmoja wa waangalizi wa Uchaguzi ule. Na nilikuwepo Nyerere alipokuja na kupiga kampeni pale Nyamagana kumnadi Mkapa. Hata hivyo nakumbuka mambo fulani:
a. Hoja yake ilikuwa ni usafi wa kiongozi anayekuja
b. Upinzani ulikuwa bado haujakomaa kuongoza labda wakipewa muda.
c. Sikumbuki hata mara moja kuwa alitumia yaliyotokea Rwanda kuwa ni mfano wa kile kinachoweza kutokea Tanzania ati wakichagua upinzani na nitakuwa tayari kusahihishwa na wengine waliomsikia mahali pengine kwani kama ingekuwepo CCM wangeweza hata kutumia hotuba hiyo kwenye kampeni zao leo hii kwa mafanikio makubwa.
Nabakia najiuliza:
Kama Nyerere ambaye alijua mambo ya Rwanda vizuri sana na alikuwa karibu zaidi kihistoria na matukio hayo hakuweza kutumia hoja ya umwagikaji damu kuwatisha Watanzania wasichague upinzani kwanini hawa watawala wetu wanapata u jasiri huo sasa? What is wrong with this picture?
Nakumbuka kampeni ile vizuri zaidi kwani nilikuwepo mmoja wa waangalizi wa Uchaguzi ule. Na nilikuwepo Nyerere alipokuja na kupiga kampeni pale Nyamagana kumnadi Mkapa. Hata hivyo nakumbuka mambo fulani:
a. Hoja yake ilikuwa ni usafi wa kiongozi anayekuja
b. Upinzani ulikuwa bado haujakomaa kuongoza labda wakipewa muda.
c. Sikumbuki hata mara moja kuwa alitumia yaliyotokea Rwanda kuwa ni mfano wa kile kinachoweza kutokea Tanzania ati wakichagua upinzani na nitakuwa tayari kusahihishwa na wengine waliomsikia mahali pengine kwani kama ingekuwepo CCM wangeweza hata kutumia hotuba hiyo kwenye kampeni zao leo hii kwa mafanikio makubwa.
Nabakia najiuliza:
Kama Nyerere ambaye alijua mambo ya Rwanda vizuri sana na alikuwa karibu zaidi kihistoria na matukio hayo hakuweza kutumia hoja ya umwagikaji damu kuwatisha Watanzania wasichague upinzani kwanini hawa watawala wetu wanapata u jasiri huo sasa? What is wrong with this picture?