Kwa wanaohusika: Acheni uchuro!

Status
Not open for further replies.

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,460
39,928
Jana Jumamosi habari zilianza kuenea katika maeneo mbalimbali nyumbani hasi miongoni mwa vigogo kuwa Balali amefariki. Simu zikapigwa na sisi wengine ambao tunaelewa hali ya mgonjwa tukashtushwa. Labda ni kweli mnataka afe ili aende kwa muumba na siri zenu. Bahati mbaya mpango huo hadi hivi sasa ahera madukani wameuharisha na akirudisha namba yake itakuwa ni kwa kibali cha Aliye Juu. Sasa acheni kumchuria msije mkalazimisha kutimiza unabii wenu wenyewe. Kule kwetu huo unaitwa uchuro! Nawashauri mtangulie nyinyi kwanza lakini baada ya kusema siri zenu! Na mtake msitake atarudi nyumbani na kama kuna mashtaka yoyote ambayo mko tayari kuyaandaa mjue kabisa hatasimama kizimbani peke yake! Mmelikoroga wenyewe, sasa mtalinywa! Tuliwaambia mkatuona siye tuna wivu..
 
Jana Jumamosi habari zilianza kuenea katika maeneo mbalimbali nyumbani hasi miongoni mwa vigogo kuwa Balali amefariki. Simu zikapigwa na sisi wengine ambao tunaelewa hali ya mgonjwa tukashtushwa. Labda ni kweli mnataka afe ili aende kwa muumba na siri zenu. Bahati mbaya mpango huo hadi hivi sasa ahera madukani wameuharisha na akirudisha namba yake itakuwa ni kwa kibali cha Aliye Juu. Sasa acheni kumchuria msije mkalazimisha kutimiza unabii wenu wenyewe. Kule kwetu huo unaitwa uchuro! Nawashauri mtangulie nyinyi kwanza lakini baada ya kusema siri zenu! Na mtake msitake atarudi nyumbani na kama kuna mashtaka yoyote ambayo mko tayari kuyaandaa mjue kabisa hatasimama kizimbani peke yake! Mmelikoroga wenyewe, sasa mtalinywa! Tuliwaambia mkatuona siye tuna wivu..

Mkijiji Dua la kuku halimpati mwewe!

Kama kweli wanamuombea afe, na hafi ng'o!, lakini la msingi ni je yuko tayali kuja kusema kweli tupu na kweli yote?? Kama ni hivo tuzidishe maombi kwa muumba amjalie afya!

Atakuwa ni muungwana sana, na naamini watanzania walio wengi tutakuwa tayari kumsamehe pale alipo kubali kutumika kutekeleza na kulinda maslahi ya mafisadi pengine kwa kuhofia kibarua chake kisiote majani, endapo tu atasimama na kusema kweli ili wezi wetu tuwashike mashati!
 
Hao mafisadi wanajua walichomfanyia maana hata Amina (RIP) aliugua hivi hivi hadi kifo.

Tusubiri tukiwa tunaomba mungu ili apate full recovery ili apate kutueleza nini kiliendelea na wapi zilipo, au nani aliyechukua pesa zetu maana inawezekana zimewekwa mahali.
 
Wewe Mwanakijiji badala ya kusheherekea heppi besideyi, unachimbua rumours. lol.
Heppi Besideyi.
 
Mzee Mwanakijiji

Hawa MAFISADI hawana aibu! Nilitazama hicho kichwa cha habari nikasema ngoja niangalie kulikoni. Ama kweli ukistaajabu ya Musa ya F***** huyawezi.
 
Mkuu Mwenzangu MMJ,

Naona kuna info unazo kuhusiana na sakata zima la Balali, mkuu hebu liweke wazi hapa tuchambue mchele na pumba zilipo, naona kila wakati unaachia kidogo kidogo, mzee JF hapa weka maneno tuseme maneno!

Mnyonge mnyongeni lakini haki apewe, nimesema huko nyuma kuwa Balali, alikuwa a senior executive kwenye World Bank, tena for a least 25 years, na akaweza mpak kumiliki nyumba yake binafsi katika maeneo wanayoishi matajiri wengi wa US, huko DC na ni maeneo wanayokaa watu wakali huko US, kama kina Collin Powell, maana yake ni kwamba huyu mkuu alikuwa na hela na mali zake nyingi tu kabla hata ya kuingia BOT,

Sasa tufike mahali wabongo tuseme ukweli, alikuwa na mali ngapi kabla ya kuingia na akaongeza ngapi baada ya kuingia, na kujiuzulu kwake akiwa nje kusichukuliwe tu kwamba ni basi yeye ni guilty in absentia, apewe haki pia!
 
Mzee mwenzangu, nilichonacho ndicho niwapacho; Kuna mambo ambayo Balali anayafahamu na katika sakata zima la BoT anafahamu kuwa yeye ndiye mtolewa kafara wa kwanza. Endapo mautu yatamkumba kabla ya kupata nafasi ya kujitetea mbele ya chombo cha sheria; na ushahidi wa washirika wengine kutojulikana ulipo basi madudu yote atabebeshwa marehemu;

Ni kutokana na ujuzi wa hili ndio maana barua ikawa leaked to the press na hivyo pre-emptying the powers that may be; sasa ripoti ya BoT haitanoga endapo Balali atakuwa bado yuko hai kwani wakimnyoshea kidole na yeye atawanyoshea cha kwake.

Sasa sijui ni kwanini jana mtu alianzisha uvumi huo hadi watu wanapiga simu Ikulu, Ubalozini na Mambo ya Nje.. wanataka kujua kama tetesi kuwa "Balali amefariki" zina ukweli. Sasa hii si mara ya kwanza tangu mzee huyo aanze kuugua.

Kwa kifupi Balali hayuko mahututi na ameshatoka hospitali na anaendelea na matibabu vizuri na mazoezi ya viungo at "undisclosed location". Amepoteza uzito sana na bado anakula kwa msaada lakini hali yake ni bora kuliko wiki tatu zilizopita. Kupata kwake nafuu siyo habari njema kwa makumi ya watu.
 
Kwa kifupi Balali hayuko mahututi na ameshatoka hospitali na anaendelea na matibabu vizuri na mazoezi ya viungo at "undisclosed location". Amepoteza uzito sana na bado anakula kwa msaada lakini hali yake ni bora kuliko wiki tatu zilizopita. Kupata kwake nafuu siyo habari njema kwa makumi ya watu.

Mkuu kama hujali sana, hebu tuweke sawa kuhusiana na ugonjwa wake, yaani kwanza ni nini anaumwa, alianza lini, na wapi, na kama ana mpango wa kurudi bongo, maana kwa maelezo yako asiporudi nitaelewa ni kwa nini hatarudi, maana hii ishu yake inaaanza kuelekea kuwa sawa na ya Marehemu Waziri Kibona!
 
Gavana wa Benki kuu Tanzania[/QUOT

Honestly speaking!! Was this a seriouse question???

Mimi sioni sababu ya kumshumbulia huyu maaana kuna watanzania waliozaliwa nje sasa wanataka kujua maswala ya home.

Pili sio watanzania tu wanaongea kiswahili inawezekana Mkenya, Ruandees, Congo,Ethiopia Somalia, Zambia na hata wapo wazungu wengi tu wanazangumza hii lugha so mtu anapouliza swali si just mpe jibu then endelea na mada unless liwe ni halina maana yeyote.

Mfano leo kuna mtu kauliza "Kumkoma nyani Giladi" maan yake nini mtu kauliza hakujibiwa. wakati mwingine tutapoteza watu kwa sababu wanahisi hawathaminiwi pale wanapoomba clarification
 
Mkuu kama hujali sana, hebu tuweke sawa kuhusiana na ugonjwa wake, yaani kwanza ni nini anaumwa, alianza lini, na wapi, na kama ana mpango wa kurudi bongo, maana kwa maelezo yako asiporudi nitaelewa ni kwa nini hatarudi, maana hii ishu yake inaaanza kuelekea kuwa sawa na ya Marehemu Waziri Kibona!

Kweli naungana na wewe FM
wana JF wengine tunasikia tu kuwa Balali anaumwa mara amefanyiwa upasuaji mara sasa anaendelea vizuri, Mara RO,EL na Mkuu wa Kaya walienda kumuona. Kama mpaka imefikia RO alienda kumuona basi hii inaashiria kuwa kuna jambo kubwa linaloendelea, huwezi kujua huenda ni Polinium 12, au mafua ya ndege, sisi tunakisia tu.
NI ajabu sana kuona kuwa ugonjwa wa gavana wa benjki ya nchi inakuwa state secret, kama ilivyo afya ya Fidel Casto na Comrade Kim Jong Il, ajabu na Tanzania tumefikia huko! CAN WE DECLARE THAT HIS ILLNESS IS STATE SECRET?
 
Status
Not open for further replies.
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom