cheusimangala
JF-Expert Member
- Feb 27, 2010
- 2,585
- 497
Kwa huyo rafiki yako ashukuru Mungu kwani mke amekimbia tu,kuna klisa kilitokea sehemu fulani mkoani Shinyanga ila sitaitaja,mke alifumaniwa kisha jamaa(mume) akamchukua kwa upole akarudi naye nyumbani mke akajua zangu zimeisha lakini jamaa akamuambia wakaoge na wakaoga pamoja na bwana wala hakumgusa,ilipofika saa ya kulala wakalaa ila mume hakuulizia tendo na mwanamke akawa na woga akijua nikimsemesha mume wangu labda nitampandisha hasira.Zikapita wiki mbili bila tendo lakini mengine yote yalikuwa kama kawaida.Siku moja wakati jamaa amerudi kazini jioni hakumuona mkewe kama ilivyokuwa kawaida akaingia chumbani na kumkuta mkewe ameshakunywa sumu na kumuachia ujumbe kuwa hawezi kuishi kwa aibu kiasi kile na wala hawezi kushitaki kunyimwa unyumba na mumewe kwani yeye ndiye alikuwa mkosefu.Basi jamaa alilia sana kwenye msiba na alikuwa akisema kuwa zilibaki siku mbili tu ifike siku ya wapendanao na alikuwa amemuandalia surprise mke wake ili waanzishe upya penzi lao lililokuwa limeingiliwa.
paka kisa chako kimenifanya machozi yanilenge.
hapa inaonesha kabisa hawa wanandoa walikua wanapendana sana lkn kwa vile shetani hapendi kuona watu wa mungu wakiishi kwa furaha akahakikisha haya yanatokea.poor husband.