Mara nyingi tumesikia na kuona marehemu akipewa sifa chungu mzima. Sasa nauliza, kwa nini iwe ni baada ya kufa?
Maana huyu mtu utakuta tumeishi naye kwa muda mrefu sana na wala hatukuwahi kumwambia kama yeye ni mtu muhimu sana kwenye jamii, hatukuwahi kumwambia kwamba akifa pengo lake haliwezi kuzibika n.k.
Ila akishakufa tu, tunaibua sifa nyiiiiiiiingi, ambazo kama tungemueleza kabla bila shaka angefurahi sana na angeweza baadhi ya sifa kuzikataa kwamba tunamvisha kilemba cha ukoka ama tunajipendekeza kwake.
Hivi hawa mafisadi papa siku yeyote akifa {kila mtu kuna siku atakufa}, tutegemee kusikia sifa nzuri tu kwao au hata mbaya zitatajwa?
Mimi naona kwamba ni unafiki tu umetuzidi.
Maana huyu mtu utakuta tumeishi naye kwa muda mrefu sana na wala hatukuwahi kumwambia kama yeye ni mtu muhimu sana kwenye jamii, hatukuwahi kumwambia kwamba akifa pengo lake haliwezi kuzibika n.k.
Ila akishakufa tu, tunaibua sifa nyiiiiiiiingi, ambazo kama tungemueleza kabla bila shaka angefurahi sana na angeweza baadhi ya sifa kuzikataa kwamba tunamvisha kilemba cha ukoka ama tunajipendekeza kwake.
Hivi hawa mafisadi papa siku yeyote akifa {kila mtu kuna siku atakufa}, tutegemee kusikia sifa nzuri tu kwao au hata mbaya zitatajwa?
Mimi naona kwamba ni unafiki tu umetuzidi.
Last edited: