kwaherini malenga JF

Barubaru

JF-Expert Member
Apr 6, 2009
7,161
2,323
Buriani Barubaru.

1. Anayeifanya njia, usipate angamizi.
Anayekupa bamia, njaa inapokujia,
Ndio wa kumwaminia, kwa asilimia mia,
Buriani barubaru, Kwa herini JF.

2 Hewa bila kubabia,Wavuta na yabakia,
Tena bila kupapia, Taratibu yaingia,
Ni bure uja lipia, wala si bili sikia,
Buriani barubaru, Kwa herini JF.

3 Unaye mwomba mia, maelfu akwachia,
Dola na hata rupia,Riyali kwa kuwania,
Ndie pekee jalia, wengi ninawaambia
Buriani barubaru, Kwa herini JF.

4 Uwapo na malaria, Pengine ni almonia,
kwikwi vidonda kuvia, yeye ukimlilia,
Huukomesha udhia, Mola akakushindia,
Buriani barubaru, Kwa herini JF.

5 Kesi za kusingiziwa, walizonibambikia,
Wakanitia hatia, kusema kwa jumuiya,
Hufai kwa umma huu, siku mbili mahuria.
Buriani barubaru, Kwa herini JF.

6 Nawapongeza kwa dhati, wote mliopigania,
Mwanakijiji,Choveti, Maranya na fauzia,
Ritz bado sijaketi, Rejeo zomba na Paw,
Buriani barubaru, Kwa herini JF.

.

7 Wote Ninawashukuru , wanachama JF,
Nisije fanya kufuru,Mods kuwaongezea.
Mke wangu l'afuru, na watoto wangu pia
Buriani barubaru, Kwa herini JF.


8. Tamati ndio akhifu, jina langu maarufu.
Hamza wa Yousuf, Naamaniy ni sharafu,
Mkurugenzi sarafu, Qatar kwenye mafuta.
Buriani barubaru, Kwa herini JF.


Dr Hamza Yousuf Al Naamaniy (Barubaru)
Director of Finance & Admin
Qatar petrolium.
+974 4457 4888.
Doha. Qatar

mapumzikoni ,
Hesawa, mwanza.
Local number 255 684 221 077 mpaka 24 feb 12

 
kwann waondoka..bila sababu kutupatia
wengi tulipenda michango,uliyochangia
hakika siwezi kukuzuia,kwaheri nakutakia
 
Dr Hamza Yousuf Al Naamaniy (Barubaru)
Director of Finance & Admin
Qatar petrolium.
+974 4457 4888.
Doha. Qatar

mkuu,.............. subiri kidogo usilog off, ....................naku PM now!....................
 
Buriani Barubaru.

1. Anayeifanya njia, usipate angamizi.
Anayekupa bamia, njaa inapokujia,
Ndio wa kumwaminia, kwa asilimia mia,
Buriani barubaru, Kwa herini JF.

2 Hewa bila kubabia,Wavuta na yabakia,
Tena bila kupapia, Taratibu yaingia,
Ni bure uja lipia, wala si bili sikia,
Buriani barubaru, Kwa herini JF.

3 Unaye mwomba mia, maelfu akwachia,
Dola na hata rupia,Riyali kwa kuwania,
Ndie pekee jalia, wengi ninawaambia
Buriani barubaru, Kwa herini JF.

4 Uwapo na malaria, Pengine ni almonia,
kwikwi vidonda kuvia, yeye ukimlilia,
Huukomesha udhia, Mola akakushindia,
Buriani barubaru, Kwa herini JF.

5 Kesi za kusingiziwa, walizonibambikia,
Wakanitia hatia, kusema kwa jumuiya,
Hufai kwa umma huu, siku mbili mahuria.
Buriani barubaru, Kwa herini JF.

6 Nawapongeza kwa dhati, wote mliopigania,
Mwanakijiji,Choveti, Maranya na fauzia,
Ritz bado sijaketi, Rejeo zomba na Paw,
Buriani barubaru, Kwa herini JF.

.

7 Wote Ninawashukuru , wanachama JF,
Nisije fanya kufuru,Mods kuwaongezea.
Mke wangu l'afuru, na watoto wangu pia
Buriani barubaru, Kwa herini JF.


8. Tamati ndio akhifu, jina langu maarufu.
Hamza wa Yousuf, Naamaniy ni sharafu,
Mkurugenzi sarafu, Qatar kwenye mafuta.
Buriani barubaru, Kwa herini JF.


Dr Hamza Yousuf Al Naamaniy (Barubaru)
Director of Finance & Admin
Qatar petrolium.
+974 4457 4888.
Doha. Qatar

mapumzikoni ,
Hesawa, mwanza.
Local number 255 684 221 077 mpaka 24 feb 12



FANYA URUDI KUNDINI

Beti nina zianzia, kwa jina lake manani
Mola wa hii dunia, na vyote vilivyo ndani
Kaumba na Mbingu pia, hana yeye mshindani
NI WAPI WAKIMBILIA, FANYA URUDI KUNDINI

Dunia ni mitihani, Mola ametwambia
kila siku tuvitani, si vyema ukakimbia
Hebu rudi humu ndani, uanze na kuchangia
NI WAPI WAKIMBILIA, FANYA URUDI KUNDINI

Ni lipi limekughasi, mpaka waondokea
Au umepigwa tusi, na kesi walokugea?
Tueleze wacha wasi, kwa nini watokomea
NI WAPI WAKIMBILIA, FANYA URUDI KUNDINI

Kwa jamvi kuliachia, siafiki ninakana
Hakuna kunyamazia, bora hata kupigana
Yu wapi na fauzia, mngefanya kuungana
NI WAPI WAKIMBILIA, FANYA URUDI KUNDINI

Sindano Mwana wa Ganzi(SMG)
Kijijini Tongoleani
 
Baada ya kufikiri
na nena umekiri
wapajua Ikwiriri
seuse kirikiri
ukweli si mshari
kutuacha twakariri
Baada ya kufikiri
na nena umekiri

Barubaru Mzanzibari
kwao atakabari
si shari kukukariri
kujifanya mshairi
umepanda manuwari
kuja kwetu kuhariri
Baada ya kufikiri
na nena umekiri

Nimenuna nafikiri
ni nini kilojiri
wala sio mhariri
ukweli wausitiri
nakuomba we jabari
uwache kutakabari
Baada ya kufikiri
na nena umekiri

Usende kwa kiburi
baki ulete habari
si wengi walo jiri
kufikia kuwa wari
wao hawasitiri
huanza kwa ushari
Baada ya kufikiri
na nena umekiri

Usiwape tafakari
yao ni masaburi
ukienda kwa hiari
wataacha kufikiri
wala hilo sio siri
wao wana jiajiri
Baada ya kufikiri
na nena umekiri

Max amekiri
kuwa yeye si mshari
amerudi safari
akakuta wavinjari
wamejitia kabari
FaizaFoxy kumtairi
Baada ya kufikiri
na nena umekiri

MS kwa kabari
Ritz kwa mahubiri
Mike kasitiri
Kwa kujifanya mshari
tusianze kuhubiri
kujitia uhodari
Baada ya kufikiri
na nena umekiri

Barubaru sio siri
wewe ni jabari
ulishinda kule Suri
na pia kule Qatari
Barubaru tafakari
watuachia hatari
Baada ya kufikiri
na nena umekiri


Mimi sio nguri
ujabari si u kiri
nakuomba tafakari
watuacha kwenye shari
baki utusitiri
kwa usomi ulojiri
Baada ya kufikiri
na nena umekiri

Kidogo walo kariri
uyajuayo dhahiri
waachia kisirisiri
tujuao twakariri
wewe umahiri
kwako ni bahari
Baada ya kufikiri
na nena umekiri

Hawajibu zao shari
hawana lilojiri
ukweli ukidhihiri
uongo huwa shari
nakuomba jabari
baki ukifikiri
Baada ya kufikiri
na nena umekiri
 
....................

Max amekiri
kuwa yeye si mshari
amerudi safari
akakuta wavinjari
wamejitia kabari
FaizaFoxy kumtairi
Baada ya kufikiri
na nena umekiri

.....................

duh!!...................... ngoja na mimi nkajipange, ................narudi na vina timamu soon ...................
 
Usiondoke jamvini


Vuta subira wakwetu, ujumbe nimesikia
Nakataa katu katu, jamvini kuondokea
Usikimbie msitu, ni wapi wakimbilia?
Usiondoke jamvini, ni wengi twakuambia

Muungwana ni vitendo, na vyako vimeoneka
Nasema siende kando, jamvini tunakutaka
Tunautaka uhondo, wa kwako uso kauka
Usiondoke Jamvini, ni wengi twakuambia

Barubaru wenda wapi, nasema tutapooza
Turudie mara ngapi, ujuwe unaongoza?
Hoja zako si makapi, kwa mema zinaongoza
Usiondoke Jamvini, ni wengi twakuambia!

Mitihani ndiyo hiyo, nasema nawe ujuwe
Na tena yataka moyo, kwa hao wenye viwewe
Twajuwa siyo mchoyo, na tena huli mwenyewe
Usiondoke Jamvini, ni wengi twakuambia

Kaditama wa tamati, siende kaka siende
Utujulishe umati, tusherehe tule tende
Halua navyo visheti, tuvitafune vipande
Usiondoke Jamvini, ni wengi twakuambia
 
Back
Top Bottom