Kwanini Mbilikimo wengi wanapatikana kwenye Misitu ya DRC

Kennedy

JF-Expert Member
Dec 28, 2011
49,022
54,306
Wakuu jamii ya Mbilikimo wengi wamekuwa wakipatikana katika misitu ya Jamhuri ya Congo, ingawaje hata hapa Tanzania kuna wachache mfano kuna Dada mmoja ktk kundi la VITUKO SHOW.

Sasa mwenye kujua hasa kule Kongo kwanini huwa wanapatikana kwa idadi kubwa anaweza tujuza.

Mwanamuziki hayati PEPE KALE nae alikuwa anawashirikisha katika kazi zake za muziki enzi za uhai wake.

====
Majibu

Swaali zuri sana;

Kwanza fahamu kuwa kuna mbilikimo wa aina mbili: mbilikimo wa asili (pygmy) na mbilikimo wa ugonjwa (dwarf). Wale wa kongo ni mbilikiko wa asili kwa maana ya kuwa maumbile yao ni asili yao na yanatokana na mazingira yao ya asili. Umbilikimo wa aina hii ni hereditary kwa maana ya kuwa huzaliwa na mbilikimo pia. Ni kama ambavyo maumbile ya asili ya waachina yalivyo tofauti na maumbile ya asili ya wazungu, na pia wachina huzaliwa na wachina tu.

Kuna mbilikimo wa aina nyingine ambao wanapata matatizo ya mwili kushindwa kutengeneza hormones zinazohitajika mwili kukua, na hivyo kubaki na umbo la kitoto maisha yao yote; hawa wanajulikana kama dwarfs. Mbilikimo wa aina hii huweza kutokea katika familia yoyote ile, wazazi wawili warefu wanaweza kuzaa mbilikimo wa aina ya dwarf.

Theories zinazonyesha kuwa evolutionary process iliyosababisha waafrika wakawa na ngozi nyeusi kutokana na mazingira ya joto la tropical, ndiyo pia iliyosababisha watu waliokuwa wakiishi kwenye misitu mizito kama vile Kongo kuwa wafupi kwa vile miili yao ilikuwa inakosa mwanga wa jua kutengeneza vitamin D; kwa hiyo miili yao ikawa haiwezi ku-absrob calcium ya kutosha, jambo liliosababisha wawe na mifupa midogo na hivyo kuwa na miili midogo. Misitu ya Kongo ndiyo yenye mbilikimo wengi wa aina hiyo ikifuatiwa na misitu ya Amazon huko Brazili. Kuna sehemu nyingine za dunia kama Papua New Guinea na Australia ambako pia kuna mbilikimo waliotokana na misitu mikubwa iliyokuweko maeneo hayo.
 
Swaali zuri sana;

Kwanza fahamu kuwa kuna mbilikimo wa aina mbili: mbilikimo wa asili (pygmy) na mbilikimo wa ugonjwa (dwarf). Wale wa kongo ni mbilikiko wa asili kwa maana ya kuwa maumbile yao ni asili yao na yanatokana na mazingira yao ya asili. Umbilikimo wa aina hii ni hereditary kwa maana ya kuwa huzaliwa na mbilikimo pia. Ni kama ambavyo maumbile ya asili ya waachina yalivyo tofauti na maumbile ya asili ya wazungu, na pia wachina huzaliwa na wachina tu.

Kuna mbilikimo wa aina nyingine ambao wanapata matatizo ya mwili kushindwa kutengeneza hormones zinazohitajika mwili kukua, na hivyo kubaki na umbo la kitoto maisha yao yote; hawa wanajulikana kama dwarfs. Mbilikimo wa aina hii huweza kutokea katika familia yoyote ile, wazazi wawili warefu wanaweza kuzaa mbilikimo wa aina ya dwarf.

Theories zinazonyesha kuwa evolutionary process iliyosababisha waafrika wakawa na ngozi nyeusi kutokana na mazingira ya joto la tropical, ndiyo pia iliyosababisha watu waliokuwa wakiishi kwenye misitu mizito kama vile Kongo kuwa wafupi kwa vile miili yao ilikuwa inakosa mwanga wa jua kutengeneza vitamin D; kwa hiyo miili yao ikawa haiwezi ku-absrob calcium ya kutosha, jambo liliosababisha wawe na mifupa midogo na hivyo kuwa na miili midogo. Misitu ya Kongo ndiyo yenye mbilikimo wengi wa aina hiyo ikifuatiwa na misitu ya Amazon huko Brazili. Kuna sehemu nyingine za dunia kama Papua New Guinea na Australia ambako pia kuna mbilikimo waliotokana na misitu mikubwa iliyokuweko maeneo hayo.
 
Pamoja na maelezo ya Kichuguu ambayo ni mazuri, pia nadhani ufupi wao ni kwa ajili ya kuwawezesha "movements and displacements" ndani misitu minene, kwani urefu ungekuwa kikwazo kwao (kama ambavyo twiga ni warefu kwa ajili ya kufikia majani ya mbali).
 
Last edited by a moderator:
Hivi Kichuguu,

Ni kweli kabisa unaamini theory ya evolution?Wale watu weusi kule Australia na black indian unataka kuniambia hali ya hewa ya kule inafanana na ya Africa? Ni kwanini nchi moja kunakuwa na watu wenye ngozi za rangi mbili tofauti?

Kuna nadharia nyingine inadai watu wa asili ya bara hili sio weusi ni aina ya watu wanaofanana na waarabu, sijui unaifahamu nadharia hiyo?
 
Last edited by a moderator:
Hivi kichuguu,

Ni kweli kabisa unaamini theory ya evolution? Wale watu weusi kule Australia na black indian unataka kuniambia hali ya hewa ya kule inafanana na ya Africa? Ni kwanini nchi moja kunakuwa na watu wenye ngozi za rangi mbili tofauti?

Kuna nadharia nyingine inadai watu wa asili ya bara hili sio weusi ni aina ya watu wanaofanana na waarabu, sijui unaifahamu nadharia hiyo?
Sielewi iwapo unakataa maelezo niliyotoa hapo juu au unapinga theory ya evolution. Maelezo niliyotoa hapo juu yana ushahidi wa kutosha kuwa watu wa sehemu zote zenye asili ya mistu mikubwa (rainforests) kama vile Congo, Amazon, Quuensland, na papua new Guinea ni mbilikimo. Sababu yake halisi ni hiyo, mifupa hujengwa kwa calcium ambayo mwili wako utaiabsorb tu iwapo una Vitamin D ya kutosha. Na vitamin D hutokana na mwanga wa kutosha. Process hii inajijenga pole pole kwa muda mrefu san (evolution).

Kuhusu Theory ya evolution sijui nikueleze vipi iwapo huiamini. Kumbuka kuwa theory hiyo inatumia muda wa mamilioni ya miaka siyo miaka elfu moja tu. Kama umepiga shule ya kutosha kuhusu mabadiliko ya muundo wa dunia, utajua kuwa Africa, South America, Australasia na India zilikuwa ni bara moja kwenye maeneo ya tropical. Kwa hiyo watu weusi unaowaona huko wote wana asili ya tropical. Soma theory ya Pangaea kwa makini halafu ufuatilie theories za Plate Tectonics, baadaye uchunguze tena namna matetemeko ya dunia yanavyotokea leo ndipo uangalie tena ukaribu wa sehemu zote unazoona leo zina asili ya watu weusi. Uhamiaji uliotokea baada ya ugunduzi wa vyombo vya kusafuiria ndio uliosababisha watu hawa kuchanganyikana; hakukuwa na mtu mweupe kusini ya ikweta. Uhamiaji huo umetokea miaka isyozidi 2000 zilizopita, kipindi ambacho si kifupi sana katika process ya evolution.
 
Kichuguu,

Ni kuwa evolution haileti maana kwangu, kama ni hivyo kuwa mbilikimo husababishwa na jua (kwa mujibu wa theory ya evolution) kuna maeneo jua linapita mara chache sana kwa mwaka na linapoonekana ni kama vie jioni tu, basi na huko pangekua na matokeo hayo ya mbilikimo, pia mbona mbilikimo wakija kwenye maisha ya kawaida (kwenye mwanga wa kutosha) huzaa mbilikimo?

Kama chanzo cha kimo ni mwanga wa kutosha (kwa mujibu wako) basi yale maeneo ambayo jua ni kali si kungekua na watu warefu zaidi? So na Wachina nao? Au China hakuna mwanga wa kutosha? . . . . . . . Au sijakuelewa?
 
Last edited by a moderator:
Kitu kilicho wazi ni kukosekana kwa mwanga wa jua iwe ni kwenye baridi kali au kwenye misitu minene huathiri urefu wa watu. Nimeangalia urefu wa Waeskimo (na Red Indians in general), urefu wao wa wastani ni 163cm (5.3 ft) na ule wa mbilikimo ni 159 cm (5.1 ft). Hii ni kusema wote ni wafupi, isipokkuwa wale wa kwenye barafu ni warefu zaidi kidogo kuliko wale wa misituni.

Ninakubaliana na Kichuguu kuwa watu wenye asili ya maeneo ya tropikali ngozi zao kuwa zimekoza (rangi ya kahawia - brown- iliyopayuka kuelekea iliyokoza sana), bila ya kusahau athari za kijenetiki. Kumbuka kuwa kuna makaburu Afrika ya Kusini wanaoishi kule kwa karne nyingi na bado hawajabadilika rangi kwa kuishi katika tropikali.
 
Last edited by a moderator:
The Central African rainforest is home to some of the most celebrated tribal people, the so-called Pygmies of the Ituri forest in northern DRC. The tallest of these people, known as the Mbuti, rarely exceed 5 feet (1.5 m) in height. Besides the Mbuti, there are three other major rainforest peoples of Africa: the Aka (Central African Republic and northern Congo), the Baka (southern Cameroon), and the Twa (central Zaire river basin). Together these groups account for some 130,000 to 170,000 forest dwellers distributed over a large area of forest. The result is low population density; the Mbuti average fewer than one person per every one-and-a-half square miles (four square kilometers).

African forest people tend to be noticeably smaller than those from the savannas, the Pygmies being the most extreme example. Their small stature undoubtedly enables them to move about the forest more efficiently than taller peoples. Additionally, their smaller body mass allows pygmies to dissipate their body heat more efficiently.

These peoples live in bands that range in size from 15-70 people depending largely on outside factors -- hunting, trading, disease, and forest area. These groups tend to be nomadic, moving to new parts of the forest several times during the year and carrying all their possessions on their back. Their nomadic lifestyle is less damaging to the rainforest environment because it allows the group to move without over-exploiting the local game and forest resources.
 
(1) MAMMAMIA:

Uhamiaji uliotokea baada ya ugunduzi wa vyombo vya kusafuiria ndio uliosababisha watu hawa kuchanganyikana; hakukuwa na mtu mweupe kusini ya ikweta. Uhamiaji huo umetokea miaka isyozidi 2000 zilizopita, kipindi ambacho si kifupi sana katika process ya evolution. Makaburu wamehamia Afrika ya kusini kuanzia mwaka 1600 tu; hicho ni kipindi kifupi sana katika process ya evoltion ambayo inahesabika katika miaka ya mamilioni.

(2) Abunwasi

Kuweza kupita katika misitu kwa urahisi ni mojawapo ya advantages za kuwa mfupi, lakini mwili usingeweza kujibadilisha wenyewe tu kuwa mdogo kwa sababu hiyo. Iwapo mahitaji ya watu ndiyo yangekuwa yanasababisha mabadiliko ya miili, hata sisi mababu zetu walipokuwa wakiishi mapangoni walikuwa wanalazimika kuinama mara kwa mara ili kuingia humo mapangoni lakini miili yao haikubadilika kuwa mifupi. Mabadiliko ya miili yanafanyika involuntary pole pole kutokana na mazingira yanavyoathiri miili hiyo.
 
Last edited by a moderator:
Kichuguu, you have made my day!. Niombe wala ambao hawajamuelewa wajue kuwa ametoa maelezo kwa ufupi sana lakini yanayojitosheleza. Ila mnaweza kuendelea kujifunza zaidi kwa kutafiti tena na tena badala ya kubisha kwa kitu msichokijua. Unapozungumzia evolution ni kitu complex kidogo, sio cha kuendea haraka
 
Kuweza kupita katika misitu kwa urahisi ni mojawapo ya advantages za kuwa mfupi, lakini mwili usingeweza kujibadilisha wenyewe tu kuwa mdogo kwa sababu hiyo. Iwapo mahitaji ya watu ndiyo yangekuwa yanasababisha mabadiliko ya miili, hata sisi mababu zetu walipokuwa wakiishi mapangoni walikuwa wanalazimika kuinama mara kwa mara ili kuingia humo mapangoni lakini miili yao haikubadilika kuwa mifupi. Mabadiliko ya miili yanafanyika involuntary pole pole kutokana na mazingira yanavyoathiri miili hiyo.

Adaptation can lead to evolution only when changing gene survives to reproduce.
 
So what is your side of the discussion? Are the genes changed by the environment or by the wishes of the individual.
Some environmental conditions can modify the DNA controlling the switching of different genes in an organism, but then again, this process is evolutionary.
 
Back
Top Bottom