Kwanini Mikataba ya Wakurugenzi wengi Tanzania Haina kikomo na Wanachukua Mishahara mikubwa sana?

RasJah

JF-Expert Member
Nov 5, 2009
703
64
Tanzania inazidi kupoteza mwelekeo katika ngazi ya Uongozi wa Juu wazo limekuja baada ya kufanya tathmini ya muda mrefu. Mikataba mingi ya mashirika mengi haina kikomo cha mwisho kwa wakurugenzi wake. Mfano mikataba inaanzia miaka 3 - 5 na sheria inasema mkurugenzi atakaa madaraka siyo zaidi ya awamu mbili hata kama uongozi wake ni mzuri sana bado sheria ni msumeno anatakiwa kuachi madaraka.

TRA, mkusanya kodi za taifa kwa niaba ya serikali kuu, lakini wakurugenzi wake huwa wanafanya kazi kwa Mikataba ya miaka kati ya miaka 3-5 sasa wakurugenzi wao hawa kikomo sijui Hazina ambaye ndio mwajiri wao anafanya nini basi Taifa liseme kuwa TRA mikataba hakuna wawe kama watumishi wa kawaida kwani mishahara yao ni mikubwa sana na ma-fringe benefits manono Mfano mzuri DCG Luoga mkataba umekwisha tangu tarehe 15 Juni 2011 na amekaa TRA zaidi ya miaka 15 na sasa huyu mzee bado yupo TRA anasubiri serikali impe mkataba mwingine, mimi nashangaa sana ina-maana yeye Luoga hajisiki kuwa sasa ni bora aende akapumzike na kuwapisha watu wengi wenye nguvu na akili inayochemka na mawazo mapya! Hata Kitilya pia JK amemuongezea muda tayari ana umri wa miaka 60 tuna watanzania wengi uwezo kwani hawa jamaa tu!

Tuna vijana wana maliza vyuo vikuu wanatakiwa wapatiwe ajira na kwa mtindo huu hatutafika, ukilitimba, rushwa na upendeleo sehemu za kazi unalipeleka Taifa pabaya, wimbo wa Good Governance itakuwa ndoto kwa URT, tuige mtindo wa kuteua CEOs unaotumika Kenya na Ghana kwa kutumia kama za Bunge kuwahoji au kuwa interview na kuwa kuteua kama wanafaa kuongoza mashirika. Hata PS wa srikalini lazima nao wateuliwe kwa interview kuepeka bogus leaders kama David Jairo na kuondoa power ya Rais kuteua CEOs, na PSs lazima kuwe na independent elite group ambao wako highly skilled to search future leaders, not money mongers, taken up seminars and incapacitated by overseas study tours.
 
Tanzania ni nchi ambayo rais anateua viongozi wengi kuliko nchi yoyote ulimwenguni. Hilo ni tatizo la kisheria, ndio maana wale waliokaa kwenye post fulan mda mrefu wamejimilikisha madaraka na hivyo kurithisha watoto na ndugu hata kabila. Pigania katiba mpya ndo ukombozi uliobaki la sivyo tutabaki tunalia tu kila kukicha. Angalia bandarini kuna mikataba na pension za miaka mitatu mitatu, unakuta mtu katumikia mikataba zaidi ya mitano na pension amelipwa zote tano.
 
Ninaungana na wewe asilimia moja kwa yote haya madudu yatakwisha iwapo katiba mpya itafanyiwa marekebisho makubwa kwani JK anaupeo ulio mdogo sana au amekuwa na huruma sana kwa binadamu watenda maovu! Sasa je tutatfika na hizi programme zetu nzuri kkt usoma lakini ukelezaji wake ni zero!
 
katiba ni suruhisho maana rais anamadaraka makubwa mno na anateua viongozi wengi sana hivyo ndio maana utendaji unakuwa butu nawalisha elewa mteuzi wao yuko butu ndio maana hawaongopi wanafanya madudu. matatizo yataisha punde tu madaraka ya rais yatapunguzwa na kuwa nawajibu wakuajibishwa hata endapo yuko madarakani.
 
Tumshukuru mwanzilishi wa Thread hii kwa sababu ni ya umuhjmu sana katika utendaji wa siku kwa siku wa mashirika. Kwa hiyo mimi chango wangu ni kuwaorodhesha jamvini hao ma CEOs waliodumu zaidi ya miaka 5 kwenye mikataba ya ajira ili juamii iwajue. Mimi naanza na hawa

1. Harry Kitilya- TRA
2. Haruna Masebu EWURA
3. Ramadhani Dau- NSSF
4. William Erio- PPF
 
Ni mashirika mengi ya umma na pamoja na tasisi za serikali yamekuwa sasa ni mashamba ya bibi kwani wanalipwa mishahara mikubwa lakini kazi ndogo ukilinganisha na input yao katika sehemu zao za kazi kwani watendaji ni hawa officers wakawaida yenye ni kutoa directives tu. Hata haya maoni tunayotoa yanakuwa na hayana tina kwani vyombo husika sijui wanafanya nini mfano mzuri huyu Jairo kwani nchi zenye good governance tayari angekuwa chini ya ulinzi na uchunguzi ukiwa unaendelea na property zake zingekuwa under investigation or frozen na ipo mifano mingi sana ambayo serikali yetu inasjindwa kuyafanyia kazi utendaji unafanyika pale tu mbunge akitoa allegation au taarifanya ikasomwa mbele ya wabunge zidi ya kiongozi wa serikali au shirika la umma ndipo ufuatiliajia unaanza, mfano richmond, Jairo scandal. Lakini mikataba wa vongozi kwa kuwa haijapelekwa bungeni basi siyo issue kwa taifa. Hata hizo taarifa CAG Utoh huwa naona hazifanyiwi kazi kabisa. Mfano mwingine wa viongozi ambao wame-overstay katika mikataba au wamekaa kupita kiasi katika utumishi wa umma na hawa jipya ni kama ifuatavyo:-
(i) Kimei - CRDB
(ii) Luoga - TRA
(iii) Naibu Mkurugenzi Mkuu - NSSF
(iv) Hosea - PCCB
 
Izi post za kiupendeleo zinakera maana ni kwa hisani ya raisi
Naona cha msingi ni kubadili katiba tuu watu wawe wanaaply tena twawaachia iyo kazi watu kama kpmg na wasimamiwe na bunge sio raisi
 
Huyo Luhanjo naye vipi?
Juzi akizungumzia suala la Jairo mbona hata quality ya kupanga maneno yake ilionyesha wazi kwamba ni ya chini kuliko wadhifa wake?

Nasikia Kimei wa CRDB kisha anza kuona mwisho wake sasa hivi Wa-Chagga (musinipige mawe) tunapewa mikopo kama karanga za kuonjeshwa!

Ndo maasi ya watu wanaokaa kwenye madaraka kuliko mategemeo yao.
 
Mikataba hiyo ni ya kipindi cha miaka 5 au 3 lakini ni renewable upon satisfactory perfomance! So as for Kimei, Dau and Kitillya they'd performed...not so sure about Erio , Etc
 
Mikataba hiyo ni ya kipindi cha miaka 5 au 3 lakini ni renewable upon satisfactory perfomance! So as for Kimei, Dau and Kitillya they'd performed...not so sure about Erio , Etc

Nsiande asante kwa comments zako lakini ukweli unabaki pale pale kuwa mikataba yao ni kati ya 3-5 ambayo inakuwa renewable kwa muhula mmoja yaani una-save for two phases na siyo vinginevyo kwani hata kiongozi ungekuwa mzuri sana. Yote haya vyombo husika vimeshindwa kazi wanasubiri mpaka rais aseme au Luhanjo au PM au bunge, kwani kazi tume ya maadili inafanya nini, na kazi magazeti inatusaidi vp katika suala zima kwani wote tunajua kuwa serikali yetu inayafumbia macho mauchafu haya na zaidi kwa nchi kama TZ tunatengeneza bomu letu wenyewe. Vijana wetu watatuhukumu kwani hawa jinsi ya kujikwamua yaani nchi imekosa uzalendo kwa kizazi chao wenyewe. Nyerere na Sokoine watakumbukwa kwa kuwa wazalendo zaidi kwani waliheshimu maadili ndio maana nchi ikawa na rasilimali nyingi na viongozi walikuwa wanaheshimu kazi kwakuogopa kalipio toka kwa mchonga na masai. Vongozi wa leo ni walafi tu! Hakuna utu na uzalendo ee mungu tuokoe nchi itakuwa kama misri, libya, yemen we ngoja tu!
 
Unajua ma-comrade hata nyerere bado alikuwa na uwezo mkubwa sana wa kuiongoza nchi and mind u was very genius than any creature in this planet. Lakini muda ulipofika akasema naona ninyatuke ili watu wengine wachukue nafasi na yenye anagalie je wenzie wanaweza au kiuntedaji wako wazuri na punde anapoona madudu alikuwa anakemea na kutoa kalipio kali sana mfano Mwinyi alipata maswahiba mengi wakati wa mchonga, mkapa alikuwa mpole sana wakati JK alipokuwa hai punde alipokufa yenye akafungua makucha na kuwa chui, fisi, simba n.k. Leo Jk ****** huo nae u-friend umekuwa inaghalimu nchi kichizi, mfano Luhanjo is over 60 years lakini amemuongeza muda wa miaka miwili, kitilya is also 60 years nae kapewa kasema amalizie mkataba uliobaki wa miaka miwili. Nchi haiendi mbele kwa kukitumia kizazi hiki bali inaendeleza urafiki na mambo yanazidi kuharibika. Hawa wazee uwezo wa kufikiri umefika kikomo, u can't compare 40's and 60's yrs in terms thinking and executing, administering to bring efficiency and effectiveness in any institution hawa madingi kazi yako ni totoz na kulewa tu!
 
Haya sasa tena kama iwapo TRA mikataba ya wazee kama Kitilya na Luoga ime-expire kwanini serikali imekuwa kimya take them out and let other brightt fellows compete for the posts. Ndio serikali yetu inaendekeza usingizi ktk masuala mengi ya maendeleo.
 
Mambo haya hayakuhusu wewe, kwani wewe ni mtoto wa mjomba. Kamuulize mjomba. Tena wewe sio mwenzetu.
 
Radar zangu zinadetect kawivu kwenye hii subject. Kama wanaperform wabaki, vinginevyo waondoke sioni ulazima wa kuweka limit ya miaka.
 
Kang pole sana!

Concept ya JF niku moderate nchi na kuendeleza ile dhana ya good governance! Mfano USA Presida Clinton alikuwa the kipenzi cha wamerikani punde alipo-save for two terms hapakuwepo na nyongeza na ndiye rais aliweza kunisha USA reserves kwenye position nzuri sana kuliko rais yeyote aliwahi kuiongozi US. Na wengi ya wachangia hapa JF we are not after posts na kifupi nchi hii haina dira we are trying to shape it! One day our voice will be heard.
 
Haya tena ule msemo wa kuwa Tanzania haina dira na nchi hii haijui nini maana ya mikataba leo yule kiongozi ambaye ni uozo pale TRA Director of Research and Policy tayari ameongezwa mkataba wa miaka miwili kwa pale awali alipewa mkataba wa mwaka 1 baada ya ku prove failure. Luoga mkataba umekwisha tangu juni 15 2011 mapaka hii leo bado yupo ofcn anafanya nini je inamaana hapa tanzania hakuna people wa kuchukua nafasi hiyo, Kamugisha yupo TRA kama Director of Special Duty (without portfolio) and the guy is very bright and young he can delivery stuff.
 
Back
Top Bottom