The sage
Member
- May 25, 2011
- 29
- 4
Hapa naomba tuwe wakweli. Kwa maneno yao wenyewe viongozi wa juu wa CCM wameshuhudia kuwa chama kimepoteza mvuto kwa watanzania na hasa kwa vijana. Wakati huohuo CHADEMA ni chama kilichojipatia umaarufu mkubwa na kukifunika CCM kwa kila namna, hasa kwa wakati huu.
Hivyo mtu anaporudisha kadi ya CHADEMA na kujiunga na CCM ni wazi kuwa ni kwa maslahi binafsi hasa kwa kujipatia fedha za kujikimu kutokana na hali ngumu ya maisha au kwa tamaa tu ya kujilimbikizia mali. Kwa mtu mzalendo kweli na anayejali maslahi ya Taifa hawezi kujiunga na chama cha magamba ambacho badala ya kurekebisha kasoro zake kinazunguka kuupotosha ukweli ambao wakombozi wa kweli wamejitahidi kuwafumbua macho watanzania.
Jamani watanzania tuamke, tuache kurubuniwa na visenti vichache huku tukiviweka hatarini haki na uhuru wetu kwa chama hiki kisicho na huruma kwa watanzania!
Hivyo mtu anaporudisha kadi ya CHADEMA na kujiunga na CCM ni wazi kuwa ni kwa maslahi binafsi hasa kwa kujipatia fedha za kujikimu kutokana na hali ngumu ya maisha au kwa tamaa tu ya kujilimbikizia mali. Kwa mtu mzalendo kweli na anayejali maslahi ya Taifa hawezi kujiunga na chama cha magamba ambacho badala ya kurekebisha kasoro zake kinazunguka kuupotosha ukweli ambao wakombozi wa kweli wamejitahidi kuwafumbua macho watanzania.
Jamani watanzania tuamke, tuache kurubuniwa na visenti vichache huku tukiviweka hatarini haki na uhuru wetu kwa chama hiki kisicho na huruma kwa watanzania!