apprentice1997
Senior Member
- Jun 8, 2016
- 107
- 99
Shikamoni wakubwa wangu,
Mimi ni kijana wa kiume umri wangu ni miaka 19. Nimebakiwa na wiki moja kabla sijayaanza maisha yangu mapya ya kimasomo kama mwanachuo. Natambua kuwa mpaka hapa nilipofikia si mimi bali ni Mungu tu na ninashukuru hata kwa kuendelea kunifichia aibu yangu ya kufanya ngono miaka 2 iliyopita na toka hapo sijafanya tena.
Nina nia ya dhati ya kufanikiwa maishani na pia natamani sana kukua nikiwa na heshima inayotakiwa kwa jamii na pia nikue nikiwa sina scandal za mambo yoyote maovu maishani mwangu. Kiukweli mimi sio mlokole na wala sio mshika dini sana ila ninalitunza neno la Mungu ndani yangu na ninaamini kuwa ni yeye tu anayenitunza hivyo basi mimi ni kijana wa kawaida ila sifanyi mambo ambayo vijana wengi wanayafanya.
Ninamuomba Mungu nisifanye ngono hadi siku nitakapooa nikiamini kuwa sihangaiki na maisha na Mungu atanipatia mtu ambaye atakuwa sahihi kwangu kuliko kuhangaika na watu ambao hawatanijali na kunitesa. Ninatamani kufanya hivi ili niweze kufanikiwa katika masomo yangu na kazi zangu.
Naombeni ushauri wenu jinsi gani nitafanikiwa nia yangu na je. faida zipi nitapata kwa maamuzi haya kama una ushuhuda wowote wa kunitia moyo ningependa kuusikia.
Mbarikiwe.
Cc heaven sent Valentina THT
Mimi ni kijana wa kiume umri wangu ni miaka 19. Nimebakiwa na wiki moja kabla sijayaanza maisha yangu mapya ya kimasomo kama mwanachuo. Natambua kuwa mpaka hapa nilipofikia si mimi bali ni Mungu tu na ninashukuru hata kwa kuendelea kunifichia aibu yangu ya kufanya ngono miaka 2 iliyopita na toka hapo sijafanya tena.
Nina nia ya dhati ya kufanikiwa maishani na pia natamani sana kukua nikiwa na heshima inayotakiwa kwa jamii na pia nikue nikiwa sina scandal za mambo yoyote maovu maishani mwangu. Kiukweli mimi sio mlokole na wala sio mshika dini sana ila ninalitunza neno la Mungu ndani yangu na ninaamini kuwa ni yeye tu anayenitunza hivyo basi mimi ni kijana wa kawaida ila sifanyi mambo ambayo vijana wengi wanayafanya.
Ninamuomba Mungu nisifanye ngono hadi siku nitakapooa nikiamini kuwa sihangaiki na maisha na Mungu atanipatia mtu ambaye atakuwa sahihi kwangu kuliko kuhangaika na watu ambao hawatanijali na kunitesa. Ninatamani kufanya hivi ili niweze kufanikiwa katika masomo yangu na kazi zangu.
Naombeni ushauri wenu jinsi gani nitafanikiwa nia yangu na je. faida zipi nitapata kwa maamuzi haya kama una ushuhuda wowote wa kunitia moyo ningependa kuusikia.
Mbarikiwe.
Cc heaven sent Valentina THT