SCAM: Rifaro Africa, hii ni DECI nyingine?

Special agent.

Senior Member
Aug 25, 2015
101
71
Duh? Mimi siamini kampuni za kibongo hata kidogo,hadi leo walioweka Pesa zao DECI zimepotea hawajalipwa,vp kuhusu hii Rifaro Africa? Hapana hii ni DECI nyingine.
Hii kampuni inajihusisha na uuzaji wa muda wa maongezi kwa njia ya kielectroniki kwa wateja wa mitandao yote.Wanasema changamkia fursa,simu yako jembe lako.Sasa wanachofanya wao ni kwamba wameeliminate superdealer,agent na retailers na kukuweka wewe kama ukijiunga nao ili ununue kutoka kampuni moja kwa moja na kumuuzia mteja.

Kwa hiyo wewe sasa ndio unakua unalipwa commission ambayo wangetakiwa walipwe hao watu uliowaeliminate.Malipo yao ni kwa week kila jumatano na tarehe 5 ya kila mwezi.Ukimuunganisha mtu akawa anatoa hiyo huduma utalipwa 20,000 nae akamuunganisha mwingine utalipwa 8000 na akimuunganisha mwingine utalipwa 5000,mwingine tena 3000 mpaka 2000.

Mtoa semina wake sasa jamaa wa kikenya anajua kuhamasisha balaa,anaongea ukweli sema anatoa ukweli nusu ili kuaminisha watu kua Mo Dewji utajiri wake unatokana na u-superdealer alionao wa vocha za voda, hapa ndio nikaona huyu jamaa yuko hapa kutapeli tu watu kwanini asiseme ukweli halisi?

Na cha mwisho sasa eti unahitaji kuwalipa 128,500 ili wakuunganishe uwe unaweza kuuza na kununua vocha kwa njia hii!!!Yani utajiri wote wanaoongelea upatikane hivi?Labda waseme wao ndio watapata utajiri ila sio wewe mteja wao.

Nimepata wasiwasi nao kusema na ukweli.Nitaendelea kuaminu kua kwenye utajiri kamwe watu hawaalikani na kutoleana siri kama hivi.
KUNA MTU KULE FACEBOOK WALL YAKE ALIANDIKA HIVI.

Network Marketing, mfumo wa kibiashara wa Kipyramid, athari zake kwa Nchi masikini hauna kipimo:
1)Baadhi ya Makampuni Hayaruhusu mtu kuwa na duka la bidhaa zao, bali unaruhusiwa kuwa mchuuzi, kutembezatembeza kama machinga
2) Vijana wengi wameacha Professions zao kama vile Udaktari, Ualimu, Uinjinia na kujikuta wakiwa busy kutengeneza Network zao,Matokeo yake Taifa lililoinvest mabilioni kuwatrain hawa watu likiwa halinufaiki nao, hii inafanya Taifa hilo liendelee kuwa tegemezi kwa Wataalam wa nje
3) Ni njia ya kijanja sana ya kujenga Monopoly, Makampuni mengi hutarget vijana wenye elimu na ambao wanakipato fulanifulani, Unapowaingiza hawa watu katika Network ni sawasawa na Unewabatiza au umewafanya kuwa wanachama, Hawa watakuwa loyal kwa network husika, na wataendelea kurecruit watu katika network hiyo na kuendelea kusambaza " Habari njema" ya products husika.
4) Ni pyramid Scheme ambayo eventually itacollapse, NI KWELI Wajanja waliowahi na kuingia mapema WANAPIGA HELA, ila tatizo ni vijana waliomaliza chuo wanaokuja katika link ya chini katika chain. Rate ya recruitment inadecrease kwa sababu market iko saturated, Je Commision za kuwalipa zitatoka wapi kama hakuna new recruits?, Eventually ina collapse!
5) Ni kweli wanalipa kodi serikalini, lakini kodi wanayolipa ni ndogo kuliko wanayokwepa!. Hakuna namna ambavyo Commision ya kila member inavyokuwa Taxed, kwa sababu wanavyolipana ni ngumu kutrace.
USHAURI WANGU
Vijana msitake utajiri wa "kiexponential", Tengenezeni utajiri kwa kutoa huduma na Kuzalisha, hii ya Kusubiri kulipwa kutokana na Kiingilio cha wanachama wapya katika chain yako ni kula pesa bila kuzalisha, na mimi binafsi nadhani ni Morally wrong!
 
Hii kampuni inajihusisha na uuzaji wa muda wa maongezi kwa njia ya kielectroniki kwa wateja wa mitandao yote.Wanasema changamkia fursa,simu yako jembe lako.Sasa wanachofanya wao ni kwamba wameeliminate superdealer,agent na retailers na kukuweka wewe kama ukijiunga nao ili ununue kutoka kampuni moja kwa moja na kumuuzia mteja.

Kwa hiyo wewe sasa ndio unakua unalipwa commission ambayo wangetakiwa walipwe hao watu uliowaeliminate.Malipo yao ni kwa week kila jumatano na tarehe 5 ya kila mwezi.Ukimuunganisha mtu akawa anatoa hiyo huduma utalipwa 20,000 nae akamuunganisha mwingine utalipwa 8000 na akimuunganisha mwingine utalipwa 5000,mwingine tena 3000 mpaka 2000.

Mtoa semina wake sasa jamaa wa kikenya anajua kuhamasisha balaa,anaongea ukweli sema anatoa ukweli nusu ili kuaminisha watu kua Mo Dewji utajiri wake unatokana na u-superdealer alionao wa vocha za voda, hapa ndio nikaona huyu jamaa yuko hapa kutapeli tu watu kwanini asiseme ukweli halisi?

Na cha mwisho sasa eti unahitaji kuwalipa 128,500 ili wakuunganishe uwe unaweza kuuza na kununua vocha kwa njia hii!!!Yani utajiri wote wanaoongelea upatikane hivi?Labda waseme wao ndio watapata utajiri ila sio wewe mteja wao.

Nimepata wasiwasi nao kusema na ukweli.Nitaendelea kuaminu kua kwenye utajiri kamwe watu hawaalikani na kutoleana siri kama hivi.
 
KUNA MTU KULE FACEBOOK WALL YAKE ALIANDIKA HIVI.

Network Marketing, mfumo wa kibiashara wa Kipyramid, athari zake kwa Nchi masikini hauna kipimo:

1)Baadhi ya Makampuni Hayaruhusu mtu kuwa na duka la bidhaa zao, bali unaruhusiwa kuwa mchuuzi, kutembezatembeza kama machinga

2) Vijana wengi wameacha Professions zao kama vile Udaktari, Ualimu, Uinjinia na kujikuta wakiwa busy kutengeneza Network zao,Matokeo yake Taifa lililoinvest mabilioni kuwatrain hawa watu likiwa halinufaiki nao, hii inafanya Taifa hilo liendelee kuwa tegemezi kwa Wataalam wa nje

3) Ni njia ya kijanja sana ya kujenga Monopoly, Makampuni mengi hutarget vijana wenye elimu na ambao wanakipato fulanifulani, Unapowaingiza hawa watu katika Network ni sawasawa na Unewabatiza au umewafanya kuwa wanachama, Hawa watakuwa loyal kwa network husika, na wataendelea kurecruit watu katika network hiyo na kuendelea kusambaza " Habari njema" ya products husika.

4) Ni pyramid Scheme ambayo eventually itacollapse, NI KWELI Wajanja waliowahi na kuingia mapema WANAPIGA HELA, ila tatizo ni vijana waliomaliza chuo wanaokuja katika link ya chini katika chain. Rate ya recruitment inadecrease kwa sababu market iko saturated, Je Commision za kuwalipa zitatoka wapi kama hakuna new recruits?, Eventually ina collapse!

5) Ni kweli wanalipa kodi serikalini, lakini kodi wanayolipa ni ndogo kuliko wanayokwepa!. Hakuna namna ambavyo Commision ya kila member inavyokuwa Taxed, kwa sababu wanavyolipana ni ngumu kutrace.

USHAURI WANGU:
Vijana msitake utajiri wa "kiexponential", Tengenezeni utajiri kwa kutoa huduma na Kuzalisha, hii ya Kusubiri kulipwa kutokana na Kiingilio cha wanachama wapya katika chain yako ni kula pesa bila kuzalisha, na mimi binafsi nadhani ni Morally wrong!
 
KUNA MTU KULE FACEBOOK WALL YAKE ALIANDIKA HIVI.

Network Marketing, mfumo wa kibiashara wa Kipyramid, athari zake kwa Nchi masikini hauna kipimo:
1)Baadhi ya Makampuni Hayaruhusu mtu kuwa na duka la bidhaa zao, bali unaruhusiwa kuwa mchuuzi, kutembezatembeza kama machinga
2) Vijana wengi wameacha Professions zao kama vile Udaktari, Ualimu, Uinjinia na kujikuta wakiwa busy kutengeneza Network zao,Matokeo yake Taifa lililoinvest mabilioni kuwatrain hawa watu likiwa halinufaiki nao, hii inafanya Taifa hilo liendelee kuwa tegemezi kwa Wataalam wa nje
3) Ni njia ya kijanja sana ya kujenga Monopoly, Makampuni mengi hutarget vijana wenye elimu na ambao wanakipato fulanifulani, Unapowaingiza hawa watu katika Network ni sawasawa na Unewabatiza au umewafanya kuwa wanachama, Hawa watakuwa loyal kwa network husika, na wataendelea kurecruit watu katika network hiyo na kuendelea kusambaza " Habari njema" ya products husika.
4) Ni pyramid Scheme ambayo eventually itacollapse, NI KWELI Wajanja waliowahi na kuingia mapema WANAPIGA HELA, ila tatizo ni vijana waliomaliza chuo wanaokuja katika link ya chini katika chain. Rate ya recruitment inadecrease kwa sababu market iko saturated, Je Commision za kuwalipa zitatoka wapi kama hakuna new recruits?, Eventually ina collapse!
5) Ni kweli wanalipa kodi serikalini, lakini kodi wanayolipa ni ndogo kuliko wanayokwepa!. Hakuna namna ambavyo Commision ya kila member inavyokuwa Taxed, kwa sababu wanavyolipana ni ngumu kutrace.
USHAURI WANGU
Vijana msitake utajiri wa "kiexponential", Tengenezeni utajiri kwa kutoa huduma na Kuzalisha, hii ya Kusubiri kulipwa kutokana na Kiingilio cha wanachama wapya katika chain yako ni kula pesa bila kuzalisha, na mimi binafsi nadhani ni Morally wrong!

Get rich quickly schemes hizi itakua tu na hakuna lolote hapa
 
HABARI NDG,

JE UNA HABARI KWAMBA UNAWEZA KUTIMIZA NDOTO ZAKO KUBWA KUPITIA SIMU YA MKONONI?

TAMBUA UTAJIRI ULIOPO KWENYE SECTA YA MAWASILIANO. KULINGANA NA TAARIFA YA TCRA WATANZANIA TAKRIBANI BILIONI 36 WANAMILIKI SIMU ZA MKONONI NA WANATUMIA WASTANI WA SH. 1,000 KWA SIKU KUPIGA SIMU NA KUTUMA SMS HAPO HAKUNA HESABU YA INTERNET.HIVYO KWA SIKU MOJA NI ZAIDI YA SH.BILIONI 36 ZINATUMIKA KUPIGA SIMU NA SMS....NA KATI YA HIZO 10℅ ZINAKWENDA KWA MASUPER DEALER"

HIVYO KWA MTU MAKINI KUINGIA UBIA KTK SECTA INAYOKUWA KIUCHUMI KWA KASI HIVYO HALINA MJADALA "

NAWATAMBILISHA KWENU KAMPUNI YA RIFARO AFRICA ILIYOPEWA DHAMANA NA MAKAMPUNI YA SIMU KUWA SUPER DEALER (Msambazaji Mkuu)
KUPITIA DHAMANA HIYO HII IKAJENGA MFUMO AMBAO UTASHIRIKISHA WATANZANIA KUJIPATIA KIPATO BILA KUACHA SHUHULI ZAO ZA KILA SIKU.
MFANO WENYEWE NI BIASHARA YA MTANDAO( NET WORK MARKETING)
BIASHARA YA MTANDAO NI NINI?
Ni Mfumo wa kisasa wa kusambaza Bidhaa kwa TAARIFA.
Ni Mfumo ambao Mtaji wake ni RASILI MALI WATU.
Ni Mfumo wa Biashara unaokuwezesha KUPATA kipato BILA YA uwepo wako.

Wengi wetu tunauzoefu KUPITIA MAKAMPUNI kama Forever living, GNLD, EDMARK TREVO N.K
MAKAMPUNI haya mengi WANATUMIA Mfumo huu lakini wana Bidhaa zinazoshikika za Virutubisho Vipodozi n.k.

KAMPUNI YA RIFARO AFRICA INATUMIA BIDHAA YA MUDA WA MAONGEZI(Air Time)
Bidhaa inayotumika sana NA KILA MTU sababu ya Umuhimu wake. Haina haja ya kumshawshi MTU atumie.

KIPATO KINAKUJAJE?
KUNA KIPATO CHA AINA MBILI.KIPATO CHA WIKI NA KIPATO CHA MWEZI

KIPATO CHA WIKI:
Kipato CHA WIKI kinatokana NA MATANGAZO, Tangazo GANI? Tangazo ni kuabarisha Ndg, Jamaa NA Marafiki Jinsi ya kutumia MFUMO wa kununua Muda wa MAONGEZI KUPITIA SIMU yake YA MKONONI MOJA KWA MOJA kiwandani Ikiwa na maana KWAMBA atanunua MOJA KWA MOJA KWA KAMPUNI husika ya SIMU NA Sio VOUCHER za kukangua. HAPO inasemekana umefanya Tangazo na Unahitajika kulipwa.

MALIPO:
WIKI INAHESABIWA Jumapili mpaka Jumapili
Mfano. Ukiabarisha WATU 5 wataitwa kizazi chako CHA kwanza, kizazi CHA kwanza KILA Mmoja utalipwa SH. 20,000×5=100,000
Hao 5 nao wana NDG Jamaa NA marafiki nao wakiabarisha 5 KILA Mmoja 5×5=25
Hao wataitwa kizazi chako CHA pili.

Kizazi CHA pili KILA Mmoja utalipwa SH. 8,000×25=200,000

Kizazi CHA pili kitakuzalia kizazi cha Tatu, hao 25 @ akiabarisha 5 ×25= 125
Kizazi CHA Tatu @ utalipwa sh. 5,000×125=625,000

Kizazi cha Tatu kitakuzalia kizazi cha Nne,hao 125@ akiabarisha 5×125=625
Kizazi cha Nne @ utalipwa sh. 5,000×625= 3,125,000

Kizazi cha Nne kitakuzalia kizazi cha Tano, hao 625 @ akiabarisha WATU 5×625=3,125
Kizazi cha 5 @ utalipwa sh. 5,000×3,125= 15,625,000

Kizazi hivi vinaendelea mpaka kizazi cha 15
NB. Kizazi cha 6 @ utalipwa sh.3,000
Kizazi cha 7-15 utalipwa sh.2,000

HII ndio Siri ya Biashara YA Mtandao, Unaokuwezesha kutengeneza pesa KUPITIA RASILI MALI WATU.

KIPATO CHA MWEZI;
KIPATO cha MWEZI kinatokana na Matumizi yako YA Muda wa MAONGEZI NA Matumizi YA WATU wote walio KWENYE Mtandao wako. Utapewa Pacenti

Pia kuna Zawadi mbali mbali kulingana NA wingi wa WATU walioko KWENYE timu yako. Kuna Zawadi YA Kiwanja,gari,nyumba

Kwa maelezo ya jinsi ya kujiunga au maswali yoyote nipigie/whatsapp 0718511073 (namba ya mdhamini ni R211016)

WATALAAM WA UCHUMI WANASEMA
MAFANIKIO AU UTAJIRI NI SECTA + BIDHAA +BIDII + MTAZAMO SAHIHI.
 
Waungwana

Kuna kampuni inayoitwa Rifaro Africa, ambayo imeanzishwa na kampuni nyingine, inaitwa Selcom. Rifaro Africa inajiendesha kwa mfumo wa Multi Level Marketing (MLM) au kwa jina lingine Network Marketing (NM), huku bidhaa kuu ikiwa manunuzi ya muda wa matumizi ya simu, yaani, mobile phone airtime.

Rifaro Africa imewawekea sharti wateja wake, wanaoitwa wanachama, sharti la kuwa na matumizi ya simu yasiyopungua Shs. 15,000 kwa mwezi.

Ninaomba kupata taarifa zaidi kuhusu kampuni hii kwani "machale" yananicheza.

Mtu yeyote mwenye kuijua kampuni hii kwa undani wake tafadhali tuelimishane kwa kina.

Asante.
 
Hizi Network Marketing nyingi hazieleweki, mwenye ujuzi wa kina achambue hapa watu waelewe clearly...
 
Hizi Network Marketing nyingi hazieleweki, mwenye ujuzi wa kina achambue hapa watu waelewe clearly...
Nasikia kuwa wanajiunga na kabla ya kujiunga unatoa kiasi cha fedha ndio unakuwa unauza muda wa maongezi wa mitandao yote kadili ya unavyofikisha watu wengi kwa kuwaunga ndio muda wa kwako kupata faida kubwa biashara ni nzuri mno kwa sababu unaanza ww unajiunga na unawaunga wa ukoo wako ndugu jamaa unapata faida sio tofauti Sana living forever tofauti huko madawa huku vocha
 
Waungwana

Kuna kampuni inayoitwa Rifaro Africa, ambayo imeanzishwa na kampuni nyingine, inaitwa Selcom. Rifaro Africa inajiendesha kwa mfumo wa Multi Level Marketing (MLM) au kwa jina lingine Network Marketing (NM), huku bidhaa kuu ikiwa manunuzi ya muda wa matumizi ya simu, yaani, mobile phone airtime.

Rifaro Africa imewawekea sharti wateja wake, wanaoitwa wanachama, sharti la kuwa na matumizi ya simu yasiyopungua Shs. 15,000 kwa mwezi.

Ninaomba kupata taarifa zaidi kuhusu kampuni hii kwani "machale" yananicheza.

Mtu yeyote mwenye kuijua kampuni hii kwa undani wake tafadhali tuelimishane kwa kina.

Asante.
Muda kama saa moja iliyopita staff mwenzangu ameniapproach na dili la aina hiyo. ametoa maelezo mengi sana ya kuvutia na kuniwekea clip ya maelezo toka kwa wenye kampuni. Kimsingi ni namna ya kutengeneza mapato kwa mgumo wa pyramid na generations, ambapo unaanza wewe, unashawishi mtu, akijiunga naye anaendelea kushawishi wengine etc..etc, na wewe unafaidika na kila anayejiunga kwenye generation uliyoanzisha wewe!
Mimi niko very cautious na hizi kitu, nimemwambia jamaa anipe muda niifuatilie kampuni hii, ila inajinadi kuwa ina vibali vyote vya Brela, TISS na TRA, japokuwa nashangaa Usalama wa Taifa wamejiingizaje kubariki aina fuklani za biashara!
Vinginevyo jamaa anasema kuwa vocha za kukwangua zitakwenda kuisha, na hii Rifaro ndio itakamata ukanda, na hivyo ukiwahi kujiunga na kuwa agent una nafasi kubwa ya kuwa Milionea.

Nashauri tufuatilie zaidi hii kitu!
 
Duhh mkuu ok upooaisee


Ngoja nigogogo kama wako member ea tea maana wakijabanwaasalio yetu yote yanafinywa jutoi uingizi mpaka wamalizane NA tra...loh

NA nani mmiliki hivi vitu muhimui sana NA iweje ties ikaingizwa humor kunanini

Msinikumbushe ya ........sijui kama zilepesa bado ziko BOT AMA
 
Nami nimeisikia pia... Mtindo wa kama forever living... Utatafuta wanachama pia, wawe chini yako
Kuna maelezo kwamba kampuni hii inafanya kazi na mitandao mikuu minne, yaani, Zantel, Airtel, Tigo na Voda. Wanauza airtime (sio vocha), kwa njia ya elektroniki, za mitandao hiyo, kwa mikataba rasmi. Yaani, unapokuwa "mwanachama" na wewe unakuwa unanunua airtime za mitandao hiyo bila kutumia vocha za kukwangua.

Wanatumia lugha tamu ya kushawishi, lakini mimi bado nina hofu.

Labda niongee na wahusika kwenye hizi kampuni. Nitarudi.

Update: Jumamosi, Januari 23, 2016

Baada ya kupata ufafanuzi, nimeamua kujiunga na kuwa mwanachama wa Rifaro Africa, kwa sababu zifuatavyo:

1. Kampuni hii imesajiliwa kwa mujibu wa sheria, kwa hiyo inafanya biashara halali. Hakuna utapeli.
2. Kutokana na uhalali wake, kampuni ya Selcom Wireless (ambayo tayari imekuwa ikifannya shughuli zake kwa zaidi ya miaka 7) ndiyo pekee inayosimamia malipo yote yanayofanyika kati ya Wanachama na kampuni ya Rifaro Africa Ltd.
3. Mwanachama anapojiunga kwa kulipa kiingilio cha Shs. 128,500/=, anapewa kadi ya Selcom (Selcom Card) ambayo inatumika kwa malipo yote: (1) Malipo kutoka Rifaro kwenda kwa Mwanachama, (2) Malipo anayofanya Mwanachama kufanya manunuzi ya salio la simu, (3) Kuhamisha fedha kwenda kwenye akaunti za Airtel Money, M-Pesa, TigoPesa na EzyPesa, (4) Mwanachama kutoa fedha na kupata fedha taslimu kupitia kwa wakala wa Selcom/Rifaro, na (5) Mwanachama kuweka pesa kwenye Selcom Card, kwa ajili ya kununua airtime kupitia wakala wa Selcom/Rifaro.
4. Kila Mwanachama hulipwa kamisheni kwa kuwaunganisha wanachama wengine chini yake, kupitia mfumo wa udhamini, akiwapa namba yake ya uanachama, ambayo ndiyo inayomtambulisha yeye kwa kampuni (Rifaro) kama mdhamini wa wanachama hao wapya.

Tofauti na kampuni nyingine zinazutumia mfumo wa Multi Level Marketing (MLM) na Network Marketing (NM), mwanachama wa Rifaro Africa HANA BIDHAA YOYOTE ILE ya kumwuzia mtu, isipokuwa kumwunganisha kwenye kampuni. Bado sijajua iwapo (pengine inawezekana) mwanachama mwenye Selcom Card anaweza kuwa wakala wa kampuni ya Selcom, na kuweza kufanya biashara ya kuwa wakala wa malipo kwa "bidhaa" zote zinazopatikana kwenye mfumo wa Selcom Paypoint, kama vile manunuzi ya airtime (muda wa maongezi ya simu), malipo ya visambuzi vya luninga kama vile Zuku, Startimes na DSTV, n.k. Nitafuatilia kuhusu jambo hili na kuwapa taarifa baadae.

Mimi nilikuwa na HOFU KUBWA (lazima niwe mkweli) lakini baada ya kuongea na mmoja wa wakurugenzi wa Selcom, hofu yote imenitoka. Sikutaka kuongea na viongozi wa Rifaro ili kufahamu juu ya uhalali wa kampuni hii, kwa kuwa wao wasingeweza kuitendea haki hofu yangu hiyo (Mwamba ngoma huvutia kwake).

Kama kuna mwenye maswali zaidi, nitumie ujumbe binafsi (PM).

Asante.
 
Back
Top Bottom