Kwanini BAKWATA wawe na kibali cha kuagiza sukari?

Ozzanne Issakwisa

JF-Expert Member
Mar 7, 2016
288
239
Utolewaji wa vibali vya kuagiza sukari nje ya nchi, sio kitu rahisi.

Nilikuwa nasoma gazeti la Jamhuri, nikashangaa kuona BAKWATA ni kati ya taasisi ambazo zina kibali cha kuagiza sukari toka nje ya nchi. Na kwamba wana kibali cha kuagiza tani 2,500/=. Nikajiuliza hii sukari wanayoagiza ni kwa ajili ya uji wa watoto katika vituo vya watoto yatima? Au kuna watu wanatumia taasisi kujinufaisha na kuichafua taasisi?

Labda ni vizuri tukajua ni kina nani hawa waliokuwa wakipewa hivi vibali maalumu vya kuagiza sukari. Nao ni wafuatao: Tanzania Commodities Trading Co. LTD (tani 26), TPM LTD (tani 12), Matunda B.C. LTD (tani 12), East Coast Oils and Fats Ltd (tani 1,292) na New Tradeco Investment Ltd.

Wengine ni, Mohamed Enterprises (T) LTD (tani 8), Decent Investment Ltd (2,116), Rubab Investment Ltd (tani 12), Multi Modal Transport Africa (tani 2), Trade Logistics (EA) Ltd (tani 12), Ngawaiya Stores (tani 100), DRTC Trading Company Ltd (tani 2,522) na Market Makers (T) Ltd (tani 480).

Wengine ni Supermarket (tani 910), Power Roads (tani 1,170), A. O. K. Investment (tani 500), B. F. K. Company Ltd (tani 500), Kigwaza Holdings (tani 500), Sofia International (tani 500), Conti Africa Ltd (tani 260), Masooma Supermarket (tani 208), BAKWATA (tani 2,500), Saddique Supper Service Station (tani 1,700) OLAM Tanzania Ltd (tani 832), United Youth Shipping Co. Ltd (tani 494) na EDISABA General Supplies Ltd (tani 1,000).

Inawezekana wengi kati ya hawa ni wafanyabiashara wa sukari, isipokuwa Bakwata. Mimi sina hakika kama wao pia wanafanya biashara ya kuagiza na kuuza sukari. Labda wahusika watatueleza.

Source: Tunazuia Sukari Kutoka Nje Kwa Maslahi Ya Nani? | Gazeti La Jamhuri
 
Wasitumie mgongo wa dini kukwepa kodi hili ni dili kati ya wafanyabiashara wakubwa wa sukari na tasisi hii nyeti nchini hebu ona bakwata wanavyohujumu uchumi wa nchi bila huruma wafutiwe hiki kibali maana mabaraza mengine ya dini pia yatalazimisha yapewe
 
Hili suala halina muislamu wala mkristo isipokuwa hili suala litaleta mkanganyiko kwenye taifa...kwani inafahamika kuwa BAKWATA ni taasisi ya kidini na sio kampuni ya biashara...sasa hicho kibalj cha kuagiza hiyo sukari kwa kiwango hicho ni kwa manufaa ya nani.....??
Ni kwamba kuna maduka ya BAKWATA yanayouza sukari au kuna magodown ya BAKWATA yanasambaza sukari au tuseme ni kwa ajili kuwa gawia waislamu wasiojiweza....???
Na tangu kupata hicho kibali imeshaagiza tani ngapi na zimeenda wapi maana hatujui hayo magodown ya BAKWATA yalipo.....

Hili suala linahitaji maelezo ya kina ili kuweka mambo sawa....kwa maslahi ya taifa....
 
Hili suala halina muislamu wala mkristo isipokuwa hili suala litaleta mkanganyiko kwenye taifa...kwani inafahamika kuwa BAKWATA ni taasisi ya kidini na sio kampuni ya biashara...sasa hicho kibalj cha kuagiza hiyo sukari kwa kiwango hicho ni kwa manufaa ya nani.....??
Ni kwamba kuna maduka ya BAKWATA yanayouza sukari au kuna magodown ya BAKWATA yanasambaza sukari au tuseme ni kwa ajili kuwa gawia waislamu wasiojiweza....???
Na tangu kupata hicho kibali imeshaagiza tani ngapi na zimeenda wapi maana hatujui hayo magodown ya BAKWATA yalipo.....

Hili suala linahitaji maelezo ya kina ili kuweka mambo sawa....kwa maslahi ya taifa....
point
 
Toni 2500 za kazi gani, au BAKWATA siku hizi wanajishughulisha na biashara ya sukari.

Hawa BAKWATA waliwahi hojiwa kwa ukwepaji kodi wa malori wakati wao hawana hata moja.

Inaonekana hiyo taasisi inatumika kwa maslahi ya wachache.
kanisa nalo liagize matarumbeta na misalaba
 
Back
Top Bottom