Kwanini Kikwete hakusimama na Lowassa?

Rais Kikwete na Lowassa hawakukaa chini kuzungumza baada ya tuhuma nzito zilizotolewa Bungeni na hasa maneno makali ya Wabunge mbalimbali. Kwa yeyote aliyesikiliza hoja za Wabunge ni wazi kuwa Waziri Mkuu alikuwa implied na kuna waliothubutu kutaja na majina kabisa.

Kujiuzulu kwa Waziri Mkuu si jambo dogo hata kidogo hata kama mtu humpendi. Moja ni kwa sababu za kikatiba na jingine ni suala la gharama.

Kikatiba, Waziri Mkuu anapojiuzulu Baraza la Mawaziri linavunjika na hivyo Rais anatakiwa kuanza mchakato mpya wa kupata Waziri Mkuu mpya na Baraza jipya la Mawaziri. Sasa kama Taifa hatuwezi kuruhusu iwe rahisi kwa Waziri Mkuu kujiuzulu na kuanza moja kila inapotolewa tuhuma dhidi yake. NI lazima Rais (anayemteua Waziri huyo) kuwa na msimamo unaoeleweka ili wananchi waridhike kuwa kweli kosa fulani la Waziri Mkuu linamstahilisha kujiuzulu.

Sasa Waziri Mkuu anapotolewa tuhuma nzito ni wajibu wa Rais kumuita na kumsikiliza kabla Waziri huyo hajafanya uamuzi wowote wa papara (kama wa Lowassa). Kwa wanaokumbuka Rais alikuwa mikoa ya Kusini na Makamu alikuwa sehemu nyinyine na wao kama Taifa zima walisikia kujiuzulu kwa Lowassa "radioni". Kwanini Kikwete hakumuita Waziri wake Mkuu na kuhoji tuhuma dhidi yake na kusikia utetezi wake?

Kigharama, kujiuzulu kwa Waziri Mkuu kunasababisha gharama zisizo za lazima za kuunda Wizara mpya au kuingiza mawaziri wapya. Kikwete alilazimika kuunda wizara mpya na kuleta mawaziri wapya na yote hayo yana gharama. Hivyo, hatuwezi kuchukuliwa kwa urahisi tu kujiuzulu kwa Waziri Mkuu kana kwamba ni kitu kidogo.

Pia watu wanasahau kikao alichofanya Rais Kikwete na wazee wa Dar kuelezea mshtuko wake wa kujiuzulu kwa Lowassa. Tukumbuke kuwa Kikwete hakusema Lowassa amefanya makosa yoyote na alisema kuwa kujiuzulu kwa Lowassa kulikuwa ni kwa "ajali ya kisiasa". Sasa kama Rais alijua Lowassa hakufanya makosa kwanini hakusimama naye na kuepusha maamuzi ya kisiasa?

Je, tunaweza kukubali hizi "ajali za kisiasa" kwa kushindwa kuzizuia?

Kidemokrasia, naamini Watanzania tulinyimwa nafasi ya kuona demokrasia yetu inavyoweza kufanya kazi unapotokea mgongano kati ya Bunge na Rais. Kikwete angeweza kukaa na Lowassa, kuangalia ushahidi uliotolewa na Kamati Teule, kupima uzito wa hoja za wabunge na kuandaa majibu kwa kila hoja.

Ninaamini hakuna mwanasiasa wa Tanzania ambaye angeweza kupangua hoja za kamati teule kwa urahisi na kwa umahiri kama siasa (na hapa namaanisha). Ingekuwa vizuri kweli kwa Rais Kikwete kuchukua upande wa Waziri wake Mkuu ili tuone mgongano kati ya Mwenyekiti wa CCM na wabunge wa CCM! Je, kweli mnafikiri Bunge la CCM lingeweza kwenda kinyume na Rais wake? Je wale waliokuwa vinara wangeweza kuendelea kuwa vinara baada ya Rais kuchukua msimamo wa kumtetea Lowassa? Je yawezekana ushujaa wao ni kwa sababu Kikwete hakuchukua msimamo na hivyo ni kuwa kama bingwa ambaye hakutaka kuingilia mapambano ya ridhaa!?

Kama hakukuwa na ushahidi wa moja kwa moja wa Lowassa kunufaika na mkataba wa Richmond, kama hakukuwa na ushahidi wa moja kwa moja wa kuonesha kuwa Lowassa ndiye Richmonduli, kama Kamati haikuweza kuonesha kuwa mtoto wa Lowassa ndiye alihusika na Richmond na kwa mujibu wa sheria ya Maadili huo ni mgongano wa Maslahi kwa Lowassa, ninajiuliza Lowassa alijiuzulu kwa sababu gani hasa?

Jibu ni kuwa Lowassa alijiuzulu ili kumkomoa Kikwete! Alijiuzulu kama spite ya Kikwete na urafiki wao; hakujiuzulu kwa sababu nyingine yoyote isipokuwa kwa sababu rafiki yake, mtu aliyehangaika kumuweka madarakani na mtu ambaye kwa kiasi kikubwa ni mshirika wake wa kisiasa alimtosa wakati alipotakiwa kusimama naye.

Je, ina maana kwa Kikwete kusimama na Lowassa kunamfanya Lowassa asiwe na makosa? Na kama alikuwa na makosa ni kweli yalimstahilisha ajiuzulu kwa namna ile ya utekaji nyara nchi?

Mzee mwanakijiji salam na heshima natangliza;
Ninachosoma hapo juu kinanizungusha kichwa kidogo na naamini sitakua peke kwani nimeona wachangiaji kadhaa wameleweshwa na main Thread uliyotuwekea hapa.
Hivi KWELI UNA HAKIKA NA IMANI kuwa LOWASA ni **** wa mtaani kiasi hichooooooo??? awe hana KOSA LOLOTE na AKAACHE NAFASI KAMA WAZIRI MKUU ati kwa KUMKOMOA KIKWETE!!! kumkomoa for WHAT???
Ati lowasa kasaidia kumuweka Kikwete madarakani (pengine) Lakini Lowasa huyo ana kura moja tu Hata ukijumlisha familia yake marafiki na hao atakaowapa hongo wakati wa kampeni bado walikuwa na hiyari ya kutumia kura zao watakavyo.Na kama alikuwa na nguvu na uwezo huo kwa nini asingeutumia na kugombea yeye nafasi ya Urais. Jibu liko wazi WATANZANIA wote tunakumbuka alivyoumbuliwa na Baba wa Taifa hayati Mwl Nyerere kuwa nafasi hiyo haimfai kutokana na TABIA zake in fact Kikwete ni wa kujilaumu mwenyewe kwani the WRITING WERE ON THE LOWASAS FACE kwa kipofu kuweza kuona na kujua kuwa hafai. Kwa hiyo Kikwete asingejitendea HAKI kama angeruhusu URAFIKI UMPONZE kwa mara ya pili.Kama siasa na dhamana zina fadhila basi Kikwete alilipa kwa Lowasa, ilikuwa ni wajibu wa Lowasa kutambua na kuafanya KAZI ALIYOPEWA KWA ADABU. Sasa MMJJ Lowasa kaonewa ??? au Kajionea??? na wewe unaonaje arudishiwe ofisi yake?? AU unamenej kampeni yake ya 2010??
 
Nihitimiesh mchango wangu kwenye hoja hii kwa kitu kimoja tu... na hiki ni kuhusu Katiba ya Tanzania.

Natamani sana siku katiba yetu itakapokuwa hivi.!
President: Head of State, Commander in Chief
Prime Minister: Head of Government, Ministers Cabinet

Nasema haya kwa kuwa kuna jambo mengi tunajadili hatuweki vitu vyote into perspective... hatuji ni kwa kiasi gani demokrasia na ICT ilivyofanya wetu wengi kuweza kujua mambo mengi kiasi hicho kuliko ilivyokuwa zamani... angali nguvu ya JF kwa mfano. hii wanasiasa hawakuitegemea hata kidogo... wenzetu wa 50 years walikuwa hawajajiandaa na haya mambo ya demokrasia na ICT ya sasa ndugu zangu.

Ndio maana ukiangalia ilani zote za vyama hazitofautiani sana... bado ahadi ukiingia kwa undani utagundua zimezama kwenye uzamani zaidi kuliko ukisasa zaidi.

Mwisho mnataka kuniambia hapa kwa mfano JF kuna zaidi ya 10% ya watu wenye umri wa miaka 50? Jibu ni hapana... sasa maana yake ni kwamba wanaoendesha serikali wengine na ninyi ni wengine... matazamia/matarajio/expectation tofauti?

Mungu Ibariki Tanzania.
 
wandugu,

..Mwinyi na Mkapa walichapa kazi awamu ya kwanza, wakaanza kuiba wakati wa awamu ya pili.

..JK na serikali yake wamekiuka "utamaduni" huo, na kuamua kuiba tangu siku ya kwanza wanaingia madarakani.

..wananchi tuelewe kwamba wakati tunaendelea kubishana, viongozi wetu wanaendelea kutuibia na kuhujumu taifa.
 
Jk akikuteua ujue you are on your own
Hata kama nitakubaliana na usemi huu, sitaki kukubali kama ni mapungufu, naamini ndiyo style yake ya kazi. JK is a populist politician, yeye atafanya chochote kinachowezekana ili mradi asihusishwe na jambo lolote ambalo in the public eye, ni negative. Kitu kikifanyika na kufanikiwa, he will be there to support fully, lakini hatatokea kwenye tukio mpaka ajue outcome ya jambo ni negative au la, kwahiyo kufanya maamuzi ni ngumu. Maoni yangu ni kwamba Tanzania needed a president like Kikwete kwa wakati huu, kwasababu people needed to be united and started feeling good about their government & country. He is the kind of the guy that make people feel good, na amefanikiwa sana kujenga uzzalendo wa watu – which is good, kwasababu inakuwa rahisi kwa serikali kufanya mabadiliko na maamuzi magumu wakati you have support ya wananchi. Kipaji kikubwa cha uongozi ni kujua strength & weaknes zako na za wateule wako na viogozi wenzako, mimi naamini katika kumteua EL kuwa PM alionyesha hichi kipaji dhahiri. JK alisema bungeni kwenye hotuba yake kwamba nimemteua siyo kwasababu ni rafiki bali ni mfuatiliaji na msimamizi mzuri sana wa mambo ya nchi, kwahiyo team ya Jk ilitakiwa iundwe na watu wote wenye guts za kufanya kazi na maamuzi magumu kama EL, wakati JK akitoa support yake iliyo na public backing nyuma yake. Unfortunately, vurugu za mchakato 2005 nadhani zilikuwa under-estimated na JK na administration yake yote, maadui wake walirudi kwenye drawing table na kuandaa master plan ya kuisambaratisha administration yote na mtandao kwa ujumla, na kwa asilimia kubwa sana wamefanikiwa almost 90%. Adiminsitration ilisambaratika 2006, malengo yote na mipango ya regime yaka-colapse, kwasababu ya richmond – hili jambo tukilijadili leo baada ya hasira kushuka baada ya mwaka mmoja, unaona clearly kwamba ilikuwa political move, lakini ambayo ilichezwa vizuri, wananchi waliweza kuaminishwa mambo. Suala la Richmond/Dowans ni mwaka wa tatu sasa inaisumbua nchi, hivi kweli is it a worthy issue ya ku-engage nchi nzima siku zote hizi, halafu je hatima yake ni nini? Any benefits kwa wananchi? Watapata maji zaidi? NO, shule bora? NO, i hope Rais anakaa na Bunge kulimaliza hilo suala ili yaongelewe mambo ya wananchi.
Leo lakini JK is on his own, a lonely man in the office, hii siyo nzuri kwa CCM na siyo nzuri kwa nchi, ni rahisi kusema aondoke 2010, lakini wote tunajua hiyo siyo realistic and the country is hurting. Ni viongozi wachache sana wanoamini kwenye agenda yake sasa hivi, kwasababu imesambaratishwa na maadui, all through out the country watu wanasubiri uchaguzi tu, hamna discussion ya maendeleo. I believe JK needs a re-launch ya administration, public opinion is bad as it is, lets not fool ourselves, just go for a do or die, for the country and the party. JK AKAE CHINI NA WAZEE NA WATAALAMU ANAOWAAMINI WAPANGE RE-LAUNCH, aende kwenye uchaguzi na agenda of the ‘new administration’ ambayo itakuwa tayari imejiestablish na imeleta a new wave of optimism kwa wananchi.
EL alikuwa anaamini 100% kwenye agenda ya JK, hamna mtu ataniambia zile ziara kule vijijini zilikuwa hazina maana, they were ENGAGING ziaras, zile enzi za wenyeji kusafisha barabara na kuchinja kuku tu kwaajili ya mgeni ziliisha. Vikao vyote vilikuwa intensive na maswali ya kutosha, back & forth, na ma-DC wanasema hata jamaa wakiondoka wasaidizi wanaendelea kufuatilia kwa karibu makubaliano yote. Hii ilikuwa inamfanya JK kuwa POWERFUL zaidi, kwasababu kama PM amepita ndiyo hivi, tutafanyeje mwenye nyumba mwenyewe akija?? It was working perfectly, hata posture ya JK in public was that of a ‘powerful president in deep thought’, sasa hivi its all gone. Either ni urafiki wanao au ushirikiano tu, sijui, lakini i believe Tanzania needed a bit more of the partnership btn JK & EL. All in all we wish them both the best of luck, lakini nchi inaumia sana.

Pamoja na kukubaliana kwa kiasi fulani na tathmini yako, napinga sehemu kubwa ya tathmini hiyo (JK & EL partnership).

Mkuu KGBtz, Hakuna uwiano wowote kati ya JK na EL. Hawawiani kwenye nia, kwenye imani kuhusu kazi, kwenye fikra kuhusu ustawi wa Taifa n.k.

Nadhani nia ya JK imekuwa na ilikuwa ni kuleta ustawi wa kweli na wa kudumu kwa Tanzania. Alijaribu sana kuwa karibu na wananchi ili aelewe kero zao, na kusikiliza mahitaji yao. Alikuwa na amekuwa mvumilivu kwenye criticism nyingi zitolewazo kuhusu serikali yake. Na matokeo ni haya ya viongozi wake kuumbuka kila kukicha, wananchi kujua mambo yanayofanywa na serikali na kuyatolea kauli kila iwezekanavyo.

Kwa upande mwingine, EL alikuwa ndio kinara wa uzuiaji wa kauli zinazopingana na matendo ya serikali yake. Bungeni alikuwa akizuia wabunge wa CCM kuchangia hoja yoyote kinyume na mapenzi ya serikali (sio lazima chama). Alikuwa akiilinda serikali yake kwa yote mabaya na mazuri iliyokuwa ikiyafanya (kwa nguvu sana). Zaidi ya hayo, hakuwa na nia thabiti ya kuneemesha mwananchi hasa wa kawaida. Mifano ya kashfa zilizotokea inatosha kuelezea hili.

Kama ulivyosema, EL kwa kweli alikuwa akifanya kazi kwa bidii sana. Alizunguka nchi nzima (japokuwa kuna baadhi walihoji kama alifanya hivyo kujenga nchi ama kujitengenezea njia). Baada ya kutoka, hakuna anaefanya lolote. Jitihada zote zimekwenda na nae.

Kwa kumalizia tu, kinachosumbua utawala wa JK sasa ni jinsi ulivyofanya kampeni zake 2005. Walitumia nguvu nyingi sana kufika Ikulu. Siamini kuwa walihitaji kutumia nguvu kiasi hicho, kwa kuwa tayari JK alikuwa ameshakubalika kwa wengi. Maumivu waliyowaachia washindwa katika kinyang'anyiro kile, hawakuyafanyia kazi yoyote. Walisherehekea na kuamini kuwa hawakuwa wakihitaji lolote kutoka kwa yeyote aliekuwa nje ya mtandao. Wanamtandao wakijiona kuwa wameshinda vita, na nchi imekuwa yao. Wakaanza kufuja mali na kuchota visivyo vyao kwa faida zao. Hapo ndipo wataalam walipogundua kuwa wameingizwa mkenge wakaenda kwenye drawing board.
 
Recta,

..Kikwete alitumia dirty politics au siasa za maji taka kuingia madarakani.

..for 10 solid years he was busy mudslinging any one who he thought was capable of running against him.

..tatizo lililopo sasa hivi ni kwamba JK yuko madarakani, hajui cha kufanya, and basically there is no one else to mudsling.
 
Tuiangalie kidogo hotuba ya Rais na tuone kama alikuwa anajua Lowassa ataenda kujiuzulu siku ile ya kukumbukwa:

Wazee Wangu;
Nilisema mwanzoni kuwa, nilipokwenda Dodoma tarehe 06 Februari, 2008 nilienda kwa ajili ya kikao cha Baraza la Mawaziri.

FACT 1: Rais anasema kuwa wakati anaenda Dodoma alienda kwa sababu ya kuongoza kikao cha baraza la mawaziri. Kilichompeleka Dodoma haikuwa kwa ajili ya Lowassa au mambo ya kamati teule. Kwa vile mawaziri ni wabunge na wengi walikuwa Dodoma kwenye kikao ilikuwa ni makini kwenda huko kuliko kutaka mawaziri wote waje Dar kufanya mkutano huo.

Lakini nilipofika nikapata taarifa kuwa baada ya Ripoti ya Tume ya Mwakyembe kuwasilishwa, Uongozi wa Wabunge wa CCM Bungeni umeamua kuitisha kikao cha Kamati ya Uongozi ya Chama mchana ule na usiku Kamati ya Wabunge wote wa CCM.


FACT 2: Rais anasema kuwa taarifa aliyopata ilikuwa inahusu mkutano wa Uongozi wa CCM Bungeni ambao uliitisha kikao cha Kamati ya Uongozi waya Chama. Uamuzi huu kwa mujibu wa Rais ulikuja baada yakusomwa kwa ripoti ya Mwakyembe na mijadala iliyoendelea kutwa ile ya Tarehe 6 FEBRUARY, 2008
Mimi nilikuwa nimeamua kikao changu cha Baraza la Mawaziri nikifanye usiku lakini Mawaziri ni Wabunge wa Kamati ya Chama ya Bunge hivyo nikaamua niahirishe kikao changu. Nilifanya hivyo kwa kuzingatia uzito wa suala lenyewe na unyeti wa hali pale Bungeni baada ya taarifa ile kutolewa. Nilifurahi kuwa Kamati ya CCM ya Bunge itahusishwa kwa ukamilifu.

FACT 3: Rais anarudia kuwa kilichompeleka ni mkutano wa Baraza la Mawaziri na Waziri Mkuu ni mmoja wa wajumbe wake. Haoneshi kuwa Waziri Mkuu hakumpokea au vinginevyo na alikuwa anaamini kuwa kikao cha baraza la mawaziri kitafanyika bado na ndiyo sababu ya "kuahirisha". Mtu haarishi kitu ambacho hana uhakika kitafanyika!

Baadae usiku nilipokea taarifa ya vikao hivyo viwili vya Chama chetu.

FACT 4: Rais anasema kitu pekee alichopokea ni taarifa ya vikao viwili vya chama. Hasemi lolote kuhusu kupokea barua au maneno yoyote toka kwa Waziri Mkuu. Hasemi lolote kuwa alizungumza na Waziri Mkuu usiku ule (hili ni la maana katika FACT 5. Bila ya shaka taarifa iliyotolewa ni hiyo ya mvutano wa Lowassa na wabunge wajiuzulu au wasijiuzulu na mapendekezo yao. Yawezekana vikao vilikubaliana Lowassa atakiwa kujiuzulu, lakini hilo halisemwi mahali popote kuwa walimuambia Lowassa ajiuzulu, kwa sababu mtu pekee anayeweza kufanya hivyo ni aliyemteua! Hivyo yawezekana walitoa mapendekezo na JK alikuwa amuambie Lowassa maamuzi yale ya kichama.


Baada ya kufuatilia mjadala Bungeni siku iliyofuata na kusikiliza hisia za watu nchini ndipo tukafikia kwenye maamuzi yale magumu na mazito tuliyofanya. Maamuzi ambayo yalipelekea kuvunjwa kwa Baraza la Mawaziri. Ni maamuzi magumu, lakini yalikuwa hayana budi kufanyika kwa maslahi ya utangamano wa taifa letu. Uamuzi mwingineo tofauti ulikuwa unaliingiza taifa letu kwenye matatizo makubwa zaidi.

FACT 5: Hili ni muhimu kulielewa. Rais anasema kuwa "baada ya kufuatilia mjadala Bungeni siku iliyofuata na kusikiliza hisia za watu nchini".. .Hili ni muhimu kwa sababu Lowassa alijiuzulu asubuhi ya tarehe 7 akiwa mzungumzaji wa kwanza Bungeni. Maamuzi yaliyofikiwa HAIWEZEKANI kuwa yalifikiwa kabla ya Lowassa kuzungumza bali ni maamuzi ya KUKUBALI Lowassa kujiuzulu.

Maamuzi yale yalizingatia kwa maneno ya Rais "mjadala bungeni na kusikiliza hisia za watu nchini". Kwa maneno mengine, zile shamrashamra za watu kufurahia Lowassa kujiuzulu na malumbano baadaye Bungeni yalimfanya ashindwe kuwa na uamuzi mwingine isipokuwa wa kukubali. Ndiyo sababu tamko lake la kumkubalia Lowassa lilikuja baadaye. Na ndiyo sababu Lowassa hakuweza kusema kuwa Rais amekubali kujiuzulu kwake.
Ni uamuzi mgumu kwa sababu unawahusu watu ambao ni wenzangu wa karibu kimaisha na kikazi kwa miaka mingi. Na pia kwa sababu unaona wazi kuwa kama mambo fulani fulani yangefanyika mambo yasingefikia kuwa yalivyo. Lakini, ndiyo imeshafikia hapo. Imeshakuwa na fursa ya kufanya vinginevyo kwa maslahi ya taifa haikuwepo. Kama ilikuwepo ni finyu sana na haingeleta hatima tofauti na ile tuliyoifikia.

FACT 6: Hapa ukisoma vizuri utaona kuwa Rais hakupewa muda au nafasi ya kufikiria njia nyingine. Kwa maneno mengine alikuwa "between the rock and a hard place". Ni uamuzi ambao ulimuumiza kwa sababu kama mambo fulani yangefanyika (EL kumuambia mapema adhama yake???) labda jambo fulani lingefanyika. Lakini kwa jinsi ilivyotokea aliachwa hana nafasi ya kufanya lolote.

Yaliyotokea ni ajali katika maisha ya siasa, lakini naamini historia itamhukumu kwa haki stahiki.

FACT 7: Ajali huwa haipangwi!

UTHIBITISHO NJE YA MANENO YA RAIS:

Wakati Spika amepokea habari za Lowassa kujiuzulu alisema hivi Bungeni kama mtu aliyeshtukizwa.

Sehemu ya kwanza:

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Waziri Mkuu. Umeniondoa katika utata wa
kujaribu kujibu swali ambalo kwa kweli kwa maoni yangu lilikuwa linatangulia mjadala wenyewe. Kwa sababu mazingira hayo yalitakiwa yazingatiwe kwenye mjadala na wote tutawapa nafasi. Napenda kukuarifuni kwamba Kamati ya Uongozi imeniruhusu kwamba ikiwa itabidi tutaendelea hadi Jumatatu. Kwa hiyo, mtu asiwe na shaka kwamba
amejiorodhesha atakosa nafasi ya kusema. (Makofi)

FACT 8: Spika alikuwa anapanga taratibu zake kama kawaida akiamini kuwa mjadala wa Richmond ungeweza kuendelea hadi Jumatatu. Hakuwa na fununu yoyote ile kuwa dakika chache baadaye Lowassa atabwaga manyanga chini. Vinginevyo angeweza kusema maneno yoyote ya kuyeyusha.

Katika nukuu ya hapo juu, Spika alikuwa na majina ya wachangiaji 51 ambao siku ile waliongezeka wengine 7. Na baada ya kuwaahidi kuwa kila mmoja atapata nafasi ya kusema basi akaanza kumuita mzungumzaji wa kwanza. Na Lowassa aliposimama kuzungumza alimshukuru Spika "kunifanya msemaji wa kwanza katika hoja hii". Kwa maneno mengine na kiutaratibu Waziri Mkuu anakuwa precedence na kwa kawaida akimaliza yeye kuchangia anayefuatia ni kiongozi wa kambi ya upinzani wakati wowote wa mijadala. Hivyo, Waziri Mkuu kupewa nafasi ya kwanza siyo jambo geni au lilitokea kwa bahati. Lakini Spika hakuwa na idea kuwa EL amejiandaa kuwapa mshtuko wa mwaka.

baada ya Lowassa kutoa ile hotuba yake ya "nimefadhaishwa sana" Spika alisema yafuatayo:

SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tamko hilo ni zito sana na wala sikulitegemea. Sasa ningeomba ushauri tuendeje? Tuchangie tu hakuna haja ya kunong’ona na kupiga kelele?

FACT 8: Spika kwa mara ya kwanza anasema kuwa hakutegemea tamko hilo (la kujiuzulu).


SPIKA: Hadi sasa sijapata mawasiliano yoyote kutoka kwa Mheshimiwa Rais kunieleza kama amekubali kujiuzulu kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu. Kwa sababu utaratibu ndio huo alichoeleza Mheshimiwa Waziri Mkuu hapa ni kwamba amewasilisha kwa Mheshimiwa Rais kama mamlaka ya uteuzi kusudio lake la kujiuzulu.

FACT 9: Ukisoma vizuri alichosema Lowassa na alichosema Spika ni vitu viwili tofauti. Go and check. Na hili ndilo lilikuwa tatizo. Lowassa hakusema "amewasilisha" kwa Mhe. Rais kusudio lake la kujiuzulu. Lowassa alisema "nimeamua kumwandikia Rais Barua"!

SPIKA: ...kutokana na hali hii isiyo ya kawaida; na kutokana na ukweli kwamba lazima Spika apate ushauri mzuri wa kisheria na pia aweze kuwasiliana na mamlaka ambazo hazimo humu Bungeni nasitisha Shughuli za Bunge hadi hapo saa kumi na moja.

NI wazi kuwa Spika hakuwa na taarifa za kujiuzulu kwa Lowassa ni wazi kuwa JK hakuwa na taarifa hizo wakati EL anajiuzulu vinginevyo angekwisha mtonya Spika kujiandaa na jambo hilo. Kama alikuwa anajua kuwa Lowassa anajiuzulu muda ule, na yeye hakumuambia Spika n.k then ninamashaka zaidi juu ya uongozi wake kuliko kitu kingine chochote kuruhusu Bunge litekwe namna ile.

Kwa ufupi, hakuna ushahidi wowote ule kuwa Rais Kikwete alikuwa anajua Lowassa atajiuzulu muda ule. Hii haiondoi ukweli kuwa y awezekana alipokea mapendekezo ya kumtaka Lowassa ajiuzulu. Je yawezekana Lowassa hakutaka kusubiri Rais amuambie ajiuzulu na akaamua kumpiku kwa sababu baadhi ya watu wake walikuwemo kwenye mikutano ile ya Kamati ya Chama na wanajua mapendekezo yao?

Je yawezekana sababu ya JK kutosimama na EL ni kwa vile EL hakumshirikisha katika kufikia uamuzi huo? Kwamba labda siku ile ya kikao cha Baraza la Mawaziri (kilichoahirishwa jana yake) labda Rais angeweza kupata ushauri wa baraza zima kwanza. Kwamba EL hakutaka kutoa nafasi kwa JK au mtu mwingine kuingilia uamuzi wake huo kwa kuwajulisha mapema?
 
Sijaona hasilani sababu za yeye kutakiwa kusimama naye.

Upo wakati wa kusimama na mtu wako wa karibu na uko wakati wa kukaa mbali kabisa kutegemeana na hali au niseme wazi kutegemeana na ukweli juu ya kile kilichomsibu aliye karibu yako.

Rais anakula kiapo cha kuilinda katiba ya nchi na kwa maana hiyo maslahi ya nchi na sio kumlinda wa karibu yake hata kama angekuwa mkewe! Kumbukeni kuwa kuna wakati hata Mzee mwenye kuheshimika na Dunia Nelson Mandela aliwahi kutomuunga mkono mkewe (wa kwanza) katika harakati zake.

Pengine swali lingekuwa kwa nini hakueleza kinagaubaga alichokijua na pia msimamo wake juu ya uamuzi huo ukilinganishwa na maoni ya wengi Bungeni. Maana reaction yake in public ilikuwa kama ya kuonyesha huruma tu juu ya yaliyotokea kwa aliyekuwa karibu naye na kwamba historia ndio iliachiwa itoe hukumu 'halali'!
 
Mwanakijiji,

Hivi unajua jinsi EL alivyo jeuri?.....i wish ungelijua hilo........Kuwa on top of things kama kiongozi ni jambo zuri......lakin inapofikia mpaka interest zako zina-overule misingi tuliyojiwekea.....then ni tatizo.....thats what happened kwa EL.

JK.......be it aliambiwa kabla au baada its not a point...........the point ni kuwa for how long tungeendelea na tabia hiyo........kuna maswali mengi ya kujiuliza hapo......shaking the government is not a simple thing as many of us would think.......
 
Mwanakijiji unaongea kana kwamba kila wanachosema wanasiasa kuhusu wanachokijua au wasichokijua ni kweli!
 
Safari hii amesimama naye hapa

wtcoj.jpg
 
1. Obama hakumtetea Tom Daschle, wala Bill Richardson, lakini alimtetea Treasury secretary wake.

2. Bush hakumtetea Donald Rumsfield, lakini alimtetea Brown.

3. Rais Kikwete, hakumtetea Waziri Mkuu wake wa kwanza E. Lowassa, lakini Masha ni waziri mpaka leo.

Ahsante.

William.

Duuuh,
kaazi kweli kweli.
 
Kwanza ilikuwa ni Rais Bush na Michael Brown kule Lousianna wakati wa Katrina. Wakati kelele zinapigwa za kutaka kichwa cha Brown (mkuu wa FEMA) Bush alifunga safari kujionea na kwa jinsi anavyojua yeye alisimama mbele ya waandishi wa habari na kusema yale maneno ambayo yamebakia kama mwangwi "Brown you are doing a heck of a job".

Bush alisimama na mtu wake aliyemteua licha ya kelele..

Sasa wiki ile iliyopita hata leo hii kumekuwa na kelele za kutaka Waziri wa Fedha wa Marekani Bw. Geithner kujiuzulu. Mara tatu sasa Rais Obama amejitokeza pasipo woga kumtetea mteule wake na kusimama naye na kusema kama kuna mtu anataka wa kumlaumu basi wamlaumu yeye na kamwambia hata akileta barua ya kujizulu hatoikubali (basically asijisumbue).

Obama amesimama na mtu wake aliyemteua!

Ndiposa, nikabakia kujiuliza.. nini kilitokea Februari ile? Kwanini Kikwete hakusimama na mteule wake na kukubali kubeba lawama zote za Richmond yeye mwenyewe? Kwanini hakusimama na Karamagi, Chenge (ya Chenge labda haifai!) au Msabaha?

Je kila watu walio chini yake wakilaumiwa yeye atawatosa tu? NI lini atakubali kubeba lawama na kusema kuwa "mnilaumu mimi"? Je yawezekana tunu hiyo ya kukubali kubeba mzigo kama kiongozi Rais wetu hana na badala yake ni bora watu watoswe ilimradi yeye anaendelea kuonekana ni msafi? Je kuna siku atasimama kuwatetea watu aliowateua au atawaacha wamomonyoke na hivyo kuthibitisha ni jinsi gani asivyo mwangalifu katika uteuzi (maana anashindwa hata kuwatetea!)!

Ninaamini, hakuna wakati ambapo Kikwete alionesha udhaifu mkubwa kama kiongozi kama kushindwa kusimama na Waziri wake Mkuu au kupanga naye mkakati wa kujibu mashambulizi ya Bunge. Ndiyo maana ninaamini Lowassa hana sababu ya kumlaumu mtu mwingine yoyote (siyo Spika, CCM au Mwakyembe) kwa kujiuzulu kwake bali mtu mmoja tu ambaye alishindwa kuchukua msimamo mgumu!

Lakini labda alijua maji yamemwagika? Je kama JK angesimama na Lowassa na kukubali uchafu na lawama zote za Richmond (as a matter of fact nakumbuka mkutano wake na waandishi wa habari nadhani alistahili kuubeba mzigo huo!).

Kama mtu ukiteuliwa na Kikwete jua jambo moja.. you are on your own!!

Bila ya shaka Unampigia kampeni Kikwete kupitia mlango wa nyuma
 
Mwanakijiji kumbuka jambo moja muhimu sana,Kikwete asingeweza kugagamara na Lowasa ili abebe yeye lawama,kwani Lowasa ndiye aliyemwezesha kuingia Ikulu.Tena kabla mambo hayajapendeza tulimtonya pale Maelezo vipi huyo rafiki yako tumesikia utampa nafasi nzito katika serikali yako,Unajua alijibu nini,"Kwani kuna ubaya gani kama anazo sifa?"Kwa hiyo Kikwete alijua strength za EL kwamba alikuwa hata na uwezo wa kumu-over shadow huyu Kiranja Mkuu,Lakini sasa afanyeje?Kama siyo kumtosa?Kulikuwa na ukweli usopingika kabisa kwamba Bwana EL alikuwa na uwezo mkubwa wa maamuzi kuliko mwenyewe JK.Hata baada ya kumtosa amebakia kutapatapa tu bila kuwa na hoja kwani hajui EL anajipanga kumfanya nini.

Kwa maneno hayo hapo juu hakuna wa kumzuia EL kuwa the next president labda kifo
 
Mzee mwanakijiji salam na heshima natangliza;
Ninachosoma hapo juu kinanizungusha kichwa kidogo na naamini sitakua peke kwani nimeona wachangiaji kadhaa wameleweshwa na main Thread uliyotuwekea hapa.
Hivi KWELI UNA HAKIKA NA IMANI kuwa LOWASA ni **** wa mtaani kiasi hichooooooo??? awe hana KOSA LOLOTE na AKAACHE NAFASI KAMA WAZIRI MKUU ati kwa KUMKOMOA KIKWETE!!! kumkomoa for WHAT???
Ati lowasa kasaidia kumuweka Kikwete madarakani (pengine) Lakini Lowasa huyo ana kura moja tu Hata ukijumlisha familia yake marafiki na hao atakaowapa hongo wakati wa kampeni bado walikuwa na hiyari ya kutumia kura zao watakavyo.Na kama alikuwa na nguvu na uwezo huo kwa nini asingeutumia na kugombea yeye nafasi ya Urais. Jibu liko wazi WATANZANIA wote tunakumbuka alivyoumbuliwa na Baba wa Taifa hayati Mwl Nyerere kuwa nafasi hiyo haimfai kutokana na TABIA zake in fact Kikwete ni wa kujilaumu mwenyewe kwani the WRITING WERE ON THE LOWASAS FACE kwa kipofu kuweza kuona na kujua kuwa hafai. Kwa hiyo Kikwete asingejitendea HAKI kama angeruhusu URAFIKI UMPONZE kwa mara ya pili.Kama siasa na dhamana zina fadhila basi Kikwete alilipa kwa Lowasa, ilikuwa ni wajibu wa Lowasa kutambua na kuafanya KAZI ALIYOPEWA KWA ADABU. Sasa MMJJ Lowasa kaonewa ??? au Kajionea??? na wewe unaonaje arudishiwe ofisi yake?? AU unamenej kampeni yake ya 2010??

Mkuu sidhani kama hakuna asiyefahamu kuwa EL na RA ndio walikuwa formidable force of CCM mtandao. Walikuwa ni architects na finacniaers wa fitna, they basically funded mtandao wote, na ndio maana they needed something in return after putting JK in power.

KUna siku JK alisema huu urais ni wake na hakuingia ubia na mtu yoyote, alisema anashare urais na Shein....kama ungeangalia undani wa maneno yale basi ungejua kuwa he was trying to send his message cowardly. Mwanzoni alidhani kuwa mtandao walimuingiza madarakani for fun, lakini later on aligundua kuwa he was being used. Kuna siku he was even fooled na kukaa na kuongea na waandishiwa habari kuitetea Richmond.

So you are right kuwa EL alikuwa na kura moja kama mimi na wewe, lakini alikuwa na influence kubwa. Yeye na RA mpaka sasa ni kama bado ni watu wanaoogopwa. Wanaosema kuwa mafisadi wakikamatwa nchi haitatawalika si wajinga. Serikali inaposema inaogopa kuwakamata pamoja na ushahidi wote uliopo si wajinga
 
1. Obama hakumtetea Tom Daschle, wala Bill Richardson, lakini alimtetea Treasury secretary wake.

2. Bush hakumtetea Donald Rumsfield, lakini alimtetea Brown.

3. Rais Kikwete, hakumtetea Waziri Mkuu wake wa kwanza E. Lowassa, lakini Masha ni waziri mpaka leo.

Ahsante.

William.
Haya mkuu,nimekupaata...
 
Back
Top Bottom