mwanakwetu
Member
- Mar 30, 2008
- 89
- 14
Kwa misingi hiyo wanaweza kuwa wanazuwa vilevile.
Kama wanazua basi huyo anayezuliwa anatakiwa kukanusha na kusema ukweli ni upi. Na kama yangekuwa ya kuzua basi kina Mramba, Yona, Mgonja, Liumba na wenzao wasingefikishwa mahakamani na DPP. Huu mjadala umekaa kiiushabiki wa siasa. Tuweke siasa pembeni na tuangalie sisi kama watanzania tumeifanyia nini nchi iwe ni mwanaCCM, CHADEMA, CUF na wengineo wote.
Hivi Dr. Slaa binafsi hawezi kufungua kesi dhidi ya hao anaowatuhumu kuwa ni mafisadi? Kama anakwazwa na maslahi ya chama basi na yeye hatufai kama ambavyo hawatufai wabunge wa CCM wanapotanguliza mbele maslahi ya chama chao badala ya nchi. Kwa mtaji huu hadi sasa Mtikila ndio anasimama kama mwanasiasa ambaye ni kinara wa uzalendo na kesi zake za kikatiba.