Kwanini Nyerere hakumkubali Lowassa?

Posho imenogaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa, inogile posho hiyoooooooooo,kula pesa ya white hair banaaaaaaa
daa huyu jamaa si mchezo kasi yake imekuja juu sana, ANATAKA NINI HUYU MWIZI, wewe si ndo ulisaini mkataba wa jengo la umoja wa vijana??
 
Nyerere alimkataa lowassa kwa vile yeye na baba yake waliuza kijiji kizima na watu ndani huko umachame na baadaye kukimbilia ummasaini ambako walipata hifadhi na kulelewa na familia ya marehemu moringe sokoine. Jeje wajua lowassa ni mchagga wa machame? Jiulize ni kipi kilimfanya abadilishe kabila na kujiita mmasai?

Wamasai hawana tabia za ajabu zikiwemo uroho wa madaraka na wizi wa mali za umma.
 
Ndivyo alivyowatuma Lowassa? Mwambieni amenoa. Lowassa hasafishiki kwa namna yoyote. Mwalimu hakukurupuka alipomuangushia hilo bomu na ukweli utabaki hivyo milele.

Bado hakuna hoja ya maana ya kumpinga Lowasa, wote mnasema kutokana na mazoea ya habari za kusimuliwa magengeni. Chuki haijengi.
 
Nyerere alimkataa lowassa kwa vile yeye na baba yake waliuza kijiji kizima na watu ndani huko umachame na baadaye kukimbilia ummasaini ambako walipata hifadhi na kulelewa na familia ya marehemu moringe sokoine. Jeje wajua lowassa ni mchagga wa machame? Jiulize ni kipi kilimfanya abadilishe kabila na kujiita mmasai?

Wamasai hawana tabia za ajabu zikiwemo uroho wa madaraka na wizi wa mali za umma.

Mkuu naona weye unaishi ktk sayari ya Zebaki!! Hizi habari umeziokota wapi????
 
  • Thanks
Reactions: Wit
Naona hawa watu hawachoki. Kila siku wanakuja na mbinu mpya. Naomba yule mwenye ile makala iliyoandikwa na Mzee Kasori, aliyekuwa msaidizi wa Mwalimu Nyerere aiweke tena hapa.
 
Nyerere alimkataa lowassa kwa vile yeye na baba yake waliuza kijiji kizima na watu ndani huko umachame na baadaye kukimbilia ummasaini ambako walipata hifadhi na kulelewa na familia ya marehemu moringe sokoine. Jeje wajua lowassa ni mchagga wa machame? Jiulize ni kipi kilimfanya abadilishe kabila na kujiita mmasai?

Wamasai hawana tabia za ajabu zikiwemo uroho wa madaraka na wizi wa mali za umma.

acha uongo wewe kama hujui historia za watu si lazima kusema! ni kweli lowassa si mmasai lakini pia si mchaga kama unavyosema! haya stick kwenye topic acha ukabila
 
Lowassa ashachafuka hakuna jinsi hata afanye vp akichaguliwa mgombea ccm basi ccm itamfia mikononi mwake
 
KUNDI LA LOWASSA KUMNANGA MWALIMU NYERERE KABURINI AMA KWELI NGUVU ZA FEDHA HUTIA WATU UKICHAA HATA KAMA NI ZA K-ISHETANI!!!

Enyi madalali wa Mh Lowassa kwa wapiga kura wa nchi hii,

Chezea vitu vyote Tanzania hii kwa kadri utakavyoona ni vema na inafaa LAKINI unapoligusa jina la Mwalimu Nyerere kwa kujadili mizaha kama hii wenye akili hawatolumbana nawe ila walalahoi wengi wa nchi hii hujui tu ni kwa kiasi gani utakua umewatonesha moyoni mbele ya dhuluma za VITENDO VYA KIKATILI VYA MAFISADI vilivyofanya maisha yasiwe maisha tena nchi hii.

Nasema chezeeni Richmond, Dowans, endeleeni kwani mnasita kitu gani hapo; kachezeeni pia Symbioni, TANESCO, chezeeni CCM huko hata jina la Rais Kikwetekaichezeeni huko ILA wa kumnanga Mwalimu Nyerere kwa mambo ya kihayawani humu na kote kwingineko ... be warned, hilo si jina la kuuzia dagaa masokoni. Wana-Lowassa katucheeni zaidi na zaidi kifisadi WaTanzania tulio hai maana pindi utakaporusha tu ka-shilingi kwenye sakafu la kanisa au msikiti tayari WaTanzania tutakua tushasahau yote na kukimbilia haraka haraka kumfungulia mfalme Edward lango la Ikulu Magogoni akatawale!!!!!

Ni nani atakayeweza kukuzuia kitu nchi hii; endelea mkuu kachezee kila kitu, cheza, cheza tu. Hata haya matatizo lukuki ya taifa kulala gizani kila uchao sababu ya makovu ya Richmond yote ni mapambo tu tena ya kujitakia sisi wenyewe. Yale mamilioni 150,000,000/- uliotulazimisha kwa umasikini wetu kukulipa wewe kila siku iendayo kwa Mungu shauri ya ulaghai kwa TANESCO hivi sasa ndio wakati wa kuzitumia kisawasawa kila kona ya nchi hii mpaka kila mtu atakapogundua kwamba kweli kidume nchi hii Edward Lowassa wa Monduli; nunua kila kitu wala usiache wajumbe wote ndani ya CCM mikoa kwa vipapatio vya kuku na ubwabwa, kanunue na tume ya uchaguzi upya, magazeti yote kwa kazi ya fedha si ndio hizo bana! LAKINI kwa kuchezea jina la Mwalimu Nyerere kupitia kwa walevi hawa mtandaoni mkome kabisa!!!!!!!!

Naam, kwa kundi hili linaloongozwa na nguvu za fedha za ki-mashetani, waache kundi la Lowassa wamnange salama Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, WaTanzania tunasubiri kwa hamu kubwa sana tu
KUJA KUONA MWISHO WAKE hizi lugha chafu kama atapona mtu hapo kisiasa. Jibu ni 2015 hata CCMkirongwe vipi na fedha za MAFISADI.

Imani na itikadi kali juu ya siasa ya ujamaa na kujitegemea ni kirusi kilichokuwa kimeathiri kwa kiasi kikubwa mfumo wa ufahamu wa baba wa Taifa mwalimu Nyerere na, kuamini kuwa hakuna kitakachofanya nchi isonge mbele zaidi ya siasa ya ujamaa na kujitegemea. Msimamo uliosababisha chuki kwa wajasiriamali wengi waliojitolea nguvu zao halali kuongeza vipato, mmojawapo akiwa Lowassa.

Chuki ambayo iliibuka wazi wakati wa kinyang'anyiro cha kuwania urais mwaka 1995. Kwa kuwa Nyerere tayari alikuwa ameshajichagulia mtu wa kumrithisha kiti kilichokuwa kinaachwa na mzee wa ruksa. Wengine waliokuwa na nia ya kuwania kiti hicho akawaundia zengwe la kuwaangusha.

Mmoja wa wanasiasa walioathirika na propaganda hizo ni mheshimiwa LOWASSA ambaye hivi sasa mamilioni ya watanzania wanategemea ukombozi wa kweli kutoka kwake. Mwingine aliyeathiriwa na zengwe la NYERERE ni rais wa sasa Mh JM KIKWETE.

Hakuna siri kuwa MKAPA ndiye aliyekuwa chaguo la wazi la mwalimu kiasi cha kutumia kila aina ya ushawishi wake kuhakikisha kuwa LOWASSA na KIKWETE wanaanguka. Kinachosikitisha, zaidi ya miaka 15 imepita sasa bado kuna Watanzania ambao wanaamini kile kilichosemwa na NYERERE dhidi ya LOWASSA.

Propaganda ni kitu kibaya sana, mtu anaweza kuujengea hoja uongo na kuwa ukweli na, watu wakashikilia misimamo wakitetea uongo uliogeuzwa na mwana propaganda kuwa ukweli.

NYERERE alimkataa LOWASSA kwa kisingizio cha kivuli cha ubepari, kwa bahati mbaya wakati huo hakukuwa na mtu wa kumuuliza NYERERE kwa nini hakupambana na ubepari wa LOWASSA wakati wa utawala wake badala yake iwe wakati wa uchaguzi ambao unafanyika mbali na awamu yake ya uongozi? Hapa mtu makini ataamini kuwa propaganda hizo zilikuwa zinaongozwa na chuki binafsi na wala sio uzalendo.

Mtu makini ataamini kuwa NYERERE alikuwa anajua kuwa, ujasiriamali wa LOWASSA haukuwa haramu ndiyo maana hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa dhidi yake.

Ni wakati sasa kwa wale waliorithi habari za mapokeo dhidi ya LOWASSA na kujiaminisha kuwa ni mtu asiyefaa. Wafikirishe akili zao kwa makini na sote kwa pamoja tumuunge mkono mtu huyu iwapo atasimama kwa ajili ya kuomba nafasi ya kuliongoza Taifa hili.
 
Hivi kwanini mnaompinga Lowassa hamna hoja zaidi ya chuki tu?

Hivi Nyerere alimsema Lowassa kwa ubepari wake au kwa kujikusanyia mali nyingi kwa kipindi kifupi na bila ya vyanzo vinavyoeleweka?

Mimi siyo shabiki wa sera za Nyerere hata kidogo lakini penye mantiki lazima apewe credit. Hivi mbona yeye mwenyewe ameshindwa kuueleza Umma hivyo vyanzo vyake vya utajiri au anaogopa kurogwa?
 
Nakupongeza Jumakidogo,kwani yaonesha wazi kabisa wewe ni msemaji mzuri tu.Lakini ulichokiandika kinafaa kutamkwa kuzimu labda hawamfahamu Lowasa.yeye ni mwizi asilia na hakuna njia ya kufanya tabia yake hiyo imtoke hata kama ana nia ya kuacha udokozi.Imeshakuwa kama ngozi sasa na yamfaa akubali kurudi nyumbani aachane na siasa.Na kinachomfanya ang'ang'ane huko bungeni ni kuwa,anatafuta njia ya kujilinda zaidi adui zake wasipate mwanya wa kuhoji chanzo cha mali zake.Ajue kuwa hakuna mmbongo anayempenda na hakuna sababu ya yeye kuchafua magazeti.Yeye asubiri tu aachie ubunge uone wahuni watakavozikomba mali zake.
 
Back
Top Bottom