Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 22,603
- 29,743
Kuna ule ukweli kwamba DAMU nzito kuliko maji ambao ndio hasa unambeba mtanzania hyyu ambaye ameandamwa na kila aina ya harufu ya ufisadi na ujambazi wa mali za umma.
Kwanza kwa kulazimika kujiuzulu kwa aibu baada ya deal ya RICHMONDULI kuingia mchanga kulimfanya aonekane hafai ktk jamii na ni mtu dhalili, Ila kutokana na hulka yake na UTHUBUTU wa kifisadi alio nao ameamua kujijenga upya kutamalaki himaya mwaka 2015. Amepandikiza vicheche(vibaraka) wake kuanzia ngazi za chini za uongozi ndani ya CCM, pia ndiye ambaye alipendekeza kwa JK majina mengi ya DCs na RCs ambao wanaushwishi ktk kamati za maamuzi za ccm ktk level zao. Amemijengea jina kwa style yake ya majibu na wajibu wa papo kwa hapo ambapo alishaleta madhara ktk ajira za watu hasa hulka yake ya kuwavua madaraka watendaji was erikali hadharani pasipo kutimiza ile kanuni ya NATURAL JUSTICE.
Ujambazi wake wa mali za umma ulianzia akiwa angali mdogo au kinda serikalini ambapo kila mahala alipopita aliacha makapi, na sana sana nyingi ya wizara ama ofisi alizopita ziliishia kuungua kwa moto (kupoteza ushahidi). Hatukatai kwamba anawekeza ila shida inakuja pale ambapo yeye ni mtumishi wa UMMA inazua maswali anapata wapi muda wa kutafakari na kufanya uwekezaji mkubwa alio nao ndani na nje ya nchi. Mtaji alipata wapi? maana wazazi wake hawana historia ya ubepari ambao labda alirithi kutoka kwao.
Kuna baadhi ya sababu ambazo zinamfanya aonekane shujaa nazo ni:-
Sitaki kushindwa kufikiria kwamba LOWASA amewasumisha wanamonduli kiwango hiki.
Kuhusu maswahiba zake tunafahamu kwamba wanatumikia kafiri wapate mradi wao.
Ikumbukwe LOWASA aliwahi kuwa waziri mkuu na mawaziri wakuu wengi nchini walijiingiza hata ndani ya mfumo (UwT) kwa manufaa yao ya mbeleni, sishindwi kuamini kwamba inawezekana walishawahi kuwachomeka baadhi ya watu wao humo ndani ya hilo dubwasha kwa minajili ya kujihalalishia mawasiliano ya core. Je kwa hulka ya UTAWALA aliyonayo LOWASA haiyumkiniki kwamba anao vijana wake ndani ya UwT ambao wanafuata maelekezo yake?
Mie nimewaza kwa muda mrefu naamini kuna anayejua mengi zaidu kuhusu MTU huyu. mwageni data tuzinyanyambue
Kwanza kwa kulazimika kujiuzulu kwa aibu baada ya deal ya RICHMONDULI kuingia mchanga kulimfanya aonekane hafai ktk jamii na ni mtu dhalili, Ila kutokana na hulka yake na UTHUBUTU wa kifisadi alio nao ameamua kujijenga upya kutamalaki himaya mwaka 2015. Amepandikiza vicheche(vibaraka) wake kuanzia ngazi za chini za uongozi ndani ya CCM, pia ndiye ambaye alipendekeza kwa JK majina mengi ya DCs na RCs ambao wanaushwishi ktk kamati za maamuzi za ccm ktk level zao. Amemijengea jina kwa style yake ya majibu na wajibu wa papo kwa hapo ambapo alishaleta madhara ktk ajira za watu hasa hulka yake ya kuwavua madaraka watendaji was erikali hadharani pasipo kutimiza ile kanuni ya NATURAL JUSTICE.
Ujambazi wake wa mali za umma ulianzia akiwa angali mdogo au kinda serikalini ambapo kila mahala alipopita aliacha makapi, na sana sana nyingi ya wizara ama ofisi alizopita ziliishia kuungua kwa moto (kupoteza ushahidi). Hatukatai kwamba anawekeza ila shida inakuja pale ambapo yeye ni mtumishi wa UMMA inazua maswali anapata wapi muda wa kutafakari na kufanya uwekezaji mkubwa alio nao ndani na nje ya nchi. Mtaji alipata wapi? maana wazazi wake hawana historia ya ubepari ambao labda alirithi kutoka kwao.
Kuna baadhi ya sababu ambazo zinamfanya aonekane shujaa nazo ni:-
- fabrications za habari zinazochechemizwa na magazeti yaliyo kwenye payroll yake na kutoka kwa waandishi makini waliopigwa upofu kwa fedha anazowalipa.
- Maswahiba zake ambao amewaweka ktk posts mbalimbali kwa manufaa yake ya kisiasa hasa pale wanapotumia gharama yoyote kumfuta matope aliyojitumbukiza kwayo ionekane kwamba alionewa.
- ukaribu wake na rais ambapo kama asemavyo hawakukutana njiani. IKUMBUKWE pia kwamba hawa waheshimiwa wana ubia wa kufa na kuzikana hivyo mkuu wa kaya hawezi kumwacha aanguke kibudu.
- Kukubalika umasaini hasa MBULU ambapo wapo naye pamoja kwa kila hali (hapa ndipo kwenye hoja mbadala sasa)
Sitaki kushindwa kufikiria kwamba LOWASA amewasumisha wanamonduli kiwango hiki.
Kuhusu maswahiba zake tunafahamu kwamba wanatumikia kafiri wapate mradi wao.
Ikumbukwe LOWASA aliwahi kuwa waziri mkuu na mawaziri wakuu wengi nchini walijiingiza hata ndani ya mfumo (UwT) kwa manufaa yao ya mbeleni, sishindwi kuamini kwamba inawezekana walishawahi kuwachomeka baadhi ya watu wao humo ndani ya hilo dubwasha kwa minajili ya kujihalalishia mawasiliano ya core. Je kwa hulka ya UTAWALA aliyonayo LOWASA haiyumkiniki kwamba anao vijana wake ndani ya UwT ambao wanafuata maelekezo yake?
Mie nimewaza kwa muda mrefu naamini kuna anayejua mengi zaidu kuhusu MTU huyu. mwageni data tuzinyanyambue