Ndugu Wana_Forum,
Leo kwa mara ya mwanzo niliona ile picha ya wanafunzi wa Mbagala wakisoma shule nje kwenye mchanga bila ya madeski na machozi yalinioka - yalinitoka machozi nikukumba 540,000 Sterling Pounds alizokutwa nazo Chenge na mabilioni ambayo akina Rostam wanazo. Baada ya kuiona hii picha nikaona bora nitoke kwenye hii Forum, kwani kila siku naona habari ninazozipata zinanitia uchungu kiasi ambacho afya yangu inaathirika, kutokana na pressure yangu bure bure kupanda. Kwahivyo, nimeamua bora kutoka kwenye hii Forum kabla sijapata heart attack kutokana na stress ninyoipata kutokana na news ninazozisoma hapa kwenye hii Forum. Sitaki tena kusoma habari zozote zile za hii nchi yangu kwani kila mara ninaposoma naona maisha yangu yanakuwa hatarini.
Kila la kheri / Ngida1
Pole Ngida1...
Na Hizi je??
maisha bora kwa kila mtanzania