Kwanini Mkapa hakuzungumzia EPA hadharani

Mongoiwe

JF-Expert Member
Feb 26, 2008
524
263
Kuna taarifa zinasema kuwa; Mkapa baada ya kusakamwa sana na UFISADI, siku moja akiwa nje ya nchi, alikutana na Mwandishi mmoja ambaye alikwenda huko kwa ajili ya kupokea Tuzo, baada ya kusalimiana walialikana katika Mgahawa na kunywa Chai ambapo Mazungumzo yao baada ya kujuliana hali yalikuwa hivi;

Mkapa: Vipi Siasa za kwetu, hali ikoje.
Mwandishi: Zipo zinaendelea tu.
Mkapa: Hongera kwa kuchukua tuzo, kwani huu ndiyo uandishi niliokuwa nikiusema wakati wa utawala wangu ila hamkunielewa tu.
Mwandishi: Asante. mbona umekuwa kimya sana.
Mkapa: Ahaa! Nimeamua, tena wewe si mwandishi bwana sasa leo nakupa mtihani. naomba Muulizeni Kikwete anaifahamu vipi EPA?
Mwandishi: Kwani ilikuwaje mkuu?
Mkapa: Unajua mie nikiwa Madarakani, Kikwete alikuwa akitambulika ndani ya UWT kwa Codename ya 'Malaika'. Siku Moja kabla ya kuingia katika Uteuzi wa wagombea wa Chama, nilifuatwa na watu wa Usalama na kuambiwa kuwa Malaika atashinda. Sikuwa namtaka awe kiongozi kwa vile nilimfahamu, lakini watu wa Usalama wakaniambia, Mzee hamna namna kwani ameshakamata mfumo wote wa chama na baadhi ya UWT, Jeshi na sekta muhimu, hivyo wakanitaadharisha kwamba iwapo nitamzuia nchi itayumba. Nilishangaa lakini sikuwa na namna zaidi ya kuinusuru nchi, niliwasiliana na wazee katika chama na kuamua kukubaliana nao kuiepusha nchi katika matatizo.
Lakini siki chache baada ya Dodoma kumpitisha Malaika, nilifuatwa na maofisa wake na kuelezwa kuwa Malaika alikuwa akitaka fedha kwa ajili ya kampeni, Ukweli nilimaka, na kuhoji nitazipata wapi. Wakanieleza amesema zipo BoT. Niliamua kumuuliza gavana (Balali) kwa simu, kuwa Chama kilikuwa kikitaka fedha kwa ajili ya Uchaguzi, Balali akajibu hakukuwa na fedha.
Kutokana na majibu hayo Malaika akamfuata Mkapa na kumueleza anajua kila kitu na kwamba kulikuwa na Fedha za malipo ya nje alikuwa akiomba hizo kwa ajili ya kampeni za chama. Nikamueleza Balali ambaye alisema fedha hizo haziwezi kutolewa mpaka kuwepo na doccument, baada ya majibu hayo kufikishiwa Malaika na watu wake walifika na kuwasilisha doccument kwa Balali na kuzitoa fedha hizo.
Mwandishi: Duh...inamaana EPA alicheza Malaika?
Mkapa: Ndiyo maana nakutaka ukipata nafasi muulizeni Kikwete anaijua vipi EPA?

Source: Habari hii nimeisikia kwa mwandishi mmoja nchini aliyewahi kushinda Tuzo akimsimlia mtu wangu mmoja wa Karibu nami.
 
Mhm..!
Ina maana watu wa 'Malaika' wana info za ndani kuliko hata Gavana wa BOT...system inahitaji major overhaul.
 
kuna taarifa zinasema kuwa; mkapa baada ya kusakamwa sana na ufisadi, siku moja akiwa nje ya nchi, alikutana na mwandishi mmoja ambaye alikwenda huko kwa ajili ya kupokea tuzo, baada ya kusalimiana walialikana katika mgahawa na kunywa chai ambapo mazungumzo yao baada ya kujuliana hali yalikuwa hivi;

mkapa: vipi siasa za kwetu, hali ikoje.
mwandishi: zipo zinaendelea tu.
mkapa: hongera kwa kuchukua tuzo, kwani huu ndiyo uandishi niliokuwa nikiusema wakati wa utawala wangu ila hamkunielewa tu.
mwandishi: asante. Mbona umekuwa kimya sana.
mkapa: ahaa! Nimeamua, tena wewe si mwandishi bwana sasa leo nakupa mtihani. Naomba muulizeni kikwete anaifahamu vipi epa?
mwandishi: kwani ilikuwaje mkuu?
mkapa: unajua mie nikiwa madarakani, kikwete alikuwa akitambulika ndani ya uwt kwa codename ya 'malaika'. Siku moja kabla ya kuingia katika uteuzi wa wagombea wa chama, nilifuatwa na watu wa usalama na kuambiwa kuwa malaika atashinda. Sikuwa namtaka awe kiongozi kwa vile nilimfahamu, lakini watu wa usalama wakaniambia, mzee hamna namna kwani ameshakamata mfumo wote wa chama na baadhi ya uwt, jeshi na sekta muhimu, hivyo wakanitaadharisha kwamba iwapo nitamzuia nchi itayumba. Nilishangaa lakini sikuwa na namna zaidi ya kuinusuru nchi, niliwasiliana na wazee katika chama na kuamua kukubaliana nao kuiepusha nchi katika matatizo.
Lakini siki chache baada ya dodoma kumpitisha malaika, nilifuatwa na maofisa wake na kuelezwa kuwa malaika alikuwa akitaka fedha kwa ajili ya kampeni, ukweli nilimaka, na kuhoji nitazipata wapi. Wakanieleza amesema zipo bot. Niliamua kumuuliza gavana (balali) kwa simu, kuwa chama kilikuwa kikitaka fedha kwa ajili ya uchaguzi, balali akajibu hakukuwa na fedha.
Kutokana na majibu hayo malaika akamfuata mkapa na kumueleza anajua kila kitu na kwamba kulikuwa na fedha za malipo ya nje alikuwa akiomba hizo kwa ajili ya kampeni za chama. Nikamueleza balali ambaye alisema fedha hizo haziwezi kutolewa mpaka kuwepo na doccument, baada ya majibu hayo kufikishiwa malaika na watu wake walifika na kuwasilisha doccument kwa balali na kuzitoa fedha hizo.
Mwandishi: Duh...inamaana epa alicheza malaika?
mkapa: ndiyo maana nakutaka ukipata nafasi muulizeni kikwete anaijua vipi epa?

source: habari hii nimeisikia kwa mwandishi mmoja nchini aliyewahi kushinda tuzo akimsimlia mtu wangu mmoja wa karibu nami.
duuu jamani habari hizi! Mbona nzito sana!
 
Mhm..!
Ina maana watu wa 'Malaika' wana info za ndani kuliko hata Gavana wa BOT...system inahitaji major overhaul.


Mjenga nchi ni mwananchi na mvunja nchi ni mwananchi, ukimuona utadhani kweli ni mwema lkn haya tunayoyasikia uvunguni yatasema uwanjani sikumoja ukweli na uwazi utafanyika ushahid, watajisema kidogkidogo, tutawakamata tu we ngoja.
 
Huyu the so called Kikwete (Malaika) inabidi adhibiwe, aliupata urais kwa njia chafu sana, halafu hana lolote jipya alilokuwa anataka kufanya. Alichotaka kuingia kwenye historia ya nchi kuwa naye amewahi kuwa rais!

Watanzania wenzangu adhabu yake ni kutokumchagua hili litakuwa fundisho kwa hata viongozi wajao!

Marafiki zangu na familia yangu (20) tunamchagua Dr Slaa wewe je una wangapi? Muda haujaisha ongea na walio karibu yako waeleze umuhimu wa kutomchagua huyu mkwere!

NN
 
Mhm..!
Ina maana watu wa 'Malaika' wana info za ndani kuliko hata Gavana wa BOT...system inahitaji major overhaul.

I'm not sure, Malaika was Foreign minister by then and the money was in the External payment accounts. Malaika may had all clues about the payments. Mind you those were surrendered loans by different foreign companies. Then, they plotted to pay local ghost companies as agents of foreign companies. Doesn't make sense?. Kwa Malaika kuamua kuwasamehe waliorejesha pesa, inatoa taswila hiyo hiyo kuwa anaweza kuwa muhusika muhimu katika sakata hilo.
 
Looks like a true story to me, Kikwete anauchu mno wa madaraka! Basi hata angekuwa anaweza, he is a complete naive.

Yeye kwake urais ni show off hajui kuwa ni kazi ya kuweka misingi na dira ya maendeleo ya Tanzania.

Ananiumiza kichwa sana huyu jamaa.
 
It is a great revelation close to ultimate truth. Only problem is how to share it with the public with a reliable public source
 
Kuna taarifa zinasema kuwa; Mkapa baada ya kusakamwa sana na UFISADI, siku moja akiwa nje ya nchi, alikutana na Mwandishi mmoja ambaye alikwenda huko kwa ajili ya kupokea Tuzo, baada ya kusalimiana walialikana katika Mgahawa na kunywa Chai ambapo Mazungumzo yao baada ya kujuliana hali yalikuwa hivi;

hapo kwenye bold mkuu....

kwa kiswahili cha shule zetu za kata..huo ni uvumi ambao mwenye kuleta hiyo taarifa hana uhakika na anachokisema na kujivua liability ndiyo anatumia kiswahili hicho...

kwa mantiki hiyo sidhani kama tuna haja sana ya kuchangia uvumi...

amma kwa kuongezea ni kuwa iliwahi kuandikwa katika mwanahalisi wakati habari hizi za EPA zikiwa ni moto kuwa kagoda iliwahi kuchotewa 8 bilions kabla ya uchaguzi wa mwaka 2000 kipindi hicho malaika akiwa fa na Ben akigombea miaka mitano ya mwisho na hizo 8bn zilitumiwa kupata ushindi wa mafuriko wa Ben mwaka 2000. kumbuka hakuna amabaye amewahi kukanusha habari ile ya mwanahalisi.

ukiunganisha habari hizi mbili unachokiona ni kuwa wote wawili wana mkono katika EPA bahati mbaya ni kuwa kwa sasa kuna juhudi zinafanywa na baadhi ya wa-tz kwa sababu wanazozijua kutaka kumsafisha Ben...

tusubiri tuone mwisho wa haya..........time will tell:A S angry:
 
Marafiki zangu na familia yangu (20) tunamchagua Dr Slaa wewe je una wangapi? Muda haujaisha ongea na walio karibu yako waeleze umuhimu wa kutomchagua huyu mkwere!NN

great thinker au great stinker?????

karne ya 21 unaongelea ukabila...hii ni unaccepatable stereotyping....

tujaribu kuwa objective kidogo na kuacha kujadili watu!!!!!!
 
umbeya huo na fitina zenu sasa munataka kumsafisha mkatoliki wenu mkapa kuwa hahusiki na ufisadi!!!!! Wacheni unafiki na kutuletea habari zisizo na chanzo na zenye harufu ya uoga!!!

imekuaje mkapa azungumzie epa akiwa nje ya nchi! Mbona akiwa nyumbani hafungui domo lake na zaidi tunaambiwa tumwache mzee apumzike!!!

habari hiyo imekaa kiumbea umbea na hata alieileta anaonekana amekaa kiumbea umbea!!!!!
 
great thinker au great stinker?????

karne ya 21 unaongelea ukabila...hii ni unaccepatable stereotyping....

tujaribu kuwa objective kidogo na kuacha kujadili watu!!!!!![/QUOTE

Bro mbona mkali hivyo?...kama ndugu zake wamemuambia watampigia kura Dr. Slaa kivipi unakuwa ukabila tena?
 
umbeya huo na fitina zenu sasa munataka kumsafisha mkatoliki wenu mkapa kuwa hahusiki na ufisadi!!!!! Wacheni unafiki na kutuletea habari zisizo na chanzo na zenye harufu ya uoga!!!

imekuaje mkapa azungumzie epa akiwa nje ya nchi! Mbona akiwa nyumbani hafungui domo lake na zaidi tunaambiwa tumwache mzee apumzike!!!

habari hiyo imekaa kiumbea umbea na hata alieileta anaonekana amekaa kiumbea umbea!!!!!

Hiyo bold ni evidence ya udini.
 
Hizi habari nilishazisikia tangu mwaka 2008 nilipokuja kuwaona ndugu zangu pale Dar.

Jamaa yangu mmoja aliniambia jinsi Mkapa alivyotishwa na Wanamtandao na hata Sumaye.

Habari zinadai kuwa miezi 9 kabla Mkapa hajaondoka, Mtandao walishashika nchi.

Inasikitisha tu kuwa Mkapa kama Rais, ilikuwaje AKAPINDULIWA bila ya yeye kufahamu?

Kwa maana nyingine, Kikwete ni Rais sasa karibu mwaka wa sita na si wa tano kwani ilikuwa ni kumalizia tu formalities ila jamaa alishakuwa Rais hata kabla hajachaguliwa.

Mkapa kwa haya mambo ndiyo maana wengi wanamchukia. Kuna wengine wanasema hata Kiwira ni ndugu zake walimuingiza Mkenge. Wengine wanadai Ufisadi mwingi ulifanywa na Mkewe. Sijui kwa haya, ukweli upo kiasi gani. Ili kujua ni kubadili Rais na kumpandisha kizimbani Malaika na Mkapa na hapo ukweli wote utapatikana.

Mungu Ibariki Tanzania. Utuondolee Malaika aina ya Yusufeli.
 
umbeya huo na fitina zenu sasa munataka kumsafisha mkatoliki wenu mkapa kuwa hahusiki na ufisadi!!!!! Wacheni unafiki na kutuletea habari zisizo na chanzo na zenye harufu ya uoga!!!

imekuaje mkapa azungumzie epa akiwa nje ya nchi! Mbona akiwa nyumbani hafungui domo lake na zaidi tunaambiwa tumwache mzee apumzike!!!

habari hiyo imekaa kiumbea umbea na hata alieileta anaonekana amekaa kiumbea umbea!!!!!

Hivi Zubeda Umeishi darasa la ngapi?? kwani Ulichoandika kama umenakili ubaoni (Darasa la Pili) kwani unaandika bila kujijua si kosa lako ni KOSA la wazazi wako. Hon.Dr.SLaa President of Tanzania
 
Nashukuru Mungu hatimaye kipindi cha kutajana kimewadia. Waache waungame uovu wao mmoja baada ya mwingine. Afadhali wewe mkapa kama ungamo lako ni kweli basi sisi watanzania kuanzia hapo tunaanza pata mahali pa kuanzia kukusamehe. Bado Mkwere yeye atajitokeza hadharani au bado ataendelea n msimamo wake uliopakwa chokaa ya usanii
 
ni kweli malaika hafai kabisa tena nasema hafai

mkapa yuko sahihi narudia mkapa yuko sahihi ila watu wengi ndo hawaelewi
 
Back
Top Bottom