Kwa wanaotaka ushauri

Mlenge

R I P
Oct 31, 2006
2,125
2,291
Habari wandugu,

Katika kutoa huduma kwa jamii, napenda kuwashauri watu wanaotaka kujiendeleza kielimu, maarifa na kiteknolojia. Wapo watu wanaopenda kujiendeleza kwenye nyanja hizo, na hukosa watu wa kuwauliza. Au pengine wangependa kupata mawazo mbadala.

Kama unataka kujiendeleza kielimu, na ungependa kufahamu zaidi na kupata ushauri kuendana na ulipo na unakotaka kufika, tutumie uzi huu kuweka bayana uyatakayo. Iwapo hungependa uyatumayo yaonekane kwenye hadhara, basi jiunge kwenye tovuti ifutayo kwa ajili ya faragha zaidi: https://trello.com/invite/b/sT4WMZ3C/c3e273f5230374e65b1212217a165614/shule

Wapo wengine wanaopenda kusoma nje ya Tanzania, au ndani ya Tanzania, lakini kwa malengo mahsusi. Wengine wanasoma wapate cheti tu, wengine kwa sababu fulanifulani hawakupata fursa ya kusoma, sasa wanataka kujiendeleza, wote hawa wana nafasi yao ya kupata ushauri.

Sikai sana mitandao ya kijamii, lakini nitajitahidi kumjibu kila mmoja, hata kama si papo hapo.

Kuhusu mimi, nimejaliwa kupata fursa ya kusoma zamani na miaka ya karibuni. Kadhalika nimepata uzoefu wa kozi fupi na ndefu, ndani na nje ya Tanzania.

Karibuni!
 
Mimi nimemaliza kidato cha nne na nilipata daraja la 3, nikaendelea kidato cha 5-6 kombi ya ECA, nilipata sifuri coz matatizo na changamoto za kimaisha,sikurudia mtihani coz nilikosa attention! ila malengo yangu niendelee na masomo hayohayo ya biashara ila tatizo pesa sina hata ya kwenda kusomea cheti, hata ualimu pia nilitamani nikasome ila kwa vyuo serikali ni shida kupata coz nimeshaomba Mara nyingi, kwa vyuo binafsi Ada ni tatizo pia. Nashindwa nijikwamue vipi katika hili.!!!
 
Mimi nimemaliza kidato cha nne na nilipata daraja la 3, nikaendelea kidato cha 5-6 kombi ya ECA, nilipata sifuri coz matatizo na changamoto za kimaisha,sikurudia mtihani coz nilikosa attention! ila malengo yangu niendelee na masomo hayohayo ya biashara ila tatizo pesa sina hata ya kwenda kusomea cheti, hata ualimu pia nilitamani nikasome ila kwa vyuo serikali ni shida kupata coz nimeshaomba Mara nyingi, kwa vyuo binafsi Ada ni tatizo pia. Nashindwa nijikwamue vipi katika hili.!!!

Njia mojawapo ya kujiendeleza ni kusoma professional courses. Kwa vile unataka biashara, na ulisoma ECA, huenda unapenda uhasibu. Soma professional course za uhasibu. Baada ya miaka miwili hivi ukijituma kiukweli unaweza kupata CPA ambayo ni sawa na kuzidi digrii ya kwanza ya uhasibu. Baada ya kupata CPA soma masters ya business administration au nyingine yoyote upendayo.

Edit: Nenda NBAA watakushauri pa kuanzia.
 
Mimi nimemaliza masomo ugavi ngazi ya cheti katika chuo kimoja hapa nchini hivi karibuni..na miezi ya hivi karibuni blog moja ilitoa tetesi ya kufutiwa udahili chuo hicho lakini ikatokea kukanushwa na utawala wa vyuo hivo...sasa kulingana na hali ilivo nahisi kabisa hicho chuo hakijasajiliwa nacte maana hata kwenye orodha ya cas nacte hakipo na pia kimetangaza tena udahili kupitia chuoni hapo hapo....ila hicho chuo kina usajili wa TCU maana kinatoa degree pia..sasa wasi wasi wangu kama hakikusajiri corse itakuaje na final nimefanya...je watatoa matokeo maana niliomba ruhusa kazini kusoma so lazima watadai matokeo...naomba msaada tafadhari.
 
Mimi nimemaliza masomo ugavi ngazi ya cheti katika chuo kimoja hapa nchini hivi karibuni..na miezi ya hivi karibuni blog moja ilitoa tetesi ya kufutiwa udahili chuo hicho lakini ikatokea kukanushwa na utawala wa vyuo hivo...sasa kulingana na hali ilivo nahisi kabisa hicho chuo hakijasajiliwa nacte maana hata kwenye orodha ya cas nacte hakipo na pia kimetangaza tena udahili kupitia chuoni hapo hapo....ila hicho chuo kina usajili wa TCU maana kinatoa degree pia..sasa wasi wasi wangu kama hakikusajiri corse itakuaje na final nimefanya...je watatoa matokeo maana niliomba ruhusa kazini kusoma so lazima watadai matokeo...naomba msaada tafadhari.

Kisu mchinje mbuzi
Mbuzi aliyekataa kunywa maji
Maji yaliyokataa kuzima moto
Moto uliokataa kuunguza fimbo
Fimbo iliyokataa kumchapa Kalumekenge
Kalumekenge aliyekataa kwenda shule.

Bila shaka unaikumbuka hadithi hii ya zamani sana. Mlolongo mrefu wa urasimu na umangimeza.

Wengi kwenye elimu tunatumia mfumo huo. Yaani, tunasoma kozi za kishuleshule (academic), na kuacha za kitaalam (professional).

Kwa mfano wako, unapata kazi kusoma kwenye chuo chenye/kisicho na udahili, kozi ya kishuleshule. Pindi umalizapo, utajigundua kwamba bado unahitajika kusoma kozi za kitaaluma. Kwa nini tusipunguze mlolongo wa 'maji zima moto uliokataa...'? Achana na chuo hicho. Nenda kasome kozi za kitaaluma moja kwa moja.

Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi PSPTB ni mahala pazuri pa kuanzia. Wameweka orodha ya watoa mafunzo yatakayokusaidia uweze kujiunga na taaluma hiyo rasmi. Angalia orodha hii ya baadhi ya watoa mafunzo: http://www.psptb.go.tz/uploads/files/Training provider category APRIL 2016.pdf

Kwa upande mwingine, unaweza kusoma nje ya Tanzania, na siyo mambo ya ugavi tu. Angalia hapa: http://www.edx.org ukiwa hapohapo Tanzania pasi na kulazimika kusafiri.

Mlenge
 
Mkuu kwema Mlenge
Kuna mtu anataka kujiendeleza,
elimu aliyo nayo ni degree level ya banking and finance from IFM Tanzania,
Anafikiri kujiendeleza katika mitihani ya bodi kati ya benki yani CPB au uhasibu yani CPA(naomba kama una uelewa hapa kwenye CPA kama unajua mtu wa course tajwa hapo ataanzia level gani? na pia gharama za kujisajili NBAA zipoje kwasasa?
Na pia ikiwezekana je kwenye vituo ada zipoje kwasasa? Pia vipi hizi proffessional kwa nchi za wetu kuhusu upatikanaji wake ?

Pia ana option ya kusoma masters japo kwasasa yupo mkoani na chuo kinachopatikana huko ni open university tu kwa ajili ya degree ya pili.

Naomba umshauri
 
Kwema mbota,

Kutegemea na malengo yake au mipango yake, anaweza kuhakikisha anajiandikisha katika bodi mojawapo au zote. Ila naona CPA ina uzito zaidi kama anataka kuendelea kufanya kazi Tanzania, na huenda baadaye akatoka kutoka katika sekta ya benki. CBP ni nzuri iwapo anataka kufanya kazi na mabenki yenye asili siyo ya Tanzania.

Vituo vya mitihani ya NBAA viko sehemu nyingi, mfano – Arusha, Dodoma, Iringa, Mbeya, Morogoro, Moshi, Tanga, Zanzibar, Mwanza na Dar es Salaam, mradi tu darasa lienee (angalau watahiniwa 30).

Maelezo mazuri zaidi atayapata NBAA, na kwenye linki hii: ACCOUNTING AND FINANCE PROFESSIONALS: CPA (T)
 
Habari Mlenge .Mimi ni mhitimu wa kidato cha sita mwaka mmoja uliopita kutoka sasa ,nilisoma mchapuo wa sayansi yaani PCB,nilichaguliwa kujiunga na chuo kikuu kimoja hapa nchini ila kozi ya IT degree,ila haikuwa ndoto yangu,kwani ndoto yangu ilikuwa ni udaktari.Niliamua kufanya application ya diploma ili kupata nafasi ya udaktari dip kuepuka competition ,nimechaguliwa ilakwa bahati mbaya aliyekuwa ananisomesha alifariki dunia,huku ikiwa gharama za hiyo kozi ni kubwa na hakuna any sponsorship.Na chuo tarehe 15/10/2016 kinafungua .Nianzaje kwa hili
 
Habari Mkuu
Mimi ni kijana niliyechaguliwa kujiunga na masomo yangu kwa ngazi ya degree kwa mwaka huu. Tatizo lilipo ni chuo nilichochaguliwa sihitaji kusoma hapo kwaiyo nahitaji kufanya uhamisho sasa naomba unisaidie naanzaje anzaje kufanya uhamisho huo. Natanguliza shukran
 
Samahani ningependa kujua chuo cha Nit kinaanza masomo take terehe ngapi?
Sifahamu kwa hakika, ila nadhani itakuwa wiki mbili hivi kuanzia sasa, ikiwa kalenda yao inafanana na vyuo vingine. Ni vema ukawasiliana nao moja kwa moja: Contact Us

Hongera kwa kuchaguliwa kujiunga na NIT.
 
Habari Mlenge .Mimi ni mhitimu wa kidato cha sita mwaka mmoja uliopita kutoka sasa ,nilisoma mchapuo wa sayansi yaani PCB,nilichaguliwa kujiunga na chuo kikuu kimoja hapa nchini ila kozi ya IT degree,ila haikuwa ndoto yangu,kwani ndoto yangu ilikuwa ni udaktari.Niliamua kufanya application ya diploma ili kupata nafasi ya udaktari dip kuepuka competition ,nimechaguliwa ilakwa bahati mbaya aliyekuwa ananisomesha alifariki dunia,huku ikiwa gharama za hiyo kozi ni kubwa na hakuna any sponsorship.Na chuo tarehe 15/10/2016 kinafungua .Nianzaje kwa hili
Hongera kwa kuchaguliwa kozi ya Diploma. Pole kwa kufiwa.

Pa kuanzia ni kuamini kwamba with persistence, utaweza kuendelea na masomo yako.

  1. Changanua ni gharama zipi zinazohitajika ili uweze kuanza masomo yako.
  2. Changanua gharama za ujumla za kukamilisha elimu yako.
  3. Katika hizo gharama zote, wewe unaweza kuchangia asilimia ngapi?
Ukianzia na kiasi fulani unachoweza kuchangia, na ukijua jumla ya gharama, unaweza kuwa na mkakati wa kutafuta namna ya kuzipata.

Findology 101 inadai uanzie kutafuta pale ulipo. Je, una mali yoyote unayoweza kuibadilisha iwe hela za kukuwezesha kusoma? Njia yoyote nyingine mbadala?

Mahali pa kuanzia baada ya hapo ni kwenye chuo unachotaka kwenda kusoma. Wana skolashipu yoyote? Je, wanakubali kulipwa ada kwa mikupuo mingi, ili kusaidia wale wasio na uwezo? Wana waiver ya ada? Discount? Baadhi ya vyuo vinatoa punguzo la ada kwa wanafamilia wa wafanyakazi. Huna mzazi au mlezi kwenye chuo hicho?

Umeenda Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto? Hapo utaweza kuambiwa njia mbadala zinazoweza kukufaa katika lengo lako. Jaribu kuulizia miradi mbalimbali iliyoko au fursa ambazo zitaweza kuenda na lengo lako.

Asasi zisizo za Kiserikali zenye malengo anuai ambayo yanasharibiana na wewe kupata diploma ya Clinical Officer. Uko radhi kwenda kufanya kazi vijijini kusiko na madaktari baada ya kuhitimu. Wakikusomesha wewe watakuwa wanasaidia kupunguza vifo na magonjwa ya mama na mtoto, kwa vile utaenda kijijini kwenye zahanati zenye majengo bila matabibu. Kutasaidia kuimarisha huduma za afya ya uzazi na watoto kwa vile kule kijijiini utakakoenda hakuna huduma rasmi za ukunga. Kutaimarisha afya ya jamii, hasa kwa makundi yaliyoko kwenye mazingira ya hatari kwa vile utaweza kuwafikia na kutoa uelimishaji-umma kwa makundi hayo yasiyofikiwa vijijini; kutaboresha mazingira kwa kuwa na watu wenye afya bora.

Jaribu kuwasiliana na asasi hizo, japo zenyewe siyo 'scholarship-granting organizations', lakini pengine zinaweza kuwa na fursa ya kukuunga mkono katika kusoma utabibu ili malengo hayo hapo juu yatimizwe.

Mf.,
Tanzania : EngenderHealth
Tanzania | Jhpiego
http://sawatanzania.org/

Nenda kwa watafiti mbalimbali wa afya, ambao wataweza kukutumia kama field-assistant. Eg., NIMR Tanzania

Fika kwenye halmashauri yako ya wilaya/mji/jiji. Ulizia fursa zilizopo zinazoweza kutumika kukamilisha elimu yako.

Waone sekta binafsi pia, ukiahidi na kuingia makubaliano ya ajira ya muda fulani baada ya kuhitimu au wakati wa fieldwork.

Waone wafadhili mbalimbali wengine walioko Tanzania, kama vile, https://vodacom.co.tz/foundation/projecta/improving_health/healthy_motherhood ,
Asante Africa Foundation | A US Charity to Educate Children in Tanzania and Kenya - Asante Africa Foundation
FCS inspire formation of Tanzania philanthropy forum to serve the vulnerable
MO Dewji Foundation

Of course, tumia scatter-gun approach. Tuma maombi kamilifu sehemu nyingi. Kwa mujibu wa Pareto Principle, lazima utapata walau kutoka sehemu moja kwa kila application tano.

Bottom line: Kwa nini wakusomeshe wewe na siyo mtu mwingine? Ndoto za kuwa daktari ni sababu ambayo haina mashiko. Wewe kusomeshwa kutasaidia vipi jamii, on the short-term, na kutafikisha vipi malengo ya kusaidia jamii, aliyonayo mwenye kushikilia pochi?

Mbadala mwingine ni kutumia skills ulizonazo kujitengenezea kipato kwa kutumia Intaneti. Zipo njia nyingi, ila kwa kuanzia nakupatia linki hizi: 40 easy ways to make money quickly (Soma komenti!);
5 Real Ways to Actually Make Money Online
50 Legitimate Ways to Make Money from Home in 2016

All the best!
 
Habari Mkuu
Mimi ni kijana niliyechaguliwa kujiunga na masomo yangu kwa ngazi ya degree kwa mwaka huu. Tatizo lilipo ni chuo nilichochaguliwa sihitaji kusoma hapo kwaiyo nahitaji kufanya uhamisho sasa naomba unisaidie naanzaje anzaje kufanya uhamisho huo. Natanguliza shukran
Hongera kwa kuchaguliwa; Nenda TCU ukawaone in-person watakushauri nini cha kufanya. Pana nafasi huko unakotaka kuenda? Cut-off points za huko unakotaka kwenda zinalinganaje na ulizo nazo? Utaenda kusoma kozi ileile au tofauti?

Ndege aliye mkononi vs aliye mwituni: angalia unapofuatilia haya, usije ukakosa kote.

Mlenge
 
Back
Top Bottom