olele
JF-Expert Member
- Dec 2, 2010
- 1,303
- 1,559
Hi wana jf, juzi wakati nasoma my bible niligundua kitu cha ajabu kweli
Adam kwa mara ya kwanza alipoamka usingizini akakuta ameumbiwa mwanamke pembeni yake akasema huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu basi ataitwa mwanamke (mwanzo 2:23) but baada ya kufanya makosa ya kula tunda baada ya kudanganywa na nyoka unajua adam alivyomuita? (Mwanzo 2:20) Adam akamwita mkewe jina lake HAWA kwa kuwa yeye ndiye aliye MAMA yao wote walio hai. Ni hivi hakumuona tena kama alivyomuona mwanzo mfupa wake, nyama yake, mwanamke wake, ee mrembo wake nk. Bali akaanza kumuona kama mama, mzazi, kazi yake ni kuzaa.
Nimewahi kuwasikia wanaume wengi wakiwaita wake zao MAMA hata pia wanawake wanawaita waume zao BABA ni kipindi gani katika ndoa unaanza kumuona mke/mume wako baba au mama, na kwa sababu gani anaanza kuwa hivyo?, je ni sawa? Ni aina fulani ya heshima? Unajisikiaje wewe ukiitwa hivyo?
mawazo yenu yanahitajika sana.
Adam kwa mara ya kwanza alipoamka usingizini akakuta ameumbiwa mwanamke pembeni yake akasema huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu basi ataitwa mwanamke (mwanzo 2:23) but baada ya kufanya makosa ya kula tunda baada ya kudanganywa na nyoka unajua adam alivyomuita? (Mwanzo 2:20) Adam akamwita mkewe jina lake HAWA kwa kuwa yeye ndiye aliye MAMA yao wote walio hai. Ni hivi hakumuona tena kama alivyomuona mwanzo mfupa wake, nyama yake, mwanamke wake, ee mrembo wake nk. Bali akaanza kumuona kama mama, mzazi, kazi yake ni kuzaa.
Nimewahi kuwasikia wanaume wengi wakiwaita wake zao MAMA hata pia wanawake wanawaita waume zao BABA ni kipindi gani katika ndoa unaanza kumuona mke/mume wako baba au mama, na kwa sababu gani anaanza kuwa hivyo?, je ni sawa? Ni aina fulani ya heshima? Unajisikiaje wewe ukiitwa hivyo?
mawazo yenu yanahitajika sana.