Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,460
- 39,928
Kwanza ilikuwa ni Rais Bush na Michael Brown kule Lousianna wakati wa Katrina. Wakati kelele zinapigwa za kutaka kichwa cha Brown (mkuu wa FEMA) Bush alifunga safari kujionea na kwa jinsi anavyojua yeye alisimama mbele ya waandishi wa habari na kusema yale maneno ambayo yamebakia kama mwangwi "Brown you are doing a heck of a job".
Bush alisimama na mtu wake aliyemteua licha ya kelele..
Sasa wiki ile iliyopita hata leo hii kumekuwa na kelele za kutaka Waziri wa Fedha wa Marekani Bw. Geithner kujiuzulu. Mara tatu sasa Rais Obama amejitokeza pasipo woga kumtetea mteule wake na kusimama naye na kusema kama kuna mtu anataka wa kumlaumu basi wamlaumu yeye na kamwambia hata akileta barua ya kujizulu hatoikubali (basically asijisumbue).
Obama amesimama na mtu wake aliyemteua!
Ndiposa, nikabakia kujiuliza.. nini kilitokea Februari ile? Kwanini Kikwete hakusimama na mteule wake na kukubali kubeba lawama zote za Richmond yeye mwenyewe? Kwanini hakusimama na Karamagi, Chenge (ya Chenge labda haifai!) au Msabaha?
Je kila watu walio chini yake wakilaumiwa yeye atawatosa tu? NI lini atakubali kubeba lawama na kusema kuwa "mnilaumu mimi"? Je yawezekana tunu hiyo ya kukubali kubeba mzigo kama kiongozi Rais wetu hana na badala yake ni bora watu watoswe ilimradi yeye anaendelea kuonekana ni msafi? Je kuna siku atasimama kuwatetea watu aliowateua au atawaacha wamomonyoke na hivyo kuthibitisha ni jinsi gani asivyo mwangalifu katika uteuzi (maana anashindwa hata kuwatetea!)!
Ninaamini, hakuna wakati ambapo Kikwete alionesha udhaifu mkubwa kama kiongozi kama kushindwa kusimama na Waziri wake Mkuu au kupanga naye mkakati wa kujibu mashambulizi ya Bunge. Ndiyo maana ninaamini Lowassa hana sababu ya kumlaumu mtu mwingine yoyote (siyo Spika, CCM au Mwakyembe) kwa kujiuzulu kwake bali mtu mmoja tu ambaye alishindwa kuchukua msimamo mgumu!
Lakini labda alijua maji yamemwagika? Je kama JK angesimama na Lowassa na kukubali uchafu na lawama zote za Richmond (as a matter of fact nakumbuka mkutano wake na waandishi wa habari nadhani alistahili kuubeba mzigo huo!).
Kama mtu ukiteuliwa na Kikwete jua jambo moja.. you are on your own!!
Bush alisimama na mtu wake aliyemteua licha ya kelele..
Sasa wiki ile iliyopita hata leo hii kumekuwa na kelele za kutaka Waziri wa Fedha wa Marekani Bw. Geithner kujiuzulu. Mara tatu sasa Rais Obama amejitokeza pasipo woga kumtetea mteule wake na kusimama naye na kusema kama kuna mtu anataka wa kumlaumu basi wamlaumu yeye na kamwambia hata akileta barua ya kujizulu hatoikubali (basically asijisumbue).
Obama amesimama na mtu wake aliyemteua!
Ndiposa, nikabakia kujiuliza.. nini kilitokea Februari ile? Kwanini Kikwete hakusimama na mteule wake na kukubali kubeba lawama zote za Richmond yeye mwenyewe? Kwanini hakusimama na Karamagi, Chenge (ya Chenge labda haifai!) au Msabaha?
Je kila watu walio chini yake wakilaumiwa yeye atawatosa tu? NI lini atakubali kubeba lawama na kusema kuwa "mnilaumu mimi"? Je yawezekana tunu hiyo ya kukubali kubeba mzigo kama kiongozi Rais wetu hana na badala yake ni bora watu watoswe ilimradi yeye anaendelea kuonekana ni msafi? Je kuna siku atasimama kuwatetea watu aliowateua au atawaacha wamomonyoke na hivyo kuthibitisha ni jinsi gani asivyo mwangalifu katika uteuzi (maana anashindwa hata kuwatetea!)!
Ninaamini, hakuna wakati ambapo Kikwete alionesha udhaifu mkubwa kama kiongozi kama kushindwa kusimama na Waziri wake Mkuu au kupanga naye mkakati wa kujibu mashambulizi ya Bunge. Ndiyo maana ninaamini Lowassa hana sababu ya kumlaumu mtu mwingine yoyote (siyo Spika, CCM au Mwakyembe) kwa kujiuzulu kwake bali mtu mmoja tu ambaye alishindwa kuchukua msimamo mgumu!
Lakini labda alijua maji yamemwagika? Je kama JK angesimama na Lowassa na kukubali uchafu na lawama zote za Richmond (as a matter of fact nakumbuka mkutano wake na waandishi wa habari nadhani alistahili kuubeba mzigo huo!).
Kama mtu ukiteuliwa na Kikwete jua jambo moja.. you are on your own!!