Mizizi
JF-Expert Member
- Mar 8, 2008
- 1,275
- 391
Katika hali isiyofurahisha, baada ya malalamiko kadhaa juu ya kuwepo kwa kupeana madaraka mbalimbali katika ofisi za umma kwa kujuana na kwa kujali uswahiba katika serikali ya JK, baada ya mambo kudorora, kilio hicho kilionekana kusikika na ule mtandao kuonekana kusambaratika, Mtoto wa mheshmiwa huyo RJK amethibitika kuanzisha mtandao mpya ndani ya jumuiya ya vijana ya CCM (uvccm). Habari zilizokuwa za wazi kabisa, Ridhwan amefanikiwa kushawishi na kufanikisha kupanga safu za watendaji, ambao ni makatibu wa uvccm wa mikoa na wilaya kote nchini. Habari zaidi zinaeleza kuwa, lengo kuu la kufanya hayo ni kumuandalia rafiki yake beno malisa kuchukua nafasi ya uenyekiti wa jumuiya hiyo kitaifa. shutuma zaidi kutoka kwa baadhi ya wanajuiya na viongozi wa chini wanasema kwamba, Ridhwan na Benno walifanikisha kutoa mkopo wa zaidi ya shilingi millioni mbili kwa kila katibu wa mkoa wa jumuiya hiyo ili kupata uungwaji mkono zaidi. lakini baada ya chama hicho kupeleka nafasi ya uenyekiti kupelekwa zanzibar, kasi hiyo ya mtandao ilipungua nguvu.
Zaidi inasemekana kwamba, Ridhwan alishiriki katika kujenga mtandao huo ambao unaonyesha haukuwa na nia ya kujenga jumuiya hiyo. kwani makatibu wengi waliopewa nafasi hizo hawana sifa wala ari ya kiutendaji na hivyo kutoleta mabadiliko yoyote katika jumuiya na chama cha mapinduzi.
Inasemekana na yeye ridhwan ni mgombea katika jumiya hiyo.
Zaidi inasemekana kwamba, Ridhwan alishiriki katika kujenga mtandao huo ambao unaonyesha haukuwa na nia ya kujenga jumuiya hiyo. kwani makatibu wengi waliopewa nafasi hizo hawana sifa wala ari ya kiutendaji na hivyo kutoleta mabadiliko yoyote katika jumuiya na chama cha mapinduzi.
Inasemekana na yeye ridhwan ni mgombea katika jumiya hiyo.