Kwanini Nassari atashinda kwa 65%?

EasyFit

JF-Expert Member
Jul 4, 2011
1,269
1,082
Amezaliwa pale,
Ni mwenyeji wa pale wazee kwa vijana wanamjua,
Anakubalika hata na wazee wa CCM.

.......................................
attachment.php

Mfuasi wa CCM, Ester Leusha akimuombea dua Mgombea Ubunge Jimbo la Arumeru Mashariki, Joshua Nassari baada ya kumaliza kuongea na wananchi wa kijiji hicho jana na kuwaomba wampigie kura katika uchaguzi mdogo wa jimbo hilo.
MJANE wa mpigania Uhuru wa Tanganyika, Nderetwa Kirilo (85), amekutana na mgombea ubunge wa Chadema katika uchaguzi mdogo wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari na kumshika kichwa kama ishara ya kumkubali na kumtaka kulinda haki za Wameru kama alivyokuwa mume wake Japhet Kirilo.

Akizungumza jana nyumbani kwake katika Kata ya Poli, mara baada ya kukutana na Nassari, Nderetwa alisema, atamkubali hata kama ni mgombea Ubunge kwa tiketi ya chama kingine ambacho sio tawala, ili mradi alete maendeleo kwa watu wa Meru.

Alisema mume wake Kirilo aliyezaliwa mwaka 1921 na kufariki Mei 30, 1997 alishirikiana na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere na hata wakati mwingine alilala kwake wakiwa katika harakati za kudai uhuru wa Tanganyika.

Alikumbushia kuwa Wameru walichangisha fedha walizoweka ndani ya chungu maalumu na kumwezesha Kirilo kwenda Umoja wa Mataifa (UN) kudai haki ya ardhi ya Wameru.

Alisema kuwa mume wake aliyeacha udaktari na kuingia katika siasa, alikuwa mwanaharakati wa siasa aliyetetea watu wa Meru, ambao walimchangia kwa moyo mmoja na kupata nauli ya kwenda UN kudai ardhi ya Wameru.

"Nassari amejitokeza katika siasa na kugombea nafasi hii ya kutuwakilisha mimi nambariki ili Mungu amtangulie na akienda bungeni awe chachu kwa kutetea ardhi ya Wameru," alisema.

Nassari alimshukuru Nderetwa na kumuahidi kuendeleza aliyoasisi Kirilo kwa kutetea haki za Wameru hasa katika suala la ardhi.

Akiomba kura katika kata ya Songoro, katika kijiji cha Sura na kijiji cha Ndatu, alisema kuwa endapo atachaguliwa atawatetea bungeni kuhakikisha fedha zilizoliwa na wajanja za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Sh milioni 26 za ujenzi wa barabara ya Nkoakirika hadi kijiji cha Sura zinapatikana na kufanya kazi iliyokusudiwa.

Gazeti la HabariLeo
 
Huu utabiri kiboko aise!! Yaani kushikwa kichwani tu tayari atashinda kwa 65% hata Sheikh Yahya hakufikii.
 
(1)Anatokea chama makini kisicho na mafisadi,
(2)Wananchi wamechoshwa na CCM kwa wizi,unyonyji,uuwaji,uonevu nk.
 
Amezaliwa pale,
Ni mwenyeji wa pale wazee kwa vijana wanamjua,
Anakubalika hata na wazee wa CCM.

.......................................
attachment.php

Mfuasi wa CCM, Ester Leusha akimuombea dua Mgombea Ubunge Jimbo la Arumeru Mashariki, Joshua Nassari baada ya kumaliza kuongea na wananchi wa kijiji hicho jana na kuwaomba wampigie kura katika uchaguzi mdogo wa jimbo hilo. Picha na Edwin Mjwahuzi
To be honest in relation to the current wave of politics and globe, these are not constructive logic and standing point.
 
Amezaliwa pale,
Ni mwenyeji wa pale wazee kwa vijana wanamjua,
Anakubalika hata na wazee wa CCM.

.......................................
attachment.php

Mfuasi wa CCM, Ester Leusha akimuombea dua Mgombea Ubunge Jimbo la Arumeru Mashariki, Joshua Nassari baada ya kumaliza kuongea na wananchi wa kijiji hicho jana na kuwaomba wampigie kura katika uchaguzi mdogo wa jimbo hilo. Picha na Edwin Mjwahuzi

vice versa also is true
 
Amezaliwa pale,
Ni mwenyeji wa pale wazee kwa vijana wanamjua,
Anakubalika hata na wazee wa CCM.

.......................................
attachment.php

Mfuasi wa CCM, Ester Leusha akimuombea dua Mgombea Ubunge Jimbo la Arumeru Mashariki, Joshua Nassari baada ya kumaliza kuongea na wananchi wa kijiji hicho jana na kuwaomba wampigie kura katika uchaguzi mdogo wa jimbo hilo. Picha na Edwin Mjwahuzi

vice versa also is true
Kenge lisilotaga
 
MJANE wa mpigania Uhuru wa Tanganyika, Nderetwa Kirilo (85), amekutana na mgombea ubunge wa Chadema katika uchaguzi mdogo wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari na kumshika kichwa kama ishara ya kumkubali na kumtaka kulinda haki za Wameru kama alivyokuwa mume wake Japhet Kirilo.

Akizungumza jana nyumbani kwake katika Kata ya Poli, mara baada ya kukutana na Nassari, Nderetwa alisema, atamkubali hata kama ni mgombea Ubunge kwa tiketi ya chama kingine ambacho sio tawala, ili mradi alete maendeleo kwa watu wa Meru.

Alisema mume wake Kirilo aliyezaliwa mwaka 1921 na kufariki Mei 30, 1997 alishirikiana na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere na hata wakati mwingine alilala kwake wakiwa katika harakati za kudai uhuru wa Tanganyika.

Alikumbushia kuwa Wameru walichangisha fedha walizoweka ndani ya chungu maalumu na kumwezesha Kirilo kwenda Umoja wa Mataifa (UN) kudai haki ya ardhi ya Wameru.

Alisema kuwa mume wake aliyeacha udaktari na kuingia katika siasa, alikuwa mwanaharakati wa siasa aliyetetea watu wa Meru, ambao walimchangia kwa moyo mmoja na kupata nauli ya kwenda UN kudai ardhi ya Wameru.

"Nassari amejitokeza katika siasa na kugombea nafasi hii ya kutuwakilisha mimi nambariki ili Mungu amtangulie na akienda bungeni awe chachu kwa kutetea ardhi ya Wameru," alisema.

Nassari alimshukuru Nderetwa na kumuahidi kuendeleza aliyoasisi Kirilo kwa kutetea haki za Wameru hasa katika suala la ardhi.

Akiomba kura katika kata ya Songoro, katika kijiji cha Sura na kijiji cha Ndatu, alisema kuwa endapo atachaguliwa atawatetea bungeni kuhakikisha fedha zilizoliwa na wajanja za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Sh milioni 26 za ujenzi wa barabara ya Nkoakirika hadi kijiji cha Sura zinapatikana na kufanya kazi iliyokusudiwa.

Gazeti la Habari Leo.
 
Back
Top Bottom