Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
1) Sikatai kabisa ATCL ilifanya madudu mengi sana katika nyanja zifuatazo:-
a) uteuzi wa wakurugenzi waandamizi bila ya kufuata taratibu.
b) Ukodishaji wa ndege kinyume na utaratibu na kulisababishia taifa hasara za mabilioni.
Hapa na pale anakuja Waziri Mwakyembe - huyu ni mpya kabisa kutoka dukani - badala ya kuiwajibisha Bodi inayoongozwa na Mustafa Nyang'anyi yeye anawawajibisha watendaji waandamizi kazi ambayo siyo yake ni ya Bodi ya wakurugenzi.
Mimi nilifikiri waziri shupavu atakachofanya ni kuiondoa Bodi ya wakurugenzi kwa kuhalalisha madudu lakini yeye anairuka Bodi iliyoko ndani ya uwezo wake na kuingilia kwenye majukumu ambayo yako nje ya uwezo wake na kuyafanya! Huu kweli ndiyo utawala bora?
2) Sikatai kwenye shirika la TBS upo ushahidi wa kutosha wa ya kuwa TBS kufanya madudu makubwa ambayo yameligharimu taifa zaidi ya mabilioni 30.
Sasa Waziri mpya kabisa naye kanunuliwa kwa bei mbaya kutoka dukani anakuja kuiagiza Bodi ya TBS kumsimamisha kazi Mtendaji Mkuu kwa minajili ya kupisha uchunguzi, kazi ambayo Bodi hiyo walipaswa waifanye na hawakuifanya.
Kwa lugha nyingine Bodi tajwa imeshindwa kulisimamia shirika tajwa na ndiyo ilipaswa kufanya kazi na imechelea kwa sababu wazijuazo wao. Huu kweli ni utawala bora wa kuacha kuwajibisha chombo kilichoko ndani ya uwezo wa waziri na kuingilia Bodi kwenye majukumu yake?
Sababu kubwa ya kuziweka Bodi za wakurugenzi ni kupunguza na kufifilisha wanasiasa kuendesha taasisi za umma kwa minajili ya kukidhi mahitaji yao ya muda mfupi ya kisiasa.
Pamoja na nia nzuri ya kufuta ubadhirifu na matumizi mabaya ya madaraka ndani ya taasisi za umma lakini mawaziri hawa wapya wa JK wanapovunja taratibu kwa visingizio kuwa lengo ni kurekebisha makosa siyo sahihi hata kidogo. Huwezi kuvunja sheria na kutumia visingizo vya kuboresha wakati wewe mwenyewe ni mkosaji tu............
Nionavyo mimi ni kuwa hawa mawaziri wapya wa JK wanawaogopa wenyeviti wa Bodi kwa sababu hawakuwateua wao bali wameteuliwa na Raisi. wanaogopa kuhatarisha posho yao n ahivyo wanzilinda Bodi za wakurugenzi lakini wanaelewa pia ili kuulinda mlo wao lazima wachukue hatua na hivyo kusababisha huu muingiliano wa majukumu ambao unakatzwa na sheria.
Hivyo badala ya kuwaondoa watajwa hao basi mawaziri wanawaingilia kwa kufanya yale ambayo wao mawaziri wanataka yafanyike kwa sababu zao za kisiasa na hivyo kufifilisha maana nzima ya kuwa na hizi Bodi za wakurugenzi ambazo zinatugharimu mapesa mengi sana katika kuzikarabati.
a) uteuzi wa wakurugenzi waandamizi bila ya kufuata taratibu.
b) Ukodishaji wa ndege kinyume na utaratibu na kulisababishia taifa hasara za mabilioni.
Hapa na pale anakuja Waziri Mwakyembe - huyu ni mpya kabisa kutoka dukani - badala ya kuiwajibisha Bodi inayoongozwa na Mustafa Nyang'anyi yeye anawawajibisha watendaji waandamizi kazi ambayo siyo yake ni ya Bodi ya wakurugenzi.
Mimi nilifikiri waziri shupavu atakachofanya ni kuiondoa Bodi ya wakurugenzi kwa kuhalalisha madudu lakini yeye anairuka Bodi iliyoko ndani ya uwezo wake na kuingilia kwenye majukumu ambayo yako nje ya uwezo wake na kuyafanya! Huu kweli ndiyo utawala bora?
2) Sikatai kwenye shirika la TBS upo ushahidi wa kutosha wa ya kuwa TBS kufanya madudu makubwa ambayo yameligharimu taifa zaidi ya mabilioni 30.
Sasa Waziri mpya kabisa naye kanunuliwa kwa bei mbaya kutoka dukani anakuja kuiagiza Bodi ya TBS kumsimamisha kazi Mtendaji Mkuu kwa minajili ya kupisha uchunguzi, kazi ambayo Bodi hiyo walipaswa waifanye na hawakuifanya.
Kwa lugha nyingine Bodi tajwa imeshindwa kulisimamia shirika tajwa na ndiyo ilipaswa kufanya kazi na imechelea kwa sababu wazijuazo wao. Huu kweli ni utawala bora wa kuacha kuwajibisha chombo kilichoko ndani ya uwezo wa waziri na kuingilia Bodi kwenye majukumu yake?
Sababu kubwa ya kuziweka Bodi za wakurugenzi ni kupunguza na kufifilisha wanasiasa kuendesha taasisi za umma kwa minajili ya kukidhi mahitaji yao ya muda mfupi ya kisiasa.
Pamoja na nia nzuri ya kufuta ubadhirifu na matumizi mabaya ya madaraka ndani ya taasisi za umma lakini mawaziri hawa wapya wa JK wanapovunja taratibu kwa visingizio kuwa lengo ni kurekebisha makosa siyo sahihi hata kidogo. Huwezi kuvunja sheria na kutumia visingizo vya kuboresha wakati wewe mwenyewe ni mkosaji tu............
Nionavyo mimi ni kuwa hawa mawaziri wapya wa JK wanawaogopa wenyeviti wa Bodi kwa sababu hawakuwateua wao bali wameteuliwa na Raisi. wanaogopa kuhatarisha posho yao n ahivyo wanzilinda Bodi za wakurugenzi lakini wanaelewa pia ili kuulinda mlo wao lazima wachukue hatua na hivyo kusababisha huu muingiliano wa majukumu ambao unakatzwa na sheria.
Hivyo badala ya kuwaondoa watajwa hao basi mawaziri wanawaingilia kwa kufanya yale ambayo wao mawaziri wanataka yafanyike kwa sababu zao za kisiasa na hivyo kufifilisha maana nzima ya kuwa na hizi Bodi za wakurugenzi ambazo zinatugharimu mapesa mengi sana katika kuzikarabati.