Hakuna asiye fahamu kuwa biashara katika karne hii ya utandawazi, matangazo ni lazima. Mimi huwa nashangaa kila kukicha nchi kama Angola iko kwenye CNN au BBC. Wanatangaza uwekezaji na utalii na wanatangaza kweli. Hivi karibuni Pakistani nayo haiko nyuma kwenye utangazaji, jamani hata Pakistani? CNN waliturusha hewani siyo zaidi ya mara mbili tangu JK aingie madarakani na kuahidi kuwa tutainadi nchi yetu kwa hali na mali. Kenya pamoja na matatizo yao ya kisiasa lakini hazipiti siku mbili bila kuiona kwenye vyombo vya dunia. WEBSITE YA TANZANIA INAONYESHA KUWA TANZANIA INAHITAJI UWEKEZAJI KATIKA KILIMO, VIWANDA NA UTALII SASA WAWEKEZAJE WATAJUAJE, WATALII WATAJUAJE KUHUSU BONGO? NA LA MSINGI ZAIDI, WATAJUAJE KUHUSU AMANI NA UTULILIVU TULIONAO AMBAO NDO ADVANTAGE TUNAYO WAZIDI WENZETU?