Kwani ni lazima serikali iingilie sekta binafsi ya Mafuta?

tetesi: rais kikwete amewapa maagizo wanajeshi kuingilia shell binafsi kuzikagua na kuwalazimisha na ikibidi MPs wa jeshi wauze kwa nguvu

note:bado sijaweza kuzithibitisha habari hizi




Yesu Wangu!

Hii ibaki kuwa rumour kwa sababu itakuwa ni kosa kubwa sana mbele ya dunia.

Chonde, chonde, chonde! Kama serikali inataka kuingilia kati, basi iwe ni kuiamuru EWURA iondoe agizo la bei hii ya 2,004/=. Warudishe ile bei ya 2,090/=, ambayo ndiyo bei itayowawezesha hawa wa mafuta kupata faida waliotarajia.

Kisheria, haya mafuta ni ya hao wafanya biashara pamoja na principals wengine kama mabenki yaliyowakopa kuagizia mafuta. Hauwezi ukawalazimisha wayauze, lakini unaweza ukaweka mazingira yatayowafanya wasione faida ya kuyauza kama walivyofanya EWURA na hili agizo lao la 2,004/=.
 
serikali ikiamua kukaa pembeni kutakuwa na athari gani? Maana bei ikipanda sana watu hawatanunua! Hapa ndio suala la UDA linapokuja!!

MM wakikaa pembeni bei zipande kuna athari kwao maana umma utasukumwa hadi kikomo cha uvumilivu.

Kwa kuachia kila kitu mikononi mwa watu binafsi/capitalists serikali inavuna ilichopanda.

Kwa vile hawajui kujiafunza kwa makosa ya jana, hata UDA wanampa mtu binafsi/capitalist siku moja nchi/miji utakuwa paralyzed kwa wasafirishaji wa umma kutia mgomo kama huu wa wauza mafuta unaoendelea sasa.

Kifupi serikali imetiwa mfukoni kitu ambacho Nyerere alimshikisha adabu Giriki kwa kutamka tu kwamba katia serikali mfukoni.
 
MMKJ,
maswali yako yote nadhani yana jibu hili:
hatuna viongozi bali tuna watawala. Wanatawala si kwa maslahi ya watawaliwa bali watawala.

Najua kuna viongozi wachache, lakini aidha wamefunikwa au wapo ngazi za chini na hawana any big effect
 
Yesu Wangu!

Hii ibaki kuwa rumour kwa sababu itakuwa ni kosa kubwa sana mbele ya dunia.

Chonde, chonde, chonde! Kama serikali inataka kuingilia kati, basi iwe ni kuiamuru EWURA iondoe agizo la bei hii ya 2,004/=. Warudishe ile bei ya 2,090/=, ambayo ndiyo bei itayowawezesha hawa wa mafuta kupata faida waliotarajia.

Kisheria, haya mafuta ni ya hao wafanya biashara pamoja na principals wengine kama mabenki yaliyowakopa kuagizia mafuta. Hauwezi ukawalazimisha wayauze, lakini unaweza ukaweka mazingira yatayowafanya wasione faida ya kuyauza kama walivyofanya EWURA na hili agizo lao la 2,004/=.

lakini tambua kitendo cha wenye mafuta kukataa kushusha bei si cha kizalendo kwani wakati serikali haijashusha kodi wao walikuwa wanauza sh 2090 lakini serikali wameshusha kodi na tozo kwa zaidi ya sh 150 sasa kwanini wao wasishuke japo kidogo ili tuone kuwa nao ni wazalendo badala ya kusimama kwenye vyombo vya habari na kuipa serikali masaa 24

hii si sahihi na kama tuna rais basi na tuone nguvu zake sasa na ata ikibidi kujiingiza kwenye biashara ya mafuta na sasa iingie
 
Yesu Wangu!

Hii ibaki kuwa rumour kwa sababu itakuwa ni kosa kubwa sana mbele ya dunia.

Chonde, chonde, chonde! Kama serikali inataka kuingilia kati, basi iwe ni
kuiamuru EWURA iondoe agizo la bei hii ya 2,004/=. Warudishe ile bei ya 2,090/=, ambayo ndiyo bei itayowawezesha hawa wa mafuta kupata faida waliotarajia.

Kisheria, haya mafuta ni ya hao wafanya biashara pamoja na principals wengine kama mabenki yaliyowakopa kuagizia mafuta. Hauwezi ukawalazimisha wayauze, lakini unaweza ukaweka mazingira yatayowafanya wasione faida ya kuyauza kama walivyofanya EWURA na hili agizo lao la 2,004/=.

Sema kwa vile serikali yenyewe ni legelege lakini serikali makini haiwezi kurudia matapishi yake maana ni kujinyonga yenyewe, haitakaa isikilizwe tena na hawa wafanyabiashara.
Viko wapi vyombo vya dola, usalama wa Taifa uko mashakani ili hali taasisi tuloijua miaka ile imelala.

Leo wamegoma kuwauzia wananchi mafuta vipi kesho tukiwa vitani wakagoma ku-supply mafuta itakuwaje??
 
Sema kwa vile serikali yenyewe ni legelege lakini serikali makini haiwezi kurudia matapishi yake maana ni kujinyonga yenyewe, haitakaa isikilizwe tena na hawa wafanyabiashara.
Viko wapi vyombo vya dola, usalama wa Taifa uko mashakani ili hali taasisi tuloijua miaka ile imelala.

Leo wamegoma kuwauzia wananchi mafuta vipi kesho tukiwa vitani wakagoma ku-supply mafuta itakuwaje??


Tofautisha kati ya serikali per se na EWURA.

Serikali (Wizara) inaweza kabisa ikaiagiza EWURA, ambayo ni Executive Arm yake, kubadilisha determination yake bila ya kuonekana kuwa imekula matapishi yake.
 
lakini tambua kitendo cha wenye mafuta kukataa kushusha bei si cha kizalendo kwani wakati serikali haijashusha kodi wao walikuwa wanauza sh 2090 lakini serikali wameshusha kodi na tozo kwa zaidi ya sh 150 sasa kwanini wao wasishuke japo kidogo ili tuone kuwa nao ni wazalendo badala ya kusimama kwenye vyombo vya habari na kuipa serikali masaa 24

hii si sahihi na kama tuna rais basi na tuone nguvu zake sasa na ata ikibidi kujiingiza kwenye biashara ya mafuta na sasa iingie


Kwani tangu watangaze kuondoa 150, na leo, zimepita siku ngapi? Jee Shilingi imeanguka kwa kiasi gani katika kipindi hicho?

Je, unafikiri kuwa hawa wa mafuta wanapata faida gani kugomea kuuza mafuta kwa wiki nzima? Au ni ule mtazamo wa kuwa bepari yoyote ni mbaya, anapenda kutesa watu, anakula watoto kwa breakfast na anayonya watu damu?
 
<b>tetesi: rais kikwete amewapa maagizo wanajeshi kuingilia shell binafsi kuzikagua na kuwalazimisha na ikibidi MPs wa jeshi wauze kwa nguvu <br />
<br />
note:bado sijaweza kuzithibitisha habari hizi<br />
<br />
<br />
<br />
</b>
<br />
<br />


Hii itakuwa ni temporary tu maana mafuta yakiisha kwenye pump basi tena maana huwezi kuwalazimisha kuagiza mafuta! Kwa pesa yao.
 
Hao wadosi/waarabu wana jeuri sana ya kuitunishia msuli serilkali,kwani hakuna sheria ya kutaifisha hayo mafuta?
 
Kwani tangu watangaze kuondoa 150, na leo, zimepita siku ngapi? Jee Shilingi imeanguka kwa kiasi gani katika kipindi hicho?

Je, unafikiri kuwa hawa wa mafuta wanapata faida gani kugomea kuuza mafuta kwa wiki nzima? Au ni ule mtazamo wa kuwa bepari yoyote ni mbaya, anapenda kutesa watu, anakula watoto kwa breakfast na anayonya

watu damu?

ni mwezi sasa na shillingi imedondoka kwa unit 40
 
Huenda ni vema tukajiuliza ni nani wamiliki wa kampuni za mafuta na mahusiano yao na watawala!
- je hakuna collusion ktk upangaji wa bei?
- je serikali inadhibiti vipi uwepo wa collusion?
- je serikali inatoa maelezo gani kuhusu upungufu wa mafuta baada ya kutoa bei elekezi?
Ikumbukwe kwamba soko huria haimanishi soko holela . Hapa wachumi watuambie ni nchi gani ambayo imeacha 100% market forces to determine prices or where perfect competition exist .
Mimi bado naamini serikali inayo nafasi kubwa in regulating fuel prices. Kuwachia wafanyabiashara
wapange bei wanavyotaka ni hatari kwa uchumi na usalama wetu. Wengi tumeona jinsi watu hawa walivyo collude kuficha mafuta.
Mafuta shida umeme taabu dalili za kuendelea kwa kurudi nyuma. Hakika uchumi wetu haushuki ila unaporomoka.
 
Tofautisha kati ya serikali per se na EWURA.

Serikali (Wizara) inaweza kabisa ikaiagiza EWURA, ambayo ni Executive Arm yake, kubadilisha determination yake bila ya kuonekana kuwa imekula matapishi yake.

Kiongozi unakuwa kama si mwenye kufuatilia mambo.

Katibu mkuu wa wizara alifanya kikao na hao wafanyabiashara na akasisitiza msimamo wa serikali, sasa sijui unataka serikali ipi hapo.
 
Tuwalaumu wale waliohusika kuanzisha biashara huria ikiwemo hii ya nishati ya mafuta.
Tuwalaumu wale waliohusika kuuwa Tipper.
Tuwalaumu.
 
Kiongozi unakuwa kama si mwenye kufuatilia mambo.

Katibu mkuu wa wizara alifanya kikao na hao wafanyabiashara na akasisitiza msimamo wa serikali, sasa sijui unataka serikali ipi hapo.


Basi Katibu Mkuu alifanya kosa. Asingetakiwa kujichanganya kwenye maamuzi yaliyotolewa na EWURA kwani hapo anaondoa uwezo wa Wizara kuimoderate EWURA. Sheria za EWURA, TRA, SUMATRA etc, zinaainisha kuwa "Waziri anayehusika" kama taasisi nyingine na hizi Executive Organs ili kumpa Waziri uwezo wa kuzi-overide hivi vyomba pale ambako matashi ya kisiasa au mengine yanapokuja mbele.
 
kanuni ya demand na supply inafanya kazi kwenye free market lakini kilichotokea katika soko la mafuta ni wafanyabiashara wameunda catel yani ushirika wa kudhibiti bei na sheria za tume ya ushindani inaipa nguvu serikali kuingilia inapoamini kuna nanma yeyote ya umoja wa wafanyabiashara kudhibiti bei

katika suala la upungufu wa mafuta linatokana na sababu mbili kubwa sasa.

1. kiburi cha wafanyabiashara dhidi ya serikali kwani wanaamini kuwa serikali lazima isalimu amri na haina nguvu na uwezo wa kuwadhibiti

2.kutokana na kushuka kwa bei watumiaji wengi hawaamini kuwa bei itaendelea kubaki chini na wanadhani kuwa ni wakati mfupi tu itabaki kwenye bei hii na ndio maana wamenunua na kuweka stock yao kwa siku za karibuni kwa niliweza kuzungumza na mkandarasi wa barabara anayetarajia kufanya kazi zake muda wa karibuni yeye ameweza kununua zaidi ya lita 700,000 za diesel na kuziweka akiba kwa ajili ya mitambo yake ili pia linaongeza upungufu wa mafuta

imefika wakati ambao serikali haiwezi kukwepa kuunda mfumo wa upatikanaji wa mafuta wa uhakika kwani katika nchi ambayo umeme ni shida na mafuta nayo yakiwa shida basi lazima ife

serikali lazima ifikirie kufufua kiwanda cha kusafisha mafuta cha tipper ili kupunguza bei za mafuta na kuongeza ajira kwa vijana wetu la sivyo haitaweza kusalimika kutoka katika janga la mfumuko wa bei na usalama wake yenyewe











Ni kweli mkuu,kwenye biashara huria ni kosa kwa wafanyabiashara kupanga bei kwa pamoja, ukishafanya hivyo lazima vyombo vya udhibiti viweze kuingilia kati kwani mlaji ataumizwa. tatizo ni timing ya kuchukua hatua, hawa wafanyabiashara hili wamelifanya mara nyingi mno lakini vyombo husika vilikuwa usingizini-wanakuja kushtuka wakati watu wamejijengea nguvu kubwa ambazo zinahitajika pia nguvu kubwa ili kuwadhibiti, na kwa serekali yetu hii tuliyonayo sidhani kama wana uwezo huo, ni sisi walaji tutakaoendelea kuumia
 
Back
Top Bottom