Patriote
JF-Expert Member
- Jul 13, 2011
- 1,718
- 1,047
Katika toleo la mwananchi la jana nisiloma habari kuwa Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh amesema ripoti ya Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA), ipo katika hatua za mwisho na ifikapo mwishoni mwa mwezi ujao, kila kitu kitawekwa wazi. Hakika sikuelewa kwamba Bw. Ludovick Utouh bado anaendelea kushikilia ofisi ya Umma hasa baada ya kuongea upupu katika issue ya Jairo na Bunge kuthibitisha kuwa CAG alitoa ushauri ambao ni substandard kwa lengo la kupotosha ukweli na kuhadaa umma wa watanzania na kulinda ukiukwaji wa sheria na taratibu za fedha alizoapa kuzilinda. Mtu wa aina hii kimsingi ameshapoteza sifa na imani kwa wananchi kwa kuuthibitishia umma kuwa ni mwongomwongo na anatetea wizi wa rasilimali zetu na hivyo hapaswi kuaminiwa. Inakuwaje tena watanzania sisi sisi tunasubiri kupokea taarifa ya UDA anayoiandaa mtu wa namna hii??? Rejea sehemu ya taarifa ya kamati teule ya bunge katika sakata la Jairo.
"Katika sehemu ya ushauri na hitimisho la CAG, Taarifa ya Ukaguzi Maalum haikuzingatia yaliyojitokeza ndani ya Taarifa ili kutoa majibu kwa Hadidu za Rejea badala yake ushauri pekee unaonekana kuegemea katika idadi ya Taasisi kuwa 20 na kiwango cha fedha ilizochangwa kuwa Sh.1,000,000,000.00. Hatua hii imesababisha upotoshaji mkubwa kwa Katibu Mkuu Kiongozi ambaye naye alitumia ushauri huu kama msingi wa Maamuzi yake katika Uchunguzi wa Awali alioufanya. Hata hivyo baada ya kukabidhiwa, Katibu Mkuu Kiongozi alipaswa kuitumia Taarifa ya Ukaguzi Maalum kwa ujumla wake badala ya kipengele cha ushauri ambacho ni upotoshaji" (Taarifa ya kamati, 2011)
Hivi inamana tumeshasahau aliyoyafanya kwenye ripoti ya Jairo au ndo tutake tusitake lazma CAG awe ni huyu huyu??? Mimi nadhan kazi ya CAG inahitaji mtu muadilifu sana na mtu asiye na hulka ya uongo uongo na asili ya upotoshaji hata kidogo. Sasa kama CAG ndo anaongoza kwa uongo, upotoshaji na kuficha ukweli pamoja na kulinda wizi katika serikali yetu, anatarajia wasiadizi wake wafanye nini???Hivi kweli mtu wa hivi akiandaa report nyingine inaleta maana/mantiki yoyote kweli???Mbaya zaid report yenyewe inahusu tuhuma za ufisadi kama ila ya Jairo. Hakika sio bure "Tanzanians must be crazy"!!Hivi kuna ugumu gani kukataa mtu huyu asishike kitengo nyeti kama hicho hasa baada ya kuonekana hana uaminifu na anafumbia macho ukiukwaji mkubwa wa sheria za fedha badala ya kuzisimamia na kuzilinda kama alivyoapa????Kama hii ndiyo tabia yake, kwanini tuendelee kumuamini kiasi hiki hata kumwacha aendelee kufanya ukaguzi maalum sehemu nyingine??Ni nini kilimsukuma kulinda waharifu na kufumbia macho ukiukwaju mkubwa wa sheria na taratibu za fedha kwa Jairo??Je tuna uhakika gani kama hatorudia tena UDA?? Kimsingi alitutia hasara kwa makusudi kwa kutokuwajibika ipasavyo na hivyo kupelekea Bunge kuteua kamati maalum na kufanya kazi iliyopaswa kufanywa na CAG, Kimsingi kwa gharama ya Kodi za Wanzanchi. Kwanini mtu huyu aendelee kutumikia umma hadi leo????WANAJF NAMLETA KWENU MTU HUYU. Nini kifanyike juu yake wakati huu anasubiri adhabu kama Bunge lilivyoishauri Serikali??Mi naona hana sifa ya kushika mafile ya Serikali.........wewe waonaje??
"Katika sehemu ya ushauri na hitimisho la CAG, Taarifa ya Ukaguzi Maalum haikuzingatia yaliyojitokeza ndani ya Taarifa ili kutoa majibu kwa Hadidu za Rejea badala yake ushauri pekee unaonekana kuegemea katika idadi ya Taasisi kuwa 20 na kiwango cha fedha ilizochangwa kuwa Sh.1,000,000,000.00. Hatua hii imesababisha upotoshaji mkubwa kwa Katibu Mkuu Kiongozi ambaye naye alitumia ushauri huu kama msingi wa Maamuzi yake katika Uchunguzi wa Awali alioufanya. Hata hivyo baada ya kukabidhiwa, Katibu Mkuu Kiongozi alipaswa kuitumia Taarifa ya Ukaguzi Maalum kwa ujumla wake badala ya kipengele cha ushauri ambacho ni upotoshaji" (Taarifa ya kamati, 2011)
Hivi inamana tumeshasahau aliyoyafanya kwenye ripoti ya Jairo au ndo tutake tusitake lazma CAG awe ni huyu huyu??? Mimi nadhan kazi ya CAG inahitaji mtu muadilifu sana na mtu asiye na hulka ya uongo uongo na asili ya upotoshaji hata kidogo. Sasa kama CAG ndo anaongoza kwa uongo, upotoshaji na kuficha ukweli pamoja na kulinda wizi katika serikali yetu, anatarajia wasiadizi wake wafanye nini???Hivi kweli mtu wa hivi akiandaa report nyingine inaleta maana/mantiki yoyote kweli???Mbaya zaid report yenyewe inahusu tuhuma za ufisadi kama ila ya Jairo. Hakika sio bure "Tanzanians must be crazy"!!Hivi kuna ugumu gani kukataa mtu huyu asishike kitengo nyeti kama hicho hasa baada ya kuonekana hana uaminifu na anafumbia macho ukiukwaji mkubwa wa sheria za fedha badala ya kuzisimamia na kuzilinda kama alivyoapa????Kama hii ndiyo tabia yake, kwanini tuendelee kumuamini kiasi hiki hata kumwacha aendelee kufanya ukaguzi maalum sehemu nyingine??Ni nini kilimsukuma kulinda waharifu na kufumbia macho ukiukwaju mkubwa wa sheria na taratibu za fedha kwa Jairo??Je tuna uhakika gani kama hatorudia tena UDA?? Kimsingi alitutia hasara kwa makusudi kwa kutokuwajibika ipasavyo na hivyo kupelekea Bunge kuteua kamati maalum na kufanya kazi iliyopaswa kufanywa na CAG, Kimsingi kwa gharama ya Kodi za Wanzanchi. Kwanini mtu huyu aendelee kutumikia umma hadi leo????WANAJF NAMLETA KWENU MTU HUYU. Nini kifanyike juu yake wakati huu anasubiri adhabu kama Bunge lilivyoishauri Serikali??Mi naona hana sifa ya kushika mafile ya Serikali.........wewe waonaje??