SHIEKA
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,244
- 4,258
Habari zenu wana MMU.Mtakubaliana nami kwamba mwana mmu mwenzetu, Mtambuzi, amekuwa mstari wa mbele katika kutusimulia visa,na kesi za kimataifa zilizokamata hisia za wengi kwa wakat huo zilipotokea na mpaka sasa bado zinasisimua. Binafsi sitasahau ile kesi ya mzungu mmoja wa Afrika ya Kusini aliyepanga njama ya kumtupa mfanyakazi wake kwenye zizi la simba.Pamoja na visa vingine kadhaa. Asante sana Mtambuzi kwa kujitolea kutupakulia stori hizo. Sasa leo nakuja na ombi maalum kwako Mtambuzi. Huko Australia kuna mama mmoja(Mrs Chamberlain) alikuwa anashutumiwa kwamba alimwua mwanawe mchanga (Azaria)aliyekuwa na umri wa miezi nane. Lakini baada ya muda mrefu iligundulika kwamba huyo mtoto hakuuwawa na ***** bali alichukuliwa na mbwa mwitu wa Australia wajulikanao kwa jina la Dingo Mtambuzi, ninakuomba utupakulie kisa hiki cha mtoto Azaria.Natanguliza shukrani zangu za dhati.
Last edited by a moderator: