Kwanini mh J.kikwete asiige kutoka kwa mzee R.MUGABE?

MC babuu

Member
Jun 19, 2012
69
10
Serikali hii iliyokuwa madarakani ni wafuatiliaji wazuri wa ushuru kwa akina mamantilie,wasakatonge na wachumia tumbo tunaacha kuwabana akina (MGM) ni kwanini serikali isikopi kutoka zimbabwe baadhi ya sheria za madini.hivi karibuni serikali ya zimbabwe imetoa tangazo kwa wamiliki wa kampuni za madini zilizowekeza nchini humo kwamba inatakiwa hisa za kampuni hizo kumilikiwa na wazawa kwa 51% chini ya sheria ya wazawa.wakati mwingine nafikiria nashindwa kupata majibu nchi hii ipo na wasomi kweli au ni wanasiasa waliona uchu wa kuingia madarakani ili waweze kufanya biashara zao haramu imefika wakati tunapitwa sasa hadi na zimbabwe ambayo tumekuwa tukidharau na kumwita shujaa mugabe eti ni dikteta kama kiongozi anakuwa anaweza kuona mbali huyo ndo anastahili kuwa madarakani lakini kama anafikiria hapo alipokanyaga hafai kuongoza ata kijiji wala kata.Mugabe kwa hilo nampongeza kwanza huwavutii wawekezaji, sababu kufanya hivyo ni kujichimbia kaburi mwenyewe. Pili alichokifanya ni tendo la kishujaa yaani alichokifanya ni baada ya makampuni ya kigeni kukita mizizi kwenye madini na ndipo akahamua kuweka sheria inayoyataka kuuza hisa kwa wazawa zaidh ya nusu kwa maana hiyo umiliki wa kampuni nyingi utakuwa chini ya wazawa(wazimbabwe) na itachangia kukuza uchumi wa wananchi wa hali ya chini kutokana kwamba kazi nyingi zitafanywa na wazawa na kuongeza pato la mwananchi.kwa nini sisi pia tusiige mtindo huu tuwatege wawekezaji wakishaweka mizizi kama sasa tubadili sheria zetu ili kuwamilikisha wazawa kampuni za uchimbaji madini na mwisho tuziendeshe wenyewe.naomba kuwakilisha asanteni wadau wa jf.
 
Serikali hii iliyokuwa madarakani ni wafuatiliaji wazuri wa ushuru kwa akina mamantilie,wasakatonge na wachumia tumbo tunaacha kuwabana akina (MGM) ni kwanini serikali isikopi kutoka zimbabwe baadhi ya sheria za madini.hivi karibuni serikali ya zimbabwe imetoa tangazo kwa wamiliki wa kampuni za madini zilizowekeza nchini humo kwamba inatakiwa hisa za kampuni hizo kumilikiwa na wazawa kwa 51% chini ya sheria ya wazawa.wakati mwingine nafikiria nashindwa kupata majibu nchi hii ipo na wasomi kweli au ni wanasiasa waliona uchu wa kuingia madarakani ili waweze kufanya biashara zao haramu imefika wakati tunapitwa sasa hadi na zimbabwe ambayo tumekuwa tukidharau na kumwita shujaa mugabe eti ni dikteta kama kiongozi anakuwa anaweza kuona mbali huyo ndo anastahili kuwa madarakani lakini kama anafikiria hapo alipokanyaga hafai kuongoza ata kijiji wala kata.Mugabe kwa hilo nampongeza kwanza huwavutii wawekezaji, sababu kufanya hivyo ni kujichimbia kaburi mwenyewe. Pili alichokifanya ni tendo la kishujaa yaani alichokifanya ni baada ya makampuni ya kigeni kukita mizizi kwenye madini na ndipo akahamua kuweka sheria inayoyataka kuuza hisa kwa wazawa zaidh ya nusu kwa maana hiyo umiliki wa kampuni nyingi utakuwa chini ya wazawa(wazimbabwe) na itachangia kukuza uchumi wa wananchi wa hali ya chini kutokana kwamba kazi nyingi zitafanywa na wazawa na kuongeza pato la mwananchi.kwa nini sisi pia tusiige mtindo huu tuwatege wawekezaji wakishaweka mizizi kama sasa tubadili sheria zetu ili kuwamilikisha wazawa kampuni za uchimbaji madini na mwisho tuziendeshe wenyewe.naomba kuwakilisha asanteni wadau wa jf.

Mkuu usipoteze muda, dhaifu ni dhaifu tu, hawezi tena. Temana nae
 
Mkuu ni matusi kumfananisha RAIS MUGABE na huyu dhaifu wa musoga... Huwezi kumfananisha mtu anayetumia AKILI kufikiri na kutua maamuzi sahihi na mwingine ambaye anatumia masabur. J. K. hana moral authority ya kuwa kiongozi, yeye ni mshiriki wa EPA, yeye ni muuza unga, yeye ndiye mkumbatia uchafu wote tunaouona, sasa utasema huyo mtu anatumia nini kufikiri??
 
Nyie mnaongea kwa vile hampajui Zimbabwe acheni tu...wana hali mbaya yaani choka mbaya sababu ya itikadi na uedeshwaji mbovu wa uchumi wa huyu bwana. Wazim wote wa maana wamekimbia nchi wamejaa south africa, uk na kwingineko hao uchumi umecontract vibaya wala hauwezi kutufananisha nao. Acheni kuongelea vitu msivyovijua na siku Tz ikiwa na hali kama ya zim basi ndio mwisho wetu...inflation ilikuwa ni 9,000% sasa kweli huyo ndio shujaa.

Hiyo sera yake ya kugawa migodi na mashamba kwa wazawa yote anawapa watu wake na wafuasi wa ZANU PF, sasa mnataka na kikwete pia aanze kugawa mali zote za nchi kwa kina Riz1 na CCM...Acheni hizo fanyeni utafiki kwanza kabla ya kuongea.
 
Back
Top Bottom