Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
CCM ni tofauti sana na vyama vingine vya siasa nchini ambavyo vina usajili kamili chini ya sheria ya Vyama. Sifa pekee za CCM zinajidhihirisha wazi wazi katika masuala mazito ya kitaifa yafuatayo:-
(toka Kanuni za Uteuzi wa CCM)
(1) Azma ya kuhakikisha kwamba Muungano wa Tanzania na Mapinduzi ya Zanzibar vinaheshimiwa, vinalindwa na vinaendelezwa wakati wote.,
(2) Azma ya kuhakikisha kwamba ardhi inaendelea kuwa rasilimali kuu ya Taifa na inayoendelezwa kwa maslahi ya wananchi wote.
(3) Azma ya kutaka kuona kwamba Tanzania ni Taifa lenye Umoja, Amani, Utulivu na Mshikamano madhubuti wa kitaifa wakati wote;
(4) Azma ya kuhakikisha kwamba Utawala wa Sheria na Utawala Bora vinalindwa na kuendelezwa wakati wote;
(5) Azma ya kuhakikisha kwamba Watanzania tunajenga maadili na demokrasia ya vyama vingi katika mazingira ya amani, yanayokataa siasa za uchochezi, uzushi, kashfa, uzandiki, uongo, ubaguzi wa rangi, ukabila, umajimbo na udini, mambo ambayo ni kinyume cha Haki za Binadamu.
Wananchi kuichagua CCM maana yake ni kujihakikishia wao wenyewe kwamba wataendelea kula hayo matunda ya uhuru kwa ukamilifu.(2) Azma ya kuhakikisha kwamba ardhi inaendelea kuwa rasilimali kuu ya Taifa na inayoendelezwa kwa maslahi ya wananchi wote.
(3) Azma ya kutaka kuona kwamba Tanzania ni Taifa lenye Umoja, Amani, Utulivu na Mshikamano madhubuti wa kitaifa wakati wote;
(4) Azma ya kuhakikisha kwamba Utawala wa Sheria na Utawala Bora vinalindwa na kuendelezwa wakati wote;
(5) Azma ya kuhakikisha kwamba Watanzania tunajenga maadili na demokrasia ya vyama vingi katika mazingira ya amani, yanayokataa siasa za uchochezi, uzushi, kashfa, uzandiki, uongo, ubaguzi wa rangi, ukabila, umajimbo na udini, mambo ambayo ni kinyume cha Haki za Binadamu.
(toka Kanuni za Uteuzi wa CCM)