Kwanini Chadema haiwalipi hawa?

Kumlipa mtu elfu kumi kwa mwezi ni sawa na kutomlipa. Haya tuone mfano wa kulipa watumishi, ungependekeza walipwe kiasi gani?

Mathalani, ukialika wanataaluma jadidi ukawalipa milioni 2 kila mmoja kwa mwezi wakiwa kumi tayari ni milioni 10. Unakaribia kumaliza ruzuku ya chama ya milioni 66.

Ukweli ni kuwa sasa CHADEMA haifanyi hayo malipo makubwa lakini Chacha ndiyo anasema makao makuu wanajipendelea. Sasa itakuwaje kama makao makuu wakaanza kujilipa mafao makubwa kama ulivyoshauri?

kama unataka suala kama hili basi wakee kwanza watu kama Chacha wanaonedesha siasa kwa nadharia.

Kama makao makuu wakilipwa milioni, wilayani watalipwa bei gani? Halafu kuna wilaya zaidi ya 130? Na majimbo je? Kuna majimbo 232! Na Kwenye kata Je, kuna kata 2300. Na vijijini je? Ukishaweka suala la malipo mbele kwa mazingira ya Tanzania basi ujue huna chama!

Hebu mtu atutengenezee hapa bajeti ya milioni 59 ambayo ndio ruzuku ya CHADEMA.

Apange matumizi ya watumishi makao makuu, gharama za uenezi, ruzuku wilayani nk! Aonyeshe mfano kuwa pengine CHADEMA ingetumia hivi fedha zake.

Asha

Asha,

Ukisoma posts zote za Zemarcopolo hapa JF, asilimia zaidi ya 80 ya posts hizo ni kuipondea chadema na upinzani. Hakuna chochote kizuri toka kwa chadema au wapinzani. Yeye hata hajui bajeti ya chadema ni kiasi gani na haijalishi kuwa ni mara ngapi hapa itawekwa namna matumizi ya chadema yalivyo, yeye bado atakuja na kudai kuwa pesa hizo zinamnufaisha zitto na mbowe. huyu maelezo hayatoshi maana kazi yake hapa ni kutetea ufisadi na kupigana na wapambanaji. Huyu ni yuda iskariote at best.
 
Fidel80, unaweza kuonyesha wapi au lini nilitetea mafisadi?

watu wanapo kushishia flani ni fisadi mbona unakuwa wa kwanza kuclash?
Angalia post zako vizuri basi,Jitahidi kubadilika mkuu.
Wananchi wanaumia sana kwa ajili ya ufisadi.
 
CHADEMA hawawezi kutumia pesa za BOT kwa sababu hawana access nazo, tatizo lao hata zile pesa ndogo za ruzuku wanazopata zinatumika kumboresha Mbowe na marafiki zake peke yao na anayeleta fyoko tu anapigwa benchi kama Chacha Wangwe na yule aliyekuwa mwenyekiti wa Morogoro.


Tatizo la wana CHADEMA wengi wao hawataki kukubali mapungufu,kukosolewa cha mhimu kwao ukiwapinga wanakuita CCM fisadi huu si ni UDIKITETA WA MAWAZO!!

Badala ya kujadili kilichoandikwa wengi wao watakimbilia kukuambia FISADI yani ndani ya CHADEMA ni ndio mzee hakuna kupinga hata kama kuna mambo unayaona yanakimong'onya chama.

Wangwe kajifanya kwenda kupingapinga mambo yao Umeona kilichompata.

Tatizo mimi naona hatujui CORE ya chama cha siasa, watu wanafikiri nikuchukua hatamu kuingia ikulu mambo yamekwisha,ama kutafuta wafanya biashara wenye pesa zao wawafadhiri hapo kiama ndipo kinaanzia.

CORE ya chama ni kubadili ATMOSPHERE ya wananchi hatimaye nchi ,huwezi badili atmosphere ya nchi ili uje ubadili atmosphere ya wananchi.

Kwa yule anayedhani CORE ya chama ni kuombamba ili aje aiingie ikulu ili aje alipe fadhira kwa wale aliowaomba ndio chazo cha akina ROSTAM.

Kuomba omba kwa chama yaliyofanywa na akina Nyerere ni mazingira waliokua nayo na khali yao ya kwamba siamini kama serikali ya kikoloni ingependa kuona TAA inakampuni inayoiigizia fedha na hata kuombaomba kwa TAA ni kwa wakati ule na si tamaduni ya kuilinda.

kuendelea ku REF:mambo aliyofanya Nyerere miaka ile na kuyaendeleza kama ilivyo huo ndio ukosefu wa ubunifu,kinachotakiwa ni kuyangalia na kuya advance zaidi yani ya kwamba mambo ya Nyerere na TANU yake yalikua mazuri lakini yapo ANALOG sana kumbe CHADEMA ama CUF,ama CCM,ama UDP inatakiwa iya process na kuya DIGITALIZE.Mambo ya wakati ule kuyacopy kama yalivyo na kuyapaste wakati huu ndio inakuja ile phenomenani yakua ndivyo tulivyo.

Kama ingekua hivyo maendeleo yasingekuwapo.
 
unachoshindwa kujua ni kwamba JF sio chama cha siasa chenye malengo ya kuongoza nchi siku moja kama chadema, Hii ni forums ambayo watu wachache wamejitolea kwa moyo mmoja na hata wewe hujakatazwa kufanya hivyo, lakini Chadema ni chama cha siasa na kina katiba na dhumini la kuongoza nchi yetu kama ikibahatika,we unategeme siku Mbowe akisema anataka kulipwa pesa zake zote alizo jitolea wakati wako IKulu si watauza nchi yetu , kuwa makini ndugu yangu

Mchelea Mwana,

Mbowe hawezi kuidai CHADEMA imlipe fedha zake kwa sababu yeye amejitolea kwa hiari kuchangia chama chake. Mbowe atakuwa na haki ya kudai fedha yake kama kuna makubaliano ya kuwa anachofanya kwa ajili ya CHADEMA ni mkopo kwa chama hicho, na siyo mchango wa kujitolea. Kujitolea na kukopesha ni mambo mawili tofauti.
 
Haina haja ya Kumlipa Mbowe sababu hapo CHADEMA ni sehemu ambapo ni kijiwe chake cha kusemea.Yeye si Mwanazuoni maarufu hivyo hawezi kutumia Elimu kueleza watanzania wakamwelewa.ndiyo maaana alienda Shule hivi karibuni ili aonekane na yeye ana Elimu

Suala la Pili ni kwamba CHADEMA kama wao wameshindwa kutafuta Wafadhili wa kuendesha chama sababu hakuna watu wabunifu ambo wanaweza kuandika Proposal nzuri labda waandikiwe na kina Baregu au Zitto ila wengi wao ni watu wanotawaliwa na Emotion.

The Truth is Upinzani wa kweli utapatikana mpaka pale CCM itakapogawanyika na kupatikana wapinzani wenye uwezo wa kuongozi siyo wanaotafuta Uongozi.

Kimsingi ni kuwa Serikali yetu inashindwa kuendelea kwasabu ya watu wengi ambo wanafanya kazi serikalini ni Vilaza wa kutupwa na kila siku wanataka kushindana na watu wenye uwezo na wanalipwa vizuri na hii inasababisha Rushwa.The same as CHADEMA.

Gembe

You seem to suggest that there is corruption and incompetence in CHADEMA leadership. Can you sight examples by names and conducts instead of just giving a gross generalization?

Mbowe hawezi kulipwa si kwa hoja yako uliyotoa ila kwa kuwa yeye ni Mwenyekiti wa chama, a political figure so to speak, By the virtue of constitution sio day to day operator.

From your daily contributions it appears that you are within the CCM cadres. Can you tell me, is Msekwa paid? Or is he paid as an ex speaker tu?

Why did Kikwete appointed Makamba as MP for Special Seat inline with being Secretary General? Is it not because he was looking for a way to give him extra salary to be able to work as CCM SG? Coz i see him not doiing any work as mbunge but merely party work around the country?

At least CHADEMA has been honest, rather than disguising the salaries under the carpet of other titles!

About wafadhili, you guys are joke. When CHADEMA looks for wafadhili both local and international you say or CHADEMA inategemea wazungu ama ni chama omba omba, if the party choses do depend on ruzuku you end up saying or stop depeding on ruzuku.

I remember this message was posted http://www.chadema.net/mabaraza/bavicha/08/waraka1.php

you guys were the first to say, CHADEMA si mnaruzuku? Kwanini msifanye hizo kazi kwa ruzuku?

Talk about kuandika proposal, tu who? to where? I remember here Mr. Chinga used to call CHADEMA a NGO just because Zitto, Mnyika and Kitila all came from NGO sector and they were good at writing proposal.

You talk about upinzani wa kweli must come from CCM, because you only know CCM wewe.

Can you tell me if CCM are good at writing project proposal?

If they are good tell them to return majengo yetu serikalini kama chama hakitakufa njaa. Tell them to return the Kagoda money? Do you think the Khanga and Vitenge's are from project proposals? Do yo want CHADEMA tu be Chama Cha Majambazi?

Asha
 
watu wanapo kushishia flani ni fisadi mbona unakuwa wa kwanza kuclash?
Angalia post zako vizuri basi,Jitahidi kubadilika mkuu.
Wananchi wanaumia sana kwa ajili ya ufisadi.

Kweli kabisa fidel, post za huyu zemarcopolo ziko upande wa ufisadi zaidi na sasa anataka chadema ijifunze toka kwa mafisadi. Kutetea ufisadi ni sawa na ufisadi wenyewe.
 
Zemarcopolo: Umekazana chadema wajifunze kutoka CCM, nasi tumekuuliza wajifunze nini? Kwa nini hutaki kujibu hili swali?

Halafu hiyo nadharia yako ya kisiasa inayosema kwamba chama cha siasa kijifunze kutoka kwa chama ambacho kinapinga mambo yake ulijifunzie wapi mwenzetu? Yaani Chadema inapinga itikadi, falsafa, sera na matendo ya CCM, halafu wajifunze tena kutoka mambo hayohayo?

Naona huna cha kuishauri chadema; hebu nenda kawashauri hao jamaa zako namna ya kuendesha maisha yao bila kutegemea kuiibia nchi!
 
Tatizo la wana CHADEMA wengi wao hawataki kukubali mapungufu,kukosolewa cha mhimu kwao ukiwapinga wanakuita CCM fisadi huu si ni UDIKITETA WA MAWAZO!!

Hao wanachadema unaowataja hapa ni kina nani?

Badala ya kujadili kilichoandikwa wengi wao watakimbilia kukuambia FISADI yani ndani ya CHADEMA ni ndio mzee hakuna kupinga hata kama kuna mambo unayaona yanakimong'onya chama.

Kama wewe unatetea ufisadi kwa nini usiitwe fisadi?

Wangwe kajifanya kwenda kupingapinga mambo yao Umeona kilichompata.

Hayo ya Wangwe kila mtu amesikia maelezo yake na inaonekana wewe ndiyo una mtizamo huu dhaifu kuhusu kilichompata.

Tatizo mimi naona hatujui CORE ya chama cha siasa, watu wanafikiri nikuchukua hatamu kuingia ikulu mambo yamekwisha,ama kutafuta wafanya biashara wenye pesa zao wawafadhiri hapo kiama ndipo kinaanzia.

CORE ya chama ni kubadili ATMOSPHERE ya wananchi hatimaye nchi ,huwezi badili atmosphere ya nchi ili uje ubadili atmosphere ya wananchi.

Kwa yule anayedhani CORE ya chama ni kuombamba ili aje aiingie ikulu ili aje alipe fadhira kwa wale aliowaomba ndio chazo cha akina ROSTAM.

Haya ni mawazo yako na sio general consensus.

Kuomba omba kwa chama yaliyofanywa na akina Nyerere ni mazingira waliokua nayo na khali yao ya kwamba siamini kama serikali ya kikoloni ingependa kuona TAA inakampuni inayoiigizia fedha na hata kuombaomba kwa TAA ni kwa wakati ule na si tamaduni ya kuilinda.


kuendelea ku REF:mambo aliyofanya Nyerere miaka ile na kuyaendeleza kama ilivyo huo ndio ukosefu wa ubunifu,kinachotakiwa ni kuyangalia na kuya advance zaidi yani ya kwamba mambo ya Nyerere na TANU yake yalikua mazuri lakini yapo ANALOG sana kumbe CHADEMA ama CUF,ama CCM,ama UDP inatakiwa iya process na kuya DIGITALIZE.Mambo ya wakati ule kuyacopy kama yalivyo na kuyapaste wakati huu ndio inakuja ile phenomenani yakua ndivyo tulivyo.

Kama ingekua hivyo maendeleo yasingekuwapo.

Fair enough
 
Mchelea Mwana,

Mbowe hawezi kuidai CHADEMA imlipe fedha zake kwa sababu yeye amejitolea kwa hiari kuchangia chama chake. Mbowe atakuwa na haki ya kudai fedha yake kama kuna makubaliano ya kuwa anachofanya kwa ajili ya CHADEMA ni mkopo kwa chama hicho, na siyo mchango wa kujitolea. Kujitolea na kukopesha ni mambo mawili tofauti.

Kumbukeni tamko la CHADEMA baada ya uchaguzi mkuu 2005. Mbowe alipozungumza na waandishi wakati huo alisema pale kabisa kuwa Kamati Kuu, Baraza Kuu na Mkutano mkuu 2005 wote waliruhusu chama kikope kufanikisha kampeni za 2005. Chama kilikopoa takaribani milioni 700. Kati ya hizo yeye mwenyewe alikopesha 500. Baada ya uchaguzi kamati kuu, baraza kuu na Mkutano Mkuu vilikaa mwaka 2006, Agosti 11, 12 na 13. Vikakubali kulipa madeni yote. Lakini Mbowe akasemee zaidi ya milioni 200 na akataka zingine zihesabike kama mchango wake kwa chama. Sasa badala ya Chacha Wangwe kupongeza anabaki akilalama maneno ya uwongo. Huyu ndiye Chacha Wangwe ambaye kampeni zake za Ubunge zilitumia zaidi ya milioni 20. Mbowe akiwa amempatia milioni 5, chama chake milioni 4, Tundu Lissu pamoja na kumtoa jela alipokuwa amefungwa bado akaingia gharama za milioni 11 kumwezesha kushinda. Si mnakumbuka yale mahojiano ya Chacha na Tanzania Daima baada ya uchaguzi ambapo aliwashukuru hawa? Unakumbuka wakati ule Mbowe alimsaidia Chacha kuanzia Toa Chambiri Tarime(TOCHATA) na vikao vyote kufanyika Billicanas kwa gharama za Mbowe? Hebu vuteni kumbukumbu kwa kuwa Tanzania Daima ilikuwa ikiandika vikao hivyo.

Asha
 
Kumbukeni tamko la CHADEMA baada ya uchaguzi mkuu 2005. Mbowe alipozungumza na waandishi wakati huo alisema pale kabisa kuwa Kamati Kuu, Baraza Kuu na Mkutano mkuu 2005 wote waliruhusu chama kikope kufanikisha kampeni za 2005. Chama kilikopoa takaribani milioni 700. Kati ya hizo yeye mwenyewe alikopesha 500. Baada ya uchaguzi kamati kuu, baraza kuu na Mkutano Mkuu vilikaa mwaka 2006, Agosti 11, 12 na 13. Vikakubali kulipa madeni yote. Lakini Mbowe akasemee zaidi ya milioni 200 na akataka zingine zihesabike kama mchango wake kwa chama. Sasa badala ya Chacha Wangwe kupongeza anabaki akilalama maneno ya uwongo. Huyu ndiye Chacha Wangwe ambaye kampeni zake za Ubunge zilitumia zaidi ya milioni 20. Mbowe akiwa amempatia milioni 5, chama chake milioni 4, Tundu Lissu pamoja na kumtoa jela alipokuwa amefungwa bado akaingia gharama za milioni 11 kumwezesha kushinda. Si mnakumbuka yale mahojiano ya Chacha na Tanzania Daima baada ya uchaguzi ambapo aliwashukuru hawa? Unakumbuka wakati ule Mbowe alimsaidia Chacha kuanzia Toa Chambiri Tarime(TOCHATA) na vikao vyote kufanyika Billicanas kwa gharama za Mbowe? Hebu vuteni kumbukumbu kwa kuwa Tanzania Daima ilikuwa ikiandika vikao hivyo.

Asha

Asha,

Tatizo la Wangwe ni kudhani kuwa watu hawana kumbukumbu na kinachoendelea Tanzania. Ilikuwa Wangwe atumiwe kuivuruga Chadema kabla ya uchaguzi wa 2010 na sasa afadhali akae pembeni ili chama kijipange vizuri zaidi. Wangwe hasemi kuwa Tarime ni moja ya majimbo machache ambayo yanapata pesa ya ruzuku za chadema wakati ambapo majimbo mengi hayaanza kupata chochote. Ni suala la muda tu kabla yote haya hayajawekwa wazi.
 
Asha, msemo wa Kiswahili unasema mtu hujikuna pale mkono unapofika. Kila kitu kinaenda na bajeti na bajeti ni kupanga na kupanga ni kupangua, na unapopangua unachagua. Huwezi kufanya mambo yote with a limited resources, hii ni uchumi 101. Katika kuchagua unafanya kile kinachofuata opportunity cost na unapima kipi kifanywe kwanza.

Ukinipa mimi bajeti ya 59 nitaiangalia na kukuambia ok.. hiki tunaweza kukifanya mwezi huu hiki hatuwezi kukifanya. Hiki lazima kifanyike kila mwezi na kipi kisifanyike kila mwezi. Naomba ieleweke pia kuwa sina maana kuwa wanachama wasichangie fedha zao kwenye kuendesha chama, si kweli vyama huendeshwa kwa michango ya kawaida na michango ya wanachama wake au mashabiki.

Niwape idea: Chadema ina watu maarufu kama Zitto, Chacha mwenyewe, Mbowe, Dr. Slaa na Tundu Lissu. Why not organize a fundraising gala ambapo Chadema inaandaa dinner kwa watu mbalimbali na wafanyabiashara n.k na wananchi wa kawaida? Wakati wa suala la Zitto ilikuwa ni perfect timing kwa chama kujijenga kifedha, hakikufanya hivyo. Likaja suala la Richmond, hawakufanya hivyo, na mambo haya mengine yote Chadema hawajakaa chini na kutumia clout waliyonayo kujijenga financially.

Guess what? CCM ikipata jambo lolote la msingi hawachelewi kucapitalize financially. Nakumbuka jinsi walivyoweza kuchangisha milioni 400 kule Butiama kiulaini tu...that is what political parties do. Leo hii Obama amekuwa mchangishaji wa fedha kwa chama chake kuliko hata Clinton kabla yake! Kwanini wasitumie Popularity ya Zitto na Slaa kupata fedha zaidi za kuendeshea chama au kukipiga jeki.

Leo hii kuna watu mamia wanaofurahia utendaji kazi wa Chadema na wabunge wake, kuna mtandao wa kiintaneti, kwanini hadi leo hii Chadema haijawa ya kwanza kuwa na akaunti ambayo watu wanaweza kuchangia moja kwa moja toka nje? Kwa kutumia mtandao wa intaneti wangeweza kujipatia kiasi fulani cha fedha kwa mashabiki wake. Sitoshangaa CCM muda si mrefu wakaweka akaunti zao kwenye mtandao na ya kuwa wameanza kupokea Visa, Mastercard, AE na DC na kwa kadiri wanavyofungua matawi nje ya nchi sitoshangaa wakapata fedha nyingi tu! Kwanini Chadema wameshindwa kuja na kitu kama hicho?

Kwenye kuchangia kutoka kwa prominent leaders au members.. Badala ya kuchangia hivi hivi tu why not sit down with these members na waambia ni kiasi gani wanaweza kuchangia mara moja kwa mkataba wa kama uwekezaji? Sema kina Zitto (wabunge) na wanachama wengi mashuhuri kila mmoja anasema anaweza kuchangia Shs. milioni 2.5 kuanzisha akaunti ya kuwekeza kwa muda maalumu (Fixed Deposit).

Binafsi ninachosema ni kuwa sidhani kama njia zote za kutafuta fedha za kuendeshea chama zimeweza kuangaliwa na fully explored and exhausted. Nadhani wakikaa chini wanaweza kuona jinsi nyingi tu ya kuweza kukusanya fedha za chama. Vipi kuhusu kutengeneza Tshirt za viongozi mashuhuri!? halafu zikauzwa baada ya kuwa autographed!? Siasa ni mchezo wa mikakati, mbinu, kuthubutu na kufikiri nje ya kisanduku. Chadema haina sababu ya kutegemea ruzuku tu, jinsi ile ile CCM haina sababu ya kutegemea ruzuku.

Tatizo ni kuwa wenzao CCM wana uwezo wa kuchota hata kutoka katika altare!
 
Tatizo la wana CHADEMA wengi wao hawataki kukubali mapungufu,kukosolewa cha mhimu kwao ukiwapinga wanakuita CCM fisadi huu si ni UDIKITETA WA MAWAZO!!

Badala ya kujadili kilichoandikwa wengi wao watakimbilia kukuambia FISADI yani ndani ya CHADEMA ni ndio mzee hakuna kupinga hata kama kuna mambo unayaona yanakimong'onya chama.

Wangwe kajifanya kwenda kupingapinga mambo yao Umeona kilichompata.

Tatizo mimi naona hatujui CORE ya chama cha siasa, watu wanafikiri nikuchukua hatamu kuingia ikulu mambo yamekwisha,ama kutafuta wafanya biashara wenye pesa zao wawafadhiri hapo kiama ndipo kinaanzia.

CORE ya chama ni kubadili ATMOSPHERE ya wananchi hatimaye nchi ,huwezi badili atmosphere ya nchi ili uje ubadili atmosphere ya wananchi.

Kwa yule anayedhani CORE ya chama ni kuombamba ili aje aiingie ikulu ili aje alipe fadhira kwa wale aliowaomba ndio chazo cha akina ROSTAM.

Kuomba omba kwa chama yaliyofanywa na akina Nyerere ni mazingira waliokua nayo na khali yao ya kwamba siamini kama serikali ya kikoloni ingependa kuona TAA inakampuni inayoiigizia fedha na hata kuombaomba kwa TAA ni kwa wakati ule na si tamaduni ya kuilinda.

kuendelea ku REF:mambo aliyofanya Nyerere miaka ile na kuyaendeleza kama ilivyo huo ndio ukosefu wa ubunifu,kinachotakiwa ni kuyangalia na kuya advance zaidi yani ya kwamba mambo ya Nyerere na TANU yake yalikua mazuri lakini yapo ANALOG sana kumbe CHADEMA ama CUF,ama CCM,ama UDP inatakiwa iya process na kuya DIGITALIZE.Mambo ya wakati ule kuyacopy kama yalivyo na kuyapaste wakati huu ndio inakuja ile phenomenani yakua ndivyo tulivyo.

Kama ingekua hivyo maendeleo yasingekuwapo.

Kazi kweli kweli kweli!

Huyu Bwana anadhani CORE bussiness ya chama cha siasa ni kuuza nyanya,maembe na kupata faida; hajui kuwa kazi ya chama cha siasa ni kuuza sera, viongozi na kupata kura, mamlaka na hatimaye kuleta mabadiliko.

Hebu angalia kule Marekani, yule Barack Obama wa Democrat chama chake kinaendeshwa na nani kama si michango ya wanachama na wapenzi?

Chama chaweza kuwa na miradi michache tu ya kujikimu lakini sio kujikita kwenye kufanya biashara. Chama kinapaswa kujengwa na wanachama na wapenzi.

Halafu unadhani ni rahisi tu kwa vyama vya upinzani kuanzisha makampuni na kutengeneza faida eeeh.

kama watu wanapigwa Kiteto, wafanyabiashara wanatishiwa- itakuwa makampuni ya upinzani?

Don't forget here we have a state party that knows nothing but plundering and looting!

Sasa unataka Zitto na Dr Slaa waache kutoa michango bungeni wakaendeshe TOT plus? Halafu baada ya hapo muanze propaganda kuwa wameishiwa, na muanze kuwaambie wananchi kuwa msiende ile bendi ni ya wapinzani? Halafu mpite kwenye studio na kwa wafanyabiashara mkisema msiipe tenda ile bendi ni ya wapinzani? Halafu mpite na vituo vyenu vya redio mpige marufuku nyimbo zao? Swaini!

Nakumbuka mlivyokataza ziara za Mbowe zisionyeshwe TVT, ITV, Channel Ten pamoja na kuwa CHADEMA ilitaka kulipia kama vipindi maalumu. Ni simu ya Lowassa ilitosha kuzuia. Sasa Pinda wenu nae amepinda kwa kuikataza TVT kuonesha hotuba ya mpambanaanaji Slaa.

Halafu you talk about biashara! Bongo!

Asha
 
Asha, msemo wa Kiswahili unasema mtu hujikuna pale mkono unapofika. Kila kitu kinaenda na bajeti na bajeti ni kupanga na kupanga ni kupangua, na unapopangua unachagua. Huwezi kufanya mambo yote with a limited resources, hii ni uchumi 101. Katika kuchagua unafanya kile kinachofuata opportunity cost na unapima kipi kifanywe kwanza.

Ukinipa mimi bajeti ya 59 nitaiangalia na kukuambia ok.. hiki tunaweza kukifanya mwezi huu hiki hatuwezi kukifanya. Hiki lazima kifanyike kila mwezi na kipi kisifanyike kila mwezi. Naomba ieleweke pia kuwa sina maana kuwa wanachama wasichangie fedha zao kwenye kuendesha chama, si kweli vyama huendeshwa kwa michango ya kawaida na michango ya wanachama wake au mashabiki.

Niwape idea: Chadema ina watu maarufu kama Zitto, Chacha mwenyewe, Mbowe, Dr. Slaa na Tundu Lissu. Why not organize a fundraising gala ambapo Chadema inaandaa dinner kwa watu mbalimbali na wafanyabiashara n.k na wananchi wa kawaida? Wakati wa suala la Zitto ilikuwa ni perfect timing kwa chama kujijenga kifedha, hakikufanya hivyo. Likaja suala la Richmond, hawakufanya hivyo, na mambo haya mengine yote Chadema hawajakaa chini na kutumia clout waliyonayo kujijenga financially.

Guess what? CCM ikipata jambo lolote la msingi hawachelewi kucapitalize financially. Nakumbuka jinsi walivyoweza kuchangisha milioni 400 kule Butiama kiulaini tu...that is what political parties do. Leo hii Obama amekuwa mchangishaji wa fedha kwa chama chake kuliko hata Clinton kabla yake! Kwanini wasitumie Popularity ya Zitto na Slaa kupata fedha zaidi za kuendeshea chama au kukipiga jeki.

Leo hii kuna watu mamia wanaofurahia utendaji kazi wa Chadema na wabunge wake, kuna mtandao wa kiintaneti, kwanini hadi leo hii Chadema haijawa ya kwanza kuwa na akaunti ambayo watu wanaweza kuchangia moja kwa moja toka nje? Kwa kutumia mtandao wa intaneti wangeweza kujipatia kiasi fulani cha fedha kwa mashabiki wake. Sitoshangaa CCM muda si mrefu wakaweka akaunti zao kwenye mtandao na ya kuwa wameanza kupokea Visa, Mastercard, AE na DC na kwa kadiri wanavyofungua matawi nje ya nchi sitoshangaa wakapata fedha nyingi tu! Kwanini Chadema wameshindwa kuja na kitu kama hicho?

Kwenye kuchangia kutoka kwa prominent leaders au members.. Badala ya kuchangia hivi hivi tu why not sit down with these members na waambia ni kiasi gani wanaweza kuchangia mara moja kwa mkataba wa kama uwekezaji? Sema kina Zitto (wabunge) na wanachama wengi mashuhuri kila mmoja anasema anaweza kuchangia Shs. milioni 2.5 kuanzisha akaunti ya kuwekeza kwa muda maalumu (Fixed Deposit).

Binafsi ninachosema ni kuwa sidhani kama njia zote za kutafuta fedha za kuendeshea chama zimeweza kuangaliwa na fully explored and exhausted. Nadhani wakikaa chini wanaweza kuona jinsi nyingi tu ya kuweza kukusanya fedha za chama. Vipi kuhusu kutengeneza Tshirt za viongozi mashuhuri!? halafu zikauzwa baada ya kuwa autographed!? Siasa ni mchezo wa mikakati, mbinu, kuthubutu na kufikiri nje ya kisanduku. Chadema haina sababu ya kutegemea ruzuku tu, jinsi ile ile CCM haina sababu ya kutegemea ruzuku.

Tatizo ni kuwa wenzao CCM wana uwezo wa kuchota hata kutoka katika altare!


Mwanakijiji

Hayo yote uyasemayo CHADEMA imeshayafanyia kazi. Labda uongezeke na wewe usaidie hiyo kazi. Kwani nani kakwambia kwamba CHADEMA ni Zitto na Dr Slaa tu, hivi kwanini mnapenda kukaa pembeni na kunyoosha vidole tu!

Hizo fundraising gala zinafanyika. Kwani hapa si tuliwekewa Hotuba ya Fundraising Dinner ya Arusha ambayo Mgeni Rasmi alikuwa Mtei, Zitto na Mhonga akiwepo? Iliandaliwa na vijana wa CHADEMA?

Tatizo ni kuwa wafanyabiashara wengi wanaogopa athari za kujitokeza kuchangia upinzani. CCM wanawabana. Ndio maana utawakupa wakina Ngurdoto, Impala wote wanakwenda kwenye harambee za CCM. Halafu ni huko huko wakina Johnson Lukaza wanakwenda kubariki mabilioni ya EPA kuwa fedha halali za chama.

Hamishia huu mjadala kwenye makala zako usaidie kujenga demokrasia Tanzania badala ya kulalama tu humu.

Hiyo link ya akaunti niliyotoa si iko kwenye website ya CHADEMA? Kwa nini watu wa nje hawachangii? Labda unachoweza kuwasidia ni kuwatengenezea pay pall uunganishe na hiyo akaunti namba kama ambavyo umefanya kwa KLH. Lakini jua hawa watanzania ni wakosoaji tu, maneno mengi bila vitendo.

Kama mntaka upinzani makini Tanzania chukueni hatua badala ya kukaa tu na kunyanyua vidole juu.


Ile like you because you take action. Go go go go go. Tutafika tu. Na jua wakuu wa CHADEMA wanakusoma, lakini mambo si rahisi kama unavyodhani.

Unaweza kuamua kuwaleta wakina beyonce bongo, lakini wakijua tu wanaletwa na upinzani Afrika wataishia Airport. Siasa Afrika si sawa na ulaya. We have to transform the terrain. Then we can make it

Asha
 
Mwanakijiji

Hayo yote uyasemayo CHADEMA imeshayafanyia kazi. Labda uongezeke na wewe usaidie hiyo kazi. Kwani nani kakwambia kwamba CHADEMA ni Zitto na Dr Slaa tu, hivi kwanini mnapenda kukaa pembeni na kunyoosha vidole tu!

Hizo fundraising gala zinafanyika. Kwani hapa si tuliwekewa Hotuba ya Fundraising Dinner ya Arusha ambayo Mgeni Rasmi alikuwa Mtei, Zitto na Mhonga akiwepo? Iliandaliwa na vijana wa CHADEMA?

Tatizo ni kuwa wafanyabiashara wengi wanaogopa athari za kujitokeza kuchangia upinzani. CCM wanawabana. Ndio maana utawakupa wakina Ngurdoto, Impala wote wanakwenda kwenye harambee za CCM. Halafu ni huko huko wakina Johnson Lukaza wanakwenda kubariki mabilioni ya EPA kuwa fedha halali za chama.

Hamishia huu mjadala kwenye makala zako usaidie kujenga demokrasia Tanzania badala ya kulalama tu humu.

Hiyo link ya akaunti niliyotoa si iko kwenye website ya CHADEMA? Kwa nini watu wa nje hawachangii? Labda unachoweza kuwasidia ni kuwatengenezea pay pall uunganishe na hiyo akaunti namba kama ambavyo umefanya kwa KLH. Lakini jua hawa watanzania ni wakosoaji tu, maneno mengi bila vitendo.

Kama mntaka upinzani makini Tanzania chukueni hatua badala ya kukaa tu na kunyanyua vidole juu.


Ile like you because you take action. Go go go go go. Tutafika tu. Na jua wakuu wa CHADEMA wanakusoma, lakini mambo si rahisi kama unavyodhani.

Unaweza kuamua kuwaleta wakina beyonce bongo, lakini wakijua tu wanaletwa na upinzani Afrika wataishia Airport. Siasa Afrika si sawa na ulaya. We have to transform the terrain. Then we can make it

Asha

Kwanza I take offense kuwa tunakaa Ulaya na kunyanyua vidole tu! yaani kusaidia chadema hadi wote turudi nyumbani? Hii ni argument ambayo imekuwa ikitolewa na wana CCM kila tunapotoa hoja. Ni lini Chadema wameweka akaunti yao hadharani na kuomba kuchangiwa ni mashabiki na wanachama wake walioko nje ya nchi? Hivi hili nalo inabidi hadi turudi nyumbani?

Suala la wafanyabiashara ni moja lakini ni kwa kiasi gani Chadema na vyama vingine vya upinzani vimethubutisha wafanyabiashara kujiunga nao. Hapa sizungumzii wafanyabiashara wakubwa tu nazungumzia hata wadogo. CCM na serikali yake haiwezi kuwawekea ngumu wafanyabiashara wadogowadogo bila kusababisha dhuluma!

Sasa kama mawazo na hoja ni za wale walioko nyumbani tu na michango ni mpaka turudi wote nyumbani basi endeleeni kupeana mawazo ninyi wenyewe, kwani si wote mashabiki wa Chadema ni wanachama wa Chadema!
 
Kwanza I take offense kuwa tunakaa Ulaya na kunyanyua vidole tu! yaani kusaidia chadema hadi wote turudi nyumbani? Hii ni argument ambayo imekuwa ikitolewa na wana CCM kila tunapotoa hoja. Ni lini Chadema wameweka akaunti yao hadharani na kuomba kuchangiwa ni mashabiki na wanachama wake walioko nje ya nchi? Hivi hili nalo inabidi hadi turudi nyumbani?

Suala la wafanyabiashara ni moja lakini ni kwa kiasi gani Chadema na vyama vingine vya upinzani vimethubutisha wafanyabiashara kujiunga nao. Hapa sizungumzii wafanyabiashara wakubwa tu nazungumzia hata wadogo. CCM na serikali yake haiwezi kuwawekea ngumu wafanyabiashara wadogowadogo bila kusababisha dhuluma!

Sasa kama mawazo na hoja ni za wale walioko nyumbani tu na michango ni mpaka turudi wote nyumbani basi endeleeni kupeana mawazo ninyi wenyewe, kwani si wote mashabiki wa Chadema ni wanachama wa Chadema!

Challenge has been taken for action we will make the account number public.
 
Kwanza I take offense kuwa tunakaa Ulaya na kunyanyua vidole tu! yaani kusaidia chadema hadi wote turudi nyumbani? Hii ni argument ambayo imekuwa ikitolewa na wana CCM kila tunapotoa hoja. Ni lini Chadema wameweka akaunti yao hadharani na kuomba kuchangiwa ni mashabiki na wanachama wake walioko nje ya nchi? Hivi hili nalo inabidi hadi turudi nyumbani?

Suala la wafanyabiashara ni moja lakini ni kwa kiasi gani Chadema na vyama vingine vya upinzani vimethubutisha wafanyabiashara kujiunga nao. Hapa sizungumzii wafanyabiashara wakubwa tu nazungumzia hata wadogo. CCM na serikali yake haiwezi kuwawekea ngumu wafanyabiashara wadogowadogo bila kusababisha dhuluma!

Sasa kama mawazo na hoja ni za wale walioko nyumbani tu na michango ni mpaka turudi wote nyumbani basi endeleeni kupeana mawazo ninyi wenyewe, kwani si wote mashabiki wa Chadema ni wanachama wa Chadema!


No offence meant jamani. I take my words.

I meant wote tu wanaokaa tu vidole juu, wawe ulaya au mbagala wote sawa. Unaweza kuchangia CHADEMA kama we ni mwanaCHADEMA au mpenzi wa siasa za demokrasia na maendeleo hata ukiwa mbiguni. Au unaweza kuandika makala.

By the way, mbona sijaona ukichambua masuala haya kwenye makala zako za jumatano? Hizi ni hoja zinazokosa mtetezi matokeo yake Habari za Balille za kupikwa kwenye mtanzania na Rai ndio zinawafanya wananchi waamini kuwa Chacha ni Shujaa aliyesimamishwa kama Vile Zitto alivyosimamishwa na CCM. Kumbe Chacha is a piece of crap. Nikikutana nae nitampasha maneno yake na nitawaletea mazungumzo yake nami kwenye http://ashawazenj.blogspot.com. This guy is eating his own flesh for no apparent reasons! Kila mwanachama ana haki ya kukosoa lakini hakuna mwenye haki ya kusambaza uwongo, uzushi na majungu.

Asha
 
MKJJ: Nakubaliana na analysis yako 200%. Chadema haijatumia umaarufu wa viongozi wake kujiimarisha kitaasisi na hasa kimapato, au niweke hivi: viongozi maarufu wa chadema hawajatumia vizuri umaarufu wao kuiimarisha chadema kitaasisi na kifedha ili kuondokana na utegemezi wa watu wachache. Tunaelekea kufanya kosa walilofanya akina Mrema-walijiimarisha wao bila kuimarisha NCCR institutionally kiasi kwamba walipobomoka wao kitaswira na NCCR nayo ikabomoka kitaasisi.

Nafikiri ni muhimu sana upaaji wa kisiasa wa viongozi uende sambamba na upaaji wa chama kitaasisi maana binadamu hupita lakini taasisi zinabaki. Kwa utaratibu uliopo sasa hivi ina maana siku viongozi wanaokisaidia chama ikitokea wakayumba kifedha na kitaswira ina maana kuna uwezekano mkubwa chama nacho kikayumba! Yours was a big challenge and I do hope it will be taken up somewhere in chadema's deliberation forums!

Hiki ndicho kilikuwa kilio changu siku zote, naona sasa kinaanza kusikilizwa. Kwamba tuelekeze nguvu zetu juu ya namna ya kuijenga chadema ili iwe kweli chama mbadala kwa huyu mgonjwa wetu ambaye hatutarajii apone-CCM. Huku ndiko mimi nakuita kujenga! Kudos wachangiaji wote, tuendele kuweka vitu madamu Katibu Mkuu mwenyewe wa Chadema yupo hapa hakuna kitachoharibika.
 
Asha, msemo wa Kiswahili unasema mtu hujikuna pale mkono unapofika.

Niwape idea: Chadema ina watu maarufu kama Zitto, Chacha mwenyewe, Mbowe, Dr. Slaa na Tundu Lissu. Why not organize a fundraising gala ambapo Chadema inaandaa dinner kwa watu mbalimbali na wafanyabiashara n.k na wananchi wa kawaida? Wakati wa suala la Zitto ilikuwa ni perfect timing kwa chama kujijenga kifedha, hakikufanya hivyo. Likaja suala la Richmond, hawakufanya hivyo, na mambo haya mengine yote Chadema hawajakaa chini na kutumia clout waliyonayo kujijenga financially.

Guess what? CCM ikipata jambo lolote la msingi hawachelewi kucapitalize financially.

Leo hii kuna watu mamia wanaofurahia utendaji kazi wa Chadema na wabunge wake, kuna mtandao wa kiintaneti, kwanini hadi leo hii Chadema haijawa ya kwanza kuwa na akaunti ambayo watu wanaweza kuchangia moja kwa moja toka nje?

Mnapewa idea nzuri zifanyieni kazi. Mkiendelea kudhani kufungua matawi nje ni "upuuzi" mjue mnakosea. Take this example, kila mwanachama wa CCM London anatoa pound 30 kila mwaka kwa ajili ya Chama. Kukiwa na shughuli watu huc´hangishana pia. Hivyo basi siku kukiwa na mahitaji watu wako standby kukisaidia chama. Huo ndio umuhimu wa tawi, ni tofauti na kufuata mtu mmoja mmoja.Jifunzeni toka CCM.

Dr. Slaa anaonyesha moyo wa kuwa tayari kujifunza toka kwa CCM anapotoa mfano wa wana TANU walipokuwa wanajitolea, lakini inabidi akumbuke kuwa TANU ilikufa tangu mwaka 1977 sasa CHADEMA wajifunze kwa CCM ya sasa sio TANU, hii ni karne nyingine.Acheni kulalamika, jifunzeni mtaona njia.
 
Back
Top Bottom