Byendangwero
JF-Expert Member
- Oct 24, 2010
- 871
- 56
Rais wa China yuko Marekani kwa ziara rasmi na jioni hii rais Obama atamwandalia dhifa ya kitaifa, hii itakuwa ni mara yake ya tatu tangu aingie madarakani kufanya hivyo. Viongozi wengine wote wanaofanya ziara rasmi Marekani kwa kawaida anawaandalia cha kawaida "working lunch". Kwetu hapa kila kiongozi wa nchi anayefanya ziara rasmi hapa nchini uandaliwa dhifa ya kitaifa; hivyo kwa mwaka mmoja uandaliwa dhifa nyingi za kitaifa. Tunashindwa nini kujifunza kutoka kwa wenzetu juu ya matumizi mazuri ya raslimali ya nchi.