Wasiojua wajue, na hata kama hawataki kujua walazimishwe kujua, na ccm pia wajue, kuwa chadema ipo juu na watu wanataka mabadiliko.
Naombi moja kwa makada wetu walioko Usalama wa taifa, tuendelee na uzalendo huo hata siku ya kuchokonoa kura wewe nenda hata ****** tupeni taarifa ili, pigeni hata picha mzitume tutawamaliza tu hao wezi.
Mbinu nyingine ni chafu kabisa kama hii ilivyoelezwa hapa chini niliyoinasa kwenye thread moja iliyoanzishwa mchana huu humu JF kabla ya kufutwa kwa haraka. Ni onyesho tosha ya kule tunakokwenda:
Idara ya usalama wa taifa na zoezi la uchakachuaji kura
Poleni na harakati za kuikomboa nchi yetu!
Leo napenda kuwajulisha mikakati michafu ya kupora na kuzuia maamuzi ya umma yanayofanywa na ccm kwa uratibu wa usalama wa taifa. Baada ya ku...baini dalili za kuanguka vibaya katika uchaguzi wa mwaka huu idara ya usalama wa taifa imeandaa mikakati ya kuiba kura ili kuzuia chadema msiingie ikulu. Mikakati hii inaeleweka vizuri kwa tume ya taifa ya uchaguzi ambayo inashirikiana bega kwa bega na idara ya usalama wa taifa kumtengenezea jk ushindi bandia wa 80%.
Wana hakika watanzania watagundua wizi huo na watakataa matokeo ndiyo maana kwanza waliwatumia viongozi wa dini waliotembelea makao makuu ya chadema wawasihi chadema wakubali matokeo yatakapotangazwa na juzi wamelitumia jeshi kutisha wananchi watakaoamua kupinga matokeo ya kupikwa yanayoandaliwa na nec/usalama wa taifa. Majid kikula ambaye ni government security officer ndiye mratibu wa zoezi la kuiba kura, ni mtaalamu aliyebobea katika kazi za aina hii aliratibu vizuri zoezi kama hilo mwaka 2005. Pia mwaka 2007 alitumwa kenya kwenda kumsaidia kibaki kupora ushindi wa odinga.
Kikula anatumia muda wake mwingi hivi sasa ofisi za tume ya uchaguzi kwa ajili ya uratibu wa uvurugaji daftari la kudumu la wapiga kura akiifanya kazi hiyo kwa karibu na baadhi ya watendaji wa nec na maafisa kadhaa wa usalama wa taifa kutoka kurugenzi ya IT ya idara ya usalama (DITA) ambao wako ndani ya nec kwa zaidi ya miezi sita sasa, nitawapatia majina yao. Pia kuna vijana wataalamu wa IT waliochukuliwa kutoka maeneo mbalimbali wamepewa nyumba upanga mtaa wa undali shughuli kubwa wanayofanya ni kuandaa utaratibu wa ku-access remotely daftari la kudumu la wapiga kura.
Hawa wanafanya kazi chini ya salva rweyemamu na mindi kasiga kutoka kurugenzi ya mawasiliano ikulu. Wapo vijana kadhaa leo nawapa majina ya wawili; maharage chande na edgar masatu wanafanya kazi kwa karibu na nzowa wa idara ya usalama ambaye ndiye aliyeratibu shambulio la kumwagiwa tindikali kubenea.
Pia kuna kundi linalojumuisha wataalamu wa printing wa kiwanda cha uchapaji cha usalama wa taifa kilichopo MALINDI ambao hivi karibuni walikuwa mjini tanga kwa semina fupi ya jinsi ya kughushi kura kupitia fake ballot paper, timu hii inaongozwa na ndg SINYAU.
Kwa hiyo utaona kwamba imeandaliwa mikakati mingi kuufanikisha uovu huo ili mmoja ukikwama basi mwingine utatumika ila wameamua ni lazima jk ashinde kwa 80%. Ndani ya idara ya usalama wa taifa maafisa wengi wamechoshwa na uongozi mbovu wa ccm hivyo wanataka mabadiliko ya uongozi idara imechukua hatua kadhaa kuhakikisha maafisa wote wa idara wanampigia kura jk, wote wameagizwa kuwasilisha vitambulisho vyao vya kupigia kura ili vinakiliwe namba ili atakayepigia upinzani afukuzwe kazi baada ya uchaguzi.
Fuatilieni kwa karibu haya niliyowaeleza nimeyapata kwa nafasi yangu ndani ya tiss. Huyu KIKULA mfuatilieni kwa karibu ni hatari.
HAKIKISHENI DUNIA NA WATANZANIA WOTE WANAJUA MAPEMA HILA HIZI. Jambo la kujiuliza maafisa usalama wa taifa wanafanya nini ndani ya tume ya uchaguzi wakati huu
Haya mambo ni ya kutisha sana na si ya kupuuuza hata kidogo. Hii ina maana kwamba CCM inawatayarisha Watz kuipa amani na utulivu bye bye. Hivi CCM wanajua wanachokifanya?
Mimi nadhani ni kikundi kidogo tu cha wahindi -- kinachoipeleka nchi hii pabaya sana -- huku akina JK, Makamba, Kinana na wengine wakichekelea. Kukitokea sokomoko wote hawa watakimbia kwenda nje wakituacha wengine tukisagama humu ndani.
Kelele zinazofanywa na mawaziri wanaomaliza muda wao zinatoklana na mashinikizo wanayopewa na viongozi wa CCM ambao hawapati usingizi, Kila wanakumbuka jina la Slaa basi wanapata nightmare za ajabu sana na kuanza kupiga simu huku na kule; mara Magufuri, mara kamala mara .................
Kuna mmoja kaibuka leo ETI sera za elimu bure ni za sisiem, mbona walikua wanasema hazitekelezeki? ETI ni waziri!! nani kampa uwaziri wakati tuko kwenye mchakato wa kutafuta viongozi wa nchi? nadhani makatibu wakuu ndo wanapaswa kuendesha wizara AU? nirekebisheni
Kelele zinazofanywa na mawaziri wanaomaliza muda wao zinatoklana na mashinikizo wanayopewa na viongozi wa CCM ambao hawapati usingizi, Kila wanakumbuka jina la Slaa basi wanapata nightmare za ajabu sana na kuanza kupiga simu huku na kule; mara Magufuri, mara kamala mara .................
Nimemsikiliza na kumsoma Kamala waziri wa EAC utetezi wake umekaa kipashkuna.Dr W Slaa ni mgombea urais wa JMT si Afrika mashariki.Mikataba ya kipuuzi kamwe haiwezi kuheshimiwa kwakuwa ilisainiwa na Kamala & Kikwete ,Rais ajaye ana kila sababu ya kuipitia upya kuangalia ina maslahi gani kwa wananchi wa Tanzania.
Dr Kamala kakataliwa jimboni kwake [alikozaliwa] baada ya kujua hana uwezo na ubunifu kuwawakilisha wananchi iweje leo atusemee watanzania zaidi ya milioni arobaini ?.