Kwanini maamuzi yetu hayajali impact?

Ningu

Member
Feb 5, 2011
75
10
Wana JF naomba kuuliza, kwa muda mrefu nimekuwa nikikwazwa na jambo hili ama mi ndo sielewi vizuri!
Azimio la Arusha lilileta umoja na ustawi wa Tanzania...
Azimio la Zanzibar, kama kweli lipo. Limeleta issues za Dowans etc...
Tukishuka chini zaidi kwenye decisions ndogondogo kama vile
1. Kubadili kanuni bungeni
2. kuitwa TL mahakamani akiwa bungeni
3. CDM kutoka Bungeni (mara ya pili sasa, huwenda zingine zaidi zaja)
4. Kuvuruga chaguzi eg. Arusha
5. Kutoleana kejeli zisizo na tija eg. Mgombea wa tmk cdm dhidi ya jk au wengine wanasema watrudi tu hao hawana pa kwenda!
Nawedha orodhesha mambo mengi sana. Lakini nadhani msomaji umepata taswili ya nini ni SINTOFAHAMU yangu ambayo ni kwamba!!
Watanzania wenzetu tunaowapa jukumu la kutuongoza, ni kweli hutafakari IMPACT ya maamuzi/matendo yao kabla ya kutenda? Au hufanya tu like no body is watching!
Nasema hivyo sababu nawasiwasi in a long run TZ tunakuja kutengana aidha kwa itikadi, dini, mali, elimu au chochote kile kwani kuna mbegu inaanza kuota ya sisi na wao!
Kuna makundi yanajiona bora zaidi kuliko wengine ya yameshaanza kujitokeza bayana!
Je, nikweli viongozi wanajali IMPACT (matokeo ya muda mrefu) ya yale wafanyayo sasa?
 
maamuzi yetu hayajali impact kwa sababu ya mazoea! Kila kitu tumezoea kukifanya bila kufikiria kumuumiza mtu au umma mkubwa. Kikubwa ni kwa anayefaidi kujicikia vizuri zaidi!
 
Mkuu, nadhani tuko kwenye kipindi cha mpito ambacho wawakilishi wetu wanaandaliwa mawazo ya kusema kwenye kamati za chama ( Hakuna anayetumia akili yake ) hivyo kutegemea na uelewa wa yule anayewalisha kwenye kamati mfano, kama Tambwe Hiza atawaweka sawa wabunge ili wakalinde maslahi ya chama kwenye kikao unategemea nini, lazima tushuhudie mipasho na vitu vya kufanana na hivyo, ukizingatia kuwa wazee wa chama wanakupima na kukupongeza kwa uwezo wako wa Kutema hiyo mipasho uliyolishwa. same applies to other Political parties.
 
Back
Top Bottom