Kwanini Kikwete hakusimama na Lowassa?

- Rais anatakiwa kusimamia sheria na maadili, na pia kusimama on principles na kuheshimu maamuzi ya vyombo muhimu vya taifa kama bunge, waziri mkuu wa jamhuri yetu hupendekezwa na rais, na hatimaye hupitishwa na bunge kwa hiyo huwajibika zaidi kwa bunge. Bunge liliompitisha likimuona hafai rais hawezi kuingilia kati.

- Kwenye kuheshimu maamuzi ya bunge, rais wa sasa amekuwa very consistent, na ni lazima ieleweke kuwa sometimes rais knows best on what is national interest na what is not ndio maana tukamchagua kuwa rais wetu.

- Katika mkutano mmoja na waandishi wa habari pale Diamond wakati wa wahujumu uchumi, Mwalimu aliulizwa na Eda Sanga, kama kwa nini anawalinda viongozi kama Sir George Kahama, Mwalimu alijibu kuwa haendeshi taifa kwa kusikiliza maneno ya mtaani.

- Kwa kifupi rais wa jamhuri hawezi ku-respond on kila neno linaloanzishwa mtaani bila ya facts au ushahidi wa kutosha.

William.
ndio maana Nyerere alibadili uteuzi wa, wa kiongozi moja wa juu, baada ya muhusika kumueleza Mke wake, ambaye nae alianza kusherekea kabla ya Taarifa rasimu kutolewa
 
- Kwani katiba yetu inasema nini kuhusu wajibu wa rais wa jamhuri? Maana baadhi yetu wa-Tanzania, kwenye hili la rais kutosimama mbele ya maamuzi ya bunge kuhusiana na Waziri Mkuu wake wa kwanza na waziri wake wa ndani wa sasa ndio hasa moja ya wajibu wake kama rais.

- Kama rais ni kweli ana mapungufu, lakini sio kwenye hili la kutoingilia maamuzi ya maamuzi ya bunge.

- With all due respect, samahani ndugu kwenye hili hutuwakilishi wa-Tanzania wote kama unavyosema hapo juu.



William.

Ha ha ha ha....Wewe ni lini ulichaguliwa kuwa msemaji wa Watanzania? Naona umewekwa hapa kuwakingia kifua mafisadi maana michango yako yote inaonyesha hivyo, kila la heri.
 
ndio maana Nyerere alibadili uteuzi wa, wa kiongozi moja wa juu, baada ya muhusika kumueleza Mke wake, ambaye nae alianza kusherekea kabla ya Taarifa rasimu kutolewa

Mkuu do you mean J.C Malecela?
 
Rais Kikwete na Lowassa hawakukaa chini kuzungumza baada ya tuhuma nzito zilizotolewa Bungeni na hasa maneno makali ya Wabunge mbalimbali. Kwa yeyote aliyesikiliza hoja za Wabunge ni wazi kuwa Waziri Mkuu alikuwa implied na kuna waliothubutu kutaja na majina kabisa.

Kujiuzulu kwa Waziri Mkuu si jambo dogo hata kidogo hata kama mtu humpendi. Moja ni kwa sababu za kikatiba na jingine ni suala la gharama.

Kikatiba, Waziri Mkuu anapojiuzulu Baraza la Mawaziri linavunjika na hivyo Rais anatakiwa kuanza mchakato mpya wa kupata Waziri Mkuu mpya na Baraza jipya la Mawaziri. Sasa kama Taifa hatuwezi kuruhusu iwe rahisi kwa Waziri Mkuu kujiuzulu na kuanza moja kila inapotolewa tuhuma dhidi yake. NI lazima Rais (anayemteua Waziri huyo) kuwa na msimamo unaoeleweka ili wananchi waridhike kuwa kweli kosa fulani la Waziri Mkuu linamstahilisha kujiuzulu.

Sasa Waziri Mkuu anapotolewa tuhuma nzito ni wajibu wa Rais kumuita na kumsikiliza kabla Waziri huyo hajafanya uamuzi wowote wa papara (kama wa Lowassa). Kwa wanaokumbuka Rais alikuwa mikoa ya Kusini na Makamu alikuwa sehemu nyinyine na wao kama Taifa zima walisikia kujiuzulu kwa Lowassa "radioni". Kwanini Kikwete hakumuita Waziri wake Mkuu na kuhoji tuhuma dhidi yake na kusikia utetezi wake?

Mkuu naamini huna uhakika wa hili. INASEMEKANA kwamba, Rais alikutana na PM wake na kuongelea mambo haya.

Kwa taratibu, katika hoja za nguvu kama zilivyotolewa na wabunge, Kamati Kuu ya NEC hukutana na kujadili nini cha kufanya. Inasemekana kuwa, CC-NEC ilimtaka PM ajiuzuru ili kulinda heshima ya Rais na Serikali. Hapo ndipo PM alipomuuliza Rais nae akasema sina pingamizi. Hivyo uamuzi wa PM ukawa ni kujiuzuru.

Wakati kikao cha Bunge kikizungumzia masuala ya Richmond, Makamu wa Rais alikuwa Arusha na Rais alikuwa Dar. Wote walikutana Dodoma kabla hata PM hajatangaza kujiuzuru. Rais alikutana na Kamati Kuu ya CCM Taifa kabla hata PM wake hajajiuzuru. Na kuna tetesi pia kuwa, Rais alishaamua kuwa atamteua MPP hata kabla EL hajajiuzuru.

Kigharama, kujiuzulu kwa Waziri Mkuu kunasababisha gharama zisizo za lazima za kuunda Wizara mpya au kuingiza mawaziri wapya. Kikwete alilazimika kuunda wizara mpya na kuleta mawaziri wapya na yote hayo yana gharama. Hivyo, hatuwezi kuchukuliwa kwa urahisi tu kujiuzulu kwa Waziri Mkuu kana kwamba ni kitu kidogo.

Kweli kabisa

Pia watu wanasahau kikao alichofanya Rais Kikwete na wazee wa Dar kuelezea mshtuko wake wa kujiuzulu kwa Lowassa. Tukumbuke kuwa Kikwete hakusema Lowassa amefanya makosa yoyote na alisema kuwa kujiuzulu kwa Lowassa kulikuwa ni kwa "ajali ya kisiasa". Sasa kama Rais alijua Lowassa hakufanya makosa kwanini hakusimama naye na kuepusha maamuzi ya kisiasa?

Je, tunaweza kukubali hizi "ajali za kisiasa" kwa kushindwa kuzizuia?

Rais hakushtushwa na kujiuzuru kwa EL hata kidogo. Ila naweza kusema alisikitishwa kwa uhakika.

Ni lazima tuzoee kuwa kujiuzuru katika dhamana ya umma ni jambo la lazima kama umevunja sheria za nchi au sheria za utumishi wa umma. Haiwezekani watu wakamezeana kwa kila jambo baya linalotendwa kwa kuogopa gharama ambazo zingeweza kukwepwa kwa kufanya uteuzi makini na kuwa na control kwa watu wanaoteuliwa.

Kama hakukuwa na ushahidi wa moja kwa moja wa Lowassa kunufaika na mkataba wa Richmond, kama hakukuwa na ushahidi wa moja kwa moja wa kuonesha kuwa Lowassa ndiye Richmonduli, kama Kamati haikuweza kuonesha kuwa mtoto wa Lowassa ndiye alihusika na Richmond na kwa mujibu wa sheria ya Maadili huo ni mgongano wa Maslahi kwa Lowassa, ninajiuliza Lowassa alijiuzulu kwa sababu gani hasa?
Inavyoonekana ni kuwa EL alijiuzuru kwasababu asingefanya hivyo Bunge lingeweza kumtaka ajiuzuru kwa kupiga kura za kutokuwa na imani nae. Uwezekano huo ulikuwepo. Hivyo, aliona ni busara zaidi kujiuzuru kuliko kulazimishwa kwa njia ya kura za maoni za Wabunge.

Nakubaliana na wewe sana kuwa, kama Rais angeamua kuliomba Bunge kuelewa kilichotokea, kwa yeye kuwa na imani kwamba hakukuwa na makosa yaliyofanywa moja kwa moja na waziri wake Mkuu, Bunge lingeweza kutoa onyo kali kwa PM na mambo yangekwisha na EL angeweza kuwa PM hadi leo.

Jibu ni kuwa Lowassa alijiuzulu ili kumkomoa Kikwete! Alijiuzulu kama spite ya Kikwete na urafiki wao; hakujiuzulu kwa sababu nyingine yoyote isipokuwa kwa sababu rafiki yake, mtu aliyehangaika kumuweka madarakani na mtu ambaye kwa kiasi kikubwa ni mshirika wake wa kisiasa alimtosa wakati alipotakiwa kusimama naye.
Hili pia linawezekana. Japokuwa kwa kufanya hivyo hakumuongezei/hakukumuongezea sifa yoyote ya maana kisiasa.

Je, ina maana kwa Kikwete kusimama na Lowassa kunamfanya Lowassa asiwe na makosa? Na kama alikuwa na makosa ni kweli yalimstahilisha ajiuzulu kwa namna ile ya utekaji nyara nchi?

Hapana, naamini kuwa kama Rais angesimama na EL katika yaliyomkuta, kusingefuta makosa yoyote ya EL, hata kidogo. Kwa kutegemea jinsi gani Rais angesimamia hoja, kungeweza kumuingiza Rais katika kashfa ile (angekuwa amenunua kesi) na angeweza kupoteza imani ya wananchi kwake, ama kungeweza kuisafisha serikali yake vizuri sana. Yote yanawezekana. Ila uangalifu mkubwa ulihitajika katika kuamua Rais awe upande gani. Nadhani pia alishauriwa aachie uhuru wa Bunge kufanya kazi yake.
 
- Rais alikuwepo Dodoma, Ikulu ya Chamwino siku waziri mkuu wake wa kwanza alipojiuzulu.

Nadhani uko sahihi; lakini Kikwete hakujua wala kamati yao haikujua Lowassa anajiuzulu siku ile. Hili nina uhakika nao.

- Suala zima la kujiuzulu kwa waziri mkuu Mh. E. Lowassa, lilikuwa handled na bunge kama katiba yetu inavyosema, rais wetu aliheshimu mgawanyo wa madaraka kati ya bunge, Mahakama na Ikulu.

Hapana, kujiuzulu kwa Waziri Mkuu Bunge halina usemi nao. Bunge lina uwezo wa kumpigia kura ya kutokuwa na imani waziri mkuu na kumlazimisha kuondoka, lakini anapoamua kujiuzulu Bunge halina usemi hadi wasikie majibu ya Rais. Ndiyo sababu ya Spika kuahirisha Bunge kufuatia pendekezo la Masilingi ili awasiliane na Rais kwanza.
- Kwa kutoingilia kati maamuzi ya bunge, rais wetu aliheshimu katiba, na anahitaji heshima kubwa for that, kwa sababu aliweka msingi mzito wa kuheshimu katiba kwa kizazi kijacho

Hapana kwa kutokusimama na Waziri wake Mkuu au kushauriana naye kabla hajaleta hoja yake Bungeni, Rais wetu alionesha udhaifu mkubwa wa uongozi na kusababishia Taifa usumbufu mkubwa usio wa lazima.
 
Mwanakijiji,

..hoja yako hii inanifanya nirudi kwenye ripoti ya kamati ya uchunguzi ya Bunge iliyoongozwa na Dr.Mwakyembe.

..katika ripoti hiyo kuna taarifa za Waziri Mkuu Lowassa kukiuka maamuzi ya vikao vya baraza la mawaziri ktk mchakato wa mkataba wa Richmond.

..siamini kama Raisi hakuwa na habari kwamba Waziri Mkuu wake alikuwa akikiuka maamuzi ya vikao alivyoviongoza Raisi mwenyewe.

..mipaka ya kimadaraka ya Waziri Mkuu wa Tanzania haimruhusu kufanya jambo lolote lile la kuingilia maamuzi ya waziri mwingine, au kumshinikiza waziri huyo, bila baraka za Raisi.


..Waziri Mkuu Kawawa alipokwenda mbali na Azimio la Arusha mpaka kufunga maduka binafsi ya nyama, Mwalimu Nyerere alitamka waziwazi kwamba hakumtuma kufanya hivyo. sasa kwanini Raisi Kikwete amekosa ujasiri wa kutamka kwamba hakumtuma Waziri Mkuu Lowassa kuingilia na kuvuruga mchakato wa mkataba wa Richmond?

..kauli ya Raisi kwamba kujiuzulu kwa Waziri Mkuu Edward Lowassa ni "ajali ya kisiasa" kunazidi kunishawishi kwamba madudu aliyokuwa akiyafanya yalikuwa na baraka za Raisi.

..swali langu ni hili: kama Raisi alisimama upande wa Lowassa wakati akivuruga na kuingilia mchakato wa mkataba wa Richmond, kwanini alishindwa kumtetea wakati alipopata matatizo?


NB:

..Lowassa alisema bungeni kitu kama shida yao ni waziri mkuu/uwaziri mkuu etc etc.

..hiyo nayo inaweza kumshawishi mtu aamini kwamba Lowassa alikuwa "bangusilo" tu.

..PAMOJA NA HAYO, NILIFURAHIA KUONDOLEWA KWA LOWASSA KUTOKANA NA KASHFA HII -- HATA KAMA HAKUWA "KILONGOLA."

..vilevile Dr.Mwakyembe alidai kuna mambo hakuyaweka ktk ripoti yake ambayo yangeweza kuiaibisha serikali.

..sasa ni aibu gani hiyo iliyofichwa inayozidi ile ya Waziri Mkuu wa Tanzania kuwa implicated kiasi kile?
 
Last edited:
- Rais anatakiwa kusimamia sheria na maadili, na pia kusimama on principles na kuheshimu maamuzi ya vyombo muhimu vya taifa kama bunge, waziri mkuu wa jamhuri yetu hupendekezwa na rais, na hatimaye hupitishwa na bunge kwa hiyo huwajibika zaidi kwa bunge. Bunge liliompitisha likimuona hafai rais hawezi kuingilia kati.

- Kwenye kuheshimu maamuzi ya bunge, rais wa sasa amekuwa very consistent, na ni lazima ieleweke kuwa sometimes rais knows best on what is national interest na what is not ndio maana tukamchagua kuwa rais wetu.

- Katika mkutano mmoja na waandishi wa habari pale Diamond wakati wa wahujumu uchumi, Mwalimu aliulizwa na Eda Sanga, kama kwa nini anawalinda viongozi kama Sir George Kahama, Mwalimu alijibu kuwa haendeshi taifa kwa kusikiliza maneno ya mtaani.

- Kwa kifupi rais wa jamhuri hawezi ku-respond on kila neno linaloanzishwa mtaani bila ya facts au ushahidi wa kutosha.

William.

Rais pia anatakiwa kuhakikisha kwamba ufujaji wa mali ya umma na rasilimali kwa wizi au ufisadi kama uliofanywa kwenye pesa za EPA, Rada, Kagoda, Gharama za ujenzi wa Twin Towers, Richmond/Dowans, Meremeta, Deep Greens, Kiwira, mikataba ya uchimbaji wa dhahabu.

Itakuwa ni kichekecho na uzembe wa hali ya juu kwa Rais wa chi kunyamaza kimya pale watendaji wake wengi aliowateua katika nyadhifa mbali mbali ambao wanaonyesha dhahiri kwamba utendaji wao katika nyadhifa mbali mbali walizopewa ni mdogo mno au umegubikwa na ufisadi.

Kutokana na tuhuma mbali mbali kuna viongozi ambao walitakiwa wawe wameondolewa madarakani siku nyingi sana.
Kwa mfano kamati ya Mwakyembe ilishauri kuondolewa kwa Mkuu wa TAKUKURU, na Mwanasheria Mkuu lakini hadi hii leo bado wapo madarakani na Rais hajasema lolote, yaliyosemwa na kamati ya Mwakyembe si maneno ya mtaani.

Baada ya aliyekuwa gavana wa BoT Ballali kukimbia nchi, Serikali ilikuwa na muda wa kutosha kuhakikisha anahojiwa ili kupata ushahidi toka kwake kutokana na wizi mkubwa wa shilingi 133 billioni lakini Rais hakuona umuhimu wa kufanya hivyo hata pale ambapo aliyekuwa balozi wa Marekani nchini alipotamka hadharani kwamba nchi yake ipo tayari kuisaidia Tanzania kumrudisha Ballali nchini ili ajibu tuhuma dhidi yake kama ikiombwa kufanya hivyo. Kikwete alinyamaza kimya badala ya kuichangamkia offer hiyo toka Marekani.

Swala la ununuzi wa Rada. Yule mhindi aliyekuwa kama wakala na kujipatia bilioni 12 za pesa za Watanzania alikuwa tayari ameshaanza kuhojiwa na vyombo vya habari. Kwa mshangao wa wengi hakuwekwa rumande ili kusaidia uchunguzi uliokuwa unaendelea na hatimaye akaweza kutoroka na hadi hii leo hakuna yeyote katika vyombo vya dola aliyechukuliwa hatua zozote kufuatia kutoroka kwa yule wakala. Na kushindwa kumchukulia hatua yeyote kunaonysha uzembe wa hali ya juu katika ngazi za juu kabisa za serikali.

Aliahidi kuipitia upya mikataba ya uchimbaji wa dhahabu. Sidhani kama inahitaji miaka minne kutoa agizo kwamba mikataba ya uchimbaji wa dhahabu ambayo haina maslahi kwa nchi ipitiwe ili kuhakikisha inakuwa modified kwa maslahi ya Watanzania. Huu pia ni uzembe mwingine.

Kiwira si maneno ya mtaani. Kuna ushahidi wa kutosha kwamba Mkapa na Yona walijiuzia mgodi ule kwa njia za kifisadi, vinginevyo wangezungumza siku nyingi sana jinsi walivyojiuzia mgodi ule. Kunyamaza kwa Kikwete katika hili pia ni dalili za kwamba hawezi kusimamia haki ndani ya nchi yetu ili kuhakikisha kwamba maslahi ya Watanzania siku zote yanalindwa bila woga wowote ule

Kwa kifupi kunapokuwa na uzembe katika utendaji wa viongozi mbali mbali walioteuliwa na Ris na Rais akakaa kimya kuhusu uzembe huo, basi hii ni dalili ya kutosha kabisa kwamba Rais ameshindwa katika uongozi. Pia kuna ahadi Kikwete alizotoa wakati wa kampeni yake hadi hii leo hajazitimiza na wala hajatoa kauli yoyote kuhusu kikwazo cha kutimiza ahadi hizo. Kwa mfano ahadi ya kuipitia mikataba ya uchimbaji wa dhahabu, ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya na maisha bora kwa kila Mtanzania…(oops! Hili tunajua kwamba uchumi wa dunia umetetereka pamoja na hayo hatukuona sera zozote zile za kufanikisha ahadi hii maana tunajua mabilioni ya Kikwete yalikupotelea tena hakuna hata uwajibikaji wa kuonyesha pesa hizo zimewasaidia vipi Watanzania na mabilioni mangapi yametolewa. Huu ni ushahidi tosha kwamba Kikwete awamu moja inamtosha kabisa hana sifa yoyote ile ya kuongezewa awamu nyingine hapo 2010.

Wakati umefika wa Watanzania kuacha unafiki wa kuwasifia viongozi ambao hawana uwezo wa kuliongoza Taifa letu, kufanya hivyo kutalisaidia Taifa letu ambalo miaka nenda miaka rudi pamoja na misaada na mikopo chungu nzima toka kwa nchi za wafadhili na mashirika mbali mbali ya kimataifa na rasilimali chungu nzima tulizojaliwa na Mwenyezi Mungu bado asilimia kubwa ya Watanzania wanaishi maisha ya umaskini wa kutisha.
 
... lakini Kikwete hakujua wala kamati yao haikujua Lowassa anajiuzulu siku ile. Hili nina uhakika nao.

Uhakika wako si sahihi.

Kikwete alijua, tena alikuwa wa kwanza kujua, siku ile kwamba Lowassa atajiuzulu.

Edward Lowassa: Mheshimiwa Spika, nimetafakari sana kwa niaba ya chama changu, kwa niaba ya Serikali yangu nimeamua kumwandikia Rais barua ya kumwomba niachie ngazi.
 
- Rais anatakiwa kusimamia sheria na maadili, na pia kusimama on principles na kuheshimu maamuzi ya vyombo muhimu vya taifa kama bunge, waziri mkuu wa jamhuri yetu hupendekezwa na rais, na hatimaye hupitishwa na bunge kwa hiyo huwajibika zaidi kwa bunge. Bunge liliompitisha likimuona hafai rais hawezi kuingilia kati.

Hapa swali ni je, Raisi anafungwa mikono asiweze kumwondoa Waziri Mkuu bila baraka za Bunge ?

- Kwenye kuheshimu maamuzi ya bunge, rais wa sasa amekuwa very consistent, na ni lazima ieleweke kuwa sometimes rais knows best on what is national interest na what is not ndio maana tukamchagua kuwa rais wetu.

Una hakika na unayosema ama ndiyo yale yale CCM knows best what's good for the country.

- Katika mkutano mmoja na waandishi wa habari pale Diamond wakati wa wahujumu uchumi, Mwalimu aliulizwa na Eda Sanga, kama kwa nini anawalinda viongozi kama Sir George Kahama, Mwalimu alijibu kuwa haendeshi taifa kwa kusikiliza maneno ya mtaani.

Yapi hayo maneno ya mitaani - EPA, Richmond, Meremeta, Tangold, Kiwira, Dowans, IPTL, List of Shame, Twin Towers, Kagoda ?

- Kwa kifupi rais wa jamhuri hawezi ku-respond on kila neno linaloanzishwa mtaani bila ya facts au ushahidi wa kutosha.

Ndiyo hawezi kwa sababu hana ubavu wala ujasiri wa ku'act'. Naamini Lowassa angekataa kujiuzulu, ingekuwa kasheshe.


Kazi kweli kweli !! Kwa mwendo huu mkate wa Salva uko hatarini.
 
Uhakika wako si sahihi.

Kikwete alijua, tena alikuwa wa kwanza kujua, siku ile kwamba Lowassa atajiuzulu.

Edward Lowassa: Mheshimiwa Spika, nimetafakari sana kwa niaba ya chama changu, kwa niaba ya Serikali yangu nimeamua kumwandikia Rais barua ya kumwomba niachie ngazi.

Huo unaweza kuuita ushahidi ?
 
Ndio ni ushahidi.

Waziri Mkuu anapotamka hadharani, Bungeni, kwamba ameshamuandikia Rais barua hawezi kuwa anaongopa. Hawezi kusema tu halafu kutoka hapo ndio akakimbia kuandika na kutuma hiyo barua.

Tunaongelea barua kutoka ofisi ya Waziri Mkuu kwenda Ikulu, zinafika almost papo hapo na zina rekodi. Barua za kawaida za mitaani tu zina rekodiwa zimekuwa dispatched lini, sembuse ya kutoka Ikulu. Asingeweza kuja kuongopa "nilituma juzi, kwani hukuipata"? Kuna rekodi ya time line.

Na sidhani kama unaweza kutangaza umejiuzulu kabla ya kukubaliwa kujiuzulu.

Kikwete alijua, alikuwa wa kwanza kujua, kwamba Lowassa atajiuzulu.

Edward Lowassa: Mheshimiwa Spika, nimetafakari sana kwa niaba ya chama changu, kwa niaba ya Serikali yangu nimeamua kumwandikia Rais barua ya kumwomba niachie ngazi.
 
Rais Kikwete na Lowassa hawakukaa chini kuzungumza baada ya tuhuma nzito zilizotolewa Bungeni na hasa maneno makali ya Wabunge mbalimbali. Kwa yeyote aliyesikiliza hoja za Wabunge ni wazi kuwa Waziri Mkuu alikuwa implied na kuna waliothubutu kutaja na majina kabisa.

Kujiuzulu kwa Waziri Mkuu si jambo dogo hata kidogo hata kama mtu humpendi. Moja ni kwa sababu za kikatiba na jingine ni suala la gharama.

Kikatiba, Waziri Mkuu anapojiuzulu Baraza la Mawaziri linavunjika na hivyo Rais anatakiwa kuanza mchakato mpya wa kupata Waziri Mkuu mpya na Baraza jipya la Mawaziri. Sasa kama Taifa hatuwezi kuruhusu iwe rahisi kwa Waziri Mkuu kujiuzulu na kuanza moja kila inapotolewa tuhuma dhidi yake. NI lazima Rais (anayemteua Waziri huyo) kuwa na msimamo unaoeleweka ili wananchi waridhike kuwa kweli kosa fulani la Waziri Mkuu linamstahilisha kujiuzulu.

Sasa Waziri Mkuu anapotolewa tuhuma nzito ni wajibu wa Rais kumuita na kumsikiliza kabla Waziri huyo hajafanya uamuzi wowote wa papara (kama wa Lowassa). Kwa wanaokumbuka Rais alikuwa mikoa ya Kusini na Makamu alikuwa sehemu nyinyine na wao kama Taifa zima walisikia kujiuzulu kwa Lowassa "radioni". Kwanini Kikwete hakumuita Waziri wake Mkuu na kuhoji tuhuma dhidi yake na kusikia utetezi wake?

Kigharama, kujiuzulu kwa Waziri Mkuu kunasababisha gharama zisizo za lazima za kuunda Wizara mpya au kuingiza mawaziri wapya. Kikwete alilazimika kuunda wizara mpya na kuleta mawaziri wapya na yote hayo yana gharama. Hivyo, hatuwezi kuchukuliwa kwa urahisi tu kujiuzulu kwa Waziri Mkuu kana kwamba ni kitu kidogo.

Pia watu wanasahau kikao alichofanya Rais Kikwete na wazee wa Dar kuelezea mshtuko wake wa kujiuzulu kwa Lowassa. Tukumbuke kuwa Kikwete hakusema Lowassa amefanya makosa yoyote na alisema kuwa kujiuzulu kwa Lowassa kulikuwa ni kwa "ajali ya kisiasa". Sasa kama Rais alijua Lowassa hakufanya makosa kwanini hakusimama naye na kuepusha maamuzi ya kisiasa?

Je, tunaweza kukubali hizi "ajali za kisiasa" kwa kushindwa kuzizuia?

Kidemokrasia, naamini Watanzania tulinyimwa nafasi ya kuona demokrasia yetu inavyoweza kufanya kazi unapotokea mgongano kati ya Bunge na Rais. Kikwete angeweza kukaa na Lowassa, kuangalia ushahidi uliotolewa na Kamati Teule, kupima uzito wa hoja za wabunge na kuandaa majibu kwa kila hoja.

Ninaamini hakuna mwanasiasa wa Tanzania ambaye angeweza kupangua hoja za kamati teule kwa urahisi na kwa umahiri kama siasa (na hapa namaanisha). Ingekuwa vizuri kweli kwa Rais Kikwete kuchukua upande wa Waziri wake Mkuu ili tuone mgongano kati ya Mwenyekiti wa CCM na wabunge wa CCM! Je, kweli mnafikiri Bunge la CCM lingeweza kwenda kinyume na Rais wake? Je wale waliokuwa vinara wangeweza kuendelea kuwa vinara baada ya Rais kuchukua msimamo wa kumtetea Lowassa? Je yawezekana ushujaa wao ni kwa sababu Kikwete hakuchukua msimamo na hivyo ni kuwa kama bingwa ambaye hakutaka kuingilia mapambano ya ridhaa!?

Kama hakukuwa na ushahidi wa moja kwa moja wa Lowassa kunufaika na mkataba wa Richmond, kama hakukuwa na ushahidi wa moja kwa moja wa kuonesha kuwa Lowassa ndiye Richmonduli, kama Kamati haikuweza kuonesha kuwa mtoto wa Lowassa ndiye alihusika na Richmond na kwa mujibu wa sheria ya Maadili huo ni mgongano wa Maslahi kwa Lowassa, ninajiuliza Lowassa alijiuzulu kwa sababu gani hasa?

Jibu ni kuwa Lowassa alijiuzulu ili kumkomoa Kikwete! Alijiuzulu kama spite ya Kikwete na urafiki wao; hakujiuzulu kwa sababu nyingine yoyote isipokuwa kwa sababu rafiki yake, mtu aliyehangaika kumuweka madarakani na mtu ambaye kwa kiasi kikubwa ni mshirika wake wa kisiasa alimtosa wakati alipotakiwa kusimama naye.

Je, ina maana kwa Kikwete kusimama na Lowassa kunamfanya Lowassa asiwe na makosa? Na kama alikuwa na makosa ni kweli yalimstahilisha ajiuzulu kwa namna ile ya utekaji nyara nchi?

Umeamkia upande gani kaka! Kwa mara ya kwanza sipati maana ya maandiko yako kabisa - na taarifa zako zimekuwa za kufikirika! Ama unataka tufanye zoezi la kinadharia tu hapa! Naona unajaribu kutafuta sababu ya supu kuchacha wakati supu ilishamwaga - ama kunasupu nyingi inakaribia kuchacha?
 
Umeamkia upande gani kaka! Kwa mara ya kwanza sipati maana ya maandiko yako kabisa - na taarifa zako zimekuwa za kufikirika! Ama unataka tufanye zoezi la kinadharia tu hapa! Naona unajaribu kutafuta sababu ya supu kuchacha wakati supu ilishamwaga - ama kunasupu nyingi inakaribia kuchacha?

Inawezekana nia ya MKJJ ni kuwapambanisha EL na JK maana keshaona zaidi ya hapo nothing else will happen,JK amecheza kama opportunist,na hivyo kuna wale wanaotaka kuona EL VS JK,Tusubiri if thats possible...It depends on who is willing to loose what and vice versa also the consequences of either or.
 
Ndio ni ushahidi.

Waziri Mkuu anapotamka hadharani, Bungeni, kwamba ameshamuandikia Rais barua hawezi kuwa anaongopa. Hawezi kusema tu halafu kutoka hapo ndio akakimbia kuandika na kutuma hiyo barua.

Ndiyo maana huwa nasema soma kilichoandikwa; Lowassa alisema hivi:

"nimeamua kumwandikia Rais barua ya kumwomba niachie ngazi."

Sasa umesoma wapi kuwa amesema ameandika barua ya kuomba kujiuzulu?

Tunaongelea barua kutoka ofisi ya Waziri Mkuu kwenda Ikulu, zinafika almost papo hapo na zina rekodi. Barua za kawaida za mitaani tu zina rekodiwa zimekuwa dispatched lini, sembuse ya kutoka Ikulu. Asingeweza kuja kuongopa "nilituma juzi, kwani hukuipata"? Kuna rekodi ya time line.

Ni uamuzi tu tunauzungumzia. Unajuaje kama barua ilikuwa inaandikwa baada ya hotuba yake hiyo maana amesema tu "nimeamua" hajasema "Nimeandika barua kwa Rais".. ni vitu viwili tofauti. Yawezekana (na ndivyo ilivyokuwa) wakati anazungumza ndiyo barua inaenda kwa Rais. Vinginevyo tukiamini kuwa Rais alijua ina maana alimficha Spika kitu ambacho Spika anasema hakuwa na mawasiliano na aliyemteua (Rais).

Na sidhani kama unaweza kutangaza umejiuzulu kabla ya kukubaliwa kujiuzulu.

Ni wazi hukumbuki kilitokea nini Bungeni. Kaangalie rekodi zao.

Kikwete alijua, alikuwa wa kwanza kujua, kwamba Lowassa atajiuzulu.

Katika maneno ya Lowassa na katika mjadala wa Bunge hakuna ushahidi huo, pia zingatia hotuba ya Rais kwa wazee wa Jiji la Dar.
 
Umeamkia upande gani kaka! Kwa mara ya kwanza sipati maana ya maandiko yako kabisa - na taarifa zako zimekuwa za kufikirika! Ama unataka tufanye zoezi la kinadharia tu hapa! Naona unajaribu kutafuta sababu ya supu kuchacha wakati supu ilishamwaga - ama kunasupu nyingi inakaribia kuchacha?

Ahsante,

Ndiyo maana niliuliza

Is this anything than an exercise in futile, and flawed at that, rhetoric ?

Mwanakijiji kama mtu uliyemsema sana Lowassa unashangaa nini kikwete alivyomtosa? Asingemtosa napo ungeandika makala ya kushangaa equally?
 
Ndiyo maana huwa nasema soma kilichoandikwa; Lowassa alisema hivi:

"nimeamua kumwandikia Rais barua ya kumwomba niachie ngazi."

Sasa umesoma wapi kuwa amesema ameandika barua ya kuomba kujiuzulu?



Ni uamuzi tu tunauzungumzia. Unajuaje kama barua ilikuwa inaandikwa baada ya hotuba yake hiyo maana amesema tu "nimeamua" hajasema "Nimeandika barua kwa Rais".. ni vitu viwili tofauti. Yawezekana (na ndivyo ilivyokuwa) wakati anazungumza ndiyo barua inaenda kwa Rais. Vinginevyo tukiamini kuwa Rais alijua ina maana alimficha Spika kitu ambacho Spika anasema hakuwa na mawasiliano na aliyemteua (Rais).



Ni wazi hukumbuki kilitokea nini Bungeni. Kaangalie rekodi zao.



Katika maneno ya Lowassa na katika mjadala wa Bunge hakuna ushahidi huo, pia zingatia hotuba ya Rais kwa wazee wa Jiji la Dar.

Hivi MKJJ anaweza akaandika barua kama hajaamua?
Nadhani hiyo ni past tense so na kwa maana hiyo aliposema "Ameamua" kwa wakati ule,ina maana kwamba ni jambo ambalo alishalifanyia maamuzi na kulitekeleza,unless kuna technicallities hapo mtueleze...Nilivyoelewa mimi hilo alilizungumzia kama past tense.
 
Ahsante,

Ndiyo maana niliuliza



Mwanakijiji kama mtu uliyemsema sana Lowassa unashangaa nini kikwete alivyomtosa? Asingemtosa napo ungeandika makala ya kushangaa equally?

Una maana gani "kumsema sana"? Hakuna ushahidi wa mimi "kumsema sana" Lowassa.
 
Duh,kweli hapa tutajuwa mengi,kwanza hapo kwenye kuamua kuandika barua,kwasababu atakuwa alilidanganya bunge kama akisema ameamua kuandika barua ya kujiuzulu kwa rais na wakati hakufanya hivyo,hilo pekee lina utata sana.
 
Back
Top Bottom