Mamzalendo
JF-Expert Member
- Dec 29, 2010
- 1,670
- 558
Ndugu zangu nafikiri kuna kulaumu serikali kulikozidi,wananchi pia tuna wajibu wa kutenda na kuisaidia serikali,mfano katika suala la umeme je wahandisi umeme wa nchi nzima wakijitolea kutafuta suluhu ya hili jambo hata kama ni njia nyingine mbadala kweli hatutapata majibu kwani lazima wazungu tunasomesha vijana wa nini?mfano wa pili ni mtu anayelalamika njaa wakati maji yanapita hapo mdomoni kwake anapewa chakula sawa na m2 aliyepo sehemu yenye jangwa pasipo kuwajibishwa?kweli serikali inatakiwa kutembea na viboko kufundisha wananchi kila kaya kulima mboga kwenye bustani zao je elimu ya sayansi kilimo tuliyopata haitoshi kila mtanzania kulima bustani ya mboga?mfano wa tatu mtu umeajiriwa lakini mara nyingi unakuta ofisini ni internet na zogo serikali ifanyaje,ingawa serikali ina mapungufu lakini hata sisi wananchi tuna mapungufu,kama hata mitaro kando ya barabara ya kwenda kwako huwezi kuzibua ili mvua ikinyesha usidhurike unasubiri serikali kuna tatizo,jamani huu ndio mtizamo wangu mwenye hoja tofauti,nyongeza au masahìhisho nawakaribisha tujadili pamoja tusonge mbele.