Kwanini Kikwete hakusimama na Lowassa?

Mkjj,
Hii sentesi ya mwisho inaweza isiwe sahihi. Kumbuka Mkurugenzi wa Tanesco aliandika barua ya kujiuzulu mapema tu na kututangazia Umma. Lakini mheshimiwa alikataa.

Kama mtu ukiteuliwa na Kikwete jua jambo moja.. you are on your own!![/QUOTE]
 
Kwanza ilikuwa ni Rais Bush na Michael Brown kule Lousianna wakati wa Katrina. Wakati kelele zinapigwa za kutaka kichwa cha Brown (mkuu wa FEMA) Bush alifunga safari kujionea na kwa jinsi anavyojua yeye alisimama mbele ya waandishi wa habari na kusema yale maneno ambayo yamebakia kama mwangwi "Brown you are doing a heck of a job".

Bush alisimama na mtu wake aliyemteua licha ya kelele..

Sasa wiki ile iliyopita hata leo hii kumekuwa na kelele za kutaka Waziri wa Fedha wa Marekani Bw. Geithner kujiuzulu. Mara tatu sasa Rais Obama amejitokeza pasipo woga kumtetea mteule wake na kusimama naye na kusema kama kuna mtu anataka wa kumlaumu basi wamlaumu yeye na kamwambia hata akileta barua ya kujizulu hatoikubali (basically asijisumbue).

Obama amesimama na mtu wake aliyemteua!

Ndiposa, nikabakia kujiuliza.. nini kilitokea Februari ile? Kwanini Kikwete hakusimama na mteule wake na kukubali kubeba lawama zote za Richmond yeye mwenyewe? Kwanini hakusimama na Karamagi, Chenge (ya Chenge labda haifai!) au Msabaha?

Je kila watu waliochini yake wakilaumiwa yeye atawatosa tu? NI lini atakubali kubeba lawama na kusema kuwa "mnilaumu mimi"? Je yawezekana tunu hiyo ya kukubali kubeba mzigo kama kiongozi Rais wetu hana na badala yake ni bora watu watoswe ilimradi yeye anaendelea kuonekana ni msafi? Je kuna siku atasimama kuwatetea watu aliowateua au atawaacha wamomonyoke na hivyo kuthibitisha ni jinsi gani asivyo mwangalifu katika uteuzi (maana anashindwa hata kuwatetea!)!

Ninaamini, hakuna wakati ambapo Kikwete alionesha udhaifu mkubwa kama kiongozi kama kushindwa kusimama na Waziri wake Mkuu au kupanga naye mkakati wa kujibu mashambulizi ya Bunge. Ndiyo maana ninaamini Lowassa hana sababu ya kumlaumu mtu mwingine yoyote (siyo Spika, CCM au Mwakyembe) kwa kujiuzulu kwake bali mtu mmoja tu ambaye alishindwa kuchukua msimamo mgumu!

Lakini labda alijua maji yamemwagika? Je kama JK angesimama na Lowassa na kukubali uchafu na lawama zote za Richmond (as a matter of fact nakumbuka mkutano wake na waandishi wa habari nadhani alistahili kuubeba mzigo huo!).

Kama mtu ukiteuliwa na Kikwete jua jambo moja.. you are on your own!!

Mkjj, Kikwete alaumiwe kwa lipi!? Maana tumeshaambiwa na Comical Salva kwamba yeye hahusiki. Hivyo uzembe wote, ufisadi ndani ya Serikali na mashirika ya umma kama ATCL, TANESCO, Harbours n.k. Kikwete hahusiki hivyo tumtafute mwingine wa kumlaumu.

Ndiyo maana nimeshasema hapa jamvini kwa kuwa yeye hahusiki basi hastahili tena kurudishwa madarakani 2010 maana Watanzania tunataka kiongozi anayehusika na lolote lile liwe baya au zuri ndani ya Serikali na vyombo vingine vya umma.
 
Watanzania tunataka kiongozi anayehusika na lolote lile liwe baya au zuri ndani ya Serikali na vyombo vingine vya umma.

- Kwani katiba yetu inasema nini kuhusu wajibu wa rais wa jamhuri? Maana baadhi yetu wa-Tanzania, kwenye hili la rais kutosimama mbele ya maamuzi ya bunge kuhusiana na Waziri Mkuu wake wa kwanza na waziri wake wa ndani wa sasa ndio hasa moja ya wajibu wake kama rais.

- Kama rais ni kweli ana mapungufu, lakini sio kwenye hili la kutoingilia maamuzi ya maamuzi ya bunge.

- With all due respect, samahani ndugu kwenye hili hutuwakilishi wa-Tanzania wote kama unavyosema hapo juu.



William.
 
me nadhani viongozi wataeliwapo kushika au kuongoza nyadhifa mbalimbali(serikalini etc) wanapaswa kwanza kujua na kutambua vyema wako pale kwa ajili ya kulitumikia taifa na kuwatumikia wananchi wao waliowachagua kipindi cha uchaguzi.

Pia kuna mgawanyo wa madaraka kati ya Rais na Wzr Mkuu wake na kila mtu anamipaka yake ya maamuzi katika jambo.Lowassa kwa upande wa pili am sure alijisahau sn kwa kasi ile aliyokuwanayo akajua yy ndie the top, kumbe kuna utaratibu bwana katika serikali.

Na kunavitu ktk scandal ya Richmond au scandal zingine tu ambazo zimo ndani white house na za uhakika nadhani ndizo zilimfanya Rais kutombeba kabisaaaaa.

Na ili kumwelewa vyema Wzr Mkuu aliye jiuzuru ni kupata profile lake tokea alipo anza shughuri zake za kisiasa na kuingia serikali na kujua utendaji wa kazi yake na kujua uwajibikaji wake katika jamii iliyokuwa inamzunguka na tena kwa ukaribu
 
1. Obama hakumtetea Tom Daschle, wala Bill Richardson, lakini alimtetea Treasury secretary wake.

2. Bush hakumtetea Donald Rumsfield, lakini alimtetea Brown.

3. Rais Kikwete, hakumtetea Waziri Mkuu wake wa kwanza E. Lowassa, lakini Masha ni waziri mpaka leo.

Ahsante.

William.

Masha ni waziri mpaka leo lakini Sio kwa sababu ya kutetewa na Kikwete. Kama alifanya kimya kimya kimikakati kwenye vikao vya bia na totoz, hayo ni mengine. Tunachojua mpaka sasa ni kuwa ukiwa na issue yako utaibeba mwenyewe, dont count on the presidaa.
 
Masha ni waziri mpaka leo lakini Sio kwa sababu ya kutetewa na Kikwete. Kama alifanya kimya kimya kimikakati kwenye vikao vya bia na totoz, hayo ni mengine. Tunachojua mpaka sasa ni kuwa ukiwa na issue yako utaibeba mwenyewe, dont count on the presidaa.

- Ni kamati ya bunge na wabunge wengi ndiyo waliomuona waziri mkuu wa kwanza kuwa na utata kwenye Richmond, lakini bunge hilo hilo majuzi lilikataa kujadili hoja ya waziri Masha na vitambulisho,

- Rais wa jamhuri amekua akifuata sana maamuzi ya bunge kwenye kutetea au kutotetea viongozi wake, hizi ni facts sio maoni yangu.


William.
 
Lead post ya mleta hoja ina falacy na matatizo lukuki.

Imejengwa na premise kwamba ilikuwa sawa kwa George Bush na Barack Obama kusimama kidete na viongozi wao walipokuwa matatizoni.

Kwanza, Bush alipata a vicious backlash kwa kusimama na Brown. Haikuwahi kukubalika hata kidogo. Baraka Obama alishambuliwa vikali aliposimama kutetea walioharibu. Mfano ulio wazi -ambao mleta hoja kauficha - ni Tom Daschle, ambae siku moja baada ya kutetewa na Rais, mwenyewe akajitoa. Obama akaonekana kachemsha vibaya sana kutoona mabaya ya mteule mpaka mtu anajitoa mwenyewe.

Mleta hoja kaongelea mfano wa Geithner huku akijua fika kwamba kuna situation ya mtu aliyeharibu zaidi na uteuzi wake kumomonyoka kama wa Lowassa, na Rais aka pay a heavy political price for it.

Moja, la pili ni kwamba mleta hoja alikuwa katika watu waliobeba bango kubwa la kum lambast Lowassa mpaka siku ya mwisho. Nimesikia mpaka ameitwa Lowassa's nemesis, nikasoma alikuwa msumari wa mwisho wa jeneza la kisiasa la Lowassa. Sijui kama yeye ndio alimwangusha Lowassa, sikuwepo jamvini nyakati hizo, but suffice is to say, the commentator reveled, alifurahia sana kuanguka kwa Lowassa kama wengi wetu humu. Sasa leo anajifanya kusema "ukiteuliwa na Kikwete jua uko peke yako"?

Halafu ni lini Lowassa alimlaumu Spika na, au, CCM kwa kuangushwa kwake? Tunajuaje hakumlaumu Kikwete?

Lead post imesheheni ma assumptions na ma premises yalo pinda pinda, na ma double talk ya kumlima Kikwete kwa kushindwa kumlinda Lowassa. Well, tulifurahia kuanguka kwa Lowassa, Mwanakijiji, sasa usianze kusua sua.
 
sababu
hawa ni watu ambao wanatishia usalama wa kikwete
1.msabaha, karamagi - timua character assasination
2.lowasa - timua character assasination na kuhakikisha azinduki tena.

ukurasa mpya watu wake
1.masha
2.membe
3.ngeleja
4.mkullo
5.pinda
anahakikisha kila sehemu ana watu wake
rostam kamwiba kuna msemo unasema muindi anakujali ukiwa nacho tu
kwa hiyo sasa hivi rostam amewakimbia wakina lowasa,karamagi na msabah


hawa ni watu ambao wanatishia usalama wa kikwete lakini ajui hawafanye nini
1.magufuli - minofu (kikwete ajui cha kumfanya) kampa wizara hii ili asisikike
2.mwandosya - umwagiliaji (kikwete ajui cha kumfanya) kampa wizara hii ili asisikike
3.dr shein - vice president (kikwete ajui cha kumfanya) pinda anafanya shughuli za shein nyingi
itakapotokea magufuli, mwandosya au shein kufanya kosa dogo tu ndio itakua mwisho wao
 
1.
Kuhani;404790]Lead post ya mleta hoja ina falacy na matatizo lukuki. Imejengwa katika assumption, au niseme premise, kwamba ilikuwa sawa kwa George Bush na Barack Obama kusimama kidete na viongozi wao walipokuwa matatizoni.Kwanza, Bush alipata a vicious backlash kwa kusimama na Brown. Haikuwahi kukubalika hata kidogo.

- Talking about falacy na matatizo lukuki, US Senate iliposimama kumtetea Clinton na impeachment ya Congress kwani ilikubalika na wananchi wote wa US? Point ya mtoa mada ni rais kusimama au kutosimama na wasaidizi wake aliowachagua mwenyewe wanapokuwa wamekiuka sheria au maadili, lakini sio anything else!

2.
Baraka Obama alishambuliwa vikali aliposimama kumtetea walioharibu. Mfano ulio wazi -ambao mleta hoja kauficha - ni Tom Daschle, ambae siku moja baada ya kutetewa na Rais mwenyewe akajitoa. Obama akaonekana kachemsha vibaya sana kutoona mabaya ya mteule mpaka mtu anajitoa mwenyewe?

- Tom Daschle na Geithner, wote hawakulipa kodi sasa Obama alichemshaje huku Tom akijitoa na mwenziwe akipitishwa na Senate kuwa waziri wa fedha wakati wote walikuwa na tatizo moja tu la kutokulipa kodi?

3.
Mleta hoja kaongelea mfano wa Geithner huku akijua fika kwamba kuna mfano wa mtu ambae aliharibu zaidi na uteuzi wake ulimomonyoka kama wa Lowassa, na Rais aka pay a heavy political price for it.

- Waziri Mkuu wetu wa zamani na waziri wa sasa wa fedha wa US, wote walikutwa na matatizo yanayofanana ya kuliletea taifa hasara, wa US alilazimishwa kulipa huku kwetu aliamua kujiuzulu mwenyewe, kwa hiyo mtoa mada yuko right.

4.
Halafu ni lini Lowassa alimlaumu Spika na, au, CCM kwa kuangushwa kwake? Tunajuaje hakumlaumu Kikwete?

- Hapa uko right 100%.

5.
Lead post imesheheni ma assumptions na ma premises yalo pinda pinda, na ma double talk

- Mhhhhh! ni vyema kutoa boriti kwenye jicho lako kwanza.

Aahsante.

William.
 
Mweeeeee....naona ligi ya kombe la mbuzi inaendelea.....

Ukiondoa vi agenda vingine mlivyonavyo watu, the moral of the story is: lini raisi wetu naye atabeba lawama (when will the buck stop with him?
 
Je Rais anatakiwa kumtetea mteule wake hata pale anapofanya makosa makubwa dhidi ya nchi kama ilivyothibitika kwa Lowassa?
 
Je Rais anatakiwa kumtetea mteule wake hata pale anapofanya makosa makubwa dhidi ya nchi kama ilivyothibitika kwa Lowassa?

Jibu langu ni: Kama anaamini ni kosa anatakiwa KUMFUKUZA KAZI, na kama anaamini sio kosa ila lina mtazamo huo anatakiwa amtetee mbele ya umma, amsafishe. Mheshimiwa hakufanya hata moja kati ya hayo.
 
Je Rais anatakiwa kumtetea mteule wake hata pale anapofanya makosa makubwa dhidi ya nchi kama ilivyothibitika kwa Lowassa?

hamuwezi kufananisha makosa yanayofanywa na viongozi wa TZ na wa ulaya

hao wakina lowasa karamagi na wengine wangekuwa ni viongozi ulaya ungekuta wananyea debe, TZ kama kiongozi asipokupiga risasi awezi kufungwa hata kidogo na hata hiyo risasi inaweza ikageuka ikawa bahati mbaya "there is no justice in TZ".

Fact: makosa ambayo wanatuhumiwa hawa viongozi wa ulaya ingekuwa TZ hata kwenye JF jukwaa la siasa yasingejadiliwa.

eti mnataka kikwete amsaidie lowasa, au mnataka mpaka lowasa ampige mtu risasi wewe mwanakijiji sijui unafikiria nini

hao wakina lowasa wangekuwa marekani ma private lawyers wangejitolea kuwapeleka mahakamani
 
huwezi kusema kuwa mtu ni mchafu hadi uwe na ushahidi! Hata kama ni mchafu kwa masuala mengine, hili lililomwondoa halikuwa na ushahidi. Mwakyembe alitaka kupitisha mambo yake mwenyewe. Ukiongeza na chuki za Sitta kuukosa uPM basi likazuliwa zengwe kuwa Lowassa ana nia ya kumwondoa JK 2010. Kikatafutwa kisingizio cha Richmond.

Jobo,
Ulisikiliza vizuri ripoti ya Mwakyembe dhidi ya Richmond? Lowasa alikuwa ndo kasimama kidete akiagiza nini kifanyike mpaka Richmond wakapewa hiyo tenda. Na kwa taarifa yako ni kwamba aliamua kuiweka pembeni tenda bodi ya TANESCO katika manunuzi hayo akaunda tenda bodi yake ya watu watatu special kushughulikia suala hilo na akafanikiwa, hapo bado unasema hakuhusika? Pia usisahau uswahiba wa EL na Rostam, na huo ilikuwa mradi wao.
 
Je Rais anatakiwa kumtetea mteule wake hata pale anapofanya makosa makubwa dhidi ya nchi kama ilivyothibitika kwa Lowassa?

- Rais anatakiwa kusimamia sheria na maadili, na pia kusimama on principles na kuheshimu maamuzi ya vyombo muhimu vya taifa kama bunge, waziri mkuu wa jamhuri yetu hupendekezwa na rais, na hatimaye hupitishwa na bunge kwa hiyo huwajibika zaidi kwa bunge. Bunge liliompitisha likimuona hafai rais hawezi kuingilia kati.

- Kwenye kuheshimu maamuzi ya bunge, rais wa sasa amekuwa very consistent, na ni lazima ieleweke kuwa sometimes rais knows best on what is national interest na what is not ndio maana tukamchagua kuwa rais wetu.

- Katika mkutano mmoja na waandishi wa habari pale Diamond wakati wa wahujumu uchumi, Mwalimu aliulizwa na Eda Sanga, kama kwa nini anawalinda viongozi kama Sir George Kahama, Mwalimu alijibu kuwa haendeshi taifa kwa kusikiliza maneno ya mtaani.

- Kwa kifupi rais wa jamhuri hawezi ku-respond on kila neno linaloanzishwa mtaani bila ya facts au ushahidi wa kutosha.

William.
 
Kwanza ilikuwa ni Rais Bush na Michael Brown kule Lousianna wakati wa Katrina. Wakati kelele zinapigwa za kutaka kichwa cha Brown (mkuu wa FEMA) Bush alifunga safari kujionea na kwa jinsi anavyojua yeye alisimama mbele ya waandishi wa habari na kusema yale maneno ambayo yamebakia kama mwangwi "Brown you are doing a heck of a job".

Bush alisimama na mtu wake aliyemteua licha ya kelele..

Sasa wiki ile iliyopita hata leo hii kumekuwa na kelele za kutaka Waziri wa Fedha wa Marekani Bw. Geithner kujiuzulu. Mara tatu sasa Rais Obama amejitokeza pasipo woga kumtetea mteule wake na kusimama naye na kusema kama kuna mtu anataka wa kumlaumu basi wamlaumu yeye na kamwambia hata akileta barua ya kujizulu hatoikubali (basically asijisumbue).

Obama amesimama na mtu wake aliyemteua!

Ndiposa, nikabakia kujiuliza.. nini kilitokea Februari ile? Kwanini Kikwete hakusimama na mteule wake na kukubali kubeba lawama zote za Richmond yeye mwenyewe? Kwanini hakusimama na Karamagi, Chenge (ya Chenge labda haifai!) au Msabaha?

Je kila watu waliochini yake wakilaumiwa yeye atawatosa tu? NI lini atakubali kubeba lawama na kusema kuwa "mnilaumu mimi"? Je yawezekana tunu hiyo ya kukubali kubeba mzigo kama kiongozi Rais wetu hana na badala yake ni bora watu watoswe ilimradi yeye anaendelea kuonekana ni msafi? Je kuna siku atasimama kuwatetea watu aliowateua au atawaacha wamomonyoke na hivyo kuthibitisha ni jinsi gani asivyo mwangalifu katika uteuzi (maana anashindwa hata kuwatetea!)!

Ninaamini, hakuna wakati ambapo Kikwete alionesha udhaifu mkubwa kama kiongozi kama kushindwa kusimama na Waziri wake Mkuu au kupanga naye mkakati wa kujibu mashambulizi ya Bunge. Ndiyo maana ninaamini Lowassa hana sababu ya kumlaumu mtu mwingine yoyote (siyo Spika, CCM au Mwakyembe) kwa kujiuzulu kwake bali mtu mmoja tu ambaye alishindwa kuchukua msimamo mgumu!

Lakini labda alijua maji yamemwagika? Je kama JK angesimama na Lowassa na kukubali uchafu na lawama zote za Richmond (as a matter of fact nakumbuka mkutano wake na waandishi wa habari nadhani alistahili kuubeba mzigo huo!).

Kama mtu ukiteuliwa na Kikwete jua jambo moja.. you are on your own!!

Is this anything than an exercise in futile, and flawed at that, rhetoric ?
 
Rais Kikwete na Lowassa hawakukaa chini kuzungumza baada ya tuhuma nzito zilizotolewa Bungeni na hasa maneno makali ya Wabunge mbalimbali. Kwa yeyote aliyesikiliza hoja za Wabunge ni wazi kuwa Waziri Mkuu alikuwa implied na kuna waliothubutu kutaja na majina kabisa.

Kujiuzulu kwa Waziri Mkuu si jambo dogo hata kidogo hata kama mtu humpendi. Moja ni kwa sababu za kikatiba na jingine ni suala la gharama.

Kikatiba, Waziri Mkuu anapojiuzulu Baraza la Mawaziri linavunjika na hivyo Rais anatakiwa kuanza mchakato mpya wa kupata Waziri Mkuu mpya na Baraza jipya la Mawaziri. Sasa kama Taifa hatuwezi kuruhusu iwe rahisi kwa Waziri Mkuu kujiuzulu na kuanza moja kila inapotolewa tuhuma dhidi yake. NI lazima Rais (anayemteua Waziri huyo) kuwa na msimamo unaoeleweka ili wananchi waridhike kuwa kweli kosa fulani la Waziri Mkuu linamstahilisha kujiuzulu.

Sasa Waziri Mkuu anapotolewa tuhuma nzito ni wajibu wa Rais kumuita na kumsikiliza kabla Waziri huyo hajafanya uamuzi wowote wa papara (kama wa Lowassa). Kwa wanaokumbuka Rais alikuwa mikoa ya Kusini na Makamu alikuwa sehemu nyinyine na wao kama Taifa zima walisikia kujiuzulu kwa Lowassa "radioni". Kwanini Kikwete hakumuita Waziri wake Mkuu na kuhoji tuhuma dhidi yake na kusikia utetezi wake?

Kigharama, kujiuzulu kwa Waziri Mkuu kunasababisha gharama zisizo za lazima za kuunda Wizara mpya au kuingiza mawaziri wapya. Kikwete alilazimika kuunda wizara mpya na kuleta mawaziri wapya na yote hayo yana gharama. Hivyo, hatuwezi kuchukuliwa kwa urahisi tu kujiuzulu kwa Waziri Mkuu kana kwamba ni kitu kidogo.

Pia watu wanasahau kikao alichofanya Rais Kikwete na wazee wa Dar kuelezea mshtuko wake wa kujiuzulu kwa Lowassa. Tukumbuke kuwa Kikwete hakusema Lowassa amefanya makosa yoyote na alisema kuwa kujiuzulu kwa Lowassa kulikuwa ni kwa "ajali ya kisiasa". Sasa kama Rais alijua Lowassa hakufanya makosa kwanini hakusimama naye na kuepusha maamuzi ya kisiasa?

Je, tunaweza kukubali hizi "ajali za kisiasa" kwa kushindwa kuzizuia?

Kidemokrasia, naamini Watanzania tulinyimwa nafasi ya kuona demokrasia yetu inavyoweza kufanya kazi unapotokea mgongano kati ya Bunge na Rais. Kikwete angeweza kukaa na Lowassa, kuangalia ushahidi uliotolewa na Kamati Teule, kupima uzito wa hoja za wabunge na kuandaa majibu kwa kila hoja.

Ninaamini hakuna mwanasiasa wa Tanzania ambaye angeweza kupangua hoja za kamati teule kwa urahisi na kwa umahiri kama siasa (na hapa namaanisha). Ingekuwa vizuri kweli kwa Rais Kikwete kuchukua upande wa Waziri wake Mkuu ili tuone mgongano kati ya Mwenyekiti wa CCM na wabunge wa CCM! Je, kweli mnafikiri Bunge la CCM lingeweza kwenda kinyume na Rais wake? Je wale waliokuwa vinara wangeweza kuendelea kuwa vinara baada ya Rais kuchukua msimamo wa kumtetea Lowassa? Je yawezekana ushujaa wao ni kwa sababu Kikwete hakuchukua msimamo na hivyo ni kuwa kama bingwa ambaye hakutaka kuingilia mapambano ya ridhaa!?

Kama hakukuwa na ushahidi wa moja kwa moja wa Lowassa kunufaika na mkataba wa Richmond, kama hakukuwa na ushahidi wa moja kwa moja wa kuonesha kuwa Lowassa ndiye Richmonduli, kama Kamati haikuweza kuonesha kuwa mtoto wa Lowassa ndiye alihusika na Richmond na kwa mujibu wa sheria ya Maadili huo ni mgongano wa Maslahi kwa Lowassa, ninajiuliza Lowassa alijiuzulu kwa sababu gani hasa?

Jibu ni kuwa Lowassa alijiuzulu ili kumkomoa Kikwete! Alijiuzulu kama spite ya Kikwete na urafiki wao; hakujiuzulu kwa sababu nyingine yoyote isipokuwa kwa sababu rafiki yake, mtu aliyehangaika kumuweka madarakani na mtu ambaye kwa kiasi kikubwa ni mshirika wake wa kisiasa alimtosa wakati alipotakiwa kusimama naye.

Je, ina maana kwa Kikwete kusimama na Lowassa kunamfanya Lowassa asiwe na makosa? Na kama alikuwa na makosa ni kweli yalimstahilisha ajiuzulu kwa namna ile ya utekaji nyara nchi?
 
Kwa wanaokumbuka Rais alikuwa mikoa ya Kusini na Makamu alikuwa sehemu nyinyine na wao kama Taifa zima walisikia kujiuzulu kwa Lowassa "radioni"

- Rais alikuwepo Dodoma, Ikulu ya Chamwino siku waziri mkuu wake wa kwanza alipojiuzulu.

- Suala zima la kujiuzulu kwa waziri mkuu Mh. E. Lowassa, lilikuwa handled na bunge kama katiba yetu inavyosema, rais wetu aliheshimu mgawanyo wa madaraka kati ya bunge, Mahakama na Ikulu.

- Kwa kutoingilia kati maamuzi ya bunge, rais wetu aliheshimu katiba, na anahitaji heshima kubwa for that, kwa sababu aliweka msingi mzito wa kuheshimu katiba kwa kizazi kijacho


William.
 
Back
Top Bottom