Black Jesus
JF-Expert Member
- Mar 7, 2008
- 256
- 9
Naomba kama kuna mtu yeyote yule amabe anayo au anaweza kunambia wapi naweza kuipata ile hutuba ya Dr mwaykembe aliyohutubia na kuwambia viongozi wa ZANZIBAR kuwa hawana ADABU.
Naomba kama kuna mtu yeyote yule ambae anayo au anaweza kunambia wapi naweza kuipata ile hutuba ya Dr mwaykembe aliyohutubia na kuwambia viongozi wa ZANZIBAR kuwa hawana ADABU.
`` Mheshimiwa Spika, mimi sisemi Wakili wa Serikali alipwe kama Wakili wa Kujitegemea, hapana. Ninachosema ni kwamba, tumeshindwa kuwapa vijana wetu mahitaji ya msingi kabisa kuweza kutekeleza kazi zao. Wakili wa Serikali ambaye tunambebesha mafaili ya kesi za ujambazi, kesi za ufisadi, kesi za aina mbali mbali, hatujui analala wapi. Tunachojua tu sisi ni kumpa Sh. 70,000/= kwa mwezi akatafute chumba. Siku hizi tumeongezea eti 100,000/=. Hata kwa Dodoma hapa, hupati nyumba kwa 100,000/= na Dar es Salaam ndio shida. Kwa hiyo, vijana wetu wametawanyika hovyo kwa Mfuga Mbwa, sijui Gongolamboto Dar es Salaam na kadhalika. Tunawaweka kwenye vishawishi vikubwa mno!
....Mheshimiwa Spika, Kadhi Mkuu kwa mfano, inapendekezwa sehemu nyingi na hata hapa itapendekezwa kwamba [Kadhi Mkuu] ateuliwe na Rais. Kwa hiyo, lazima Serikali ianze kuangalia. Je, what if Rais anakuwa Mkristo, nani atakubali kwa mfano Kadhi Mkuu ateuliwe na Kafir?
wewe nae kalale sasa.......Harrison Mwakyembe ana dharau ya ajabu kwa watu wa chini. Eti wanasheria wa serikali wasiishi Manzese kwa Mfuga Mbwa na Gongolamboto, kuna vishawishi. Anaona wote wa huko ni waovu wachafu. So uppity uppity.
Halafu anadai, I am not making this up, Mwakyembe anadai Rais akiwa Mkristo waislam wote humwona Kafiri: