Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,422
- 911,172
Kwenye hili Mzee Mwanakijiji hatupo pamoja hata kidogo ebu tuangalie hoja yako hii:-
Majimbo haya tuyaite ni majimbo maalumu ambapo wagombea wa upinzani wanamtandao mkubwa sana wa kuweza kulinda kura zao lakini huwezi sasa ukachukulia mifano hii kiduchu ndiyo hali ya upinzani kwenye majimbo yote.
Hoja hizi haziwazuii mawakala na wasimamizi ambao siyo waaminifu kuiba kura kwa kutoyaheshimu matoeko ya hesabu za kura na kumbeba mgombe asiyekubalika ili mradi tu ana uwezo wa kifedha.
Hivyo hoja zako juu ya uhimili wa Mahakama haupo kabisa kwa sababu hakuna hoja zilizowahi kwenda mahakamani kuchunguza kama kweli fomu ya majumuisho ya kura ndiyo iliyo na matokeo halisi ya kura kama zilivyopigwa kwa maana ya kuhakikiwa.
Hivyo hoja zako hizi hapa chini ambazo hazijawahi kupimwa na mahakama zetu hazitusaidii sana katika kutuongezea ufahamu wetu wa nafasi ya mahakama zetu katika kuthibitisha uchakachuaji wa matokeo:-
Njia mbadala ya kuchakachua matokeo ni ile ya kuingiza kura za bandia baada ya kura kuhesabiwa kwenye vituo. Hili zamani kwetu uwezekano ulikuwa haupo lakini sasa lawezakana sana baada ya NEC kufuta utaratibu wa wapigakura kuwepo mita 200 kutoka kwenye eneo la kupiga kura.
Wapigakura wangeliweza kabisa kuzuia maboski ya kura yasiingizwe kwenye vyumba vya kupigia kura na ieleweke wenye miliki wa chaguzi si vyama vya siasa ila ni raia wote hivyo hoja za kuvimilikisha vyama vya siasa miliki hiyo kama ulivofanya hapa chini si sahihi hata kidogo:-
Mtu yeyote ambaye anaweza kutumia muda kufikiri ataona kuwa kama kuna wakati ambapo CCM ilihitaji kuiba kura ni katika uchaguzi wa Dr. Slaa ambapo mara tatu amewaangusha Karatu (na madiwani akapata), Uchaguzi wa Mzee Ndesamburo (Moshi Mjini) au hata uchaguzi wa Arfi kule Mpanda Mashariki. Katika sehemu zote hizo CCM ilikuwa na sababu kubwa zaidi ya kuiba kura kuliko majimbo mengi nchini, kama kweli upo wizi wa kura, kwanini sehemu hizi nyingine na muhimu wameshindwa?
Siyo hapo tu, kama kweli Kura zingekuwa zinaibwa kirahisi hivyo, kwanini wameshindwa kuiba kura Pemba ambapo CUF imeendelea kutesa kwa miaka 15 sasa tangu mfumo wa vyama vingi uende na kwanini kura za Jimbo la Darajani (ambalo nadhani sasa limegawanywa - niko tayari kusahihishwa) haziibwi na matokeo yake zinakuwa za karibu sana?
Majimbo haya tuyaite ni majimbo maalumu ambapo wagombea wa upinzani wanamtandao mkubwa sana wa kuweza kulinda kura zao lakini huwezi sasa ukachukulia mifano hii kiduchu ndiyo hali ya upinzani kwenye majimbo yote.
Hoja hizi haziwazuii mawakala na wasimamizi ambao siyo waaminifu kuiba kura kwa kutoyaheshimu matoeko ya hesabu za kura na kumbeba mgombe asiyekubalika ili mradi tu ana uwezo wa kifedha.
Kwenye uchaguzi wa jimbo la Starehe nchini Kenya, Askofu Magreth Wanjiru ndiye aliyetangazwa kuwa alikuwa ni mshindi wa jimbo hilo wakati ambapo mgombea wa PNU Bw. Maina Kamana alipoenda mahakamani na kudai kura zirudiwe kuhesabiwa ndiyo ikaja kubainika ya kuwa kumbe Askofu Magreth Wanjiru hakushinda kiti kile mbali ya kuwa tayari alikwisha kuapishwa hata kuwa Naibu Waziri.Kwanza kabisa, ieleweke kuwa kura zinapigwa, kuhesabiwa na matokeo yake kutangazwa kituoni (kwa kura za wabunge). Hii ina maana ya kwamba, mwisho wa kura washindi wa kila kituo watajulikana kituoni hapo kwa utaratibu uliowekwa wazi ambapo fomu mbalimbali zinatakiwa kujazwa mbele ya watu wote.
Masanduku yanaletwa kituoni na yote yanakuwa na mihuri (seals). Mihuri inapovunjwa kwa utaratibu maalum na mbele ya watu wote (wawakilishi wa vyama, waangalizi wa ndani na wa kimataifa kama wapo). Masanduku yakishafunguliwa hayahami tena hadi mwisho wa kura na kuhesabu kura na hayaruhusiwi kabisa kutoka hata kwenye jengo yalipo. Masanduku hufunguliwa hadharani, wawakilishi wa wagombea na waangalizi wanaruhusiwa kuyakagua si kwa macho tu hata kwa kuyashika na kuyapapasa ili waone kuwa hayaharibiwa au kuchezewa, wakisharidhika na hatua zote za ufunguzi wawakilishi wote hujaza fomu ya kuonesha kuwa wameridhishwa. Masanduku huwekwa mahali pa kupigia kura ambapo panampa mtu hifadhi. Lazima yawe mahali ambapo yanaweza kuonekana, hivyo hayawezi kuwekwa kwenye chumba kilichofichwa.
Hivyo hoja zako juu ya uhimili wa Mahakama haupo kabisa kwa sababu hakuna hoja zilizowahi kwenda mahakamani kuchunguza kama kweli fomu ya majumuisho ya kura ndiyo iliyo na matokeo halisi ya kura kama zilivyopigwa kwa maana ya kuhakikiwa.
Hivyo hoja zako hizi hapa chini ambazo hazijawahi kupimwa na mahakama zetu hazitusaidii sana katika kutuongezea ufahamu wetu wa nafasi ya mahakama zetu katika kuthibitisha uchakachuaji wa matokeo:-
Uchakachuaji wetu wa matokeo huwa sana sana ni kughushi fomu ya matokeo na kumtangaza mgombea ambaye wapigakura walimkataa. Kwa kufanya hivyo wanakuwa wasimamizi na mawakala wameshirikiana katika kupika matokeo kwa manufaa yao wenyewe ya kuhongwa. Hata wewe hili umeliona kama ulivyosema hapa chini:-Ipo imani ambayo imejengeka kuwa ni rahisi kwa kikundi cha watu au watu kuiba kura na kumuongezea mtu mwingine kura kinyume cha sheria. Watu wenye imani hii (naiita imani kwani hakuna ushahidi wowote kuwa kura zimewahi kuibwa, yaani ushahidi unaoweza kusimama Mahakamani!) huwa na wasiwasi kuwa uchaguzi unapofanyika basi kuna makundi ya watu ambayo yanakula njama kuiba kura na kubadilisha matokeo.
Njia hii wapigakura hatuna sauti nayo sana kwa sababu hatumo ndani ya vituo vya kupigia kura ambako huwa kura zinahesabiwa kama wenzetu wa Kenya.Lakini, kura zaweza kuchezewa lakini ili zichezewe kunahitaji ushirika wa zaidi ya mtu mmoja. Yaani, msimamizi wa kituo, wawakilishi wa wagombea, waangalizi wa ndani na wa nje na vile vile wapiga kura wenyewe.
Njia mbadala ya kuchakachua matokeo ni ile ya kuingiza kura za bandia baada ya kura kuhesabiwa kwenye vituo. Hili zamani kwetu uwezekano ulikuwa haupo lakini sasa lawezakana sana baada ya NEC kufuta utaratibu wa wapigakura kuwepo mita 200 kutoka kwenye eneo la kupiga kura.
Wapigakura wangeliweza kabisa kuzuia maboski ya kura yasiingizwe kwenye vyumba vya kupigia kura na ieleweke wenye miliki wa chaguzi si vyama vya siasa ila ni raia wote hivyo hoja za kuvimilikisha vyama vya siasa miliki hiyo kama ulivofanya hapa chini si sahihi hata kidogo:-
Kauli zako za kutubeza wenye hofu na mfumo uliopo zinakera na kusikitisha mno kwa sababu tupo kwa ajili ya vizazi vijavyo na wala siyo kwa mahitaji yetu wenyewe:-Chadema imepewa nafasi ya kihistoria kushinda uchaguzi, ilijua kwa miaka mitano kuwa mwaka huu kutakuwa na uchaguzi na inajua taratibu zote za uchaguzi - hivyo walitakiwa wawe wamejiandaa vya kutosha. Kama hawakujiandaa vya kutosha kupata wawakilishi wa kutosha kwenye kila kituo hili si tatizo la NEC wala CCM! Chadema inahitaji kushinda kisiasa kwa kuwafanya watu wengi wakipigie kura kwani ni kura zilizopigwa tu NDIZO zinazohesabiwa siyo zinazoombewa, kunuiwa au kusubiriwa mawazoni.
Ukweli ni kuwa wenye hofu hii ya "wizi wa kura" ni kwamba hawajui upigaji kura wetu ulivyo na kwanini hatua zilizochukuliwa mwaka huu na Tume ya Taifa ya Uchaguzi zitachangia sana kuondoa wasiwasi wa wizi wa kura.