Crashwise
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 22,227
- 8,735
Petrol bado bei juu, umeme hali kadhalika, kodi ya nyumba balaa, mchele na nyama ndo usiseme, starehe nazo bei juu yaani bia, wine, soda na juice bei juu. eti kilimo kwanza wakati malori marufuku kubeba mazao ya walala hoi, Dini sadaka nazo juu hawataki salafu wanataka noti tu, Mahari nazo hatari unapigiwa hesabu kuanzia mimba hadi shule. Chadema wakiomba mkutano mpaka damu imwagike, hivi CCM itatuhujumu mpaka lini? rate ya dola nayo haisemeki. ada ya shule ipo juu utadhani unanunua shule! sasa hii ndo maisha bora kwa kila Mtanzania...