Kwanini huolewi? Au una kasoro?

Da Prety, kama unataka kuolewa, jiangalie kwenye maeneo haya:
1. Je, una vi nyodo nyodo visivyo na msingi?
2. Kampani yako unayo 'hang out' nayo ni ya aina gani? Masista duu? Mashangingi? Wasela?
3. Unavaaje? Skin tyt/ jeans 24/7? Miniskirt, pedo, boobs nje nje?
4. Lifestyle yako kwa ujumla? Uko ki 'matawi' sana? Mipete ya dhahabu, cheni kubwa, vikuku, hereni 4 kila sikio, bangili za gold nk?
5. Unapendelea kutembelea maeneo gani? Hoteli kubwa kubwa? Club za gharama?
6. Unapenda kujiremba kupita kiasi?
7. Hukumbuki mara ya mwisho kuonekana kanisani/mskitini?
8. Unapenda kuwa na relaionships na 'masharobaro'?
9. 'Uzungu' mwingi?
10. Nakadhalika?
Wanaume wa sku izi wajanja. Hawataki kuoa mtu mwenye unnecessary complications hata awe mzuri kiasi gani! Wanataka mtu presentable ambaye wanaweza kumtambulisha kwa marafiki, ndugu, wazazi n.k
Ukikuta una mojawapo kati ya kasoro hizo jirekebishe haraka. Hapo utajitoa kwenye kundi la 'mademu' na kuingia kwenye 'wife material'
Kuolewa ni heshima dada, japo si lazima but inakupa a deeper purpose in life. Good luck

Maswali yako ni mazuri sana na yanajenga.
Ninaishi maisha ya kawaida sana kama binti mwenye Kumjua Mungu, nina kabila na nina wazazi pia.
Suala sio kutaka kuolewa, kikubwa ni hili swali "kwanini huolewi?" ndio linanikwaza.
 
labda na wewe utuambie kwa nini hujaolewa, hupendi au hujapata muoaji mnaeendana?
Ongeza au kwa vile sijaamua kwa sasa (Inawezekana napenda ila sijawa tayari)

Tunarudi palepale!
Lazima jibu lipo kati ya hayo lakini kwanini jamii isielewe au isisikilize kwanza wahisi ni tatizo au kasoro?
 
Naomba nieleweke.
Suala la kwa nini sijaolewa haliniumizi kichwa.
Tatizo kuulizwa na jamii kuona ni tatizo mimi kutoolewa.
Ningekua na hamu sana ya kuolewa ili niifurahishe jamii wala nisingepata tabu
Ni suala la kutafuta kijana yeyota na kumshawishi hata kwa pesa ili tukafunge ndoa jamii ijue nina mume
matatizo katika ndoa ni suala jingine ambalo kwa mimi ambae nitakua nimeolewa kufurahisha jamii suluhisho ni jepesi sana
TALAKA.
Na hili swali halipo kwangu tu, kuna rafiki yangu nae anaulizwa sana tena yeye ana hali mbaya maana hamu ya kuolewa kweli anayo sana.
 
Kuolewa sio issue sana ila kwa jamii yetu eti usipoolewa may una matatizo sio kweli bana.

Pole ila usijali watu wanaolewa na 40yrs wala isikutishe my dear

Hadithi hadithi ? Hadithi njoo, uwongo njoo, utam kolea.
 
Nakubaliana na wewe. Human being is a social animal. It matters what the society is perceiving you. Kusema usijali watu wanasemaje nakataa kabisa. Piga maombi Mungu atakupatia mume mwema. Hata hao westerners kutokuolewa au kuolewa late ni culture yao na si lazima kila cha mzungu ni kizuri. Wewe mwenyewe umesema unajisikia vibaya unavyoulizwa na watu kwa nini huolewi. Kwa sababu unahisi umepungukiwa na kama ungehisi its okay usingeleta hii mada hapa. Jamii yetu haikubaliani na mtu kuchelewa kuoa au kuolewa. As long as uko Tz tegemea maswali kama hayo kila siku.

Ushauri wangu, stop hanging out with wrong guys. Wa kukuoa utamjua tu hao wengine wanakuzehesha tu.

Da Prety, kama unataka kuolewa, jiangalie kwenye maeneo haya:
1. Je, una vi nyodo nyodo visivyo na msingi?
2. Kampani yako unayo 'hang out' nayo ni ya aina gani? Masista duu? Mashangingi? Wasela?
3. Unavaaje? Skin tyt/ jeans 24/7? Miniskirt, pedo, boobs nje nje?
4. Lifestyle yako kwa ujumla? Uko ki 'matawi' sana? Mipete ya dhahabu, cheni kubwa, vikuku, hereni 4 kila sikio, bangili za gold nk?
5. Unapendelea kutembelea maeneo gani? Hoteli kubwa kubwa? Club za gharama?
6. Unapenda kujiremba kupita kiasi?
7. Hukumbuki mara ya mwisho kuonekana kanisani/mskitini?
8. Unapenda kuwa na relaionships na 'masharobaro'?
9. 'Uzungu' mwingi?
10. Nakadhalika?
Wanaume wa sku izi wajanja. Hawataki kuoa mtu mwenye unnecessary complications hata awe mzuri kiasi gani! Wanataka mtu presentable ambaye wanaweza kumtambulisha kwa marafiki, ndugu, wazazi n.k
Ukikuta una mojawapo kati ya kasoro hizo jirekebishe haraka. Hapo utajitoa kwenye kundi la 'mademu' na kuingia kwenye 'wife material'
Kuolewa ni heshima dada, japo si lazima but inakupa a deeper purpose in life. Good luck
 
Ogopa sana ushauri wa watu ambao hawana evidence nikiwa na maana hawana ushuhuda. The effect of not getting married or marrying late utaijua 20 years to come not now. Pale ambapo umestaafu watoto wanadai school fees. Au pale ambapo umezaa na mume wa mtu watoto kakunyang'anya na hawakutambui kama wewe ndo uliwazaa. Wadada wengi hawaliangalii ili la kunyang'anywa watoto wanaozaa na wame za watu. Na sheria inasema mtoto ni wa baba. Kuna dada alizaa na lawyer tajiri sana watoto wanasoma UK na walichukuliwa kwa mama yao wakiwa wadogo sana baba akawaficha boarding, wanamuona mama yao kama kinyago kwani hajawalea na wao ni matawi ya juu.
 
Kuna mtu niliona anashauri kama unataka kuwa single parent ununue mbegu. I think that could be a solution kuepuka kunyang'anywa mtoto. Tabu inakuja pale mtoto atakapokusumbua baba yangu yu wapi. Pili ni immoral hasa kwa mtu wa dini.
 
Maswali yako ni mazuri sana na yanajenga.
Ninaishi maisha ya kawaida sana kama binti mwenye Kumjua Mungu, nina kabila na nina wazazi pia.
Suala sio kutaka kuolewa, kikubwa ni hili swali "kwanini huolewi?" ndio linanikwaza.
Naomba nieleweke.
Suala la kwa nini sijaolewa haliniumizi kichwa.
Tatizo kuulizwa na jamii kuona ni tatizo mimi kutoolewa.
Ningekua na hamu sana ya kuolewa ili niifurahishe jamii wala nisingepata tabu
Ni suala la kutafuta kijana yeyota na kumshawishi hata kwa pesa ili tukafunge ndoa jamii ijue nina mume
matatizo katika ndoa ni suala jingine ambalo kwa mimi ambae nitakua nimeolewa kufurahisha jamii suluhisho ni jepesi sana
TALAKA.
Na hili swali halipo kwangu tu, kuna rafiki yangu nae anaulizwa sana tena yeye ana hali mbaya maana hamu ya kuolewa kweli anayo sana.

...pole sana, hii inatokana na matarajio ya jamii inayokuzunguka.
Tamaduni, mila na desturi zina "wasuta" ndugu, jamaa, na marafiki zako
kiasi kwamba wanashindwa kujizuia kukuuliza kwanini huolewi.
Kwa wengi wetu (wabantu), mfumo wa maisha unakutarajia uolewe na uzae kabla hujavuka miaka 30 - 35.

Umri unavyokimbia ni viashiria bahati ya kupatikana waoaji inapungua, na hata afya ya uzazi inapungua.
Wanapohoji kwanini huolewi, indirectly wanahoji kwanini "hutaki" kuolewa. Umegusia kwamba

Ongeza au kwa vile sijaamua kwa sasa (Inawezekana napenda ila sijawa tayari)
Tunarudi palepale!
Lazima jibu lipo kati ya hayo lakini kwanini jamii isielewe au isisikilize kwanza wahisi ni tatizo au kasoro?

Je, hao wanaokuuliza pia unawajibu hivyo -HUJAWA TAYARI?
 
<p>
Haya mama..nyie ndio mnaolewa sababu ya kufwata fasheni,eti watanionaje,wengine wanadiriki kulazimishia na hamna rangi wanaacha kuona wakishaolewa,matokeo yake hata mwaka haufiki unaondoka mwenyewe bila kufukuzwa (nimeona yametokea)...THERE IS A RIGHT TIME FOR EVERYTHING my dear hapo alipo ni Mungu tu ndo anajua amempangia lini kuolewa ndo maana anatakiwa amshirikishe Mungu wake katika hili.
</p>
<p>&nbsp;</p>

dada sijakuelewa unavyosema wengine wanalazimisha, Nani kakudanganya ukimlazimisha men akuoe anakuoa pole. msipende kujifariji kupitia ndoa za watu sio kila mtu anaeteseka ndoani kwahiyo kisa ndoa za watu wengine zinavunjika ndio kigezo cha wewe na dada Pretty kutokuolewa?
 
Habari wanajamvi.
Kwa kweli hilo swali huwa linanisononesha sana.
Nina umri wa miaka 30, sijaolewa, sina mchumba wala mpenzi yapata mwaka na miezi kadhaa sasa.
Mdogo wangu anayenifuatia ana miaka 27 aliolewa akiwa na miaka 24 na ana watoto wawili sasa.
Familia yangu na jamii inayonizunguka hainielewi na mara nyingi nakutana na hilo swali
"Mbona wenzako wanaolewa wewe huolewi, au una tatizo?"
Kiukweli hua napata ugumu sana kujibu hilo swali kwa sababu sina cha kuwajibu.
Labda ningesema nina tatizo au kasoro lakini kati ya niliowahi kuwa nao kimahusiano hakuna alieoa hadi sasa japo wote walinizidi umri na kuna wawili walikua na watoto tayari na mpaka sasa hawajaoa.
Hivi kwa jamii yetu mwanamke kutoolewa ni kasoro?
Maana kuna rafiki yangu naye anapata usumbufu kama wangu kutoka kwa familia yake.
Vipi kama mwanaume ninayempata yeye hana wazo la kuoa nifanyeje?
Na wanaume huwa wanaulizwa na kuonekana wana matatizo kama wanawake?


Dah,tatizo hatuna ID za ukweli humu!

Kuna mtoto wa ant yangu,yuko 30 saivi na mdogo wake wa mwisho 23 kaolewa ila yeye bado!

Huwa natamani kujua kwanini ila ni swali ambalo anajua mtu mwenyewe!

Na kwako pia,unajua mwenyewe kwanini haujaolewa ,....maybe kila unae mpata anaona ni "gharama" kuishi na wewe,.....au labda "huoneshi kuwa na upendo kwa wandugu"......

Kwa mfano,huyu sis angu hata ningekuwa mimi ndo muoaji nisinge muoa,maana ni mtu wa yeye kama yeye tu,...sidhani kuoa mtu kama huyo atataka hata kumuona mamako akikutembelea achilia mbali wadogo zako!

Vitu kama hivyo vina repel waoaji ila vina attract wachezeaji kwa wingi na wengi tukishajua unataka kuolewa kwa ham kweli basi tunaingia na gia ya kuoa,kukisha cheza kimtindo tunaondoka!

Ila sister,Mungu peke yake ndo anaijua kesho yako,...kama uko single leo na umejiheshimu all that way (kiimani,kama hukuwahi kuiba waume za watu au kama uliiba basi repent) basi Mungu atakupa mume kwa mda anao ona unafaa maana anajua spear ya kila kiungo chako (na nani anakufaa kama mume pia)

Salute
 
Nimerudi.

Loly mpenzi,
1. miaka 30 ni mingi ukimaanisha nini?ni wapi imeandikwa mtu aolewe kabla hajafika 30 years?hapo naona umekosea kidogo
watu wanaolewa wakiwa hata na miaka 40 na kupitiliza, binafsi nadhani hakuna umri maalum ambao mwanamke anapaswa awe amekwisha olewa.

2. kuwa na majamaa ambao wao pia hawajaoa haimaanishi una nuksi...wao wana maisha yao na wewe una maisha yako..ni kama kufananisha kifo na usingizi.

3. kwa uelewa wangu,muanzapo mahusiano hamuanzi kwa kuambiana 'oo nitakuoa''au 'oo nioe'...hell no...kuoa kunakuja kama mmeridhiana,kama mnapatana,je mnaweza kuvumiliana and all that..mi sijaolewa so siwezi kuweka list ndefu hapa...kwahiyo yawezekana Da Pretty hao aliokutana nao huko nyuma (i) hawakuwa na nia ya kuoa na ndo mana mpaka leo hawajaoa (wapo wanaume wa hivyo na ninawafahamu,wao wanajiita senior bachelors)...au (ii) hawakuridhia mpaka kufikishana kuoana and vice versa its true

4. Imeandikwa kuwa 'Mume bora hupewa na Mungu'..kwa hiyo kumshirikisha Mungu kwenye maombi ni jambo la muhimu na busara pia, ingawaje sidhani kama majini sijui mahaba have nothing to do with ndoa

5. Kama usemavyo 'watoto ni hazina'..na hii kumbuka haijalishi kama umeolewa au haujaolewa,hazina ni hazina tu with or without marriage so hata akiamua kuzaa sasa hivi hatojidhalilisha kama ulivyosema (ingawaje jamii itaona amejidhalilisha)

6. Mbona wanawake wa kuoa wengi tuu,kwanza wanawake ni wengi kuliko wanaume iweje wanaume wasione wa kuoa.Mi naona hao wasioona ni kwamba hawako tayari kuoa na kujisingizia hawajaona hawana lolote

Angalizo

Yatupasa tuishi bila kujali jamii inasemaje,jamii inaonaje au jamii itakuchukulia vipi.

Da Pretty, miaka 30 sio mingi, usiharakishe kuolewa kama hauko tayari au kama hajatokea the right person to marry you just because jamii inakuonaje..Waache waulize,waseme, watajijua wenyewe,yao yanawashinda kwa nini wakuulize wewe? Kama ni mama zako,wakalishe kitako waambie bado hauko tayari au hujapata unaedhani anakufaa.kwani tatizo liko wapi hapo? at the end of the day wewe ndio utakayeishi na huyo mume,wacha upate anaefaa bwana hee!!take your time dada,chagua if u have to pembua upate unayemtaka..usiforce mambo kisa watu wanasemaje..wama maisha yao yanawasubiri kuishi ukute yameshawashinda..eboo..achana nao.

Endelea tu kumdanganya mwenzako....na wewe pia subiria ifike hiyo miaka kama utatafutwa...hao watoto uzae lini na uolewe lini????mshaurini mwenzenu vizuri na sio kumpa mawazo ambayo hayata msaidia....miaka 30 unasema mda bado......au hata 40 nani kakuambia bana???miaka 40 na watoto lini???
 
Nimerudi.

Loly mpenzi,
1. miaka 30 ni mingi ukimaanisha nini?ni wapi imeandikwa mtu aolewe kabla hajafika 30 years?hapo naona umekosea kidogo
watu wanaolewa wakiwa hata na miaka 40 na kupitiliza, binafsi nadhani hakuna umri maalum ambao mwanamke anapaswa awe amekwisha olewa.

2. kuwa na majamaa ambao wao pia hawajaoa haimaanishi una nuksi...wao wana maisha yao na wewe una maisha yako..ni kama kufananisha kifo na usingizi.

3. kwa uelewa wangu,muanzapo mahusiano hamuanzi kwa kuambiana 'oo nitakuoa''au 'oo nioe'...hell no...kuoa kunakuja kama mmeridhiana,kama mnapatana,je mnaweza kuvumiliana and all that..mi sijaolewa so siwezi kuweka list ndefu hapa...kwahiyo yawezekana Da Pretty hao aliokutana nao huko nyuma (i) hawakuwa na nia ya kuoa na ndo mana mpaka leo hawajaoa (wapo wanaume wa hivyo na ninawafahamu,wao wanajiita senior bachelors)...au (ii) hawakuridhia mpaka kufikishana kuoana and vice versa its true

4. Imeandikwa kuwa 'Mume bora hupewa na Mungu'..kwa hiyo kumshirikisha Mungu kwenye maombi ni jambo la muhimu na busara pia, ingawaje sidhani kama majini sijui mahaba have nothing to do with ndoa

5. Kama usemavyo 'watoto ni hazina'..na hii kumbuka haijalishi kama umeolewa au haujaolewa,hazina ni hazina tu with or without marriage so hata akiamua kuzaa sasa hivi hatojidhalilisha kama ulivyosema (ingawaje jamii itaona amejidhalilisha)

6. Mbona wanawake wa kuoa wengi tuu,kwanza wanawake ni wengi kuliko wanaume iweje wanaume wasione wa kuoa.Mi naona hao wasioona ni kwamba hawako tayari kuoa na kujisingizia hawajaona hawana lolote

Angalizo

Yatupasa tuishi bila kujali jamii inasemaje,jamii inaonaje au jamii itakuchukulia vipi.

Da Pretty, miaka 30 sio mingi, usiharakishe kuolewa kama hauko tayari au kama hajatokea the right person to marry you just because jamii inakuonaje..Waache waulize,waseme, watajijua wenyewe,yao yanawashinda kwa nini wakuulize wewe? Kama ni mama zako,wakalishe kitako waambie bado hauko tayari au hujapata unaedhani anakufaa.kwani tatizo liko wapi hapo? at the end of the day wewe ndio utakayeishi na huyo mume,wacha upate anaefaa bwana hee!!take your time dada,chagua if u have to pembua upate unayemtaka..usiforce mambo kisa watu wanasemaje..wama maisha yao yanawasubiri kuishi ukute yameshawashinda..eboo..achana nao.

Barikiwa sana!!! Nimepata furaha ya ziada kwa haya maneno yaliyotoka kwenye moyo wako. Namshukuru Mungu kwa ajili yako pia. Endelea kusonga Mbele.
Thanks again!!!
 
Endelea tu kumdanganya mwenzako....na wewe pia subiria ifike hiyo miaka kama utatafutwa...hao watoto uzae lini na uolewe lini????mshaurini mwenzenu vizuri na sio kumpa mawazo ambayo hayata msaidia....miaka 30 unasema mda bado......au hata 40 nani kakuambia bana???miaka 40 na watoto lini???

Kila mtu ameitwa hapa duniani kwa jinsi yake. Sio lazima kila mtu apite hapa duniani kama utaratibu wa dunia ulivyo. Cha msingi ni kutulia na kutengeneza uhusiano wako na Mungu tu. Ikiwa Mungu amekuandikia kuolewa utaolewa tu, kama hajakuandikia atakupa furaha na Neema ya kupita hapa dunia kwa njia hiyo aliyokuandikia pia.

Kumbuka sio kweli kwamba Ndoa ndiyo furaha ya mwanadamu asilimia mia moja, wakati mwingine nikujitoa sadaka tu, kuna watu wanajuta kuolewa. Kwa hiyo hapo hakuna kulazimisha mambo wala kuolewa kwa sababu fulani kasema. Ishi maisha yako mheshimu Mungu wakati ukifika itakuwa.

We unajua je bwana, yawezekana yeye ameitwa kuishi maisha kama hayo hapa duniani. Tunasahau kama sisi ni wasafiri na wapitaji tu hapa??? Yani tunadhani kila mtu lazima apite hapa kama wewe na mwingine walivyopita?? Nooooo kila mtu ana njia yake.

Dada usife moyo wala usikate tamaa, songa mbele, fanya kazi kwa bidii. Maisha yaendelee!!
 
<p></p>
<p>&nbsp;</p>

dada sijakuelewa unavyosema wengine wanalazimisha, Nani kakudanganya ukimlazimisha men akuoe anakuoa pole. msipende kujifariji kupitia ndoa za watu sio kila mtu anaeteseka ndoani kwahiyo kisa ndoa za watu wengine zinavunjika ndio kigezo cha wewe na dada Pretty kutokuolewa?

Loly,naongea from what i've seen.kuna rafiki yangu alilazimisha kuolewa mwanaume hataki ye anatumia kigezo wamekaa muda mrefu,mwanaume akaoa akaweka ndani akaendelea na mambo yake..matokeo yake dada wa watu hakuweza kuvimilia viroja alivyokuwa anafanyiwa akaomba divorce..sasa hapo imesaidia nini?au kwa kuwa itabaki historia kuwa aliolewa..acheni kudanganyana jamani.kuolewa ama kutoolewa kumepangwa na Mwenyezi Mungu..
 
Kila mtu ameitwa hapa duniani kwa jinsi yake. Sio lazima kila mtu apite hapa duniani kama utaratibu wa dunia ulivyo. Cha msingi ni kutulia na kutengeneza uhusiano wako na Mungu tu. Ikiwa Mungu amekuandikia kuolewa utaolewa tu, kama hajakuandikia atakupa furaha na Neema ya kupita hapa dunia kwa njia hiyo aliyokuandikia pia.

Kumbuka sio kweli kwamba Ndoa ndiyo furaha ya mwanadamu asilimia mia moja, wakati mwingine nikujitoa sadaka tu, kuna watu wanajuta kuolewa. Kwa hiyo hapo hakuna kulazimisha mambo wala kuolewa kwa sababu fulani kasema. Ishi maisha yako mheshimu Mungu wakati ukifika itakuwa.

We unajua je bwana, yawezekana yeye ameitwa kuishi maisha kama hayo hapa duniani. Tunasahau kama sisi ni wasafiri na wapitaji tu hapa??? Yani tunadhani kila mtu lazima apite hapa kama wewe na mwingine walivyopita?? Nooooo kila mtu ana njia yake.

Dada usife moyo wala usikate tamaa, songa mbele, fanya kazi kwa bidii. Maisha yaendelee!!

Ok sawa nimekueelwa vizuri kabisa na wala hamna tatizo wangu....kwa hiyo labda aendelee kusubiria mpaka atakapo pata mwanaume mwema.....ila zaidi ushauri wako nimeupenda.......
 
<p>
Loly,naongea from what i've seen.kuna rafiki yangu alilazimisha kuolewa mwanaume hataki ye anatumia kigezo wamekaa muda mrefu,mwanaume akaoa akaweka ndani akaendelea na mambo yake..matokeo yake dada wa watu hakuweza kuvimilia viroja alivyokuwa anafanyiwa akaomba divorce..sasa hapo imesaidia nini?au kwa kuwa itabaki historia kuwa aliolewa..acheni kudanganyana jamani.kuolewa ama kutoolewa kumepangwa na Mwenyezi Mungu..
</p>
<p>&nbsp;</p>

ndio maana nilimshauri akemee .... mahaba likishatoka atapata mchumba muoaji sio Kama wale wa zamani, sijamshauri ang'ang'anie wanaume mimi, namkizidi kuwa wabishi mtagonga 40yrs
 
Naomba nieleweke.
Suala la kwa nini sijaolewa haliniumizi kichwa.
Tatizo kuulizwa na jamii kuona ni tatizo mimi kutoolewa.
Ningekua na hamu sana ya kuolewa ili niifurahishe jamii wala nisingepata tabu
Ni suala la kutafuta kijana yeyota na kumshawishi hata kwa pesa ili tukafunge ndoa jamii ijue nina mume
matatizo katika ndoa ni suala jingine ambalo kwa mimi ambae nitakua nimeolewa kufurahisha jamii suluhisho ni jepesi sana
TALAKA.
Na hili swali halipo kwangu tu, kuna rafiki yangu nae anaulizwa sana tena yeye ana hali mbaya maana hamu ya kuolewa kweli anayo sana.

Kumbe jeuri hivyo, kaa hivyo hivyo usije sababisha pressure kwa mme atakayekuoa, na ni vema uhamie Ulaya kabisa ili usionekane wa ajabu kwani kwa Afrika haikwepeki kuonwa wa ajabu. Ni vugumu kuwa anti-social halafu utarajie kuchekewa. Ulaya wenzio mpaka anazeeka ana faili la talaka nane au zaidi kwani wao kuolewa ni kama kununua soda tu, haina thamani, fanya hima ukajiunge nao.

Nimefuatilia mchango yako hapa kwenye thread yako na hii ndio conclusions yangu, I am sorry!
 
Back
Top Bottom