kwa wale wa longtime

hii ndio a aaa
iko kama kata aaaa

hii ndio e eee
ina mkia mfupi eee

hii ndio i iii
ina kofia juu iii

hii ndio o ooo
iko kama yai ooo

hii ndio u uuu
iko kama kikombe uuu
He he he heeee!!!
 
... Chopeko na Mnofu, duh.. wakuu ninaipenda elimu ya zamani kuliko hii ya sasa iliyo-chakachuliwa...
 
Hahahahh mecheka kwelikweli...hizi hadithi na simulizi nilizisoma zote na nikizifuma popote huwa nazinunua kwaajili ya wanangu....

Wagagagigikoko....
Fimbo mpige kalumekenge ( haa hii naitumia kama mechanism ya kuwafanya wale msosi na kwenda shule )

Halafu kuna vitabu vya 'kikubwa' zaidi jamani
1.Kosa la bwana Msa
2.Kisima cha giningi
3.Hukooooo darisalama

Guess what ? Vyote nilivisoma nikiwa primary..na sasa vingi vipo scholastic bookshop mlimanicity u can get some for ur kids au kwako mwenyewe kujikumbusha..
 
Karudi baba mmoja, toka safari ya mbali
Kavimba yote mapaja, na kutetemeka mwili
Watoto wake wakaja, ili kumtaka hali
Wakataka na kauli, iwafae maishani

Akatamka mgonjwa, ninaumwa kweli kweli
Hata kama nikichanjwa, haitoki homa kali
Roho naona yachinjwa, kifo kinanikabili
Kama mnataka mali, mtayapata shambani..
Duh, loong tyme
 
Hadithi inayokuja, ni ya sungura sikia
Hadithi uliyongoja, leo ninakuletea
Alitoka siku moja, njaa aliposikia
Njaa aliposikia, sungura nakuambia

Siku ile akaenda, porini kutembelea
Akayaona matunda, mtini yameenea
Sungura akayapenda, mtini akasogea
Mtini akasogea, sungura nakuambia

Sungura karukaruka, matunda akarukia
Lakini hakuyashika, mkononi hakutia
Sijui nini na nini, sungura nakuambia..
Lol..
 
sikiri mimi masikini
uvivu wangu nyumbani
nakufa hapa kwa nn?
 
alfu lela ulela "funguka mtama, funguka ufuta, funguka mahindi." kumbe ni "funguka sesame"

Karume kenge alikata kwenda shule baba yake akamuendea mbuzi je mbuzi hutaki kuywa maji, nayo yazime moto, nao umchome fimbo, naye amchape mbwa ,naye amuume karume kenge ,naye apate kwenda shule.....:flame:
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom