Game Theory
Platinum Member
- Sep 5, 2006
- 8,545
- 835
Hili ni jambo ambalo ukimuuliza Nyerereist yoyote hatokupa jibu
Mindhali humu kuna GREAT THINKERS naamini tutapata data tuu kwa nini the so called baba wa taifa alimua hii reli ingolewe
Nawasilisha
Swali lililokuwa likiwasumbua watu wa kusini limepatiwa jibu leo bungeni baada ya Mbunge wa viti maalumu (CUF) Mhe.Clara Diana Mwantumu kuhoji sababu za kung'olewa kwa reli ukanda wa kusini?
Jibu lililotolewa ni kwamba reli ilijengwa na wakoloni kwa lengo la kusafirisha zao la karanga kuelekea bandari ya Mtwara, baadaye ikagundulika kwamba hali ya hewa ya mikoa ya kusini isingefanikisha ustawi wa zao hili na kupelekea kampuni ya British Overseas Food production Company kusitisha uwekezaji wake.
Waziri hajataja sababu nyingine zaidi ya hiyo na kumchochea Mhe.Mwantumu kuhoji ilikuwaje ikang'olewa wakati ingesaidia shughuli nyingine kama kusafirisha watu,mizingo na sasa chuma kutoka Liganga na Mchuchuma? Waziri amesema serikali ina mpango wa kujenga reli kutoka Mtwara mpaka Mbamba Bay, pia wanakaribisha wawekezaji wenye interest Kwa kuwa kuna madini ya Nikel watapatikana.
SWALI LANGU: Serikali haikuwa na alternative zaidi ya kung'oa reli?
Nimewahi kusikia kuwa kabla ya uhuru wa Tanganyika kusini mwa Tanzania Mkoa wa Mtwara kuliwahi na Railway line iliokua inaunganisha Mtwara na Wilaya ya Nachingwea. Aiadha mara baada ya uhuru wa Tanganyika serikali ya Mwalimu ikaamua kung'oa reli hiyo na kwenda kujenga reli ya Dar/Moshi.
Kwa ufahamu wangu naamini kuwa wazungu (wakoloni) walioamua kujenga reli hiyo walikua na madhumuni yao kwa mikoa ya kusini mwa Tanganyika.
Lakini mpaka hivi sasa sijui kwa nini Wazungu waliamua kujenga Reli kusini na Kwa nini serikali ya Mwalimu iliamua kung'oa reli hiyo?........Naomba wan jf kwa yeyote ambae ana ufhamu mzuri kuhus hili basi anifahamishe na mimi niongeze ufahamu wangu.....nawakilisha.
View attachment 39504
Swali na hoja hii ni nzuri sana. Project ya karanga Nachingwea ilikuwa baada ya project kama hiyo ya Overseas Food Company (OFC). Kongwa. Naikumbuka sana kwa sababu ndio wakati nilipozaliwa na mzee wangu alikuwa Agromechanic Kongwa akahamishiwa Nachingwea.
Pamoja na project hiyo kuna ile ya kufuga (NARCO) ambayo bado ipo hata baada ya kunyofolewa nyofolewa.
Hoja ni kwamba kuna uwezekano mkubwa tulipopata uhuru, ama makabidhiano ya miundombinu na mali zingine hayakufanywa kwa umakini; ama tulikuwa wachanga mno kutokujali umuhimu wa miundombinu na mali zingine kiasi ambacho hata nyaraka na mipango mbalimbali hatuiihifadhi.
Mifano mibaya inayoniuma sana
1. Master Plan ya Dar es Salaam ikiwa na underground train iliyoextend hadi Kibaha. Holela ya sasa hivi ni uswahili Dar Plan kweli ilikuwa "Heaven of Peace" ya akili na mwili.
2. Infrastructure za kilimo Kongwa zimefukiwa ambazo zilikuwa meant kwa kilimo cha kumwagilia miaka hiyo baada ya vita.
3. Unazungumzia kung'olewa reli ya Nachingwea nawakumbusha reli ya Kongwa wakati huo Kongwa ikiwa na jina la Uingereza
4. Mashule yaliyoachwa nk
Kifupi tunaendeleza tabia ile ile ya uchanga na utoto wa kupata uhuru kwa mizaha mizaha tu. Mipango yote ya uchumi iliyofanyiwa utafiti na Wajerumani na Waingereza tumeizika tunaparamia tu kwa majibu mepesi mepesi. Suala la reli ni la kiuchumi. Unapozungumzia reli, unazungumzia infrastructure yenye kudumu si chini ya maika mia (100); kwa hiyo kuing'oa ni uamuzi unaotakiwa kufanywa kwa umakini sana.
Reli ya Mbamba Bay Mtwara ililenga kuchukua mizigo ya Malawi (makaa ya mawe). Malawi sasa hivi wanapanua ziwa nyasa angalau meli zipakie ndani ya Malawi litokee bahari ya Hindi kupitia Mozambique na kazi imeanza. Lakini tungejikita zaidi kwenye miundombinu inayochochea ukuaji wa uchumi wa ndani ili mengine yawe bonus.
SAMAHANI NAYASEMA YOTE HAYA KWA SABABU KWA KAZI YANGU YA USHAURI SEKTA YA UCHUKUZI KWENYE NCHI ZOTE HIZI LABDA NAFAHAMU MAMBO AMBAYO WATAWALA HAWAYAELEWI NA WALA HAWATAKI KUYAELEWA.
Ila kwenye fani naongozwa na "FACTS YOU DECIDE" na si majibu ya kisiasa uchwara