Kwa watu wa mkoa wa Mara

Mura, Obambiri mahene mura. Tugegehiri. Bonse tuberi kya barisya!

Mkoa una mkuu wa JKT ambaye ni mzanaki, una Katibu wa Chama Cha Magamba, una Mwanasheria Mkuu (Werema) na Naibu Mwanasheria Mkuu (Masaju); hawa wote hakuna kitu! Una majenertali Kiaro, Waitara, na Musuguri; lakini mambo mabaya kabisa. Wengine ongezeni jamani!

Bila kumsahau Lieutenant General Mwana Mtoka Pabaya wa Wilaya ya Serengeti, Tarafa ya Ngoreme, Kata ya Kisaka, Kijiji cha Nyibhoko.

Ujasiri wetu uliishia katika kuwasaidia WAHAYA wasiendelee kuolewa na Iddi Amini Dadaa
 
Kwanini unasema umekaa kikabila?,tusaidiane ili turekebishe,Mara ni yetu yego.

Mkuu kitu cha kwanza ambacho naweza kushauri ni kuwa watu kutoka mkoa huo wapungue kwenye idara ambazo utendaji wake unategemea watu mechanic, yaani idara ambazo in nature ni brutal. Kama vile polisi, jeshi and alike. Kidogo hizi idara zinaleta sifa mbaya kwa mkoa na watu wake...jaribu kuangalia watu wa mkoa wenu katika vyombo vya usalama unaweza kusikitika. Sijui labda nyie wenyewe mnapenda.
 
ccm ni sehemu tu ya matatizo mengi yanayochangia kurudisha nyuma maendeleo ya wilaya yetu ya Serengeti.
SAGANKA nakushukuru kwa kuleta hoja hii, najaribu kukusoma jinsi ulivyokereka kutokana na lugha uliyotumia lakini ujumbe wako umefika, na ndugu yangu Mwitongo nimekusoma hoja zako ni za kweli kabisa.

Mimi nimezaliwa na kukulia Kijiji cha Kibeyo, kata ya Kisangura wilayani Serengeti, kwahiyo ninaifahamu vizuri sana wilaya yetu ambayo nimefanikiwa kufika/kuitembelea karibu kona zote; kuanzia Machochwe, Mbirikili, Bonchugu, Rwamchanga, Miseke,Robanda, Bwitengi, Natta, Issenye, Ring'wani, Masinki, Kisaka, Kenyamonta, Majimoto, Iramba, Mara Somoche, Kebanchebanche, Merenga, Nyansurura, Mbalibali na kwingineko kwa kutaja vijiji vichache.

Cha kwanza kabisa kilichoturudisha nyuma, kwa upande wetu wilaya ya Serengeti ni mapigano ya koo. Kulikuwa na mapigano baina ya wangoreme na wanyabasi + watimbaru tangu miaka ya sabini huko ambayo yaliua watu wengti sana, hadi miaka ya hivi karibuni mapigano yamepungua sana lakini chuki na uhasama baodo upo. Tumeshuhudia mapigano mabaya sana miaka ya 80s baina ya wanyabasi + watimbaru dhidi ya wakira + walenchoka, tumeshuhudia mapigano baina ya wanyabasi + watimbaru dhidi ya waikoma + wanata + waisenye. Kama hiyo haitoshi, kulikuwa na uhasama mkubwa sana baina ya wakurya na wamaasai toka mkoa wa Arusha ambao walikuwa wakiiba ng'ombe kwa wingi sana toka wilayani kwetu hadi mwishoni mwa miaka ya tisini ndipo hali hiyo imekaoma kabisa baada ya kufanyika jitihada kubwa na mazungumzo baina ya wamaasai na wakurya.

Kama nilivyodokeza hapo awali sasahivi mapigano baina ya koo hizi yamepungua sana kama si kuisha lakini bado kuna chuki miongoni mwao na watu hawa hawaaminiani sana. Kipindi chote cha mapigano kwa ujumla koo zote zilishindwa kuweka mazingira mazuri ya elimu na afya. Hawakuweza kuwekeza vya kutosha katika elimu, hawakusomesha watoto wao bali walijikita katika kuwafundisha ujasiri wa kupambana na kulinda koo zao. Na ikumbukwe kwamba katika mapigano yote yaliyokuwa yakitokea baina ya koo kama nilivyotaja hapo awali, wizi wa mifugo hasa ngo'mbe, mbuzi na kondoo walikuwa wakiibiwa/kutaifishwa kwa wingi sana toka upande ulioshindwa vita, na kwakuwa koo zote za wilayani serengeti kwa sehemu kubwa ni wafugaji kwahiyo wakajikuta wakiishia kuwa fukara.

Jambo jengine ambalo lilisababisha kuendelea kuwepo kwa mapigano baina ya koo zetu ni viongozi wa kisiasa na vyombo vya dola, ambao walinufaika sana na hizi vurugu kwakuwa walitumia mwanya huo kupora mifugo ya wananchi kwa kisingizio cha kukabiliana na wizi na hatimaye kujigawia wao wenyewe. Viongozi wakubwa walionufaika sana na uporaji huo walikuwa ni wakuu wa wilaya-hapa namkumbuka marehemu Makunenge na mwingine mmoja akiitwa Zuberi ama Omary aliyefariki ghafla akiwa amelala, makamanda wa polisi wilaya(OCDs), wenyeviti wa baraza la madiwani-hapa namkumbuka mwenyekiti mmoja wa baraza la madiwani mwishoni mwa miaka ya 80 hadi mwanzoni mwa miaka ya 90 aliyekuwa akitokea ngoreme akiitwa Luge(nadhani alikuwa mwanajeshi mstaafu) alifaidika sana na ng'ombe wa koo za kikurya (wanyabasi, watimbaru na wakira).

Kwahiyo hiyo utaona ni kwa kiasi gani wananchi walikosa kabisa muda wa kufanya kazi za kujiletea maendeleo. Katika hali kama hiyo hata walewachache waliokuwa wamefanikiwa kusoma na kutaka kuwekeza nyumbani walishindwa kwakuwa hali ya usalama ilikuwa ni ndogo sana. Nakumbuka majengo mengi sana yaliyokuwa yameanza kujengwa mjini mugumu miaka ile ya themanini yote yaliishia kuporomoka kufuatia vita mbaya sana baina ya wanyabasi + watimbaru dhidi ya wakira + walenchoka, hii ilitokana na ukweli kwamba watu wengi waliokuwa na uwezo na kuanza kufanya ujenzi mjini mugumu walikuwa ni wanyabasi na wakira, sasa katika mazingira yale ya vita hakuna mtu aliyekuwa na uwezo wa kufanya ujenzi.

Ni miaka ya tisini ndipo sasa mji wa mugumu ulianza kujengwa kwa kasi sana baada ya kumalizika kwa uhasama mkubwa baina ya koo hizi na watu kujielekeza katika shughuli za maendeleo. Ndipo watu wakapata mwamko wa kuanza kuwekeza katika elimu, shule ya sekondari ya Serengeti ambayo wananchi wote wa wilaya walikuwa wameichangia tangu miaka ya sabini ndipo ikapata kufunguliwa na kuanza kupokea wanafunzi. Ikumbukwe kwamba kabla ya hapo wilaya yetu ilikuwa na shule moja tu ya sekondari ambayo ni ngoreme secondary.

Jambo jingine lililopelekea wilaya yetu kuwa nyuma sana kimaendeleo ni jamaa zetu waliofanikiwa kimaisha hasa waliosoma kwakuwa miaka ile wasomi ndio walikuwa na uwezo mzuri wa kufanya uwekezaji, wakaamua kususia nyumbani kwao, wakaamua kuwekeza huko wanakofanya kazi na kusahau kwamba nyumbani nako kunawahitaji. Na kwakuwa hawakuwekeza nyumbani kwao japo kujenga nyumba nzuri tu za kuishi, hata wanapostafu utumishi wao wanalazimika kuendelea kuishi huko huko mijini walikojenga majumba mazuri na kufanya uwekezaji kadhaa. Labda sasahivi ndio watu wanajitahidi kukumbuka kwao, nimeona wasomi wa siku hizi japo si wengi wanapofanikiwa wanakumbuka kurudi nyumbani na kujenga ingawa si kwakiwango kikubwa, na hivyo inabidi tuendelee kuhamasishana ili kila mmoja aone wajibu wake wa kukumbuka kwao.

Kwa sasa niishie hapa, nikipata muda nitachangia sababu nyingine nyingi zilizosababisha kurudi au kuwa nyuma kimaendeleo kwa wilaya yetu ya Serengeti.
Nakushukuru kwa ufafanuzi mzuri,mimi ni mongoreme kama nilivyjitambulisha,kama utakumbuka vema kuna bwana mmoja aliwahi kuwa mbuge wa serenget miaka 90,bwana Maro George(Mwita) ni mongoreme,hakuwa mtu mwema,aliposhindwa kwenye uchaguzi wa mwaka 2000,aliungana kwa siri na mgombea wa CUF bwana John Mosena Nyambabe kumpigia kampeni huku akipiga nyimbo za kuchochea chuki kati ya wangoreme na wairege.Hii akiri ya kufikiria madaraka bila kujali mustakabali wa wilaya na mkoa ni hatari sana na watu kama hawa hatutakiwi kuwaunga mkono hata kidogo.Kama sasa Wahutu na Watutsi wameungana na wanafanya mambo ya maendeleo,sisi tunaweza sana.Kuhusu Luge ni kweli kabisa ulichokisema,hata wangoreme hawamwamini,alinufaika sana na vurugu.Watu wa namna hii hatuwahitaji kabisa.Nilishafika Mbalibali mara nyingi na nina marafiki huko.
 
Mimi nafikiri mtoa mada ana lengo zuri sana na kwa kweli ameeleweka. Kimsingi ni kuanza mikakati ya jinsi ya kuanzisha huu umoja.
Mimi niko Rorya - Mara na niko tayari kuunga mkono juhudi zote za kujenga na kuimarisha umoja huu.
Cha msingi ni kuachana na lawama na tuanze mshikamano kuanzia hapa tulipo kwa lengo la kusonga mbele na si vinginevyo! Ahsanteni sana, tuko pamoja!
 
Salute,
Big up kwa muanzisha mada na wachangiaji wote.
Enye Mzanaki, yika ni Busegwe mission harya wa Kohi, mzukuru WA Mtarima.

Katika msfara WA Mamba na Kenge wamo. Nasema hivyo maana tayari tumekubali weakness zetu ziendelee kutumaliza wenyewe kama wachangiaji walipita tena cha ajabu Wana iponda idea na kujitambulisha wao ni WA Mara pia...jamani are these guys seriouse? Yaan inamaana mpaka sasa hawaoni umuhimu WA kufanya mabadiliko?

Mi Sita taja majina wala kuwanyooshea vidole wale wote wazazi wetu waliotoka mkoa WA mara na kushindwa kukumbuka kwao na ndo hasa tatizo kubwa of which sisi sasa ambao tumeliona (si ajabu wao hawakuliona hahaha) inabidi tufanye hima na kuleta mabadiliko...inawezekana kabisa!! Tuweke UJINGA wetu pembeni ili iwezekane.

Saganka? We nambie whatz next ili tulianzishe, nakuunga Mkono na tuko pamoja japo nimeona umeisha aanzisha katiba na uko mbioni kuisajiri. Can u share pls?

Uzuri mwingine ni kwamba sasa Wana JF tuta anza kufahamiana uso kwa uso hahaha na nadhani hili halikwepeki iwapo tutataka kuleta mabadiliko ya kweli kwa mkoa wetu.

Hatujachelewa!!!


founder and CEO of www.oric.co.tz and www.aio.co.tz skype: alfred.kohi, 0784800989, 0715800989/0715800989
 
Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mzee Isdori Shirima aliwahi kuitisha mkutano wa uwekezaji kwenye mkoa ule. Alipohamishwa kila kitu kikapotea. Kwa maoni yangu hata hii TANAPA ilipaswa kujenga makao makuu yake pale Mugumu badala ya Arusha. Mara ina kila kitu lakini watu wake, mh! Wanaoneana wivu, wanabaguana, wanadharauliana, ubinafsi ndio wao.

Jambo moja linalonikera sana ambalo bado nalitafutia njia muafaka ya kuli address ni kitendo cha TANAPA kuweka makao makuu ya mbuga ya serengeti (SERENGETI NATIONAL PARK-SENAPA) mkoani Arusha. Hii ni dharau kubwa sana kwa wanaSerengeti lakini ajabu ni kwamba hakuna kiongozi yeyote anayeliona hili na kulipigia kelele.

Ndugu zangu wana Mara pamoja na mambo mengine, ni lazima tuishinikize serikali itupe haki yetu ya makao makuu ya mbuga ya serengeti kuwepo mkoani kwetu, wilayani kwetu mjini Mugumu.

Nimebahatika kufikka katika baadhi ya hifadhi/mbuga zetu zilizopo hapa nchini kama Mikumi, Manyara, Ngorongoro, Udzungwa, Ruaha, Kitulo, Saadani, Mkomazi, Tarangire huko kote makao makuu ya watendaji/ofisi za mbuga/hifadhi hizo ziko katika mbuga/hifadhi husika, kwanini sisi ya kwetu Serengeti iwekwe Arusha? kwa maslahi ya nani?
 
Salute,
Big up kwa muanzisha mada na wachangiaji wote.
Enye Mzanaki, yika ni Busegwe mission harya wa Kohi, mzukuru WA Mtarima.

Katika msfara WA Mamba na Kenge wamo. Nasema hivyo maana tayari tumekubali weakness zetu ziendelee kutumaliza wenyewe kama wachangiaji walipita tena cha ajabu Wana iponda idea na kujitambulisha wao ni WA Mara pia...jamani are these guys seriouse? Yaan inamaana mpaka sasa hawaoni umuhimu WA kufanya mabadiliko?

Mi Sita taja majina wala kuwanyooshea vidole wale wote wazazi wetu waliotoka mkoa WA mara na kushindwa kukumbuka kwao na ndo hasa tatizo kubwa of which sisi sasa ambao tumeliona (si ajabu wao hawakuliona hahaha) inabidi tufanye hima na kuleta mabadiliko...inawezekana kabisa!! Tuweke UJINGA wetu pembeni ili iwezekane.

Saganka? We nambie whatz next ili tulianzishe, nakuunga Mkono na tuko pamoja japo nimeona umeisha aanzisha katiba na uko mbioni kuisajiri. Can u share pls?

Uzuri mwingine ni kwamba sasa Wana JF tuta anza kufahamiana uso kwa uso hahaha na nadhani hili halikwepeki iwapo tutataka kuleta mabadiliko ya kweli kwa mkoa wetu.

Hatujachelewa!!!


founder and CEO of www.oric.co.tz and www.aio.co.tz skype: alfred.kohi, 0784800989, 0715800989/0715800989
Akohi nimekupata vema,ni kweli nina draft ya katiba hapa,nita-share na kila anaetaka.Kuendelea kuzungumza huku tumejificha nyuma ya keybord ni dalili za kushindwa hata kuliko wazazi wetu.Namba zako nimeziona,nitakutafuta baadae kidogo.Nafanya kila lililo ndani ya uwezo wangu ili katiba ipate usajiri,nitaitangaza ili kuungwa mkono,na hapo tutafahamiana sana tu.Mara ni yetu, tuna rasilimali za kutosha,tunahitaji kuijenga.
 
Binafsi origin yng sio mkoa wa mara ila nimeishi hko kwa muda mrefu sana na hasa wilaya ya serenget.Ukweli ni kwmba raia wa hko ni wachapa kazi sana hasa kilimo na ufugaji,nani asiyejua kuwa mkoa mzima na hta kanda ya ziwa wanategemea sana zao la mahindi,ulezi,mtama na mihogo kutoka wilaya ya serengeti na tarime! Tatizo kubwa la wananchi wa maeneo hayo ni kutolipa kipaumbele suala la elimu kwa muda mrefu japokuwa sasa hivi naona wameamka kwa kiasi kikubwa hasa baada ya kudhibitiwa kwa suala uwindaji wa wanayama pori, vijana wengi wa wilaya ya tarime,serenget na bunda walikuwa wamekalia uwindaji tu kama chanzo cha kupata fedha na kununua mifugo mfano vijiji vya machochwe,kisangura,bwitengi,miseke,kebosongo,koleli,natta,issenye,rwamchanga n.k ilikuwa ni full kuwinda kitu ambacho kwa sasa ni ADHIMU KWAO. Ili kutumia fursa zilizopo elimu ni muhimu sana kwa mfano SINGITA LODGE (VIP,GURUMET FUND) ajira zilikuwa nyingi sana na kila kijana kijiweni alikuwa nawaza kufanya kazi huko pamoja na kupewa kipaumbele bado ajira hizo zilijaa watu kutoka daa,arusha,moshi,mwanza n.k kwa sababu vijana wengi hsa wa serengeti walikosa sifa stahiki (hotel,tourism,wild life management skills).Amin usiamin nimeshuhudia matangazo yakipelekwa hko vijijin mara kwa mara na hata kurudiwa ili mradi tu wananchi kuzunguka maeneo yale wapatikane bado ilikuwa ni ngumu kuwapata wenye sifa.
Ukienda pale hotelini utakuta zaidi ya asilimia 85% ya wafanyakazi ni wa mikoa mingine,wana mara wengi wameajiriwa kma ant-poachers (wenye kutumia nguvu kufukuzana na majangiri porini) tena approach waliotumia wale jamaa wakati wa ajira za ant-poachers ni kutafuta wale waliokuwa majangiri/wawindaji sugu na kuwapa mafunzo ya kijeshi kisha kuwaajiri ndio maana wamefanikiwa sana kudhibiti sana uwindaji maana wale jamaa wanajua njia na mapito ya wawindaji wote.NAAMINI WANAMARA MKIAMKA KIELIMU MTAFANIKIW SANA MAANA U ARE HARD WORKERS NA KUNA FURSA NYINGI SANA ZA KIUCHUMI HASA HIFADHI YA SERENGETI NA MADINI.I wll join u mkianzisha umoja ambao unasound na sio uliokaa kisiasa siasa.MSIISHIE KULALAMIKA JITAYARISHEN KUGRASP FURSA KWA KUWA NA SIFA STAHIKI.good time mara peoples.
 
Nakushukuru kwa ufafanuzi mzuri,mimi ni mongoreme kama nilivyjitambulisha,kama utakumbuka vema kuna bwana mmoja aliwahi kuwa mbuge wa serenget miaka 90,bwana Maro George(Mwita) ni mongoreme,hakuwa mtu mwema,aliposhindwa kwenye uchaguzi wa mwaka 2000,aliungana kwa siri na mgombea wa CUF bwana John Mosena Nyambabe kumpigia kampeni huku akipiga nyimbo za kuchochea chuki kati ya wangoreme na wairege.Hii akiri ya kufikiria madaraka bila kujali mustakabali wa wilaya na mkoa ni hatari sana na watu kama hawa hatutakiwi kuwaunga mkono hata kidogo.Kama sasa Wahutu na Watutsi wameungana na wanafanya mambo ya maendeleo,sisi tunaweza sana.Kuhusu Luge ni kweli kabisa ulichokisema,hata wangoreme hawamwamini,alinufaika sana na vurugu.Watu wa namna hii hatuwahitaji kabisa.Nilishafika Mbalibali mara nyingi na nina marafiki huko.

Dr. Mwita namfahamu sana, those days akiwa mbunge alikuwa akinipa lift mara moja moja nikienda shule Moshi. Na hata hivyo mzee wangu alikuwa akimuuunga mkono sana hata kampeni zake za ubunge zilirahisishwa sana kwa kitendo cha wakurya kumuunga mkono kwa wingi sana lakini mambo aliyowafanyia baadhi ya ndugu zetu imebaki historia. Kuna baadhi ya watu alichukua watoto wao wa kike kwamba anakwenda kuwasomesha lakini alichowafanyia ni wao wenyewe wanajua.

Sasa tuliposikia kwamba baadae alianzisha siasa chafu za ukabila dhidi ya Nyambabe kwakweli watu walimshangaa sana na hali hiyo imerudisha nyuma sana hali ya maelewano iliyokuwa imeanza kujengeka miongoni mwa wangoreme na wakurya. Tunatakiwa tupambane sana na wanasiasa wanaohubiri siasa za chuki kwakuwa wataturudisha nyuma sana ambako hatuhitaji kurudi huko tena.

Btw, nina rafiki zangu wangoreme wengi tu na nikiwa nao najiona niko na brothers wa damu kabisa. Kwahiyo katika hili tuko pamoja sana.
 
Jambo moja linalonikera sana ambalo bado nalitafutia njia muafaka ya kuli address ni kitendo cha TANAPA kuweka makao makuu ya mbuga ya serengeti (SERENGETI NATIONAL PARK-SENAPA) mkoani Arusha. Hii ni dharau kubwa sana kwa wanaSerengeti lakini ajabu ni kwamba hakuna kiongozi yeyote anayeliona hili na kulipigia kelele.

Ndugu zangu wana Mara pamoja na mambo mengine, ni lazima tuishinikize serikali itupe haki yetu ya makao makuu ya mbuga ya serengeti kuwepo mkoani kwetu, wilayani kwetu mjini Mugumu.

Nimebahatika kufikka katika baadhi ya hifadhi/mbuga zetu zilizopo hapa nchini kama Mikumi, Manyara, Ngorongoro, Udzungwa, Ruaha, Kitulo, Saadani, Mkomazi, Tarangire huko kote makao makuu ya watendaji/ofisi za mbuga/hifadhi hizo ziko katika mbuga/hifadhi husika, kwanini sisi ya kwetu Serengeti iwekwe Arusha? kwa maslahi ya nani?
Hata uwanja wa ndege wa Mugumu umekuwa hadithi,Tunatangazaje Mugumu kama kitovu cha utalii Mara bila miundombinu bora,hasa usafiri.
 
Ni matumaini yangu kuwa mpo salama,kwa upande wangu namshukuru Mungu.
Kwanza kabisa ni-declare interest kwamba mimi ni wa mkoa wa Mara,wilaya ya Serengeti,tarafa ya Ngoreme,kata ya Kenyamonta.

Nina machache leo ya kuzungumza na wana-Mara wenzangu kuhusu mkoa wetu.

Mkoa wa mara ulikuwa na kasifa hivi hasa kalikoletwa na mwl nyerere,kwamba baba wa taifa kutoka mara.Zaidi ya hapo tunabaki na sifa za kijinga tu ambazo kimsingi haziujengi mkoa wetu bali kuudidimiza na sisi tunabaki kuchekelea tu huku nyumba inaungua.

Mji mkuu wa mkoa wa Mara ni Musoma mjini,mtakubaliana nami kuwa mji ule umekuwa kama mtoto aliyesumbuliwa na kwashiakoo kwa muda mrefu,yaani umedumaa,hauna mabadiliko chanya tangu nianze kuwa na ufahamu,bali unakuwa kwa kwenda nyuma.

Wilaya ya Serengeti na Taarime zimekuwa zikisifika kwa fujo na watu wake eti kuitwa majasiri,hizo ni sifa za kijinga na wanaotuita hivyo wanafanya makusudi kutudumaza kimaendeleo.

Wilaya ya Serengeti,Musoma vijijini,na Bunda zinaelekea kugeuka jangwa.Wachoma mikaa wamefyeka kupita kiasi,huku watendaji wa serikali wakiwepo tu.Hawana uchungu maana wengi wao ni wa kupita tu,sisi wakudumu ndo tumeamua kujitengenezea jangwa.


Ujasiri wetu uko wapi kama si ujinga,tuna sehemu kubwa ya ziwa victoria,samaki wanavuliwa,minofu inatolewa,kisha watu wetu wanakula mifupa(mapanki),huo ndio ujasiri.

Mbuga ya Serengeti kwa asilimia kubwa ipo mkoani Mara,lakini kupata nyama kama kitoweo kwa siku hizi kupitia mbuga ni dhambi ambayo adhabu yake ni kupigwa risasi hadi kufa.Kama mtakumbuka zamani kulikuwa na kipindi fulani kwa mwaka wanaruhusu wananchi kuwinda kwa ajiri ya kitoweo.Hakukua na tatizo,wala hatujawahi kusikia wanyama wamepungua,ilikuwa ecosystem ya kawaida kwani sisi ni sehemu ya mbuga.Mfumo umefutwa,mbuga sasa iko na VIP,ukitaka kutangulia mbele ya haki katiza mbugani.Tumebaki kuangalia tu,wamefika mahali twiga wanabebwa na kupelekwa nje,eti mkoa wa Mara ni majasiri,sifa za kijinga.


Madini ya dhahabu yapo kwa wingi mkoani Mara,kuna Nyamongo,Buhemba,Park Nyigoti,Majimoto japo kwa uchache.Tunafaidije kama si kusaidia mkoa wa Mara kuwa na takwimu ya juu kwa virusi vya ukimwi na ukimwi(7.8%)
Eti mkoa wa Mara ni majasiri,sifa za kijinga.


Mkoa umekosa chuo cha maana cha utalii na Hotel management,vipo vya hovyo tu.Vyuo vya maana vipo Arusha na hivyo waajiriwa wengi wa hotel za mbugani wanatoka Arusha,Mara tunabaki kulalamika tu.Eti sisi ni majasiri,sifa za kijinga hizi.

Rais analazimisha kupitisha barabara ya lami mbugani kwa maslahi yake binafsi(Kwa sababu ana hotel mbugani),watu wa mkoa wa mara tumenyamaza tu,wakati tunafahamu madhara yake.Eti majasiri,ujinga huu.

Mbuga ipo kwetu,ukipita barabara ya mbugani unalazimika kulipa ada ya kupita mbugani,kama vile wewe ni mtalii.Huu ni uhuni tunafanyiwa,udau wetu juu ya hii mbuga upo wapi.Kwanini ulazimishwe kukatwa pesa hiyo wakati hukuwa na mpango wa utalii.Eti Mara majasiri.

Tukiendelea kubweteka na sifa hizi za kijinga kuna wakati utafika Mara itatambulishwa kama sehemu ya Arusha,"AMINI NAWAAMBIENI"

Waliotufikisha hapa wanajulikana,imefika wakati Mkoa wa Mara kuanzisha muungano wa vijana wa MKOA.Vijana wa Mara wakiwa na sauti moja,wanaweza kupanga vipaumbele vya mkoa,na mwanasiasa yeyote atakaetaka ridhaa yetu aonyeshe nia ya dhati kabisa ya kushughulikia vipaumbele hivyo.Vijana tunaweza kufanya hivyo,lakini pia umefika wakati wa sisi vijana kuufanyia kitu mkoa wetu pamoja na taifa kwa ujumla.

Nilikuwa naongea na mmoja wa wabunge wa mkoa wa Mara eti anasema mkoa umedhorota kwa sababu vijana wake wengi ni walevi,so what?ana maanisha hakuna mabadiliko?kwanini aliomba uongozi.

Naomba tupeane maoni juu ya mkoa wetu,tukosoane kwa kujenga na ikiwezekana tuje na harakati mpya za kuujenga mkoa wetu.

Mods kama kuna madainayoendana na hii ilishatolewa naomba msii-combine,nataka kupata maoni ya wadau
.

Kwakweri inakera sana, mambo sio mazom kabisaa! inabidi juhudi zichukuriwe!!!!!
 
Hata uwanja wa ndege wa Mugumu umekuwa hadithi,Tunatangazaje Mugumu kama kitovu cha utalii Mara bila miundombinu bora,hasa usafiri.


Nimesikia Mmarekani Tudor Jones amejitolea kutoa fedha za ujenzi bado serikali ndiyo haijatoa kwa upande wake ili shughuli za ujenzi zianze kitu ambacho kimemfanya mmarekani huyo kutaka asimamie mwenyewe ujenzi kwa kutafuta mkandarasi. Nadhani bado serikali inakuna kichwa kwakuwa mmarekani yuko tayari ispokuwa wao ndio bado wanasuasua.

Vile vile tunahitaji miundombinu bora ya barabara kutoka mugumu kwenda mbugani, kutoka mugumu kwenda bunda, kutoka mugumu kwenda tarime na kutoka mugumu kwenda maeneo mengine yanayotuzunguka ili tuweze kunufaika na shughuli za utalii na kiuchumi.
 
Wewe umefanya nini mkuu au unalalamika tu, mimi binafsi sipendi watu wanaolalamika tu bila action plan.Ni kweli pana tatizo. Bunda ndo wilaya kwanza kwa umaskini, sasa chukua hatua tuanzie hapo mkuu
Mihayo,kwa kuanza tayari nime-draft katiba ya Muungano wa Vijana wa Serengeti,naomba tuungani kuiokoa Mara yetu.
 
Mtabaki hivohivo. Ukabila, ukoo zinawatafuna sana. Kokote mliko mnajitambulisha kwa vikabila na viukoo vyenu. Ninyi hamuwezi kuwa wamoja. Nani atawaunganisha? Mongoreme kama mtoa mada akiitwa Mkurya anaona katukanwa wakati mila, desturi hata matambiko ni yaleyale! Mruri au Mukwaya hataki kuitwa Mjita. Msizaki naye sio Mwikizu! Mmegawanyika sana. Vipo vyama vya watu wa Mara hapa Dar na kwingineko lakini vyote vimejengeka kikabila na kiukoo sana. Tarafa kama ile ya Kiagata wote ni Wakurya lakini angalia hata vijiji vyake vilivyojengeka kiukoo! Dhambi hii itaendelea kuwatafuna sana tu.

Naamini si kweli kwamba kuna ukabila,
Tatizo la mara nafikiri ni lile lile la mikoa mingi Tanzania, tatizo lake namba moja ni
1. Elimu, wakazi hawakwenda shule na walioenda ni wachache sana, tulikalia kuvua jiswi yani chengu, sato,gogogo, jinembe, furu, kamongo nk. wakati wengine wamekalia mifugo. Na kupigana na masai kwa kutumia mishale na kuibiana ng'ombe.
Na kama shule basi nikizazi kuanzia miaka 70-80 ndo kimegutuka.

2. Imani za kishirikina kama ilivyo kigoma, subawanga nk, hata hivyo hii point imefungamana zaidi na namba 1 juu. Hii imani inatisha wengi sana na wengi wanatimua wakijiona kama wana elimu ama mali, ni imani za kutisha hizi za kishirikina ndo zinarudisha maendeleo nyuma. Kule watakutisha kwa mamba zao na viboko vyao integrated with ungo. Maendeleo yatapatikana kweli?
Tusilaume bure watu wengine, mtu anayekuletea barabara ya rami anakutakia heri, acheni kujidanganya. waingereza wenyewe mbona wamepitisha daraja tunnel ndani ya maji hadi ufaransa, sweden mbona wamepitisha barabara juu ya maji hadi norway, na bado hatujalalamika wanawabugudhi samaki? gutukeni.
 
Nimesikia Mmarekani Tudor Jones amejitolea kutoa fedha za ujenzi bado serikali ndiyo haijatoa kwa upande wake ili shughuli za ujenzi zianze kitu ambacho kimemfanya mmarekani huyo kutaka asimamie mwenyewe ujenzi kwa kutafuta mkandarasi. Nadhani bado serikali inakuna kichwa kwakuwa mmarekani yuko tayari ispokuwa wao ndio bado wanasuasua.

Vile vile tunahitaji miundombinu bora ya barabara kutoka mugumu kwenda mbugani, kutoka mugumu kwenda bunda, kutoka mugumu kwenda tarime na kutoka mugumu kwenda maeneo mengine yanayotuzunguka ili tuweze kunufaika na shughuli za utalii na kiuchumi.
Na kutoka Mugumu kwenda Musoma mjini kupitia Kebancha,Daraja Mbili,Kenyana,Ring'wani Masinki,Sirori Simba,barabara hovyo hovyo.
 
Binafsi origin yng sio mkoa wa mara ila nimeishi hko kwa muda mrefu sana na hasa wilaya ya serenget.Ukweli ni kwmba raia wa hko ni wachapa kazi sana hasa kilimo na ufugaji,nani asiyejua kuwa mkoa mzima na hta kanda ya ziwa wanategemea sana zao la mahindi,ulezi,mtama na mihogo kutoka wilaya ya serengeti na tarime! Tatizo kubwa la wananchi wa maeneo hayo ni kutolipa kipaumbele suala la elimu kwa muda mrefu japokuwa sasa hivi naona wameamka kwa kiasi kikubwa hasa baada ya kudhibitiwa kwa suala uwindaji wa wanayama pori, vijana wengi wa wilaya ya tarime,serenget na bunda walikuwa wamekalia uwindaji tu kama chanzo cha kupata fedha na kununua mifugo mfano vijiji vya machochwe,kisangura,bwitengi,miseke,kebosongo,koleli,natta,issenye,rwamchanga n.k ilikuwa ni full kuwinda kitu ambacho kwa sasa ni ADHIMU KWAO. Ili kutumia fursa zilizopo elimu ni muhimu sana kwa mfano SINGITA LODGE (VIP,GURUMET FUND) ajira zilikuwa nyingi sana na kila kijana kijiweni alikuwa nawaza kufanya kazi huko pamoja na kupewa kipaumbele bado ajira hizo zilijaa watu kutoka daa,arusha,moshi,mwanza n.k kwa sababu vijana wengi hsa wa serengeti walikosa sifa stahiki (hotel,tourism,wild life management skills).Amin usiamin nimeshuhudia matangazo yakipelekwa hko vijijin mara kwa mara na hata kurudiwa ili mradi tu wananchi kuzunguka maeneo yale wapatikane bado ilikuwa ni ngumu kuwapata wenye sifa.
Ukienda pale hotelini utakuta zaidi ya asilimia 85% ya wafanyakazi ni wa mikoa mingine,wana mara wengi wameajiriwa kma ant-poachers (wenye kutumia nguvu kufukuzana na majangiri porini) tena approach waliotumia wale jamaa wakati wa ajira za ant-poachers ni kutafuta wale waliokuwa majangiri/wawindaji sugu na kuwapa mafunzo ya kijeshi kisha kuwaajiri ndio maana wamefanikiwa sana kudhibiti sana uwindaji maana wale jamaa wanajua njia na mapito ya wawindaji wote.NAAMINI WANAMARA MKIAMKA KIELIMU MTAFANIKIW SANA MAANA U ARE HARD WORKERS NA KUNA FURSA NYINGI SANA ZA KIUCHUMI HASA HIFADHI YA SERENGETI NA MADINI.I wll join u mkianzisha umoja ambao unasound na sio uliokaa kisiasa siasa.MSIISHIE KULALAMIKA JITAYARISHEN KUGRASP FURSA KWA KUWA NA SIFA STAHIKI.good time mara peoples.

Maelezo yako na ushauri wako nakubaliana nao kwa kiasi kikubwa.
Isipokuwa nilitaka nikufahamishe jambo moja kwamba wakazi wa serengeti kwa asili shughuli zao kubwa ni ufugaji, kilimo na uwindaji, wamekuwa wakifanya uwindaji huo miaka na miaka lakini bado hawakuvuruga ecosystem kama ambavyo tumekuwa tukilazimishwa kuamini. Wananchi wa serengeti hawajawahi kutegemea uwindaji kama njia kuu ya kujipatia kipato ama maendeleo bali kilimo na ufugaji.

Suala la vijana kukaa kijiweni lilikuwepo na bado lipo kutoakana na kutokuwa na mwamko wa elimu, ingawa sasa mambo ni tofauti sana, vijana wengi sana sasa wanasoma na hao ndio mategemeo makubwa kwa ajili ya maendeleo ya wilaya yetu.

Nikizungumzia ajira za Mahotelini sio kweli sana kama unavyodai, tunao vijana ambao si wengi waliokuwa wamesomea kozi za hoteli na utalii lakini bado hawakupata ajira katika mahoteli yaliyoanzishwa, hii ilisababishwa na mameneja waajiri wengi kuajiri watu wao ama watu kutoka huko kwao, kiujumla kulikuwa na upendeleo mkubwa sana. Mimi binafsi mdogo wangu alikuwa amemaliza certificate ya hotel management lakini alifanya intervie mara tatu na kuachwa, alipokuja dar akafanikiwa kupata kazi hotel moja hapa jijini. Baada ya wananchi kulalamika kwamba watoto wao hawaajiriwi na badala yake wanaajiriwa watu wengine hasa kutoka Arusha, Kilimanjaro, Mwanza na Kenya ndipo baadhi ya waliokuwa na sifa wakapata nafsi ya kuajiriwa na mdogo wangu wakamuita na kwakuwa walimpa maslahi mazuri comapred na huku alikokuwa nikamshauri aende.

Lakini pamoja na hayo yote niliyosema bado tunawajibika kupigana zaidi ili kufikia malengo kama mikoa na wilaya nyingine.
 
Naamini si kweli kwamba kuna ukabila,
Tatizo la mara nafikiri ni lile lile la mikoa mingi Tanzania, tatizo lake namba moja ni
1. Elimu, wakazi hawakwenda shule na walioenda ni wachache sana, tulikalia kuvua jiswi yani chengu, sato,gogogo, jinembe, furu, kamongo nk. wakati wengine wamekalia mifugo. Na kupigana na masai kwa kutumia mishale na kuibiana ng'ombe.
Na kama shule basi nikizazi kuanzia miaka 70-80 ndo kimegutuka.

2. Imani za kishirikina kama ilivyo kigoma, subawanga nk, hata hivyo hii point imefungamana zaidi na namba 1 juu. Hii imani inatisha wengi sana na wengi wanatimua wakijiona kama wana elimu ama mali, ni imani za kutisha hizi za kishirikina ndo zinarudisha maendeleo nyuma. Kule watakutisha kwa mamba zao na viboko vyao integrated with ungo. Maendeleo yatapatikana kweli?
Tusilaume bure watu wengine, mtu anayekuletea barabara ya rami anakutakia heri, acheni kujidanganya. waingereza wenyewe mbona wamepitisha daraja tunnel ndani ya maji hadi ufaransa, sweden mbona wamepitisha barabara juu ya maji hadi norway, na bado hatujalalamika wanawabugudhi samaki? gutukeni.
Kisayansi samaki wanapenda sana sauti zenye/zisizo na mpangilio maalum,lakini wanyama hawapendi.Madereva wetu pamoja na kwamba lami haijawekwa wanagonga wanyama,itakuaje ikiwekwa.Anyway kama hilo si sehemu ya tatizo itajulikana tu.
 
Mimi sio Mkurya lakini nimekaa ukuryani kwa miaka 6 sasa katika kutafuta,hakuna wilaya yoyote ya mkoa wa Mara sijawahi kufika, anzia Serengeti - Mugumu kupitia Nata, Mgeta mpaka Bunda, pitia Nyamswa, Butiama, Kyabakari mpaka Musoma,katisha pale zero kwenda mkoa mpya wa kipolisi wa Tarime, Rorya mpaka Silari kwenda mpaka majita hadi Ukrerewe, from my heart nakuambieni hata mtengeneze muungano wa vijana, wazee, watoto, wanawake na hata watoto ambao wametungwa mimba HAMTAWEZA kufanikiwa. Naesema hivo kwa sababu system imewafanya nyie mnyamaze msiweze kusema chochote, sasa unategemea kila kona ya serikali wameweka watu wa Mara nani ataweza kukohoa wakati anakulazake 10% na anataka kupata heshima serikalini.

Mfano ifuatayo inaonesha kuwa vijana wa mkoa wa Mara mtakufa maskini hata kama mna fursa nyingi sana

-Ukiingia kwenye mbuga ya Serengeti na hoteli zake 70% ya wafanyakazi hata zile kazi ndogondogo za kuosha vyombo wanatokea Arusha na Mwanza hapo inatakiwa muamke mseme inatosha,pelekeni vijana wakasomee mambo ya utalii vyuoni
- Nduguzanguni Wanata, Waikoma na Wanyichoka nyie ni bure kabisa mpo karibia na mwekezaji wa Singita Grumeti Reserves lakini kazi yenu ni kulalama tu na ajira wanachukua vijana wa mbali, kisa hamjaweka mkakati mathubuti wa kuajiriwa pale manachojua ni kwenda kuomba tumisaada twa kijinga eti mfundishwe kurina asali upuuzi mtupu
-Machimbo ya dhahabu yapo kwenu lakini waajiriwa wanatokea mali sana kisa hamna makakati wa kimaono ndio maana hata hizo sehemu za wachimbaji wadogowadogo wameamua kuwanyanganya na hamtafanya lolote milele daima maana nyie vijana wa Mara mumejaa ukabila mara utaskia yule ni mjaluo, yule ni Mtana yule ni mwisenye mara yule ni muikizu yaani bure kabisa
-Nimetembea duniani lakini sijawai kuona vijana waoga kama wa mkoa wa Mara, ukisikia Mkurya eti ni makali basi ni kwa makabila ya huko huko kwao lakini kwa kabila lolote linalotokea mkoa mwingine Mkurya anaweka mkia matakoni anamwachia anafanya anachokitaka
 
Mura, Obambiri mahene mura. Tugegehiri. Bonse tuberi kya barisya!

Mara tuamke. Kweli hata kwetu Majimoto hali ni mbaya kabisa. Kiagata ndo usiseme. juzi tumechimbiwa bwawa la hovyo kabisa kabisa! Wanaume tukalikataa. Sasa tuamke tuuendeleze mkoa wetu. lakini kwa shemeji zangu Majita nao ni bure kabisa. Kuna wasomi-madaktari na maprofesa wasiokuwa na idadi, lakini wote wanajenga Dar, Mwanza, Moshi, Arusha, Dodoma na kadhalika. Wanaogopa kujenga Murangi, Mabui Merafuru, Kinyambwiga hadi Masita (Busekera) kwa sababu ya kuogopa kulogwa. Huu nao ni ujinga mura! tuamke!

Sasa mkoa una mawaziri wasira, kabaka, makongoro mahanga, muhongo, mkangara; lakini wote bure. Una makatibu wakuu kama yule wa biashara, mifugo, maswi wa madini, na wengine kibao, lakini bure kabisa.

Mkoa una mkuu wa JKT ambaye ni mzanaki, una Katibu wa Chama Cha Magamba, una Mwanasheria Mkuu (Werema) na Naibu Mwanasheria Mkuu (Masaju); hawa wote hakuna kitu! Una majenertali Kiaro, Waitara, na Musuguri; lakini mambo mabaya kabisa. Wengine ongezeni jamani!

Ha ha haaa, mkuu hii ni kweli, na ungeanzia na Nyerere, kwani hakuchangia kuididimiza Mara? Iweje mapato mengi ya Serengeti yainufaishe Arusha? Ili suala kwa kweli huwa linaniuma sana, japo wengine wanadai hii inaonekana ni sera za majimbo ambazo ni za kibaguzi, mm nasema sera ikiyopo ni ya kipuuzi zaidi!
 
Mimi sio Mkurya lakini nimekaa ukuryani kwa miaka 6 sasa katika kutafuta,hakuna wilaya yoyote ya mkoa wa Mara sijawahi kufika, anzia Serengeti - Mugumu kupitia Nata, Mgeta mpaka Bunda, pitia Nyamswa, Butiama, Kyabakari mpaka Musoma,katisha pale zero kwenda mkoa mpya wa kipolisi wa Tarime, Rorya mpaka Silari kwenda mpaka majita hadi Ukrerewe, from my heart nakuambieni hata mtengeneze muungano wa vijana, wazee, watoto, wanawake na hata watoto ambao wametungwa mimba HAMTAWEZA kufanikiwa. Naesema hivo kwa sababu system imewafanya nyie mnyamaze msiweze kusema chochote, sasa unategemea kila kona ya serikali wameweka watu wa Mara nani ataweza kukohoa wakati anakulazake 10% na anataka kupata heshima serikalini.

Mfano ifuatayo inaonesha kuwa vijana wa mkoa wa Mara mtakufa maskini hata kama mna fursa nyingi sana

-Ukiingia kwenye mbuga ya Serengeti na hoteli zake 70% ya wafanyakazi hata zile kazi ndogondogo za kuosha vyombo wanatokea Arusha na Mwanza hapo inatakiwa muamke mseme inatosha,pelekeni vijana wakasomee mambo ya utalii vyuoni
- Nduguzanguni Wanata, Waikoma na Wanyichoka nyie ni bure kabisa mpo karibia na mwekezaji wa Singita Grumeti Reserves lakini kazi yenu ni kulalama tu na ajira wanachukua vijana wa mbali, kisa hamjaweka mkakati mathubuti wa kuajiriwa pale manachojua ni kwenda kuomba tumisaada twa kijinga eti mfundishwe kurina asali upuuzi mtupu
-Machimbo ya dhahabu yapo kwenu lakini waajiriwa wanatokea mali sana kisa hamna makakati wa kimaono ndio maana hata hizo sehemu za wachimbaji wadogowadogo wameamua kuwanyanganya na hamtafanya lolote milele daima maana nyie vijana wa Mara mumejaa ukabila mara utaskia yule ni mjaluo, yule ni Mtana yule ni mwisenye mara yule ni muikizu yaani bure kabisa
-Nimetembea duniani lakini sijawai kuona vijana waoga kama wa mkoa wa Mara, ukisikia Mkurya eti ni makali basi ni kwa makabila ya huko huko kwao lakini kwa kabila lolote linalotokea mkoa mwingine Mkurya anaweka mkia matakoni anamwachia anafanya anachokitaka
Duh! lugha kali sana hiyo.Lakini ujumbe umefika,lugha uliyotumia tutaitumia kama changamoto kuanzisha muungano huu.Asante sana
 
Back
Top Bottom